Global News

EU yamtambua mpinzani wa Maduro
Global News

Mgogoro wa kisiasa unaoendelea kuikabili Venezuela umechukua sura mpya Alhamisi mara baada ya bunge la Umoja wa Ulaya kutangaza kuwa linamtambua rasmi Juan Guaido wa Venezuela, kama rais wa muda wa nchi hiyo. Bunge hilo limesema kuwa litaendelea kumtambua Guaido kama kiongozi wa Venezuela hadi pale nchi hiyo itakapofanya uchaguzi huru na wa haki. huku wajumbe 429 wakipiga kura kuunga mkono hatua hiyo wakati wa kikao maalum mjini Brussels, Ubelgiji.   Aidha, hatua hiyo, inaendelea kuongeza changamoto zinazomkabili rais Nicolas Maduro...

Like
579
0
Friday, 01 February 2019
Raisi wa Burundi afungua mashtaka dhidi ya televisheni
Global News

Mahakama mjini Paris , nchini Ufaransa imeanza kusikiliza kesi iliyofunguliwa na Rais wa Burundi Pierre Nkurunziza dhidi televisheni moja ya nchini Ufaransa,mwanasheria wa Ubeligiji na Mwandishi wa habari wa Burundi kwa makosa ya kuikashifu nchi yake na hadhi yake. Rais Nkurunziza anadai kuwa televisheni hiyo ya Ufaransa miaka miwili iliyopita ilionyesha picha video za mauaji ya kimbari kwa madai kuwa chama tawala cha Burundi ndicho kilichohusika. Mahakama ya mjini Parisi nchini Ufaransa imeanza kusikiliza kesi iliyofunguliwa na Rais wa...

Like
896
0
Friday, 25 January 2019
Mnangagwa asitisha ziara yake ya nchi za Nje
Global News

Rais wa Zimbabwe, Emmerson Mnangagwa amekatisha ziara yake nchi za nje kufuatia kuongezeka kwa vurugu zilizosababishwa na vyombo vya ulinzi vinavyopambana na waandamanaji wanaoipinga serikali. Kiongozi huyo alipaswa kuelekea jijini Davos, Uswisi kushiriki katika Jukwaa la Kiuchumi duniani, kwa lengo la kutafuta vitega uchumi kwa ajili ya kuinusuru nchi yake iliyoporomoka kiuchumi ambapo amesema kuwa kipaumbele chake cha kwanza ni kuifanya Zimbabwe kuwa na utulivu na imara. Maandamano hayo yamesababishwa na kupanda kwa bei ya mafuta mwishoni...

Like
588
0
Monday, 21 January 2019
Jeshi la Israel limekishambulia kikosi cha Quds cha jeshi la Iran nchini Syria
Global News

Jeshi la Israel linasema limeanza kushambulia maeneo yanayodhibitiwa na jeshi la Iran nchini Syria. Kikosi cha ulinzi Israel (IDF) kinasema operesheni yake ni dhidi ya kikosi cha Quds – kikosi maalum katika jeshi la mapinduzi la Iran. Haikutoa ufafanuzi zaidi. Lakini kuna taarifa kuhusu makombora yaliofyetuliwa katika maeneo yanayo uzunguka mji mkuu wa Syria, Damascus mapema Jumatatu. Vyombo vya habari nchini Syria vinasema vikosi vya ulinzi wa angani vimezuia ‘shambulio la Israel’. Siku ya Jumapili jeshi la Isarel lilisema...

Like
478
0
Monday, 21 January 2019
Muungano wa Afrika umeiomba DR Congo uahirishe kutangaza matokeo kamili ya uchaguzi mkuu
Global News

Muungano wa Afrika (AU) umeitaka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo iahirishe kutangaza matokeo ya uchaguzi mkuu. Muungano huo unaonuia kuhimiza umoja na demokrasia, unasema una “shaka kubwa” na matokeo ya awali yaliotangazwa wiki iliyopita. Matokeo hayo yalimpa ushindi mgombea wa upinzani Felix Tshisekedi lakini mpinzani wa utawala uliopo. Matokeo ya mwisho yanatarajiwa kutangazwa leo Ijumaa. Kumezushwa maswali mengi kuhusu uhakika wa matokeo hayo huku kukiwepo shutuma kwamba Tshisekedi anapanga mpango wa kugawana madaraka na rais...

Like
455
0
Friday, 18 January 2019
Magaidi walioshambulia hoteli Nairobi wauawa
Global News

  Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta amesema kuwa magaidi waliohusika kufanya shambulio la kuvamia hoteli la kifahari ya DusitD2 iliyopo nchini Kenya jijini Nairobi tayari wameuawa na operesheni imekamilika. Hata hivyo shambulio hilo limeleta madhara makubwa ikiwemo kusababisha vifo vya watu 14 pamoja na majeruhi huku wengine 700 wakiwa wamefanikiwa kuokolewa katika janga hilo lililoikumba nchi ya Kenya siku ya jana. Ambapo kundi la kigaidi la Al-shabaab limekiri kuhusika na shambulio hilo ambapo jana majira ya saa 9 jioni walivamia...

Like
704
0
Wednesday, 16 January 2019
Marekani walaani shambulio la hoteli ya kifahari jijini Nairobi
Global News

Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika (AU) Moussa Faki Mahamat amelaani vikali shambulio la Hoteli ya kifahari ya DusitD2 jijini Nairobi. Katika taarifa yake, Faki amevisifu vyombo vya ulinzi na usalama vya Kenya kwa kuchukua hatua za uokozi wa raia na kupambana na wahalifu mapema iwezekanavyo. Pia amesema tukio hilo linaonesha umuhimu wa kupitia upya mipango ya kuongeza nguvu ya kupambana na vikundi vya kigaidi barani Afrika. “Mwenyekiti wa Kamisheni anathibitisha utayari wa AU kuendelea kufanya kazi kwa pamoja...

Like
579
0
Wednesday, 16 January 2019
Trump atishia kuuangamiza uchumi wa Uturuki kuhusu Wakurdi Syria
Global News

Rais wa Marekani Donald Trump ametishia ‘kuiangamiza Uturuki kiuchumi’ iwapo taifa hilo litawashambuliwa vikosi vya wakurdi nchini Syria baada ya wanajeshi wa Marekani kuondoka Syria. Katika ujumbe wake alioutuma kwenye mtandaoi wa kijamii Twitter, Trump amesema hakutaka Wakurdi kwa upande wao nao pia waichokoza Uturuki. Vikosi vya Marekani vimepambana kwa ushirikiano na wanamgambo wa Kikurdi kaskazini mwa Syria dhidi ya kundi la Islamic State (IS). Uturuki hatahivyo inatazama wapiganaji hao wa vitengo vya YPG kama magaidi. Rais...

Like
563
0
Monday, 14 January 2019
Mkoba wa Mugabe uliojaa  madola waibiwa
Global News

Watu watatu wamefikishwa mahakamani nchini Zimbabwe, wakishtakiwa kuiba mkoba uliokuwa na $150,000 (£117,600) pesa taslimu mali ya rais wa zamani wa taifa hilo Robert Mugabe. Washukiwa hao wa wizi wanadaiwa kutumia pesa hizo kununua magari, nyumba na mifugo. Jamaa wa rais huyo wa zamani, Constantia Mugabe, ni miongoni mwa walioshtakiwa, kwa mujibu wa taarifa katika vyombo vya habari vya serikali. Mwanamke huyo anadaiwa kuwa na funguo za nyumba ya kijijini ya Bw Mugabe iliyo eneo la Zvimba karibu na mji...

Like
591
0
Friday, 11 January 2019
Mpinzani atangazwa mshindi uchaguzi wa Urais DRC
Global News

Mgombea wa chama cha upinzani, Felix Tshisekedi ametangazwa kuwa mshindi wa uchaguzi wa Urais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC), saa chache zilizopita. Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (CENI) kupitia kwa Mwenyekiti wake, Corneille Nangaa imemtangaza Tshisekedi kuwa amepata 38.5% ya kura zote akiwashinda wapinzani wake Martin Fayulu na aliyekuwa mgombea wa chama tawala Emmanuel Shadary. Emmanuel Shadary aliyekuwa anaungwa mkono na Rais Joseph Kabila ameambulia nafasi ya tatu, huku mpinzani Fayulu akishika nafasi ya pili. Kwa mujibu...

Like
476
0
Thursday, 10 January 2019
Upinzani DRC wasema matokeo ya uchaguzi ‘hayana mjadala’
Global News

Mgombea wa urais wa upinzani nchini Congo DRC Martin Fayulu amewaonya maafisa wa uchaguzi dhidi ya ”kuficha ukweli” huku hali ya taharuki ikiendelea kutanda baada ya matokeo ya uchaguzi kucheleweshwa. Bwana Fayulu amesema “watu wa Congo tayari wanajua” matokeo ya uchaguzi uliyofanyika Desemba 30 kuahirishwa kwa wiki moja. Matokeo ya awali ya uchaguzi huo yalitarajiwa kutangazwa siku ya Jumapili ya Januari 6 lakini yakaahirishwa. Uchaguzi huo ulikuwa wa kumtafuta mrithi wa rais Joseph Kabila, ambaye anaachia madaraka...

Like
536
0
Wednesday, 09 January 2019