Local News

TRA NA POLISI WAKAMATA MAKONTENA 9
Local News

MAMLAKA ya Mapato Tanzania-TRA-kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi wamekamata Makontena tisa ambayo bado haijafahamika yana vitu gani ndani katika eneo la Tangibovu Mbezi Beach Jijini Dar es salaam yaliyosafirishwa kinyume na utaratibu usiku wa manane. Akizungumza na Waandishi wa habari katika eneo la tukio Mkurugenzi wa huduma na elimu kwa Mlipa kodi kutoka-TRA-Richard Kayombo amesema Mamlaka imebaini kuwa Muagizaji wa makontena hayo ni Heritage Empire Company Limited na wakala wa Forodha aliekuwa akishughulikia ni Napock Africa Company...

Like
257
0
Tuesday, 01 December 2015
IGUNGA: KAYA ELFU 18 KUNUFAIKA NA MPANGO WA RUZUKU ZA PEMBEJEO
Local News

ZAIDI ya kaya Elfu 18 katika kata nane za Halmashauri ya wilaya ya IGUNGA mkoani Tabora zitanufaika na mpango wa ruzuku za pembejeo katika msimu huu wa mwaka 2015-2016. Afisa Maendeleo ya Kilimo, Umwagiliaji na Ushirika wa wilaya ya Igunga, Hossea Samaruku ameeleza hayo wakati akizungumzia hali halisi ya upatikanaji wa pembejeo za ruzuku katika wilaya hiyo. Samaruku amesema vijiji 43 vya wilaya hiyo vitashiriki kutekeleza mpango huo na kata zitakazonufaika na ruzuku ni pamoja na Nyandekwa, Nkinga na...

Like
389
0
Tuesday, 01 December 2015
MAADHIMISHO YA SIKU YA UKIMWI DUNIANI
Local News

WATANZANIA leo wanaungana na watu wote duniania kuadhimisha siku ya Ukimwi ikiwa ni sehemu ya kupanua ufahamu kuhusu maafa yanayoletwa na ugonjwa huo.   Kama ilivyo katika maadhimisho ya Uhuru, Maadhimisho ya leo hayatafanyika kama ilivyozoeleka na badala yake fedha ambazo zingetumika katika siku hiyo zitatumika kununulia dawa za kupunguza makali ya Ukimwi- ARV.   Hatua hii inafuatia Agizo lililotolewa hivi karibuni na rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John Pombe Magufuli ambapo Katika uamuzi wake baada ya...

Like
236
0
Tuesday, 01 December 2015
SHULE YA SEKONDARI KIMANI YAKABILIWA NA CHANGAMOTO YA UHABA WA MAJI SAFI NA SALAMA
Local News

SHULE ya sekondari Kimani iliyopo  kisarawe  mkoani Pwani inakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo uhaba wa maji safi na salama  kutokana  na kuchangia kunywa maji  na wanyama  katika kisima kilichpo shuleni hapo. Hayo yamebainishwa na mkuu wa shule  Nazarius Hongoa wakati alipokuwa akizungumza katika mahafali ya tatu  ya kidato cha nne  yaliyofanyika shuleni hapo ambapo amesema kuwa  wapo hatarini kukubwa na maradhi kutokana na maji kutokuwa...

Like
475
0
Monday, 30 November 2015
SHEIKH PONDA AACHIWA HURU
Local News

BAADA ya kukaa zaidi ya miaka miwili mahabusu hatimaye mahakama ya hakimu mkazi mkoa wa morogoro leo imemwachia huru katibu wa taasisi na jumuiya za kiislamu Tanzania Shekhe Ponda Issa Ponda baada ya kuonekana hana hatia kwa makosa yaliyokuwa yakimkabili.   Hukumu hiyo imesomwa na hakimu wa mahakama hiyo bi Mary Moyo amesema baada ya kupitia ushahidi uliotolewa pande zote mbili yaani upande wa mashitaka na upande wa mshitakiwa mahakama imemuona mtuhumiwa hana hatia na kumwachia huru kutokana na kifungu...

Like
159
0
Monday, 30 November 2015
MSD KUFUNGUA DUKA KUBWA LA KISASA MUHIMBILI KUTEKELEZA AGIZO LA RAIS
Local News

SIKU chache baada ya Rais Dokta John Magufuli kuiagiza bohari ya dawa nchini-Msd-kufungua maduka ya dawa kwenye Hospitali za kanda na Taifa,  tayari agizo hilo limeanza kufanyiwa kazi ambapo bohari hiyo wiki ijayo inatarajia kufungua duka kubwa la kisasa ndani ya hospitali ya Taifa ya Muhimbili. Mkurugenzi wa MSD, Laurean Bwanakunu amesema tayari maandalizi ya kufungua duka hilo yamekamilika nalinatarajia kufunguliwa wiki ijayo huku akibainisha kuwa litatumia mfumo maalum wa kielektroniki ili kuhakikisha dhima ya kuwezesha upatikanaji wa dawa...

Like
236
0
Friday, 27 November 2015
WAZIRI MKUU AFANYA ZIARA YA KUSHTUKIZA BANDARI YA DARESALAAM
Local News

WAZIRI MKUU mheshimiwa Majaliwa Kasim Majaliwa awasimamisha kazi kamishna wa kodi Tiagi Masamaki na Habibu Mpozya kitengo cha huduma kwa wateja kutokana ubadhilifu wa fedha kwa makontena zaidi ya 300 yaliyopotea. Waziri Mkuu pia  ameamuru kukamatwa kwa maafisa kadhaa wa Mamlaka ya Mapato Tanzania –TRA,  na wengine kufukuzwa kazi baada ya kufanya ziara ya kushutukiza Bandarini hapo  leo. Maafisa hao wametakiwa pia kusalimisha pia hati zao za...

Like
953
0
Friday, 27 November 2015
VYOMBO VYA HABARI VIMETAKIWA KUWA NA MADAWATI YA HABARI ZA MAHAKAMA
Local News

VYOMBO vya habari nchini vimetakiwa kuwa na madawati ya habari za Mahakamani, ili kuboresha uandishi wa habari hizo.   Hayo yamebainishwa na Jaji kiongozi wa Mahakama kuu ya Tanzania Shaaban Lila alipokuwa akizungumza na wanahabari wakati wa kufunga semina ya mafunzo ya uandishi wa habari za mahakamani ambapo amesema  pindi mtuhumiwa anapopandishwa  kizimbani  vifungu vya sheria ndivyo vinavyotumika kwa kuzingatia aina ya makosa ya mtuhumiwa.   Amewataka wanahabari kutoa taarifa kwa kuzingatia hukumu iliyotolewa badala ya wao kuhukumu...

Like
147
0
Friday, 27 November 2015
ASKOFU MKUU TABORA KUONGOZA UJUMBE WA TANZANIA KWENYE ZIARA YA PAPA FRANCIS UGANDA
Local News

ASKOFU MKUU wa jimbo kuu la Tabora Mhashamu Paulo Ruzoka anaongoza ujumbe wa Tanzania kwenye ziara ya Kiongozi Mkuu wa Kanisa Katoliki duniani Baba Mtakatifu Francis nchini Uganda leo.   Papa Francis anatarajia kuwasili nchini Uganda leo kwa ziara ya siku mbili akitokea Kenya kabla ya kuelekea Afrika ya Kati.   Katibu wa Baraza la Maaskofu Tanzania–TEC, Padre Raymond Saba amesema  Mabaraza ya Maaskofu ya Kenya na Uganda kwa pamoja yalitoa mwaliko kwa TEC kushiriki katika ziara ya Baba Mtakatifu...

Like
256
0
Friday, 27 November 2015
WIZARA YA ELIMU NA MAFUNZO YA UFUNDI YAANDAA WARSHA KUENDELEZA STADI ZA KAZI
Local News

WIZARA ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi kwa kushirikiana na Wizara ya Kazi na Ajira imeandaa warsha ilinayolenga kuandaa Mkakati wa Kitaifa wa miaka 10 wa kuendeleza stadi za kazi kwa miaka mitano ya kwanza. Akizungumza na Wanahabari jijini Dar es salaam leo Mkurugenzi Msaidizi wa Idara ya Elimu ya juu kutoka Wizara hiyo Dokta Jonathan Mbwambo amesema kuwa takwimu zinaonesha Tanzania ina watu wenye ujuzi wa chini na stadi za kazi ambazo zinahitaji kukuzwa ili nchi iweze kufikia matarajio...

Like
290
0
Thursday, 26 November 2015
SERIKALI YAPIGA MARUFUKU UTENGENEZAJI NA UCHAPISHAJI WA CHRISTIMAS NA MWAKAMPYA
Local News

KATIBU Mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue amepiga marufuku utengenezaji na uchapishaji wa kadi za Christimas na mwaka mpya kwa kutumia gharama za serikali kwa mwaka huu. \Katika taarifa yake Balozi Sefue ameeleza kuwa yeyote anayetaka kutengeneza au kuchapisha kadi hizo ni vyema akafanya hivyo kwa gharama zake mwenyewe. Balozi Sefue ameagiza kuwa fedha zilizopangwa kutumika kutengenezea na kuchapisha kadi hizo zitumike kupunguza madeni ambayo wizara, Idara na Taasisi zinazodaiwa na wananchi au wazabuni...

Like
167
0
Thursday, 26 November 2015