MKUU wa mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda amewataka wanawake wote waliotelekezwa na waume zao na hawapatiwi fedha za matunzo ya mtoto wafike ofisini Jumatatu ya Aprili 9 kwa lengo la kupatiwa msaada wa kisheria. Taarifa ya Makonda kwa vyombo vya habari aliyoitoa jana amesema jopo la wataalamu wa sheria, maofisa ustawi wa jamii na askari Polisi kutoka dawati la jinsia wamejipanga ipasavyo kuwahudumia na kuhakikisha mzazi mwenza anatoa fedha kwa ajili ya matunzo ya mtoto. “Huduma hii inatolewa...
Zuckerberg aomba radhi kwa sakata la Cambridge Analytica Mmiliki wa kampuni ya Facebook Mark Zuckerberg amevunja kimya cha siku tano tangu lilipofichuliwa sakata la kutumika data za watumiaji wa Facebook, kwa kusema kampuni yake ina wajibu wa kulinda data za watumiaji wake. Zuckerberg amesema kuwa Facebook, ambao ni mtandao wa kijamii unaoongoza kwa kuwa na watumiaji wengi duniani, umechukua hatua kadhaa kuzilinda data hizo huku akikiri kuwa walifanya makosa na wanahitaji kuchukua hatua madhubuti kurekebisha makosa hayo. Kauli yake inakuja...
Mahakama Kuu nchini Kenya imeamuru mwanamke aliyeteswa na kudhalilishwa wakati wa kujifungua hospitalini alipwe fidia ya jumla ya dola 25,000 za Marekani. Mwanamke huyo alidhalilishwa miaka mitano iliyopita katika kisa ambacho kilizua lalama kutoka kwa raia na watetezi wa haki za kibinadamu baada ya kuangaziwa kwenye vyombo vya habari na mtandaoni. Jaji wa mahakama kuu ya Bungoma, magharibi mwa Kenya, Abida Aroni alisema mamlka ya afya nchini Kenya ilikiuka haki za kimsingi za Josephine Majani alipotengwa na kukosa kuhudumiwa wakati...
Binti mmoja wa Kipalestina aliyekamatwa baada ya kumchapa kofi mwanajeshi, Msichana huyo Ahed Tamimi alikiri kuwa na hatia kwa makosa manne aliyokuwa akishtakiwa kati ya 12 yaliyokuwa yakimkabili, ikiwemo shambulio la mwili, wakili wake ameeleza. Kadhalika, atalipa faini ya shekeli 5,000 sawa na dola 1,440 . Binti huyo mwenye miaka 17 alikamatwa baada ya kunaswa kwenye picha ya video akiwakabili wanajeshi wawili nje ya nyumba yake mwezi Desemba. Uamuzi wa mahakama unamaanisha kuwa ataachiwa huru kipindi cha majira ya joto...
...
Baadhi ya mifugo wakiwa katika eneo la kunywa maji kablaya kuuzwa katika Soko la Kimkakati la Longido, Wilayani Longido ambalo limejengwa kwa ufadhili wa Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF). Serikali kupitia, Programu ya Miundo mbinu ya Masoko, Uongezaji wa Thamani na Huduma za Kifedha Vijijini (MIVARF), imetekeleza maombi 5 ambayo yanawasaidia wafugaji hao kuongeza thamani ya mifugo yao kupitia Soko la Kimkakati la mifugo Longido lililojengwa na Program hiyo....
Rais wa Peru Pedro Pablo Kuczynski amepata kuwasilisha barua yake ya kujihuzulu bungeni hapo jana. Hii ni kutokana na tuhuma za kununua kura zinazomkabili na serikali yake, Amefanya hivyo kutokana na mchakato uliopambana moto wa kutaka kumng’oa...
WAKATI TANZANIA LEO INAADHIMISHA SIKU YA MAJI DUNIANI, JIJI LA DSM LIMEKUWA LIKIPOTEZA MAJI ZAIDI YA LITA MILLION 57 AMBAZO ZIMEKUWA ZIKIPOTEA KUPITIA KWA WATU WACHACHE AMBAO WAMEKUWA WAKIHUJUMU NA KUSABABISHA WANANCHI WENGI KUKOSA MAJI. JOTO TUMEZUNGUMZA NA WAKAZI WA JIJINI DAR ES SALAAM AMBAO WANAELEZA KERO MBALIMBALI WANAZOKUMBANA NAZO JUU YA MAJI SAFI NA SALAMA. KATIKA KUIADHIMISHA SIKU YA KIMATAIFA YA MAJI DUNIANI KATIBU MKUU WA WIZARA YA MAJI NA UMWAGILIAJI PROFESA KITILA MKUMBO AMESHIRIKI MKUTANO WA DUNIA...
Marekani Jumatano imeweka vikwazo kwa watendaji 15 wa mafuta wa Sudan Kusini ambao imesema walikuwa vyanzo muhimu cha fedha kwa serikali, hatua ambayo inalenga kuongeza shinikizo kwa rais Salva Kiir kumaliza mgogoro na mzozo wa kibinadamu nchini kwake. Kwa mujibu wa shirika la habari la Reuters makampuni na taasisi za serikali huenda katika siku za mbeleni zikahitaji leseni maalum ya kufanya biashara nchini Marekani, wizara ya mambo ya nje ya Marekani imesema. Serikali ya Sudan Kusini na maafisa ambao ni...