Makamu wa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan leo (Ijumaa) amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Bill & Melinda Gates Foundation, Rodger Voorhies. Mhe. Samia amekutana na Voorhies kwenye makazi ya Makamu wa Rais, Kilimani mjini...
Kikosi cha Usalama barabarani kikiongozwa na Kamanda J.T.Gwau kilifika ofisi za Efm redio Pamoja na tve kwa ajili ya kutoa elimu juu ya Usalama barabarani pamoja na Ukaguzi wa Magari ya Wafanyakazi wake. Ikiwa ni pamoja na Ubandikaji wa stika za siku ya Nenda kwa Usalama barabarani. Zoezi hilo lilikwenda vizuri bila matatatizo yoyote, wafanyakazi wa EFM Redio pamoja na TV E wamelishukuru Jeshi la Polisi kwa kuwapatia elimu hiyo, na kuhadi wataitumia vizuri pindi wawepo barabarni ili kupunguza...
Dereva wa kampuni ya Mercedes, Lewis Hamilton ameibuka kinara kwenye majaribio ya magari kabla ya kuanza kwa mashindano ya Australian GP yanayotarajiwa kuanza kutimua vumbi leo Machi 23 siku ya Ijumaa. Hamilton ameibuka kinara mara mbili kwenye mashindano hayo maarufu kwa jina la Formula One (F1) msimu huu wa mwaka 2018 na kuwazidi washindani wake wakubwa Ferrari na Red Bull. Licha ya kuongoza kwa magari hayo ya kampuni ya Mercedes yalipata ushindani mkubwa kwenye mbio hizo za majaribio kabla ya...
Kocha Mkuu wa klabu ya mashetani wekundu Manchester United, Jose Mourinho hapo jana amesema kuwa watu wenye akili na fikira za kuelewa na kuchambua mambo ya msingi wanatambua hali ya timu hiyo kwa sasa inavyopita kwenye kipindi cha mpito. Mourinho ambaye ni raia wa Ureno mara kadhaa amekuwa akishtumiwa na mashabiki kwa namna ya mfumo wake wa uchezaji ambao unadaiwa kutokuwa na ubunifu. Mashabiki wa United walizidisha shutuma zao zaidi mara baada ya klabu hiyo kutolewa kwenye mashindano ya klabu...
Mashindano makubwa ya mchezo wa tennis duniani maarufu kama French Open yametangazwa kuongezewa fedha kwa washindi watakao twaa tuzo katika kipindi cha majira ya Joto hadi kufikia pauni milioni 34. Washindi wa pili wa tuzo hizo kubwa za grand slam ambazo zinatarajiwa kuanza Mei 27, kila mmoja atajiondokea na euro milioni 2.2 ambayo ni sawa na pauni milioni 1.9 kwa makadirio wakati kwa mwaka jana kilikuwa ni kiasi cha pauni 100,000 ambacho kimetolewa. Kwenye ongezeko hilo kiasi kikubwa kimewekwa kwa...
Rais wa Marekani Donald Trump amemuomdoa Mshauri wake wa usalama wa taifa H.R McMaster na kumteua katika nafasi hiyo John Bolton mtu mwenye msimamo mkali na aliyewahi kuwa balozi wa Marekani katika Umoja wa Mataifa. Trump kama kawaida alitumia ukurasa wake wa Twitter kutoa tangazo hilo la karibuni la mabadiliko ya watumishi, hatua ya mbayo inauweka katika mashaka makubwa mustakabali wa makubaliano ya kihistoria kuhusu mpango wa nyukilia wa Iran.Hii ni mara ya tatu kwa Trump kubadilisha mshauri wake wa...
Mahakama ya Afrika na Haki za Binadamu (AfCHPR) inatoa hukumu katika kesi iliyowasilishwa na wanamuziki Nguza Viking maarufu Babu Seya na mwanaye, Johnson Nguza ‘Papii Kocha’ dhidi ya serikali ya Tanzania katika mahakama hiyo. Wawili hao waliwasilisha rufaa katika mahakama hiyo mwaka 2015 kupinga hukumu ya kifungo cha maisha iliyokuwa imetolewa dhidi yao. Walikuwa wanatumikia kifungo cha maisha jela kwa kuwabaka wasichana 10 wa shule waliokuwa na kati ya umri wa miaka 6 na 8 mwaka 2003. Walikuwa wametumikia...
Rais wa Marekani Donald Trump ameonyesha nia ya kutoa ushahidi mbele ya mwendesha mashitaka maalum anayechunguza uingiliaji kati wa Russia katika uchaguzi mkuu wa Marekani wa mwaka 2016 na mambo mengine. Ningependa Trump alijibu alipohojuiwa na waandishi wa habari kutaka kujua kama ana nia ya kuhojiwa na wachunguzi. Rais alitoa jibu hilo wakati akiondoka katika chumba cha kidiplomasia cha White house mara tu baada ya kusaini nyaraka ya kuelekeza utawala wake kuchukua hatua za kibiashara dhidi ya China. Majibu ya...
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Aliance News imesema kuwa kampuni ya De La Rue ilikuwa na mkataba na Uigereza wa miaka 10 lakini nchi hiyo imeamua kuvunja mkataba kati yake na kampuni hiyo. Imefahamika lengo la Serikali ya Uingereza kuvunja mkataba huo wa kutengenezwa hati za kusafiria ni kutokana na gharama kuwa kubwa za utengenezaji wa hati hizo na hivyo kuamua kuipa zabuni kampuni ya French firm Gemalto. “Hati mpya za kusafiria za Uingereza hazitatengenezwa tena na...
NDIMBO: Kwanza niseme watu wanashindwa kutofautisha kati ya kufungwa na timu kucheza vizuri NDIMBO: Ingawa timu imefungwa lakini timu ilicheza vizuri. SWALI KUTOKA KWA OSCA OSCA: KWA NINI MASHBIKI WAMEPUNGUA KWENDA KUANGALI MECHI UWANJANI??? NDIMBO: Jambo hili lina mitazamo mingi sana kitu kikubwa ni kuja na research na kupata jibu sahii kwa jambo hili NDIMBO: Kwa upande mwingine mashabiki wenyewe hawana uzalendo wa timu zao kwenda uwanjani OSCA OSCA: Tulikuwa tunalalamika kwamba tunapata mechi za kirafiki na nchi vibonde NDIMBO:...
HOSPITALI za Mkoa wa Dar es Salaam zimebainika zilikuwa na wagonjwa wengi ambao walikufa kutokana na malaria, Ukimwi , ajali, maambukizi ya bakteria kwenye damu, upungufu wa damu, saratani na kifua kikuu(TB) ukifuatiwa na mkoa wa Morogoro. Imefahamika malaria na upungufu wa damu ulichangia vifo vingi kwenye kundi la watoto chini ya miaka mitano na vifo kutokana na Ukimwi na Kifua Kikuu viliathiri zaidi kundi la watu wazima, vifo vinavyotokana na ajali viliathiri zaidi kundi kubwa la vijana wakati...