Global News

VIONGOZI WA NCHI ZA MAGHARIBI WAMEPENDEKEZA MIPANGO MIPYA JUU YA MGOGORO WA UKRAINE
Global News

WAKATI mapigano yakiendelea mashariki mwa Ukraine, viongozi wa nchi za magharibi wamependekeza mipango mipya kujaribu kumaliza mgogoro kati ya Majeshi ya Serikali na waasi wanaoungwa mkono na Urusi. Rais wa Ukraine Petro Poroshenko amesema mapendekezo mapya yaliyotolewa na kiongozi wa Ujerumani Kansela Angela Merkel, na rais wa Ufaransa Bwana Francois Hollande, yameongeza matumaini ya kumaliza mapigano. Mpango huo utawasilishwa kwa Urusi Ijumaa, ambako Urusi imeahidi mazungumzo yenye manufaa. Lakini hatua ya Urusi kuwaunga mkono waasi wa...

Like
197
0
Friday, 06 February 2015
WITO UMETOLEWA KWA UINGEREZA KUONGEZA MASHAMBULIZI DHIDI YA WANAMGAMBO WA IS
Global News

WITO umetolewa kwa Uingereza kuongeza nguvu za kupambana na Wanamgambo wa Islamic State, ambapo Wabunge wan chi hiyo wamesema Wanamgambo hao wamejiimarisha sehemu za nchi ya Iraq na Syria . Kamati ya kuteuliwa ya maswala ya Ulinzi ndani ya Bunge hilo imesema Uingereza imeshiriki asilimia 6 tu ya mashambulizi ya anga dhidi ya kundi hilo la Jihad na kusema kuwa wanashangazwa kwa kuwa haifanyi jitihada za hali ya juu. IS imekuwa ikishikilia maeneo mengi na imekuwa ikijihusisha na vitendo vya...

Like
206
0
Thursday, 05 February 2015
HALI BADO TETE UKRAINE KUFUATIA ONGEZEKO LA MASHAMBULIZI DHIDI YA RAIA
Global News

SHIRIKA linalojihusisha na maswala ya usalama na ushirikiano barani Ulaya-OSCE limesema hali ya Mashariki ya Ukraine inazidi kuwa mbaya na mashambulizi dhidi ya Raia yanazidi kuongezeka. Msemaji wa Shirika hilo amesema wanafuatilia hali ilivyo nchini Ukraine na kwamba silaha zilizopigwa marufuku kimataifa zilitumika juma lililopta katika mji unaoshikiliwa na waasi . Baadae hii leo, Mkuu wa Shirika la OSCE atahutubia Baraza lake la kudumu, ambapo anatarajiwa kutoa wito wa kusitisha mapigano kwa muda katika Mji unaodhibitiwa na Serikali wa...

Like
203
0
Thursday, 05 February 2015
WAFANYAKAZI KATIKA KISIMA CHA MAFUTA WAUAWA LIBYA
Global News

HABARI kutoka Libya zinasema kuwa idadi kadha ya wafanyakazi katika kisima kimoja cha mafuta wameuawa katika shambulio moja Jumanne usiku. Afisa mmoja mwandamizi wa kijeshi amesema kuwa watu kumi na watatu wameuawa katika kisima cha Mabrook. Watano ni raia wa kigeni, watatu wakiwa ni Wafilipino na wawili wanatoka Ghana. Afisa huyo amesema kuwa wote waliouawa walikatwa koromeo, mbali na Mlibya mmoja ambaye alipigwa risasi. Hakuna kundi lililodai kuhusika na shambulio hilo, ingawa taarifa za watu walioshuhudia tukio hilo wanasema watu...

Like
371
0
Thursday, 05 February 2015
MFALME WA JORDAN AMEAHIDI MAPAMBANO YASIYO NA HURUMA DHIDI YA IS
Global News

MFALME wa Jordan ameahidi mapambano yasiyo na huruma dhidi ya wapiganaji wa Islamic State kufuatia kuuawa kwa rubani wa nchi hiyo. Baada ya mkutano wa makamanda wa juu wa jeshi na maafisa usalama, Mfalme Abdullah amesema vita hivyo vitaelekezwa dhidi ya kundi hilo na damu ya rubani huyo wa ndege za kivita Muath al-Kasasbeh haitapotea bure. Hapo jana, Jordan iliwanyonga wafungwa wawili wapiganaji wenye msimamo mkali waliokuwa katika orodha ya adhabu ya kifo, kama kulipiza kisasi cha kuuawa kwa rubani...

Like
220
0
Thursday, 05 February 2015
MAREKANI YATHIBITISHA KUFANYA SHAMBULIO SOMALIA DHIDI YA AL-SHABAB
Global News

MAAFISA  wa  Marekani  wamesema  vikosi  vya  jeshi  la  Marekani vimefanya  shambulio nchini  Somalia  dhidi  ya  kiongozi mwandamizi  wa  kundi  la  al-Shabaab. Shambulio  hilo  lililofanywa  Januari  31  kwa  kutumia  ndege  isiyo na  rubani  kusini  mwa  mji  mkuu  Mogadishu  lilimlenga  Yusef Dheeq , mkuu  wa  operesheni  za  nje  na mipango  ya  upelelezi  na usalama  wa  kundi  hilo.  Hata  hivyo  haijathibitishwa  iwapo ameuwawa  katika  operesheni  hiyo. Shambulio  hilo ni kampeni ...

Like
258
0
Wednesday, 04 February 2015
SERIKALI YA JORDAN YAWANYONGA RAIA WAWILI WA IRAQ
Global News

SERIKALI ya Jordan imewanyonga  Wairaq  wawili  kwa  kulipiza  kisasi  kwa kuuliwa   raia  mmoja  wa  nchi  hiyo  na  kundi  la  Dola  la  Kiislamu. Hatua  hiyo  ya  kunyongwa  imekuja  saa  chache  baada  ya kutolewa  video  inayoonesha  rubani  wa  jeshi  la  Jordan akichomwa  moto  akiwa  hai. Ripoti  za  televisheni  ya  taifa zinasema  rubani  huyo  aliuwawa  kiasi  mwezi  mmoja  uliopita. Mchambuzi  wa  masuala  ya  mashariki  ya  kati  Randa Habib amesema mauaji  hayo ...

Like
266
0
Wednesday, 04 February 2015
NDEGE YA TAIWAN YAANGUKIA MTONI
Global News

NDEGE inayomilikiwa na Shirika la Ndege la Taiwan, la TransAsia imepata ajali na kuangukia kwenye mto katika mji mkuu, Taipei. Vyombo vya habari vya Taiwan vimesema watu zaidi ya 50 walikuwa ndani ya ndege hiyo, wakati ajali ilipotokea na idadi kubwa ya watu wameripotiwa kujeruhiwa. Shirika la Habari la Taiwan limeonesha picha ya ndege hiyo ikiwa imezama kwa kiasi kikubwa katika mto Keelung. Watu kadhaa wameokolewa na kupelekwa hospitali na wengine 10 bado wamenasa katika ndege hiyo. Chanzo cha ajali...

Like
189
0
Wednesday, 04 February 2015
WAZIRI MKUU WA UGIRIKI AENDELEZA ZIARA YAKE KATIKA MATAIFA YA ULAYA KUTAFUTA KUUNGWA MKONO
Global News

WAZIRI MKUU  mpya  wa  Ugiriki Alexis  Tsipras  anaendelea  na ziara  ya   mataifa  ya  Ulaya  tangu  aingie  madaraka  wiki  moja iliyopita, katika jitihada za  kutafuta kuungwa mkono mpango wa kutaka suala la kuiokoa nchi yake na mzigo wa madeni lijadiliwe upya. Anakwenda  Italia  leo  kwa  mazungumzo  na  waziri  mkuu  Matteo Renzi. Jana waziri mkuu huyo aliondoa  uwezekano  wa  kufanyakazi pamoja  na  kundi  la  pande  tatu la  wakopeshaji  wa ...

Like
268
0
Tuesday, 03 February 2015
UMOJA WA ULAYA UMESEMA MAHAKAMA NCHINI MISRI IMEKIUKA MAJUKUMU YAKE YA KIMATAIFA
Global News

UMOJA wa  Ulaya  umesema  leo  kuwa mahakama  nchini  Misri imekiuka  majukumu  yake ya   kimataifa  kuhusu  haki  za  binadamu kwa  kuwahukumu  watu 183 adhabu  ya  kifo  jana  kwa  kuwauwa polisi 13. Idara  ya  mambo  ya  kigeni  ya  Umoja  wa  Ulaya  imesema  katika taarifa yake kuwa  uamuzi  uliotolewa  na  mahakama  ya  Misri kuwahukumu  washitakiwa   183 adhabu  ya  kifo  kufuatia  kesi  ya jumla ni  ukiukaji  wa  majukumu  ya  Misri  ya  haki  za  binadamu. Hukumu  iliyotolewa ...

Like
190
0
Tuesday, 03 February 2015
MASHAMBULIZI YA BOKO HARAM KASKAZINI MWA NIGERIA YATIMIZA MWEZI MMOJA
Global News

LEO  ni mwezi mmoja tangu wapiganaji wa Boko Haram waliposhambulia miji ya Baga na Doron Baga kaskazini mashariki mwa Nigeria. Idadi kamili ya watu waliokufa haijulikani lakini inadaiwa kuwa ni kati ya watu mia moja na hamsini hadi elfu mbili. Wakati wapiganaji wa Boko Haram wakivamia kutoka upande wa magharibi wa Baga, kundi la vijana waliodhamiria kupambana na kundi hilo walijaribu kuulinda mji wao.  ...

Like
188
0
Tuesday, 03 February 2015