Local News

MADEREVA WA UDA WAWEKA MGOMO
Local News

Madereva wa UDA wamegoma kuingia barabarani kutokana na uongozi wa UDA kuweka kima cha juu cha kupeleka mapato kwa viongozi. Kampuni UDA wao wanaitaji laki 205000/= na madereva wao wanaitaji kupunguziwa walete sh 170000 kutokana na kuongezeka kwa magari ya UDA hivyo biashara imekuwa ngumu tofauti na awali. Uongozi wa uda ulituma meseji hii,m  kwa wafanyakazi wa uda wote.               Habari kwa madereva wote wa uda,kutokana na kikao cha uongozi wa UDA na uongozi wa madereva wa UDA,maamuzi yafuatayo yametolewa. Hesabu...

Like
376
0
Friday, 14 November 2014
UPINZANI KUTAMBULISHA USIMAMIZI WA KODI GES NA MAFUTA
Local News

KAMBI rasmi ya upinzani Bungeni imeitaka Serikali kuhakikisha kuwa inaandaa na kutambulisha Mfumo Rasmi na Imara wa Usimamizi wa Kodi katika sekta ya Gesi na Mafuta ili kuleta tija na maslahi kwa wananchi na Taifa kwa ujumla. Hayo yamesemwa leo Bungeni mjini Dodoma na Msemaji wa Kambi hiyo Mheshimiwa JAMES MBATIA wakati akitoa mapendekezo ya kambi hiyo mara baada ya Waziri wa Fedha Mheshimiwa SAADA MKUYA kusoma kwa mara ya pili Muswada wa Usimamizi wa Kodi wa mwaka 2014. Baadhi...

Like
208
0
Thursday, 13 November 2014
PAP HAINA UHUSIANO NA KIKWETE
Local News

IMEELEZWA kuwa Kampuni ya PanAfrica Power Resources -PAP haina Mahusiano ya Umiliki na Familia ya Rais JAKAYA KIKWETE kama ilivyoainishwa kwa kuweka katika mitandao mbalimbali ya Kijamii. Taarifa hiyo imetolewa na Katibu na Mshauri Mkuu wa Sheria wa Kampuni ya IPTL inayomilikiwa na PAP, JOSEPH MAKANDEGE alipozungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na tuhuma hizo. Hivi karibuni mtoto wa Rais JAKAYA KIKWETE, aitwaye MIRAJI KIKWETE alieleza kusikitishwa kwake na tuhuma hizo zinazotolewa dhidi yake kuhusishwa na umiliki wa kampuni ya...

Like
243
0
Thursday, 13 November 2014
GOOD NEWS FOR ALL MINISTRY KUMUOMBEA RAIS KIKWETE
Local News

HUDUMA ya Good News For all Ministry ya Jijini Dar es salaam imetoa wito kwa wananchi wote nchini kuhudhuria  maombezi ya kumuombea Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania JAKAYA MRISHO KIKWETE yatakayofanyika kesho ili afya yake iweze kuimarika na kurejea nchini. Akizungumza na Waandishi wa habari Mwenyekiti wa Habari Njema kwa Wote Askofu CHARLES GADI ameeleza kuwa Maombezi hayo yatafanyika Mpinga Bagamoyo na yanatarajiwa kuhudhuriwa na Viongozi  wa Dini zote sanjari na Viongozi wa Kitaifa na Serikali. Mbali na...

Like
232
0
Thursday, 13 November 2014
AKWAYA KUPUNGUZA UTAPIAMLO LUDEWA
Local News

SHIRIKA lisilo la Kiserikali la AKWAYA limeanza kutekeleza mpango wa kupunguza tatizo la Utapiamlo ambalo limekithiri Wilayani Ludewa mkoani Njombe kwa kutoa Elimu kwa Wazazi kuweza kuwa matumizi bora ya Chakula kwa watoto. Akizungumza na Wananchi katika Tamasha lililoandaliwa na Shirika hilo Ludewa vijijini ,Mkurugenzi wa Shirika hilo SAMWEL MPUTA amesema Wilaya ya Ludewa imejaliwa kuwa na mazao ya Chakula aina zote lakini inashangaza kuona hali ya utapamlo iko juu. MPUTA amebainisha kuwa Mpaka sasa Takwimu zinaonyesha kuwa zaidi ya...

Like
295
0
Thursday, 13 November 2014
JESHI LA ZIMA MOTO LAAJIRI WAFANYAKAZI 400
Local News

Katika kupambana na tatizo la upungufu wa Wafanyakazi unaolikabili Jeshi la Zima Moto na Uokoaji nchini, Serikali imeajiri zaidi ya Wafanyakazi 400 wanaotarajia kumaliza kozi Maalum ya Jeshi na kusambazwa vituoni Novemba 14. Akizungumza na EFM leo ofisini kwake Kamishna Msaidizi wa Jeshi hilo upande wa Elimu kwa Umma MIRAJI KILLO amesema jeshi limekuwa na changamoto nyingi zinazolifanya lishindwe kufanya kazi kwa ufanisi ikiwemo changamoto ya wafanyakazi ambayo Serikali imeanza kuifanyia kazi kwa kuajiri wafanyakazi...

Like
306
0
Wednesday, 12 November 2014
WIZARA YA AFYA YAWATAKA WAANDISHI WA HABARI KUSHIRIKIANA NA WIZARA HIYO
Local News

 WIZARA ya afya na Ustawi wa Jamii imewataka Waandishi wa Habari kushirikiana na Wizara hiyo katika kutoa taarifa sahihi ili kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza kwa wananchi kutokana na taarifa zisizo sahihi. Wito huo umetolewa leo Bungeni mjini Dodoma na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Dokta SEIF RASHID wakati akifafanua Muongozo kutoka kwa Mheshimiwa EZEKIA WENJE wa kutaka kujua Mikakati ya Serikali juu ya taarifa mbalimbali za Wizara hiyo zinazotolewa na kuandikwa katika vyombo vya...

Like
214
0
Wednesday, 12 November 2014
WAJASILIAMALI WAHAMASISHWA KUKOPA KUJIWEZESHA
Local News

WAJASIRIAMALI wa vikundi vya Silki nchini,wametakiwa kukopa fedha na kurejesha kwa wakati ili kuwawezesha wengine kukopa.   Naibu Meya wa Manispaa ya Morogoro MOHAMED LEKULE ameeleza hayo wakati wa kugawa hisa katika vikundi vya Pambazuko na Dhahabu, vilivyo chini ya Silki mjini humo.   Amebainisha kuwa ni vyema Wanachama wa Vikundi hivyo wakawa na utaratibu wa kukopa fedha kwa ajili kuendesha miradi mbalimbali na kuwataka kurejesha mikopo hiyo kwa wakati ili kuwawezesha wanachama wengine kukopa....

Like
239
0
Wednesday, 12 November 2014
MUHONGO KUWA MGENI RASMI MKUTANO WA SERA ZA KUKUZA MITAJI
Local News

 WAZIRI wa Nishati na Madini Profesa SOSPETER MUHONGO anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mkutano utakaozikutanisha kampuni na mashirika ya Umma,yanayojihusisha na Nishati kwa lengo la kupitia sera na kukuza mitaji. Profesa MUHONGO pia anatarajiwa kuzihamasisha kampuni zenye nia ya kuwekeza katika uzalishaji wa Nishati ya Umeme kwa lengo la kuongeza ufanisi wa upatikanaji wa Umeme nchini. Mkutano huo unatarajiwa kufanyika November 31,mwaka huu jijini Dar es salaam ,utawakutanisha Wawekezaji kutoka nchi za India, Marekani,China na Bara la...

Like
196
0
Wednesday, 12 November 2014
MKAMBA KISALAWE KUPATIWA MAJI SAFI NA SALAMA
Local News

Kilio cha mda mrefu kwa wakazi wa mtaa wa mkamba kisarawe 2 Wilaya ya Temeke hatimaye sasa hivi kimesikika kwa kupata msaada wa mradi wa maji safi ya bomba, Ila hapo awali walikuwa wanakunywa maji ya madibwi kwa mda mrefu na maji hayo yalikuwa yanapatikana umbali zaidi ya kilomita moja kutoka maeneo wanayoishi. Mwenyekiti wa mkamba HUSEN SALEH anaelezea zaidi Wakina mama wa mtaa huo wa mkamba RAMLA KASIMU na MWAJUMA HUSSEN wanaelezea.....

Like
258
0
Wednesday, 12 November 2014
WATAALAMU NISHATI NA MADINI WATAKIWA KUWA WABUNIFU
Local News

WATAALAMU kutoka Sekta za Nishati na Madini nchini wametakiwa kuwa wabunifu katika maandalizi na Usimamizi wa Miradi ili sekta hizo ziwe na mchango katika ukuaji wa uchumi wa nchi. Wito huo umetolewa na Kamishna Msaidizi wa Umeme Mhandisi INNOCENT LUOGA kwa niaba ya Kamishna wa Nishati na Maendeleo ya Petroli Mhandisi HOSEA MBISE alipokuwa akifungua mafunzo ya uandaaji wa mapendekezo ya Miradi, Sera na Mbinu za usimamizi wa Miradi. Mafunzo hayo yamewashirikisha Wataalamu kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Shirika...

Like
258
0
Tuesday, 11 November 2014