Local News

RAIS DK. MAGUFULI ATENGUA NA KUTEUA MKURUGENZI MKUU NSSF
Local News

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) Prof. Godius Kahyarara kuanzia leo 14 July 14, 2018. Prof. Kahyarara atapangiwa kazi nyingine. Kufuatia hatua hiyo, Rais Magufuli amemteua William Erio kuwa Mkurugenzi Mkuu wa NSSF. Kabla ya uteuzi huo Erio alikuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Pensheni wa PPF. Uteuzi wa Erio unaanza leo July 14,...

1
741
0
Saturday, 14 July 2018
HABARI PICHA: Mke wa Kibonde azikwa Makaburi ya Kinondoni Dar es Salaam
Local News

  Jana  July 13, 2018 Familia, ndugu, jamaa na marafiki wa karibu na mtangazaji Ephraim Kibonde wameuaga na kuuzika mwili wa marehemu Sara Kibonde ambaye ni mke wa mtangazaji Kibonde nyumbani kwake, Ubungo Kibangu na kisha baadae kuupumzisha mwili wake katika makaburi ya Kinondoni. E Digital imekuwekea  baadhi ya matukio kwa picha zilizo ripotiwa na Team yetu E Digital na kuziweka pia kwenye Ukurasa wetu wa Instagram  ...

Like
4897
0
Saturday, 14 July 2018
TAZAMA MATOKEO KIDATO CHA SITA 2018 HAPA
Local News

BARAZA la Mitihani la Taifa (Necta), limetangaza matokeo ya kidato cha sita leo Julai 13 na kuzitaja shule zilizoshika mkia kuwa ni pamoja na ya wasichana ya Jangwani, ya Jijini Dar es Salaam. Ubora wa ufaulu kwa watahiniwa wa shule unaonesha kuwa jumla ya watahiniwa 72,866 sawa na 95.52% wamefaulu katika daraja la kwanza hadi la tatu wakiwemo wasichana 30,619 sawa na 95.92% na wavulana 42,247 sawa na 95.23%. Waliopata daraja la kwanza ni 8,168.   MATOKEO YA ACSEE 2018...

Like
532
0
Friday, 13 July 2018
Rais Magufuli ateua Kamishna mpya wa Magereza
Local News

Taarifa kutoka Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais leo July 13, 2018, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Naibu Kamishna wa Magereza Phaustine Martin Kasike kuwa Kamishna Jenerali wa Magereza. Uteuzi huu umeanza leo July 13, 2018. Kabla ya uteuzi huu Kamishna Jenerali wa Magereza Kasike alikuwa Mkuu wa Chuo cha Taaluma ya Urekebishaji Tanzania (TCTA) Ukonga, DSM. Kamishna Jenerali wa Magereza Kasike anachukua nafasi ya Dkt. Juma Alli Malewa ambaye amestaafu....

Like
630
0
Friday, 13 July 2018
Ummy aagiza dereva gari la wagonjwa asimamishwe
Local News

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu ameagiza asimamishwe kazi, pamoja na maofisa waliokuwa wamepanda gari hilo Simiyu. Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amemuagiza Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Tarime, Elias Ntiruhungwa kumsimamisha kazi dereva wa gari la kubeba wagonjwa la halmashauri hiyo aliyekamatwa akiwa amepakia kilo 800 za mirungi. Kauli hiyo imetolewa leo Alhamisi Julai 12, 2018 katika uzinduzi wa mradi wa Tuwatumikie katika viwanja vya Halmashauri ya Wilaya ya Itilima mkoani Simiyu. Amesema mbali na dereva huyo, maofisa waliokuwa...

Like
370
0
Thursday, 12 July 2018
Waziri Mkuu azitaka taasisi za dini kuwekeza kwenye viwanda
Local News

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka viongozi wa dini wasibaki nyuma katika suala zima la kuwekeza kwenye viwanda ili waweze kuendana na azma ya Serikali ya kuifikisha Tanzania kwenye uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. “Serikali ya awamu ya tano imeazimia kukuza uchumi wa viwanda. Nawaomba msiwe nyuma katika suala hili, tumieni fursa ya ardhi tuliyonayo hasa katika ujenzi wa viwanda vya usindikaji ili kuongeza thamani ya mazao,” amesema. Waziri Mkuu ametoa rai hiyo leo Alhamisi, Julai 12, 2018 wakati akifungua...

Like
360
0
Thursday, 12 July 2018
Ndalichako aagiza Ofisa manunuzi wa Wizara kusimamishwa kazi
Local News

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Joyce Ndalichako, amemtaka katibu Mkuu wa wizara hiyo, Leonard Akwilapo kumsimamisha kazi Ofisa manunuzi wa wizara Audifasy Myonga kwa kufanya manunuzi ya vifaa vya maabara visivyo hitajika na kuvisambaza katika vyuo vya ualimu. Ndalichako ametoa maamuzi hayo leo Julai 12, alipotembelea chuo cha ualimu Kasulu, mkoani Kigoma na kufanya kikao na watumishi kwa lengo la kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili. Alisema chuo hicho kilipokea vifaa hivyo ambavyo viko chini ya kiwango huku...

Like
400
0
Thursday, 12 July 2018
RAIS MAGUFULI AKUTANA NA KUAGANA NA MABALOZI WATATU WALIOMALIZA MUDA WAO HAPA NCHINI
Local News

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Balozi wa Sweden hapa nchini anayemaliza muda wake Katarina Rangnitt mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.    Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwatambulisha Baadhi ya Viongozi (hawaonekani pichani ) kwa Balozi wa Sweden hapa nchini anayemaliza muda wake Katarina Rangnitt mara baada ya kuwasili Ikulu jijini Dar es Salaam.   Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John...

Like
633
0
Thursday, 12 July 2018
DAWASCO YATAKIWA KUWEKA MITA ZA KIELEKTRONIKI
Local News

Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa akizungumza na wafanyakazi na viongozi wa Shirika la Majisafi na Maji taka Dar es Salaam (DAWASCO) wakati wa ziara ya kujitambulisha mapema leo ofisi za DAWASCO. Picha zote na Cathbert Kajuna – Kajunason/MMG. Afisa Mtendaji Mkuu wa Shirika la Majisafi na Maji taka Dar es Salaam (DAWASCO), Mhandisi Cyprian Luhemeja alitoa maelekezo machache wakati wa ziara ya Waziri wa Maji na Umwagiliaji Prof. Makame Mbarawa ofisi za DAWASCO mapema leo alipofanya ziara...

1
610
0
Thursday, 05 July 2018
Tanzia: Mtoto wa Munalove amefariki dunia
Local News

Familia ya Efm redio pamoja na @tvetanzania Inatoa pole kwa familia ya Muna kwa kuondokewa na Mtoto wao Patric. Mungu awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu, Bwana ametoa na Bwana ametwaa Jina lake lihimidiwe #Amin...

Like
504
0
Wednesday, 04 July 2018
KAMANDA SIRO AFANYA MABADILIKO YA MA-RPC
Local News

Mkuu wa Jeshi la Polisi, Simon Siro amefanya mabadiliko ya Makamanda katika baadhi ya mikoa kama ifuatavyo. 1. SACP Deusdedit Nsimeki aliyekuwa Makao Makuu ya Upelelezi anakwenda kuwa RPC Simiyu. 2. SACP Ulrich Matei aliyekuwa RPC Morogoro, anakwenda kuwa RPC Mbeya. 3. Kaimu RPC Mkoa wa Mbeya, ACP Mussa Taibu amehamishiwa Makao Makuu ya Jeshi la Polisi 4. SACP Wilbroad Mutafungwa aliyekuwa RPC Tabora, anakwenda kuwa RPC mkoa wa Morogoro 5. ACP Emmanuel Nley toka Makao Makuu ya Jeshi la...

Like
1049
0
Tuesday, 03 July 2018