Sports

HUYU NDIO SHABIKI ATAKAEKUWA MILIONEA IWAPO LEICESTER CITY ITATWAA UBINGWA WA EP
Slider

Shabiki mmoja wa timu ya Leicester amesema kuwa ana uhakika klabu hiyo itashinda ubingwa wa ligi na kumfanya kupata zaidi ya pauni 20,000 ambayo ni sawa na milioni 64 za Tanzania. Leigh Herbert aliwekeza 5000 baada ya kupata vinywaji kadhaa wakati wa likizo huko Newquay ,Cornwall mwaka uliopita. Nina furaha tele kwa sababu nina uhakika wa asilimia 100 kwamba hilo litafanyika. Leigh aliweka fedha alicheza kamari hiyo kufuatia uteuzi wa mkufunzi Claudio Ranieri.Nilifikiria kwamba atailetea kilabu hiyo kitu maalum. Nilijua...

Like
269
0
Friday, 29 April 2016
ALFRED LUCAS ATEULIWA KUWA AFISA HABARI MPYA TFF
Slider

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) limemteua Alfred Lucas kuwa Afisa Habari na Mawasiliano mpya wa shirikisho kuanzaia leo Aprili 27, 2016. Alfred anachukua nafasi ya Baraka Kizuguto aliyehamishiwa katika Kurugenzi ya Mashindano kuwa Afisa Mashindano na Meneja wa Mifumo pepe ya Usajili (TMS). Alfred ana uzoefu kutoka vyombo mbalimbali alivyovitumikia kama mwandishi wa habari na mhariri.Kadhalika Alfred kitaaluma amesomea uandishi wa habari, uhusiano wa kimataifa na diplomasia pamoja na...

Like
274
0
Wednesday, 27 April 2016
TAIFA STARS KUIVAA HARAMBEE STARS
Slider

Timu ya Taifa ya Tanzania inatarajiwa kucheza mchezo wa kirafiki wa kimataifa na timu ya Taifa Kenya Mei 29, jijini Nairobi. Mchezo huo utachezwa jijini Nairobi Mei, 29 mwaka huu, ikiwa ni sehemu ya maandalizi kwa timu zote mbili kujiandaa na michezo ya kuwania kufuzu kwa Fainali za Mataifa Afrika mwezi Juni, 2016 ambapo Taifa Stars itacheza dhidi ya Misri Juni 04, mwaka huu katika uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. TFF kwa kushirkiana na FKF zimekubaliana kuwepo kwa...

Like
223
0
Wednesday, 27 April 2016
WENGER AONYESHA HOFU EPL
Slider

Meneja wa klabu ya Arsenal Arsene Wenger amesema ameanza kuingiwa na wasiwasi kuhusu Ligi Kuu ya Uingereza msimu huu. Anasema wasiwasi zaidi unatokana na hatari ya klabu hiyo kushindwa kufuzu kwa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya kwanza katika miaka 19. The Gunners walipoteza nafasi ya kupanda hadi nambari tatu kwenye jedwali baada ya kutoka sare tasa na Sunderland ugenini Jumapili. “Tuna haja sana na hilo na tuna wasiwasi kuhusu hilo kwa sababu sasa yatakuwa ni mapambano,” alisema...

Like
216
0
Monday, 25 April 2016
YANGA, TP MAZEMBE NJE MICHUANO YA KLABU BINGWA AFRIKA
Slider

Wakicheza Ugenini huko Nchini Misri, Yanga wamefungwa 2-1 na Al Ahly na kuondolewa katika michuano ya klabu bingwa Africa. Mabingwa watetezi Tp Mazembe wakaondolewa katika michuano hiyo baada ya sare ya 1-1 dhidi Wydad de Casablanca, na Casablanca wakisonga mbele kwa ushindi 3-1. Enyimba wakasonga mbele kwa ushindi wa penati 4-3 dhidi ya Etoile du Sahel ,As Vita Club nao wakasonga mbele licha ya kufungwa kwa mabao 2-1 na Mamelod Sundowns . Al Ahli Tripoli wakawachapa Asec Mimosas kwa mabao...

Like
295
0
Thursday, 21 April 2016
EPL KUTIMUA VUMBI WEEKEND HII
Slider

Ligi kuu ya England inatarajiwa kuendelea tena wikiendi hii kwa michezo kadhaa, Jumamosi Norwich itaikaribisha Sunderland, Everton wao watakuwa wenyeji wa Southampton, Man Utd watakuwa wenyeji wa Aston Villa katika dimba la Old Traford , Newcastlle itamenyana na Swansea city, West Brom watawaalika Watford na Chelsea watakuwa darajani Stamford dhidi ya Manchester City. Jumapili Vinara wa ligi Leicester city watakuwa nyumbani na West Ham,Bournemouthwatawaalika Liverpool na Arsenal itamenyana na Crystal...

Like
237
0
Friday, 15 April 2016
UFISADI: DROGBA APANGA KUSHTAKI GAZETI LA DAILY MAIL
Slider

Gwiji la soka toka Ivory Coast na nyota wa zamani wa klabu ya Chelsea Didier Drogba amesema atachukua hatua za kisheria dhidi ya gazeti la Daily Mail.   Hii ni baada ya gazeti hilo kuchapisha habari zinazodai kuwa kati ya pesa anazokusanya kupitia wakfu wake wa kusaidia jamii, ni chini ya asilimia moja ndizo zinazotumika kusaidia jamii. Gazeti hilo limesema ni £14,115 pekee kati ya £1.7m zinazotolewa na wachezaji nyota na wafanyabiashara ambazo husaidia watoto Afrika. Drogba, 38, ametoa taarifa...

Like
199
0
Thursday, 14 April 2016
KOBE BRYANT ACHEZA MECHI YAKE YA MWISHO
Slider

Mmoja wa nyota wa mpira wa vikapu duniani Kobe Bryant, amecheza mechi yake ya mwisho ya kulipwa nchini Marekani. Mchezo huo utafikisha kikomo uchezaji wake wa zaidi ya miongo miwili ambapo Bryant amekuwa wa tatu kwa kuandikisha alama nyingi zaidi katika historia ya mchezo huo. Alishinda mataji matano ya NBA akiwa na LA Lakers ambao amewachezea muda wote huo. Lakini mwandishi mmoja wa BBC anasema Bryant hajaenziwa kwa njia sawa na mashabiki. Wakati mwingine alikuwa hachezaji vyema na mara kwa...

Like
269
0
Thursday, 14 April 2016
BARCELONA YAAGA MICHUANO YA UEFA
Slider

Klabu ya soka ya Barcelona Jumatano ilivuliwa taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya baada ya kuchapwa mabao 2-0 na Atletico Madrid huku Mabao yote ya Altletico Madrid yakifungwa na Antoine Griez-mann na bao la pili likifungwa kwa mara nyingine na Antoine kwa njia ya penalti . Kwa matokeo hayo Atletico Madrid wanasonga mbele kwa ushindi wa jumla ya mabao 3 -2 baada ya awali kufungwa 2-1 na Barcelona katika Uwanja wa Camp Nou. Katika mchezo mwingine Bayern Munich imefakiwa kutinga...

Like
289
0
Thursday, 14 April 2016
MOURINHO AKATAA KAZI SYRIA
Slider

Aliyekuwa meneja wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho amekataa ombi la kumtaka awe meneja wa timu ya taifa ya Syria, wakala wake amesema. Kupitia barua pepe iliyotumwa kwa shirika la habari la Associated Press, Jorge Mendes amesema Mourinho aliambia Shirikisho la Soka la Syria kwamba “ameshukuru sana kupokea mwaliko, lakini hawezi akaukubali kwa sasa”. Mreno huyo mwenye umri wa miaka 53 alifutwa kazi na Chelsea kwa mara ya pili Desemba. Mourinho, ambaye amewahi kuwa meneja Porto, Real Madrid na Inter...

Like
262
0
Monday, 11 April 2016
GWIJI WA SOKA BARANI AFRIKA NWANKWO KANU AFANYA EXCLUSIVE INTERVIEW NDANI YA EFM REDIO
Slider

Mchezaji wa zamani wa kimataifa wa Nigeria na club za Ajax, Inter Milan, Arsernal, na Portsmouth Nwankwo Kanu ambaye pia ni balozi wa Startimes akiwa katika kituo cha EFM REDIO kwa ajili ya kufanya mahojiano ya moja kwa moja katika kipindi cha SportsHeadquarters. Mtaalamu huyo wa mpira wa miguu akizungumza jambo katika studio za EFM redio Nwankwo Kanu akiwa katika mahojiano studio za EFM redio kwenye kipindi cha sports headquarters. Watangazaji wa sports headquarters katika picha ya pamoja na Nwankwo...

Like
1179
0
Thursday, 07 April 2016