Local News

MKUU WA MKOA PAUL MAKONDA KUTIA TIMU NDANI YA EFM REDIO
Local News

Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Paul Makonda atia timu ndani ya EFM redio leo, ziara hiyo ni katika kuangalia utendaji kazi wa redio hiyo pamoja na kujadiliana mambo kadha wa kadha yahusianayo na jamii kwa ujumla. Mkurungenzi wa EFM redio Francis Siza katika picha ya pamoja na Mh. Paul Makonda leo alipotembelea kituo hicho. Paul Makonda akiwa studio akiongea na baadhi ya watangazaji wa kipindi cha UHONDO ambao ni Dina Marios, Swebe Santana pamoja na Sofia Amani...

Like
1072
0
Friday, 01 April 2016
SERIKALI YAKEMEA TABIA YA KUSHAMBULIA WATUMISHI WA AFYA
Local News

SERIKALI imekemea tabia inayotaka kujengeka ndani ya jamii ya kuwashambulia watumishi wa afya hasa Madaktari na Wauguzi. Kufuatia hatua hiyo, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, mheshimiwa Ummy Mwalimu amevitaka vyombo ya dola kuwachukulia hatua wananchi wanaojihusisha na vitendo hivyo ambavyo vitaathiri utoaji wa huduma za afya kwa wananchi hasa wa kipato cha chini. Amewaonya wananchi kutoitumia vibaya dhamira ya dhati ya Rais Dkt. John Magufuli na Serikali ya kuimarisha nidhamu na uwajibikaji katika utumishi wa...

Like
192
0
Thursday, 31 March 2016
KIGOMA: KUFUNGULIWA KWA BARABARA ZA RAMI MWEZI MEI MWAKANI
Local News

MAKANDARASI wanaojenga barabara ya Kidahwe-Kasulu Km 50 na Kibondo-Nyakanazi Km 50 wametakiwa kukamilisha ujenzi huo mwezi Mei mwakani badala ya Novemba ili kuharakisha mkakati wa Serikali wa kuufungua mkoa wa Kigoma kwa barabara za lami.   Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amesema hayo mara baada ya kukagua ujenzi wa barabara hiyo uliyogawanywa sehemu mbili, Kidahwe-Kasulu inayojengwa na China Railway 50 Group na Kibondo-Nyakanazi inayojengwa na Nyanza Road Works. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano...

Like
1147
0
Thursday, 31 March 2016
VIETNAM: BUNGE LAPATA MWENYEKITI WA KWANZA MWANAMKE.
Local News

Bunge la Vietnam limepiga kura na kumpitisha Nguyen Thi Kim Ngan kuwa mwenyekiti wa bunge hilo kwa ushindi wa asilia 95.5% ya kura zilizopigwa. Ushindi huo wa Ngan, 61, unamfanya aingie kwenye rekodi ya kuwa mwanamke wa kwanza kukamata nafasi hiyo ya uongozi katika taifa hilo. Kabla ya ushindi huo hapo awali Ngan alikuwa mkurugenzi wa idara ya fedha katika jimbo la nyumbani kwake la Ben...

Like
218
0
Thursday, 31 March 2016
MAKONDA AKABIDHIWA OFISI RASMI DARESALAAM
Local News

ALIYEKUWA mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Said Meck Sadick leo amemkabidhi rasmi ofisi mkuu wa mkoa mpya wa Dar es salaam Mheshimiwa Paul Makonda ambapo amemuomba Mkuu huyo mpya wa mkoa kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wananchi ikiwemo afya na elimu. Akizungumza mbele ya maofisa na watendaji mbalimbali ambao wamejitokeza kwa ajili ya kushuhudia makabidhiano hayo Mheshimiwa Sadick amesema licha ya yeye kufanya kazi kwa mafanikio bado kuna changamoto ambazo anaamini kutokana na uzoefu alionao mkuu huyo wa mkoa...

Like
218
0
Tuesday, 29 March 2016
SUMATRA NA JESHI LA POLISI WAKAMATA AMABASI 105 NA 36 YAFIKISHWA MAHAKAMANI
Local News

MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri wa Nchi Kavu na Majini (SUMATRA) kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi, Kikosi cha Usalama Barabarani wamefanya ukaguzi katika Jiji la Dar es salaam na kufanikiwa kukamata mabasi  105 na kati hayo 36 yamefikishwa mahakamani  baada ya kukiuka masharti ya leseni ya usafirishaji abiria.   Hayo yamebainishwa leo na Meneja Mawasiliano wa SUMATRA David Mziray wakati wa mkutano na vyombo vya habari uliolenga kutoa ufafanuzi kuhusu hatua zinazochukuliwa na Mamlaka hiyo katika kutatua kero zinazowakabili...

Like
221
0
Tuesday, 29 March 2016
MKURUGENZI HALMASHAURI YA WILAYA YA ITILIMA ASIMAMISHWA KAZI
Local News

MKURUGENZI wa Halmashauri ya wilaya ya Itilima mkoani Simiyu John Aloyce amesimamishwa kazi kwa tuhuma za kushindwa kuisimamia halmashauri hiyo na kusababisha kuwepo kwa migogoro kati ya madiwani na watendaji. Uamuzi huo umechukuliwa na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Antony Mtaka katika kikao cha dharura cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa Halmashauri hiyo. Mbali na uamuzi huo Mtaka amefuta posho zote kwa wakuu wa Idara na vitengo katika halmashauri zote zilizopo mkoani hapo wanaoingia katika vikao vya madiwani...

Like
375
0
Tuesday, 29 March 2016
RAIS MAGUFULI APOKEA TAARIFA YA CAG
Local News

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa dokta John pombe Magufuli, jana amepokea taarifa ya ukaguzi wa hesabu za serikali kutoka kwa Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) Profesa Mussa Assad Ikulu Jijini Dar es salaam. Kwa mujibu wa taarifa ya Ikulu Rais Magufuli amepokea taarifa hiyo yenye ripoti tano, ikiwa ni utaratibu wa kikatiba unaomtaka Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali kukabidhi kwa Rais taarifa ya ukaguzi kabla ya mwisho wa mwezi Machi....

Like
224
0
Tuesday, 29 March 2016
MIONGOZO RAHISI YA USIMAMIZI WA MISITU YAZINDULIWA
Local News

MRADI wa MAMA MISITU kwa kushirikiana na Serikali na wadau mbalimbali wamezindua miongozo rahisi ya usimamizi shirikishi wa misitu kwa jamii, vijiji na kwa pamoja. Akizungumza na waandishi wa Habari katika uzinduzi huo, Meneja Mradi wa MAMA MISITU Gwamaka Mwakyanjala amesema kuwa lengo la uzinduzi wa Miongozo hiyo ni kuwawezesha wananchi kufahamu zaidi ni nini wanapaswa kufanya katika utunzaji wa misitu ili wafaidike na malighafi zinazotokana na...

Like
228
0
Thursday, 24 March 2016
SHEIN AAPISHWA ZANZIBAR LEO
Local News

RAIS Mteule wa Zanzibar, Dokta Ali Mohammed Shein anaapishwa leo kwenye Uwanja wa Aman mjini Zanzibar. Kuapishwa kwa Dk Shein kunamfanya apate nafasi nyingine ya kuongoza Zanzibar kwa muda wa miaka mitano ijayo, baada ya mgombea huyo wa CCM kushinda urais wa Jumapili kwa kujinyakulia asilimia 91 ya kura zilizopigwa. Serikali pia imetangaza kuwa leo pia ni siku ya mapumziko visiwani humo ili kuwapa nafasi wananchi wahudhurie sherehe za kuapishwa kwa kiongozi wao. Wageni ambao wanatarajia kuhudhuria kwenye sherehe hizo...

Like
254
0
Thursday, 24 March 2016
WANANCHI NA MADEREVA WA DALADALA WAMEIOMBA SERIKALI KUBORESHA MIUNDOMBINU KATIKA VITUO VYA MAWASILIANO NA MAKUMBUSHO
Local News

WANANCHI na madereva katika vituo vya daladala vya Makumbusho na Mawasiliano, wameiomba serikali kutengeneza barabara ziingiazo katika vituo hivyo kwani ni mbovu na zinasababisha uharibifu wa magari. Wakizungumza na efm baadhi ya madereva hao wamesema kuwa barabara hizo ni finyu na mbovu hususani zinazoingia katika kituo cha makumbusho ambazo pamoja na Serikali kumwaga vifusi lakini kwa mvua iliyonyesha leo imekuwa ni kero ya tope kwa waenda kwa...

Like
273
0
Wednesday, 23 March 2016