BOMU FEKI LAAHIRISHA MECHI YA MAN UNTD

BOMU FEKI LAAHIRISHA MECHI YA MAN UNTD

Like
193
0
Monday, 16 May 2016
Slider

Polisi nchini Uingereza imethibitisha kuwa kitu kilichokuwa kinadhaniwa kuwa ni bomu kilichoonekana kwenye uwanja wa timu ya Manchester United wa Old Trafford hakikuwa bomu kama ilivyodhaniwa bali kilikuwa ni kifaa cha wanausalama cha mazoezi kwa ajili milipuko.

Kifaa hicho kiliachwa na walinzi wa kampuni moja ya binafsi baada ya kufanya mazoezi yaliyowahusisha mbwa wenye kunusa vifaa na vitu vya kihalifu.

Kutokana na kuonekana kwa kifaa hicho mechi kati ya Manchester United na Bournemouth iliahirishwa.

Tayari kifaa hicho kimeshaharibiwa chini ya uangalizi mkali wa timu ya kuthibiti milipuko.

Tayari maafisa wa mji wametaka uchunguzi ufanyike na kuita kitendo hicho kuwa ni cha kizembe na cha kudhalilisha.

Maelfu ya mashabiki walioondolewa katika uwanja wa Old Trafford ambapo mechi baina ya wenyeji Machester United na Bournemouth iliahirishwa na itachezwa siku ya jumanne.

Comments are closed.