Author: E-FM CO LTD

  • Korea kaskazini imefyatua ”kombora” la tatu ndani ya siku 8

    Korea kaskazini imefyatua ”kombora” la tatu ndani ya siku 8

    Korea kaskazini imefyatua kombora la masafa mafupi ambalo halijabainika mara mbili , kwa mujibu wa maafisa wa Korea Kusini , katika jaribio la tatu la silaha hizo katika kipindi cha wiki moja pekee.

    Ufyatuaji wa makombora hayo ulifanyika katika eneo la mwambao wa mashariki mwa taifa hilo mapema Ijumaa.

    hatua hiyo inaonekana kama hatua ya taifa hilo inayolenga kujibu mazoezi ya kijeshi ya baina ya Korea Kusini na Marekani yanayotarajiwa kuanza mwezi huu.

    Wakati huo huo Uingereza, Ufaransa na Ujerumani zimeitaka Korea kaskazini kushiriki maungumzo ya “maana ” na Marekani.

    baada ya mkutano wa faragha katika baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa , mataifa yalisema kuwa vikwazo vya kimataifa vinapaswa kuimarishwa hadi utawala wa Pyongyang utakapoangamiza mipango yake ya nyuklia makombora ya masafa.

    Ufyatuaji wa makombora hayo ulifanyika katika eneo la Yonghung katika jimbo la South Hamgyong katika bahari ya Japan, inayofahamika pia kama Bahari ya Masharik , kwamujibu wa Mkuu wa kikosi cha pamoja cha Korea kaskazini na Korea Kusini (JCS)

    Eneo hilo linaonekana kama kituo cha kufyatulia makombora ambacho hakijawahi kutumiwa awali , amesema Ankit Panda, afisa katika shirikisho la wanasayansi wa Marekani – Federation of American Scientists.

    “Hiki ni kielelezo kingine cha enzi ya Kim Jong-un zaidi ya ufyatuaji wa makombora ya usiku : kufyatua kutoka vituo ambavyo havikuwahi kutumiwa awali au ambavyo havitumiwi .”

    Akizungumza katika ikulu ya White House, rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa hana hofu na ufyatuaji wa hivi karibuni w amakombora kwasababu ni ya masafa mafupi na “ni ya kiwango cha kawaida “.

    Vipi kuhusu majaribio mengine?

    Jumatano , Korea Kaskazini ilirusha makombora mawili ya masafa yanayopaa kilomita 250 (maili 155 ) na kufikia urefu wa kilomita 30 kabla ya kutua kwenye bahari ya Japan, inayofahamika a Bahari ya mashariki , k wamujibu wa Korea Kusini.

    Korea Kusini iliyatambua makombora hayo ya masafa kuwa yalikuwa ni aina tofauti na yaliyofyatuliwa awali . Lakini Alhamisi , Pyongyang ilitoa kauli tofauti , ikisema kuwa ilifanya majaribio ya mfump mpya wa ufyatuzi wa roketi, lakini haikutoa maelezo.

    Mnamo Julai 25, Korea kaskazini ilifyatua makombora mengine mawili, moja likiwa na uwezo wa kusafiri takriban kilomita 690.

    Ufyatuaji huo wa makombora ulikuwa ni wa kwanza kufanyika tangu Bwana Trump na kiongozi wa korea Kim Jong-un wafanye mkutano ambao haukupangwa mwezi Juni katika eneo lisilokuwa na silaha ,, ambalo linatenganisha Korea mbili , ambako walikubaliana kuanzisha mazungumzo ya kuacha matumizi ya nyuklia.

    Ni nini kinachoendelea sasa?

    Korea kaskazini hivi karibuni ilipaza sauti ya hasira yake dhidi ya mazoezi yaliyopangwa kufanyika baina ya Marekani na Korea Kusini, tukio la mwaka ambalo washirika wamekataa kuachana nalo ,lakini limeleta athari kubwa.

    Korea kaskazini inayaona mazoezi hayo ya kijeshi lama maandalizi ya vita na iliyaita “uvuriugaji wa roho ” wa kauli ya pamoja aliyoisaini Bwana Trump na Kim katika kikao chao cha kwanza cha ana kwa ana cha mwaka jana cha Singapore.

    Pyongyang ilikuwa imeonya kwamba mazoezi hayo yanaweza kuathiri kufufuliwa kwa mazungumzo ya kuanchana na nyuklia.

    Jumatatu waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Mike Pompeo alisema kwamba anatumaini mazungumzo haya yanaweza kuanza “haraka sana ”, lakini hakuna mkutano uliopangwa.

    Mwaka jana , Bwana Kim alisema Korea Kaskazini ingesitisha majaribio ya nuklia, na ingeacha kufyatua tena makombora ya masafa marefu yanayoweza kuvuka mipaka ya mabara.

    Shughuli za nyuklia zinaelekea kuendelea, hata hivyo , na picha za setilaiti za kituo kikuu cha nyuklia cha Korea Kaskazini mwezi uliopita zilionyesha kuwa taifa hilo huenda linatengeneza mionzi ya inayochochea makombora.

    Serikali ya Pyongyangpia inaendelea kuonyesha uwezo wake wa kutengeneza silaha mpya licha ya kuwekewa vikwazo vikali vya kiuchumi.

    Ilifyatua kombora la masafa mafupi la aina hiyo mapema mwezi Mei ,likiwa ni kombora la kwanza la aina yake tangu iliporusha kombora la ballistic mnamo mwaka 2017.

    Korea Kaskazini pia ilionyesha manuwari yake ya kijeshi wiki iliyopita, ambayo maafisa wa Korea Kusini wamesema ina uwezo wa kubeba makombora hadi matatu ya masafa ya ballistic.

    cc;BBCswahili

  • Mtoto wa kiume wa Bin Laden ”amefariki”

    Mtoto wa kiume wa Bin Laden ”amefariki”

    Mwana wa kiume wa muasisi wa al-Qaeda Osama Bin Laden, Hamza,amefariki , kwa mujibu wa maafisa wa ujasusi wa Marekani.

    Taarifa kuhusu mahala au tarehe ya kifo cha Hamza Bin Laden bado haijawa wazi katika ripoti ya chanzo hicho cha habari.

    Mwezi Februari, Serikali ya Marekani iliahidi kutoa dola milioni 1 kwa ajili ya yeyote atakayetoa taarifa zitakazosaidia kutambua ni wapi alipo.

    Hamza Bin Laden, anayedhaniwa kuwa na umri wa miaka 30, alikuwa ametoa ujumbe mbalimbali wa sauti na video akitoa wito wa kufanya mashambulio dhidi ya Marekani na nchi nyingine.

    Ripoti zilitolewa kwanza na mashirika ya habari ya NBC na New York Times.

    Hamza Bin Laden aliwatolea wito wapiganaji wa jihadi kulipiza kisasi mauaji ya baba yake aliyeuliwa na kikosi maalum cha Marekani nchini Pakistan mnamo mwezi Mei 2011.

    Kadhalika alikuwa amewatolea wito watu wa rasi ya Arabia kulipiza kisasi. Saudi Arabia ilimyang’anya uraia mwezi Machi.

    Aliaminika kuwa katika kifungo cha nyumbani nchini Iran lakini ripoti nyingine zilisema kuwa huenda alikuwa akiishi katika mataifa ya Afghanistan, Pakistan na Syria.

    Wizara ya mambo ya nje ya Marekani ilisema kuwa nyaraka zilizokamatwa katika uvamizi wa mwaka 2011 katika nyumba ya baba yake ya Abbottabad, Pakistan, zinaonyesha kuwa Hamza Bin Laden alikuwa anaandaliwa kuchukua utawala wa al-Qaeda.

    Vikosi vya Marekani pia viliripotiwa kubaini video hii ya harusi yake akimuoa binti wa afisa mwingine wa ngazi ya juu wa al-Qaeda ambayo ilidhaniwa kufanyika nchini Iran

    Baba mkwe wake alikuwa ni Abdullah Ahmed Abdullah au Abu Muhammad al-Masri, ambaye anatafutwa kwa madai ya kuhusika katika mashambulio ya ugaidi ya mwaka 1998 dhidi ya balozi za Tanzania na Kenya.

    Al-Qaeda lilikuwa ni kundi lililotekeleza mashambulio mabaya ya ugaidi ya Septemba 11, 2001 dhidi ya Marekani, lakini hadhi yake kwa sasa imeshuka katika kipindi cha miongo kadhaa iliyopita baada ya kuibuka kwa umaarufu wa kundi la Islamic State.

    Ni ishara ya jinsi taarifa chache kumuhusu Hamza Bin Laden kiasi kwamba maafisa hawakuweza kuthibitisha umri wake.

    Katika miezi ya hivi karibuni walisema kuwa huenda alikuwa nchini Afghanistan, Pakistan au Iran. lakini hawakuweza hata kusema ukweli hasa ni nchi gani mmoja wa watu ambao Marekani ”inawatafuta sana” anaishi.

    Zawadi ya dola milioni moja kwa yeyote atakayetoa taarifa kumuhusu ilikuwa ni hatua si tu ya uwezekano wa hatari anayoweza kusababisha lakini pia ilikuwa ni ishara ya umuhimu kwa al-Qaeda na propaganda yao.

    Hamza alikuwa ni mtoto pekee aliyekuwepo wakati baba yake aliposaidia kupanga njama za mashambulio ya Septemba 11 lakini, kwa mujibu wa wakuu wa kundi hilo lenye itikadi kali, alikuwa pamoja naye wakati wa mashambulio hayo.

    Kwa mtoto wa kiume ambaye alikuwa akifundishwa kuichukia Marekani, kukwepa mauaji ya ulipizaji kisasi mikononi mwa kikosi maalumu lingekuwa ni jambo ambalo lingesalia akilini mwa watu.

    Katika miaka ya hivi karibuni alituma ujumbe mtandaoni akitoa wito kwa mashambulio dhidi ya Marekani na washirika wake.

    Al-Qaeda: Taarifa muhimu

    • Alifahamika nchini Afghanistan katika miaka ya mwisho ya 1980, kama mwarabu aliyejitolea kujiunga na kikosi cha Afghanstan kilichoungwa mkono na mujahideen kilichopigana kuvifukuza vikosi vilivyoteka eneo la Usovieti
    • Osama Bin Laden alianzisha shirika la kusaidia wahudumu wa kujitolea ambalo lilikuja kutambuliwa kama al-Qaeda, au “ngome”
    • Aliondoka Afghanistan mnamo mwaka 1989, na kurejea tena mwaka 1996 kuongoza makambi ya mafunzo ya kijeshi ya maelfu ya waislamu kutoka mataifa ya kigeni.
    • Al-Qaeda ilitangaza “vita vitakatifu ” dhidi ya Wamarekani,wayahudi na washirika wao.

    cc;BBCswahili

  • Mamilioni ya watu bado wanakabiliwa na njaa Afrika

    Mamilioni ya watu bado wanakabiliwa na njaa Afrika

    Zaidi ya watu milioni 820 au 10.8% duniani bado wanakabiliwa na njaa, inasema ripoti ya Umoja wa Mataifa wakati dunia ikiadhimisha siku ya njaa siku ya njaa.

    Kiwango cha njaa kimepanda karibu katika maeneo yote ya Afrika, na kulifanya bara la Afrika kuwa kanda yenye idadi kubwa ya watu wenye utapiamlo, kwa takriban asilimia 20, ikifuatiwa na Asia ambako zaidi ya asilimia 12 ya wakazi wa bara hilo wana tatizo hilo.

    Asilimia 7 ya watu wa Amerika Kusini na Caribbean pia wameathiriwa na utapiamlo. Kuna watoto zaidi ya milioni 40 wenye uzito wa mwili wa kupindukia duniani ,hili kikiwa ni ongezeko la watoto milioni 10 wenye tatizo hilo tangu mwaka 2000.

    Japo idadi ya watoto idadi ya watoto walio chini ya umri wa miaka 5 waliodumaa, imepungua kwa ujumla duniani, bado watoto milioni 149 au asilimia 21.9 ya watoto walio chini ya umri wa miaka 5 wamedumaa. Hata hivyo Afrika bado ina kiwango cha juu kuliko mabara mengine cha watoto waliodumaa katika ukuaji.

    Mnamo mwaka 2018, mabara ya Africa na Asia ayalikuwa na kiwango cha tisa kwa kumi cha watoto wote waliodumaa duniani (sawa na asilimia 54.9 kwa Afrika na asilimia 39.5 kwa Asia).

    Kiwango hicho kinafanya idadi ya waathiriwa wa ukosefu wa usalama wa chakula kufikia zaidi ya watu bilioni mbili.

    Tathmini ya kipekee kuhusu kuongezeka kwa uzito wa mwili inaonyesha kwamba kuna ongezeko la haraka la uzito wa mwili miongoni mwa watoto wa shule na watu wazima katika maeneo yote ya Afrika.

    Kulingana na Umoja wa Mataifa watoto wa shule hawali matunda na mboga za kutosha, mara kwa mara hula vyakula vyenye kutia nguvu na joto mwilini , na mara nyingi hula vyakula vinavyotengenezwa haraka kama vile vibanzi na vinywaji vya sukari nyingi kama vile soda, na hawafanyi mazoezi ya mwili.

    Mazowea haya mabaya , yanaweza kuwa yanachangia kwa sehemu fulani, kuongezeka kwa uzito wa mwili miongoni mwa watoto wa shule, inasema ripoti.

    Tatizo hilo linachangiwa, kwa sehemu moja na kuongezeka kwa masoko ya vyakula vilivyopitia mchakato wa viwandani na upatikanaji wake, pamoja na viwango vya chini vya mazoezi ya mwili.

    Kudorola wa chumi za dunia pamoja na kufungwa kwa biashara kuu za dunia kumeelezewa kuchangia kwa ukosefu wa hivi karibuni wa usalama wa chakula pamoja na ukosefu wa virutubisho vya mwili unaoendelea, pamoja na na ukosefu wa sera za muda mfupi na mrefu ambazo ni muhimu katika kulinda usalama wa chakula, iwe nyakati za matatizo ya kiuchumi au katika kuandaa sera hizo.

    Mabadiliko ya hali ya hewa pia yamechangia kuathiri kilimo na kusababisha kupungua kwa idadi ya wakulimana shughuli za kilimo . “haya yote yamesababisha mabadiliko ya namna chakula kinavyozalishwa, kugawanywa na kuliwa kote duniani – na kujitokeza kwa changamoto mpya za usalama wa chakula na afya .” wanasema wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa.

    Wakizungumza kuhusiana na baa la njaa, wakuu hao wa mashirika ya Umoja wa Mataifa wameapa kuandaa mikakati ya kukabiliana na baa la njaa duniani.

    ” Matendo yetu ya kukabilana na hali ya njaa inayotatiza dunia yatakuwa thabiti,” Walisema viongozi hao wa Umoja wa Maraifa. na kuongeza kuwa: “Lazima tukabiliane na umaskini na kuandaa muundo wa mikakati ya mabadiliko inayoshirikisha ikiwalenga watu na kushirikisha jamii zilizozo katika hatari ya kuathirika kiuchumi na kujipanga wenyewe ili kumaliza njaa, kuweka usalama wa chakula na kukabiliana na aina zote za utapiamlo.” Wanasema maafisa wa Umoja wa mataifa.

    Umoja wa mataifa unasema kuwa kasi ya mafanikio katika kukabiliana na kudumaa kwa mtoto na kupungua kwa idadi ya watoto wachanga wanaozaliwa na uzito wa chini wa mwili ni ya kiwango cha chini sana, na hivyo kupunguza fursa za kufikia mafanikio malengo mengine ya kudumu.

    Umoja wa Mataifa unasema kuwa licha ya kwamba kiwango cha kudumaa kwa watoto kimepungua duniani kwa asilimia 10 katika kipindi cha miaka sita, bado mafanikio ni ya taratibu sana kulingana na malengo ya 2030 ambapo kiwango cha watoto wanaodumaa katika ukuaji kinatarajiwa kupunguzwa kwa asilimia 50.

     

  • Iran imefanya kosa  kubwa sana

    Iran imefanya kosa kubwa sana

    Rais wa Marekani aliidhinisha majeshi ya Marekani kuishambulia siku ya Alhamisi na kisha kubadili msimamo, vyombo vya habari vya nchi hiyo viaripoti.

    Mashambulizi hayo ilikuwa yawe ya kulipiza kisasi baada ya Iran kuitungua ndege isiy na rubani ya Marekani.

    Kwa mujibu wa gazeti mashuhuri la The New York Times, tayari matayarisho ya awali ya mashambulizi hayo yalikuwa yakiendelea wakati Trump alipobadili mawazo na kuamuru yasitishwe.

    Gazeti hilo linamnukuu afisa mmoja mwanandamizi wa Ikulu ya White House.

    Hata hivyo bado hakuna taarifa rasmi kutoka Ikulu hiyo juu mipango hiyo ya mashambulizi.

    Iran inasema ndege hiyo ya kijasusui ilikuwa ndani ya anga lake wakati wakiitungua, lakini jeshi la Marekani limekanusha na kusema ilikuwa ikipaa katika anga la kimataifa.

    Tukio hilo linaendeleza suitafahamu baina ya mataifa hayo mawili hususani katika eneo la mpaka baina ya Ghuba ya Omani na Ghuba ya Uajemi.

    Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran Javad Zarif amesema nchi yake itapeleka malalamiko Umoja wa Mataifa (UN) kuwa Marekani inavamia eneo lake.

    Balozi wa Iran wa UN Majid Takht Ravanchi amesema ni dhahiri kuwa ndege hiyo ilikuwa inafanya operesheni ya kijasusi wakati ikitunguliwa, kitu ambacho amesema ni uvunjifu wa wazi wa sheria za kimataifa.

    Katika barua aliyomuandikia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Baraza la Usalama, Bw Ravanchi amesema, Japo Iran haitaki kuingia vitani, lakini ina haki ya kujilinda dhidi ya vitisho vya maadui.

    Trump amesema nini?

    Rais Trump mpaka sasa hajazungumza chochote kuhusu mipango ya mashambulizi ya kulipa kisasi.

    Akizungumza awali kutokea Ikulu ya White House, amesema Iran imefanya makosa makubwa kwa kuitungua ndege hiyo na kuwa kuna ushahidi kuwa ilikuwa katika anga la kimataifa na si eneo la Iran.

    Hata hivyo Trump amewaeleza waandishi wa habari kuwa tukio hilo yawezekana lilisababishwa na makosa ya kibinaadamu.

    “Ni vigumu sana kwangu kuamini kwamba tukio hilo lilikuwa la makusudi,” amesema Trump.

    “Nafikiri, huenda Iran ilifanya kosa – Yawezekana kuna jenerali ama mtu mwengine ambaye alifanya kosa hilo la kutungua ndege ile,” amesema.

    “Yawezekana alikuwa ni mtu mmoja mpuuzi (ndio alitoa amri ya kutungua).”

    Viongozi wengine wamesema nini?

    Rais wa Urusi Vladimir Putin ameonya kuwa vita baina ya mataifa hayo mawili italeta janga ambalo madhara yake hayayumkiniki.

    Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres amezitaka pande zinazokinzana kujizuia.

    Nchini Marekani, Spika wa Bunge la Wawakilishi kutoka chama cha upinzania cha Democrats Nancy Pelosi amesema Marekani haina hamu ya vita dhidi ya Iran.

    Aliyekuwa Makamu wa Rais wa taifa hilo, na kinara wa kutaka tiketi ya urais kupitia Democrats, Joe Biden, amemkosoa Trump kwa kusema sera zake dhidi ya Iran ni “janga la kujitakia”.

    Kiongozi wa wawakilishi wa chama tawala cha Republicans bungeni, Kevin McCarthy, ametaka kuchukuliwe hatua za kipimo baada ya kufuatia tukio hilo.

    Viongozi wengine wamesema nini?

    Rais wa Urusi Vladimir Putin ameonya kuwa vita baina ya mataifa hayo mawili italeta janga ambalo madhara yake hayayumkiniki.

    Katibu Mkuu wa UN Antonio Guterres amezitaka pande zinazokinzana kujizuia.

    Nchini Marekani, Spika wa Bunge la Wawakilishi kutoka chama cha upinzania cha Democrats Nancy Pelosi amesema Marekani haina hamu ya vita dhidi ya Iran.

    Aliyekuwa Makamu wa Rais wa taifa hilo, na kinara wa kutaka tiketi ya urais kupitia Democrats, Joe Biden, amemkosoa Trump kwa kusema sera zake dhidi ya Iran ni “janga la kujitakia”.

    Kiongozi wa wawakilishi wa chama tawala cha Republicans bungeni, Kevin McCarthy, ametaka kuchukuliwe hatua za kipimo baada ya kufuatia tukio hilo.

    cc;BBCswahili

  • Morsi Azikwa saa chache baada ya kifo

    Morsi Azikwa saa chache baada ya kifo

    Rais wa zamani wa Misri, Mohamed Morsi amezikwa saa chache baada ya kufariki dunia akiwa mahakamani siku ya Jumatatu.

    Wakili wake ameliambia shirika la habari la Ufaransa, AFP kiongozi huyo wa zamani alizikwa Mashariki mwa jiji la Cairo asubuhi ya Jumanne familia yake ikiwepo

    Morsi,aliyekuwa na miaka 67, alikuwa kizuizini tangu alipoondolewa madarakani mwaka 2013.

    Makundi ya watetezi wa haki za binaadamu , ambayo yalikosoa mazingira ambayo Morsi aliwekwa,wametoa wito wa kufanyika uchunguzi kuhusu kifo chake.

    Familia yake na wanaharakati wamezungumzia kufo chake na muda ambao aliwekwa katika seli ya peke yake, akizuiwa kutembelewa na wanasheria na familia yake.

    Mtoto wake, Abdullah Mohamed Morsi, ameliambia shirika la habari la Uingereza, Reuters siku ya Jumatatu kuwa mamlaka za Misri ziliikatalia familia yake kufanya maziko katika mji yalipo makazi yake.

    Kiongozi wa juu wa zamani wa kundi lililopigwa marufuku nchini humo, Muslim Brotherhood, Morsi alikua kiongozi wa kwanza kuchaguliwa kidemokrasia mwaka 2012.

    Aliondolewa na kushikiliwa baada ya mapinduzi ya kijeshi mwaka mmoja baadae baada ya kufanyika maandamano makubwa kupinga utawala wake.

    Abdul Fattah al-Sisi, Kiongozi wa zamani wa kijeshi, amekuwa madarakani tangu mwaka 2014.

    Baada ya kuondolewa madarakani, mamlaka zilipambana na wafuasi wake na wapinzani wengine, na kukamata maelfu ya watu.

    Muslima Brotherhood na Rais wa Uturuki, Recep Tayyip Erdogan, mshirika wa karibu wa Morsi ni miongoni mwa walioshutumu utawala wa Misri kuhusu kifo cha Morsi.

    Kulitokea nini Mahakamani ?

    Morsi alikua mjini Cairo siku ya Jumatatu kwa shutuma za kufanya vitendo vya kijasusi ikihusisha kuwa na mawasiliano na kundi la wanamgambo wa kiislamu la kipalestina, Hamas.

    Maafisa wanasema aliomba kuzungumza mahakamanu na kuongea kwa dakika tano kutoka kwenye kizimba kilichokua na kioo ambacho alikuwamo ndani yake na washtakiwa wengine.

    Dakika chache baadae alizimia wakati wa mapumziko mahakamani hapo.

    ”Alipelekwa hospitali ambapo alithibitishwa kupoteza maisha,”taarifa ya mwendesha mashtaka ilieleza.

    Maafisa wamesema katika ripoti yao kuwa , hakuna majeraha yeyote ambayo yalionekana kwenye mwili wake.

    Televisheni ya taifa ilieleza awali kuwa chanzo cha kifo chake ni mshtuko wa moyo.

    Mosri tayari alikuwa anatumikia kifungo kutokana na mashtaka matatu yaliyokuwa yakimkabili.Awali alihukumiwa adhabu ya kifo,ambayo baadae ilitenguliwa.

    Watu wanazungumza nini baada ya kifo chake ?

    ”Kifo cha Rais wa zamani, Morsi kimetokea kutokana na kutendewa isivyo haki na serikali, kuwekwa katika gereza la peke yake, alipatiwa huduma mbovu za matibabu, kumzuia kuonana na familia yake na mawakili wake.Alieleza Bi Whitson kwenye taarifa yake.

    Shirika la Amnesty International pia limetaka uchunguzi ufanyike kuhusu kifo chake.

    Shirika limesema Morsi alikua akiruhusiwa kutembelewa mara tatu tu kwa kipindi cha takribani miaka sita na hakuruhusiwa kuonana na mawakili wake wala daktari.

    Mfalme wa Qatar,Sheikh Tamim bin Hamad Al Thani, mshirika mwingine wa Morsi ameeleza masikitiko yake kutokana na kifo chake.

    Mbunge wa nchini Uingereza, Crispin Blunt, aliyeongoza jopo la wanasiasa na kutoa tahadhari kuhusu kutendewa kwa Morsi mwaka 2018, ametaka ufanyike ”uchunguzi huru kimataifa”

    Tawi la kisiasa la kundi la Muslim Brotherhood, chama cha Freedom and Justice, kimesema kuwa kifo cha Morsi ni ”mauaji”.

    Rais wa Uturuki ameshutumu ”wakandamizaji” wa Misri kwa kifo chake na kumuelezea Morsi kuwa shahidi.

    Morsi ni nani?

    Mohammed Morsi alizaliwa katika kijiji cha El-Awwadh katika jimbo lililopo kwenye delta za mto Nile la Sharqiya mwaka 1951.

    Alisomea Uhandisi katika chuo Kikuu cha Cairo katika miaka ya 70 kabla ya kuhamia nchini Marekani ambapo alitunukiwa Shahada ya Uzamivu (PhD) katika Uhandisi.

    Morsi aliweka rekodi ya kuwa kiongozi wa kwanza kuchaguliwa katika uchaguzi wa haki na huru mwaka 2012, akiwa kiongozi mwandamizi wa kundi la kiislamu la Muslim Brotherhood ambalo limepigwa marufuku kwa sasa nchini humo.

    Hata hivyo utawala wake ulikumbwa na wimbi la maandamano ya wanaharakati ambao walimshutumu yeye na kundi la Muslim Brotherhood kujilimbikizia madaraka.

    Baada ya maandamano kuwa makubwa, na wafuasi wa Morsi kushambulia wapinzani wake, jeshi likiwa chini ya rais wa sasa Abdel Fattah el-Sisi liliendesha mapinduzi na kumng’oa Morsi madarakani, Juni 2013.

    Jeshi liliendelea kupambana na wafuasi wa Morsi baada ya mapinduzi, na zaidi ya wafuasi wake 1,000 waliuawa Agosti 2013.

  • Omar All bashir ashtakiwa kwa Ufisadi

    Omar All bashir ashtakiwa kwa Ufisadi

    Rais aliyeng’olewa madarakani nchini Sudan Omar al-Bashir ameshtakiwa kwa kosa la ufisadi.

    Mashtaka yanahusiana na sheria zinazohusu “utajiri haramu na maagizo ya dharura “,imesema ofisi ya mwendesha mashtaka, ambayo haikutoa taarifa zaidi.

    Jeshi lilimuondoa madarakani rais huyo wa muda mrefu mwezi April kufuatia miezi ya maandamano dhidi yake.

    Msemaji wa jeshi aliesma Alhamisi kuwa makosa yalifanyika wakati majeneraliwalipoamrisha kumalizika kwa mhgomo wa kukaa mbele ya makao makuu ya jeshi ambapo waandamanaji wanadai kurejeshwa kwa utawala wa kiraia nchini humo.

    Ghasia za mwezi Juni zilisababisha vifo vya watu 61, kwa mujibu wa maafisa, au 118,kwa mujibu wa madaktari wanaounga mkono waandamanaji wanaodai demokrasia.

    Mazungumzo baina ya waandamanaji na baraza la kijeshi la mpito yalivunjika baada ya ghasia.

    Viongozi wa maandamano baadae waliyaita maandamano kuwa ni ukaidi wa raia , ambayo walisema hayana budi kukoma ili kufufuliwa kwa mazungumzo ya amani.

    Baada ya mkutano baina ya Tibor Nagy, naibu waziri wa mambo ya nje wa Marekani anayehusika na masuala ya Afrika ,na Luteni Jenerali Abdel Fattah al-Burhan,jeshi lilisema kuwa lina matumaini Marekani inaweza “kuwa na mchango mzuri”.

     

    Bwana Bashir alipinduliwa na kukamatwa tarehe 11 Aprili baada ya miongo mitatuya utawala wa kiimla nchini Sudan. Hajawahi kuonekana kwa umma tangu alipokamatwa.

    Mwezi May alishtakiwa kwa makosa ya kuchochea nana kuhusika na mauaji ya waandamanaji.

    Mashtaka hayo yametokana na uchunguzi uliofanywa kuhusu kifo cha ddaktari aliyeuawa wakati wa maandamano yaliyosababisha kumalizika kwa utawala wake mwezi uliopita.

    Hatma ya Bwana Bashir haijawa wazi. Aliripotiwa kutiwa nguvuni mara baada ya kupinduliwa.

    Mnamo mwezi Disemba, waandamanaji walianza maandamanano dhidi ya uamuzi wa serikali wa kupandisha mara tatu kwa bei ya mkate.

    Maandamano hayo ghafla yalibadilika kuwa hasira iliyosambaa kote nchini dhidi ya kiongozi huyo ambaye alikuwa mamlakani kwa miaka 30, yakiongozwa na madaktari.

    Maandamano yalifanyika kwa wiki tano na shahidi mmoja anasema tarehe 17 Januari, vikosi vya usalama viliwafyatulia risasi waandamanaji na kumuua daktari.

    Utawala wa rais wa Sudan Omar al-Bashir uligubikwa na mapigano.

    Aliingia madarakani kupitia mapinduzi ya kijeshi mwaka 1989 na ameiongoza taifa hilo lililokuwa kubwa zaidi barani Afrika zama hizo hadi mwaka 2011 alipochaguliwa kwa njia ya kidemokrasia.

    Alipochukua madaraka, Sudan ilikuwa katika mwaka wa 21 wa mapigano makali ya wenyewe kwa wenyewe kati ya Kaskazini na Kusini.

    Japo serikali yake ilitia saini makubaliano ya kumaliza vita mwaka 2005, vita vingine vilizuka tena – katika eneo la magharibi mwa Darfur.

    Bw. Bashir alituhumiwa na mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa jinai ICC kwa kupanga uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binadamu katika eneo hilo.

    Licha ya ICC kutoa waranti ya kimataifa ya kukamatwa kwake, ameshinda uchaguzi mara mbili mwaka 2010 na 2015, japo vyama vya upinzani vilisusia uchaguzi uliyopelekea ushindi wake.

     

  • wanne waripotiwa kuuawa nchini Sudan

    wanne waripotiwa kuuawa nchini Sudan

    Watu wanne wameripotiwa kuuawa nchini Sudan katika siku ya kwanza ya maandamano ya kitaifa ya kupinga utawala wa Kijeshi nchini humo.

    Vikosi vya Usalama nchini Sudan viliwarushia mabomu ya machozi baridi na kutumia risasi halisi kuwatawanya waandamanaji hao katika mkuu wa nchi hiyo Khartoum.

    Wanaharakati wameitisha maandamano ya kupinga utawala huo kuanzia Jumapili, siku kadhaa baada ya msako wa kijeshi uliosababisha vifo vya mamia ya watu katika mji mkuu wa Khartoum.

    Aidha, Wafanyikazi kadhaa wa benki, Viwanja wa Ndege pamoja na wa shirika la umeme nchini humo walikamatwa kabla ya mgomo wa kitaifa wa kupinga utawala wa kijeshi, limedai kundi kuu la waandamanaji

    Wanaharakati wa kupigania demokrasia nchini humo wanasema kuwa baraza la jeshi haliwezi kuaminiwa baada kuzuka kwa ghasia ambapo wafuasi wengi wa Upinzani waliuawa jijini Khartoum na wamekataa kufanya mazungumzo ya amani na viongozi wa baraza hilo.

    Jeshi lilichukua uongozi baada ya kumng’oa madarakani kiongozi wa muda mrefu wa nchi hiyo, Omar al-Bashir mwezi Aprili mwaka huu na kuahidi kurejesha utawala wa kiraia baada ya kipindi cha mpito.

    Hata hivyo, mpaka sasa baraza la Kijeshi linalotawala nchi hiyo (TMC) halijatoa tamko lolote kuhusiana na madai hayo.

     

  • Kiboko cha mbu wa malaria chapatikana

    Kiboko cha mbu wa malaria chapatikana

    Ukungu (fangasi) – ambao umeboreshwa kisayansi kutoa sumu ya buibui – unaweza kuua idadi kubwa ya mbu wanaoambukiza malaraia, utafiti mpya wa kisayansi umebaini.

    Majaribio ya ukungu huo, ambayo yamefanyika nchini Burkina Faso, Afrika Magharibi yameonesha kuwa idadi ya mbu iliteketezwa kwa 99% ndani ya siku 45.

    Watafiti wanasema si lengo lao kutokomeza mbu hao bali kusaidia kuzuia maambukizi ya malaria.

    Ugonjwa wa malaria, unaoambukizwa na mbu jike aina ya Anopheles wanyonyao damu huua zaidi ya watu 400,000 kwa mwaka.

    Duniani kote, wagonjwa milioni 219 wa malaria kila mwaka huripotiwa.

    Utafiti huo umefanywa na wataalamu kutoka Chuo Kikuu cha Maryland cha Marekani – na kituo cha utafiti cha IRSS cha Burkina Faso.

    Wataalamu hao kwanza walianza kwa kutambua kuvu ama ukungu aina ya Metarhizium pingshaense ambao kiasili kudhuru mbu waambukizao malaria.

    Hatua iliyofuatia ilikuwa ni kuuongezea nguvu ukungu huo.

    “Kuvu hiyo ni rahisi kuiongezea kitu kisayansi, hivyo ni rahisi kuifanyia uhandisi jeni,” amesema Profesa Raymond St Leger, kutoka Chuo Kikuu cha Maryland.

    Wanasayansi hao wakageukia sumu itokanayo na aina ya buibui wa funnel kutoka Australia.

    Vipimo vya maambara vikathibitisha ufanisi wa kiwango cha juu cha sumu hiyo katika kuteketeza mbu.

    Baada ya maabara, wataalamu hao wakatengeneza kijiji maalum kwa ajili ya utafiti nchini Burkina Faso.

    Kijiji hicho kilizungushiwa neti ili kuzuia ukungu ama mbu kutoka kwenye eneo la utafiti.

    Ukungu huo kisha ukachanganywa na mafuta ya ufuta na kumwagiwa kwenye mashuka meusi ya pamba.

    Mbu hao walidhurika punde tu walipotuwa kwenye mashuka hayo.

    Watafiti walianza kazi hiyo na mbu 1,500.

    Matokeo ya utafiti huo, yaliyochapishwa kwenye jarida la kisayansi yalionesha kuwa idadi ya mbu inaongezeka kama wakiachwa bila ya ukungu.

    Ila, baada ya ukungu wenye sumu kuingizwa kwenye kijiji hicho, walisalia mbu 13 tu baada ya siku 45.

    Aina mpya za kupambana na malaria zinahitajika kwa haraka duniani, kutokana na mbu hao kutengeneza usugu wa dawa.

    Shirika la Afya Duniani (WHO) tayari limeshaonya kuwa idadi ya wagonjwa itaendelea kuongezeka kwenye nchi 10 ambazi zimeathirika zaid na malaria barani Afrika.

     

    cc;BBCswahili

  • Njiwa amuepusha dereva  na faini

    Njiwa amuepusha dereva na faini

    Dereva aliyekua akiendesha Gari kwa kasi nchini Ujerumani alinusurika kulipa faini ya pauni 93 baada ya njiwa mweupe kumuepusha kutambulika sura yake.

    Dereva alinaswa kwenye kamera za mwendo kasi lakini sura yake ilifichwa na mabawa ya ndege huyo alipokua akiruka mbele ya kioo cha gari.

    Taarifa ya polisi inasema pengine ”Roho mtakatifu” aliingilia kati- ishara ya njiwa mweupe kama alama ya uwepo wa Mungu katika imani ya dini ya kikristo.

    ”Tumeelewa ishara hiyo na kumuacha dereva kwa amani wakati huu.”

    Lakini maafisa katika mji wa Viersen, karibu na mpaka wa Ujerumani waliongeza: ”Tuna matumaini kuwa dereva huyo aliyesaidiwa anaelewa ‘onyo hili kutoka juu’ na kuwa ataendesha vizuri siku za usoni.”

    Dereva alikua akisafiri kwa kasi ya kilometa 54 kwa saa katika barabara ambayo alipaswa asafiri kwa kilomita 30 kwa saa, polisi wameeleza

    Kutokana na gari pekee kubainika na si dereva, alinusurika kulipa faini hiyo ”ashukuriwe malaika yule mwenye mabawa ambaye mbawa zake zilizuia sura ya dereza”.

    Polisi wa mji wa Viersen amesema kuwa Njiwa huyo naye angetozwa faini kwa kupita kwa kasi kwenye eneo asilopaswa kupita.

     

  • Afa kwenye Ndege kwa kumeza dawa za kulevya

    Afa kwenye Ndege kwa kumeza dawa za kulevya

    Mwanaume mmoja raia wa Japan, amepoteza maisha ndani ya Ndege akitokea Mexico City baada ya kumeza kete 246 za Cocaine.

    Ndege hiyo, iliyokuwa ikielekea katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Narita nchini Japan ililazimika kutua kwa dharura katika jimbo la Sonora nchini Mexico mwanaume huyo alipoanza kupoteza fahamu.

    Mamlaka zimesema mtu huyo aliyejulikana kwa jini la Udo N, alipoteza maisha baada ya ubongo wake kujaa maji kutokana na matumizi ya madawa kupita kiasi.

    Kwa mujibu wa taarifa ya mwanasheria mkuu wa jimbo la Sonora, Kete zilizokua na urefu wa sentimita 2.5 na upana wa sentimita 1 zilikutwa tumboni na kwenye utumbo wakati wa uchunguzi.

    Abiria wengine 198 waliobaki waliendelea na safari baada ya kutua kwa dharura katika mji wa Hermosillo.

    Mamlaka za Mexico zimesema zitaendelea na uchunguzi.

     

  • Brexit ilivyomuondoa madarakani Theresa May

    Brexit ilivyomuondoa madarakani Theresa May

    Waziri mkuu wa pili mwanamke Uingereza, kama ilivyo kwa wa kwanza, mwishowe ameondolewa madarakani kutokana na mvutano wa ndani ya chama cha Conservative kuhusu Ulaya.

     

    Lakini huenda Theresa May asiwe kama Margaret Thatcher katika orodha ya viongozi walioacha alama ya kudumu katika nchi yao.

    Angalau sio kwa namna ambavyo angetamani wakati alipoingia Downing Street mnamo Julai 2016.

    Maazimio aliyokuwa nayo – kufikia maenoe yaliosahauliwa katika taifa hilo, au kusahihisha masuala nyeti ya dhulma katika jamii ya Uingereza – yaligubikwa kwa neno moja: Brexit.

    Takriban muda wa miaka mitatu aliyohudumu yote yalifafanuliwa kwa uamuzi wa kujiondoa katika Umoja wa Ulaya na jitihada zake kupata ufumbuzi wa matokeo ya kura ya maoni iliyoitishwa na mtangulizi wake David Cameron.

    Hata wakosoaji wake wakali walishangazwaa kwa uwezo wake wa kuhimili adhabu na aibu iliyofuata wimbi baada ya wimbi kutoka Brussels na Westminster.

    Mpambano wa kuwasilisha Brexit

    Kujiuzulu kwa mawaziri na wabunge wa upinzani ambayo yote yangebaini mwisho wa uhusiano wa kawaida kwa waziri mkuu yalioonekana kutomtetelesha.

    Aliendelea ni kana kwamba hata hatambui kizaa zaa kinachomzungka na kuwamabia wabunge “hakuna kilichobadilika” na kuahidi kutekeleza “wanachotaka” raia wa Uingereza, hata wakati nguvu zake bungeni na udhibiti wa chama chake kilichoshuka umaarufu ukiendelea kupungua.

    Huenda taswira ingekuwa tofuati iwapo angeshinda katika uchaguzi mkuu aliouitisha mnamo 2017.

    Lakini badala ya kurudi Downing Street na jukumu kubwa mikononi, kama alivyotarajia, alipoteza uwingi katika bunge la wawakilishi na imbidi ategemee uungwaji mkono wa kutoka chama cha Ireland kaskazini Democratic Unionist Party.

    Hakupoa kidonda hichi, na kumekuwana hisia kwamba wabunge wake wengi walikuwa wamemaucha aendele kuhdumu mpaka pale atakapofanikiwa kuwasilisha mpango wa Uingereza kujitoa katika Umoja wa Ulaya kabla ya kumtema baada ya kupata mpango mbadala unaovutia.

    Kwa wakati mmoja, ilibidi aahidi atajiuzulu kabla ya uchaguzi ujao wa 2022 wakati akijizatiit kuponea kura ya kutokuwana imani naye iliyooidhinishwa na wabunge wake mwenyewe.

    Na baada ya kutengwa na wabunge wengi kwa kuwalauamu kwa mkwamo wa Brexit, alilazimika hatimaye kukubali kwamba chama chake, cha Conservative hakikumtaka aendelee kuhudumu tena.

    Ajitolea mara ya mwisho

    Amejitolea kuondoka kama hatua ya mwisho kwa wakosoaji wakena kuwamabi kwamba atajiuzulu iwapo wtaapiga kura kukubali mpango wa kujitoa katika Umoja wa Ulaya aliyoupigia upatu huko Brussels.

    Januari 2019, bunge lilipinga mpango huo kwa uwingi mkubwa kuwahi kufanyika dhiid ya serikali Uingereza katika historia.

    May amejaribu tena mara mbili kupata ridhaa ya bunge, kwa kukarabati mpango huo na alishindwa tena mara zote.

     

    Watu wanaounga mkono kusalia walidhani kwamba makubaliano hayo ni makali mno, huku wa Conservative wakisema haujatimiza Uingereza kujitoa kikamilifu kutoka Umoja wa Ulaya.

    Katika jitiahada ya kujadiliana makubaliano ya Brexit ambayo yanaweza kupita katika bunge la wawakilishi alishauriana na kiongozi wa chama cha Leba Jeremy Corbyn.

    Lakini mazungumzo ya wiki sita pasi kufikiwa makubaliano , matokeo ambayo wabunge wengi wa Conservative wanasema yalitabirika na ni ya kuvunja moyo.

    Izara nyingine ilifuata wakati alilazimika kukubali Uingereza kushiriki katika uchaguzi kwenye Umoja wa Ulaya – jambao ambalo hapo awali alisema halitokubalika.

    Kufikia hatua hii wabunge waliacha kumsikiliza, kwa kufikia uamuzi kwamba May ni kizuizi kwa Brexit wanayoitamani- au ya aina yoyote ile.

    Hatimaye May alilazimika kukubali kwamba hawezi kuendelea “katika kazi anayeoipenda” na muda wake huko Downing Street sasa umemalizika.

    Sauti yake ilitetereka na alikuwa mwingi wa hisia alipomaliza hotuba yake akisema: “Nitaondoka katika wadhifa huu hivi karibuni lakini imekuwa heshima kubwa maihsani mwangu kuhudumu.

    Atajiuzulu kama kiongozi wa chama hicho Juni 7 na uteuzi wa waziri mkuu mpya unatarajiwa kuanza wiki inayoafuata baada ya hatua hiyo.

     

    cc;BBCswahili