Sports

FIFA KUPANGA TAREHE YA UCHAGUZI WA RAIS
Global News

RAIS wa shirikisho la soka duniani FIFA Sepp Blatter na bodi ya utawala ya shirikisho hilo pamoja na viongozi wengine wa juu wa shirikisho hilo wanakutana leo kupanga tarehe ya uchaguzi wa rais wa shirikisho hilo. Blatter alitangaza mwezi uliopita kuwa atajiuzulu kama rais wa FIFA baada ya wiki ya tuhuma za ufisadi kwa baadhi ya viongozi wa shirikisho hilo. Mkutano huo wa leo pia unatarajia kutaja baadhi ya mambo yatakayorekebishwa ikiwa ni pamoja na kikomo cha urais na viongozi...

Like
197
0
Monday, 20 July 2015
LIVERPOOL YAKUBALI KUMSAJILI BENTEKE
Slider

Liverpool imekubali kumsajili mshambuliaji Christian Benteke kutoka kwa wapinzani wao kwenye Premier League klabu ya Aston Villa kwa kitita cha pound milioni 32.5. Mchezaji huyo wa kimataifa kutoka Ubelgiji  mwenye miaka 24 kwa sasa anafanyiwa vipimo na daktari wa klabu ya Liverpool. Benteke aliwasili Villa akitokea Genk kwa pound milioni 7 mwaka 2012 akiwa na rekodi ya magoli 49 katika michezo 101 na klabu ya Birmingham. Liverpool inamchukua nyota huyu akiwa amebakiza miaka miwili katika mkataba wake na...

Like
202
0
Monday, 20 July 2015
LEGENDARY WA URUGUAY ALCIDES EDGARDO GHIGGIA AFARIKI DUNIA
Slider

Mshambuliaji nguli wa Uruguay Alcides Edgardo Ghiggia ambaye ndiye aliyeifungia timu yake goli la ushindi dakika 10 kabla ya mchezo kwisha katika michuano ya kombe la Dunia mwaka 1950, amefariki dunia. Ghiggia mchezaji pekee aliyekuwa amesalia hai kati ya wachezaji wote wa kikosi cha kombe la dunia kilichoishinda Brazill mwaka 1950,ambapo dakika za lala salama zilizmuingiza katika historia ya kuipatia ushindi Uruguay. Mchezaji huyo amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 88 ambaye kifo chake kinatajwa kuwa ni pigo kubwa...

Like
228
0
Friday, 17 July 2015
FIFA KUZIFANYIA MAREKEBISHO KANUNI ZAKE
Slider

Shirikisho la soka ulimwenguni FIFA lina mpango wa kuzifanyia marekebisho kanuni zake ili kuzibana nchi zinazowania kuandaa Kombe la Dunia, zisitumie mwanya wa misaada ya kifedha kwa nchi nyingine kama rushwa. Kipengele kile kinachoziruhusu nchi zinazoshindania nafasi ya kuandaa Kombe la Dunia kusambaza pesa katika nchi nyingine huenda kikafutwa. Aidha FIFA inazitaka nchi zote zinazowania nafasi hiyo kuzingatia haki za binadamu na sheria za kazi wakati wote. Hivi sasa nchi zinazotupiwa jicho ni Urusi inayoandaa kombe la dunia mwaka 2018...

Like
180
0
Friday, 17 July 2015
SUNDERLAND YAMNYAKUA YOUNES KABOUL
Slider

Klabu ya soka ya Sunderland  imemsajili mchezaji wa Ufaransa Younes Kaboul kutoka Tottenham, klabu hiyo ya Uingereza ilitoa taarifa hiyo siku ya jumatano. Akizungumza mara baada ya kutangazwa rasmi kujiunga na klabu hiyo Kaboul amesema amefurahi kujiunga na ametoa shukrani zake kwa uongozi mzima akiwemo mwalimu wa Sunderland kwakufanya maamuzi sahihi ya...

Like
192
0
Friday, 17 July 2015
VICTOR VALDES KUUZWA KWA UTOVU WA NIDHAMU
Slider

Meneja wa klabu ya Manchester United Louis van Gaal ametangaza uamuzi wake wa kumuuza mlinda mlango Victor Valdes huku sababu ya msingi ikiwa ni utovu wa nidhamu. Hatua hiyo inakuja baada ya mlinda mlango huyo kukataa kucheza kwenye kikosi cha pili ndani ya Manchester United. Van Gaal amesema mlinda mlango huyo wa zamani wa klabu ya Barcelona ambae alimwaga wino mwezi wa kwanza atakutana utakuwa ni mwisho wake kuitumikia klabu hiyo baada ya kushindwa kufuata filosofia za meneja huyo “kama...

Like
178
0
Thursday, 16 July 2015
CLASICO ZA UHISPANIA KUTIMUA VUMBI NOVEMBA, APRIL
Slider

Ligi mpya ya kabumbu itang’oa nanga wikendi ya Agosti 23, na mechi kali za “clasico” kati ya Real Madrid na Barcelona zitachezwa Novemba na Aprili, shirikisho la soka nchini humo lilisema Jumanne. Mechi hizo kati ya mahasimu hao wa jadi zitachezwa Novemba 8 mjini Madrid na Aprili 3 mjini Barcelona, Shirikisho la Soka la Uhispania lilisema baada ya droo kufanywa makao makuu ya shirikisho hilo. Mabingwa wa ligi Barcelona watakuwa wakipigania kuhifadhi mataji ya Ligi ya Uhispania, Kikombe cha Ligi...

Like
254
0
Thursday, 16 July 2015
RONALDINHO AREJEA BRAZIL KUITUMIKIA FLUMINENSE
Slider

Aliyewahi kuwa mchezaji bora wa dunia kupitia timu ya taifa ya Brazil huyu ni Ronaldinho hatimae amerudi nyumbani  na kuingia mkataba wa kuitumikia timu ya Fluminense huko Rio de Janeiro nchini Brazil. Picha ya mchezaji huyu akiwa na jezi ya timu hiyo ilipostiwa kwenye mtandao wa Twitter kupitia akaunti ya klabu hiyo mapema mwishoni mwa wiki pindi alipokubali kuungana na Fred aliyewahi kuwa mchezaji mwenzake kutoka Brazil Baadae Ronaldinho alitweet kuelezea furaha yake kurudi nyumbani na kuitumikia timu...

Like
150
0
Tuesday, 14 July 2015
KAGAME CUP VIWANJA KUWAKA MOTO
Slider

Michuano ya klabu bingwa Afrika Mashariki na Kati jumamosi wiki hii inaanza kutimua vumbi mjini Dar es Salaam Tanzania huku jumla ya vilabu 13 vikishiriki. Rais wa Rwanda Paul Kagame anatarajiwa kutoa kiasi cha dola elfu 60 za marekani kama zawadi kwa washindi. Kundi A itajumuisha timu za Yanga yaTanzania, Gor Mahia ya Kenya, Kmkm Zanzibar, Telecom ya Djibout na Khartoum- Sudani Kaskazini. Kundi B – APR Rwanda, Al Shandy ya Sudan, LLB FC Burundi naHeegan Somalia. Wakati kundi C...

Like
129
0
Tuesday, 14 July 2015
SIMBA ACHENI VITA NA SINGANO, ELEKEZENI NGUVU KUIANDAA TIMU IBEBE MATAJI
Slider

Na Omary Katanga. Mzozo kati ya klabu ya Simba na mchezaji Ramadhani Singano “Messi” ndiyo habari iliyochukua nafasi kubwa kwenye vyombo vya habari kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa,huku kila upande ukidai kuwa na haki katika kile inachokiamini. Hebu nikukumbushe kidogo mzozo huu ulipoanza,siku chache kabla ya dirisha la usajili kufunguliwa klabu ya Simba ilianza kupekuwa mikataba ya wachezaji wake kujua ni yupi mkataba wake umekwisha na yupi bado,ndipo jicho la upekuzi wao likanasa kwa mchezaji Ramadhani Saingano. Hapo wakagundua...

Like
279
0
Monday, 13 July 2015
SCHWEINSTEIGER ATHIBITISHA KUHAMIA UNITED
Slider

Bastian Schweinsteiger alithibitisha Jumapili kwamba ataondoka na Bayern Munich na kujiunga na Manchester United, ikitegemea matokeo ya uchunguzi wa afya yake, licha ya kwamba mabingwa hao wa Ujerumani wamepoteza mechi mbili zao za kwanza za kabla ya msimu wakicheza bila yeye. Bayern walitangaza Jumamosi kwamba walikuwa wameafikiana kuhusu bei ya mchezaji huyo mwenye miaka 30, ambaye atafikisha kikomo kipindi chake cha miaka 17 katika klabu hiyo na kutia saini mkataba wa miaka mitatu na klabu hiyo ya Uingereza. Kiungo huyo wa...

Like
167
0
Monday, 13 July 2015