RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Ali Mohamed Shein amewaeleza wananchi kisiwani Pemba kuwa Zanzibar hapatakuwa tena na uchaguzi hadi mwaka 2020 na kwamba kwa sasa yeye ndiye Rais aliyechaguliwa kihalali na wananchi. Dokta Shein ameyasema hayo huko Tibirinzi Chake Chake Pemba, alipokwenda kukagua Tawi la CCM lililochomwa moto katika ziara yake ya kukagua athari zilizofanywa dhidi ya Wana CCM kwa kuendelea kukiunga mkono chama hicho kiswani humo. Mbali na hayo amewataka wananchi kuyapuuza maneno ya utani na dhihaka...
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta ameingoza KRC Genk kufuzu kucheza Ligi ya Europa baada ya kuichapa Sporting Charleroi kwa mabao 5-1 na kushinda kwa jumla ya mabao 5-3. Kulingana na gazeti la Mwananchi, Samatta, ambaye katika mchezo wa kwanza walionyukwa 20 alianzia benchi, jana aliaminiwa kuanza mchezo huo na kocha wake Peter Maes, akicheza pamoja na Nikos Karelis katika safu ya bora ya ushambuliaji. Katika mchezo huo, Samatta alifunga bao moja na kutegeneza mengine mawili yaliyofungwa na Karelis...
Kesi ya mashtaka ya ukiukaji wa kibinaadamu dhidi Mke wa aliyekuwa rais wa Ivory Coast Simone Gbagbo,imeanza katika mahakama ya mji mkuu wa Abidjan. Simone, anayejulikana kwa jina maarufu kama ‘mwanamke mkakamavu’ amewahi kuhudumia miaka 20 jela kwa uvamizi wa mamlaka ya serikali dhidi ya jukumu lake katika ghasia za baada ya uchaguzi wa mwaka 2010 uliosababisha vifo vya watu elfu 3. Vita hivyo viliisha baada ya mumewe, Laurent Gbagbo kukamatwa na Umoja wa Mataifa na jeshi la ufaransa kumuunga...
ALIYEKUWA rais wa Chad Hissene Habre amehukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya kuhusika kwenye uhalifu dhidi ya ubinadamu , ubakaji na utumwa wa ngono. Habre alihusika moja kwa moja katika uhalifu huo ambao ulifanyika wakati akiwa rais wa Chad. Waathiriwa waliokuwa ndani ya mahakama wakati wa kusomwa kwa hukumu hiyo mji Dakar nchini Senegal, wameshangilia wakati jaji alipomaliza kusoma...
JESHI la polisi kanda maalumu ya Dar es salaamu limethibitisha kuundwa kwa timu maalumu kwa ajili ya kuchunguza na kupeleleza kifo cha dada wa bilionea Msuya ambapo tayari wanamhoji aliyekuwa mume wake . Kwa mujibu wa Kamanda wa polisi kanda hiyo, kamishina SIMON SIRRO, Jeshi hilo pia limefanikiwa kutoza faini a magari yanayo kiuka sheria za usalama barabarani ambapo kiasi cha shilingi milino 548 laki 1 na sitini zimeweza kukusanywa. Kamanda SIRRO amewaambia wandishi wa Habari leo kuwa...
RAIS wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli amemteua Jaji shabani Ally Lila, kuwa Jaji wa Mahakama ya Rufani ambaye kabla ya uteuzi huu alikuwa Jaji Kiongozi. Wakati huo huo rais Magufuli amemteua Mheshimiwa Anne Semamba Makinda kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya mfuko wa Bima ya Afya-NHIF. Uteuzi wa Mheshimiwa Makinda ambaye ni spika mstaafu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, umeanza Mei 25 mwaka huu. ...
Mahakama ya kijeshi kwenye mji mkuu wa Somalia Mogadishu, imewahukumu kifungo cha maisha wanaume wawili ambao walipatikana na hatia ya kupanga shambulizi dhidi ya ndege ya shirika la Daallo mwezi Februari. Bomu lililipuka ndani ya ndege hiyo muda mfupi baada ya kupaa kutoka uwanja wa ndege wa Mogadishu ikiwa safarini kwenda nchini Djibouti. Shimo lilitobolewa kando mwa ndege hiyo lakini hata hivyo ndege haikusambaratika. Abiria mmoja ambaye alitupwa nje ya ndege hiyo aliaga dunia na wengine wawili wakajeruhiwa. Washtakiwa wengine...
Mauaji ya Sokwe katika mbuga ya wanyama ya Cincinnati nchini Marekani yamezua utata katika mtandao wa Twitter. Sokwe huyo anadaiwa kumuangusha na kumvuruta kijana wa miaka minne. Sokwe huyo alipigwa risasi na kuuawa kufuatia kisa hicho cha kumvuruta mtoto. Watu katika mtandao wamesema sokwe huyo kwa jina Harambe hangestahili kuuawa kwani hakuwa na niya ya kumdhuru mtoto huyo. Wengi walitumia#hakikwaHarambe. Huku wengine wakisema wazazi wa kijana huyo ndio wa kulaumiwa kwa kukosa kumuangalia mwanawe. Maafisa wa shirika la wanyama pori...
Naibu kiongozi wa Chama cha kupambana na uhamiaji nchini Ujerumani amezungumza maneno ya kibaguzi dhidi ya mchezaji nyota wa Ujerumani Jerome Boateng ambaye baba yake ni raia kutoka Ghana. Alexander Gauland,aliliambia Gazeti la Ujerumani la (the Frankfurter Allgemeine) kuwa watu wanafikiri Boateng ni mchezaji mzuri lakini kamwe hatomuhitaji kama rafiki yake. Gauland alilaaniwa vikali na wachezaji mbalimbali,Waziri wa mambo ya ndani pamoja na Rais wa shirikisho la soka nchini Ujerumani ,Reinhard Grindel amesema maneno yake kuwa hayana maana....
Aliyekuwa mshambuliaji wa klabu ya PSG nchini Ufaransa Zlatan Ibrahimovic amesema kuwa alipokea ombi la kujiunga na kilabu moja ya ligi ya Uingereza lakini akakataa kuthibitisha iwapo klabu hiyo ni Manchester United au la. Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 yuko huru baada ya kuondoka PSG na amehusishwa na uhamisho wa United. Alipoulizwa iwapo ombi hilo linatoka Old Trafford ,alisema :Wacha tuone kitakachofanyika. Aliyekuwa kocha wa Chelsea Jose Mourinho anatarajiwa kutangazwa mkufunzi wa Manchester United na alifanya kazi na...
RAIS wa Zimbabwe Robert Mugabe amesema kuwa yeye sio Mmarekani wala Muingereza wakati akiwahutubia karibu watu elfu 50,000, wafuasi wake kwenye mkutano uliofanyika kwenye mji mkuu Harare kwa heshima yake. Mugabe mwenye umri wa miaka 92 amekana uwezekano wowote wa kuondoka madarakani na kuwashambulia viongozi hasimu ndani ya chama tawala cha ZANU-PAFU kwa kupanga kumrithi. Amesema kuwa yeye anawahudumia watu wa Zimbabwe na kuwa ataondoka tu ikiwa watu wangetaka afanye...