Category: Sports

  • BAADA YA CAF KUITAKA MTIBWA ILIPE DOLA 15,000, UONGOZI WAKE WASEMA HAWAKO TAYARI KULIPA

    BAADA YA CAF KUITAKA MTIBWA ILIPE DOLA 15,000, UONGOZI WAKE WASEMA HAWAKO TAYARI KULIPA

    Shirikisho la soka nchini (TFF), kupitia kwa Katibu mkuu wake Kidao Wilfred leo wameweka wazi kuwa, wanalishughulikia suala la faini waliyopigwa Mtibwa Sugar na CAF na watahakikisha timu hiyo inashiriki michuano ya Kombe la Shirikisho barani Africa.

    Akizungumza na wanahabari leo, Kidao amesema suala la Mtibwa Sugar na faini waliyopigwa na CAF mwaka 2003 ya dola za Kimarekani 15000, wanalifanyia kazi na watajitahidi kuhakikisha faini hiyo inalipwa kabla ya Julai 20 ili timu hiyo iweze kushiriki.

    Mwaka 2003, Mtibwa Sugar ilipigwa faini na CAF pamoja na kufungiwa kutoshiriki michuano yoyote inayosimamiwa na shirikisho hilo kwa misimu miwili, kutokana na kushindwa kwenda kucheza mechi ya marudiano dhidi ya Santos FC ya Afrika Kusini katika mchezo wa Kombe la Shirikisho Afrika. Katika mchezo wa kwanza hapa nyumbani Mtibwa Sugar ilifungwa mabao 3-0.

    Hata hivyo kwa mujibu wa uongozi wa Mtibwa Sugar wao wanadai wameshalipa faini hiyo, kipindi ambacho Shirikisho la soka lilikuwa linaitwa FAT. Kidao amesema wao kama TFF hawajaziona rekodi hivyo itawalazimu kuwasiliana na CAF ili kujua kama faini hiyo ililipwa.

     

  • Rooney Atimka Everton, Akimbilia Marekani

    Rooney Atimka Everton, Akimbilia Marekani

    Aliyekuwa mshambuliaji wa Everton, Wayne Rooney (32) amesaini kandarasi ya miaka mitatu na nusu kuitumikia Klabu ya DC United inayoshiriki Ligi Kuu ya nchini Marekani.

    Rooney ambaye atakamilisha uhamisho wake huo wakati dirisha la usajili litakapofunguliwa Julai 10 mwaka huu, atalipwa mkwanja kiasi cha Pauini Milioni 10 (sawa na Tsh. Bilioni 26.47) ambapo atakuwa ni mchezaji mwenye kulipwa pesa ndefu zaidi nchini Marekani.

    Rooney ambaye anashikilia rekodi ya mfungaji Bora wa muda wote wa Manchester United na Uingereza amekatisha mkataba wake wa miaka miwili aliosaini mwaka jana kuitumikia Everton..

    Staa huyo ambaye pia ni mfungaji Bora wa Pili wa Ligi Kuu ya Uingereza akiwa na mabao 208 nyuma ya kinara Alan Shearer aliyekuwa na mabao 260, anatengengeneza rekodi nyingine ya kuungana na mastaa kibao wa soka waliowahi kutoka Uingereza na kwenda kucheza soka la kulipwa Marenaki.

    Miongoni mwao ni David Beckham, Thierry Henry, David Villa, Steven Gerrard, Didier Drogba, Andrea Pirlo Zlatan na Ibrahimovic.

     

  • Ratiba ya 16 Bora Kombe la Dunia  2018

    Ratiba ya 16 Bora Kombe la Dunia 2018

    Alhamisi ya June 28 tumeshuhudia michuano ya Kombe la Dunia 2018 hatua ya makundi ikimalizika kwa Afrika kupoteza timu zote 5 katika hatua ya makundi kutokana na kukosa point za kutosha kuingia hatua ya 16 bora.

    Katika hatua hiyo ya makundi timu zote 5 za Afrika zimeyaaga mashindanl hayo kutokana na kukosa alama za kuwavusha kwenye hatua hiyo ya makundi.

    Timu 16 zilizofuzu hatua ya 16 bora ni Ubelgiji, England, Argentina, Colombia, Japan, Croatia, Hispania na Ureno.

    Nyingine ni Brazil, Switzerland, Mexico, Ufaransa, Uruguay, Urusi, Denmark na Sweden, hatua hiyo ya 16 bora itaanza kesho Jumamosi ya June 30 na kufikia tamati Jumanne ya July 03.

    Hii hapa ratiba kamili ya 16 bora

    Jumamosi ya June 30-2018
    Uruguay vs Portugal saa 21:00 jioni

    France vs Argentina saa 17:00 usiku

    Jumapili ya July 01-2018
    Span vs Russia saa 17:00 jioni

    Croatia vs Denmark saa 21:00 usiku

    Jumatatu ya July 02-2018
    Brazil vs Mexico saa 17:00 jioni

    Belgium vs Japan saa 21:00 usiku

    Jumanne ya July 03-2018
    Sweden vs Switzerland saa 17:00 jioni

    Colombia vs England saa 21:00

  • Filimbi ya Kagame Cup Kuanza Kupulizwa Leo

    Filimbi ya Kagame Cup Kuanza Kupulizwa Leo

    Kikosi cha JKU
    Kikosi cha Vipers SC
    Kikosi cha Azam FC
    Kikosi cha Kator FC
    Kikosi cha Singida United
    Kikosi cha APR FC

    Michuano ya Kagame Cup inaanza rasmi leo kwa mechi tatu kupigwa ambapo saa 8 mchana JKU ya Zanzibari itaanza kibarua chake dhidi ya Vipers SC kutoka Uganda.

    Baadaye saa 10 mechi ya rasmi ya ufunguzi itakuwa baina ya mabingwa watetezi, Azam FC dhidi ya Kator FC kutoka Sudan Kusini. Baada ya mechi hiyo majira ya saa 1 jioni, Singida United itacheza na APR ya Rwanda.

    Tutarajie nini kwenye Mashindano haya ??

  • UONGOZI GOR MAHIA WAJA JUU KUHUSIANA NA KAGERE, WAELEZA ALIDANGANYA

    UONGOZI GOR MAHIA WAJA JUU KUHUSIANA NA KAGERE, WAELEZA ALIDANGANYA

    Imeelezwa uongozi wa Gor Mahia FC umeshangazwa na kitendo cha mshambuliaji wao tegemeo, Meddie Kagere kujiunga na klabu ya Simba kwa kusaini mkataba wa miaka miwili.
    Wakati Kagere akiwa nchini Kenya ikiwa ni wiki kadhaa zimepita baada ya mashindano ya SportPesa Super Cup kumalizika, aliomba ruhusa kuelekea kwao Rwanda kwa ajili ya masuala yake binafsi.
    Lakini kilichokuja kuwashangaza ni Kagere kuchukua ndege ya kuelekea jijini Dar es Salaam akiwa na wakala wake kwa ajili ya kuja kufanya mazungumzo na Simba kisha kusaini mkataba wa miaka miwili.
    Kitendo hicho kimewaumiza Gor Mahia na kuona kama Kagere ni msaliti wakati walikuwa kwenye mazungumzo naye ya kuongeza mkataba mwingine baada ya ule aliokuwa anao ndani ya klabu hiyo kumalizika.
    Aidha, imeelezwa viongozi wa Gor Mahia wameshangazwa na Kagere kushindwa kuwaeleza hali halisi kuwa alikuwa anataka kusafiri kuelekea Tanzania na badala yake alidanganya kuwa anaenda kwao Rwanda.
    Tayari Kagere ni mali ya Simba na anatarajiwa kuwa sehemu ya kikosi hicho katika michuano ya KAGAME inayotaraji kuanza Jun
  • Ujeruman Yaendeleza Record ya Bingwa Mtetezi Kutolewa Htaua ya Makundi

    Ujeruman Yaendeleza Record ya Bingwa Mtetezi Kutolewa Htaua ya Makundi

    Imekuwa kawaida kwa bingwa wa Kombe la Dunia kutolewa hatua ya makundi, lakini hakuna aliyetegemea hilo lingetokea kwa Ujerumani.

    Ujerumani haikuwahi kutolewa katika hatua ya makundi katika miaka 80 iliyopita.

    Korea Kusini wameilaza kwa mabao 2-0 na kuitupa nje katika Kombe la Dunia katika hatua ya makundi. Maana yake wameivua ubingwa.

    Kipigo hicho kimezua hofu kubwa kwa mashabiki wa timu hiyo ya taifa na huo ndiyo ukweli usiopingika.

     

    1998: France alikuwa bingwa

    2002: France alitoka hatua ya makundi

    2006: Italy alikuwa bingwa

    2010: Italy alitoka hatua ya makundi

    2010: Spain alikuwa bingwa

    2014: Spain alitoka hatua ya makundi

     

    Kwa nini Mabingwa wa kombe la Dunia hutolewa hatua ya Makundi tena kwa kufungwa na Timu dhaifu kabisa ??

  • NI VITA KOMBE LA DUNIA,  URENO VS URUGUAY HUKU SPAIN WAKIKIPIGA NA URUSI

    NI VITA KOMBE LA DUNIA, URENO VS URUGUAY HUKU SPAIN WAKIKIPIGA NA URUSI

    Baada ya kwenda sare ya bao 1-1 na Iran usiku wa jana, timu ya taifa ya Ureno sasa itakutana na Uruguay katika mchezo unaofuata ya 16 bora kwenye michuano ya Kombe la Dunia nchini Urusi.

    Mchezo huo ulimazika kwa sare hiyo huku nyota na nahodha wa Ureno, Cristiano Ronaldo akikosa penati ambayo ingeweza kuiongezea alama timu yake.

    Uruguay anayoichezea nyota Luis Suarez sasa itakuwa inakipiga na Ureno baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Urusi.

    Wakati huo Spain iliyokwenda sare ya mabao 2-2 na Morocco itakuwa inakipiga dhidi ya Russia iliyopokea kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa Uruguay.

    Mechi hizo za mkondo wa hatua ya 16 bora zitaanza kuwaka moto Juni 30 kwa mujibu wa ratiba ya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).

  • Brazili Yaitandika Costa Rica Dakika zanyongeza

    Brazili Yaitandika Costa Rica Dakika zanyongeza

    Kikosi cha timu ya taifa ya Brazil kimesafisha makosa yake iliyoyaonyesha katika mchezo wa kwanza dhidi ya Switzerland kwa kuibuka na ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Costa Rica leo.

    Mabao ya Brazil yamewekwa kimiani katika dakika za nyongeza kuelekea mchezo kumalizika kupitia kwa Philippe Countinho na Neymar Jr.

    Ushindi huo umemfanya Neymar ashindwe kuamini matokeo hayo baada ya kumwaga machozi ya furaha baada ya kufunga bao la pili.

    Katika kundi E Brazil imeongoza kwa kuwa na alama 4 ikifuatiwa na Serbia yenye 3 huku Uswizi ikiwa na 1 na Costa Rica wakiwa na 0.

    Matokeo hayo yamefuta kiu ya Wabrazil wengi ambao waliponda namna timu yao ilivyocheza mchezo wa kwanza dhidi ya Uswizi.

  • APR ya Rwanda Yaomba Kubadiishiwa Ratiba Mashindano ya Kagame CUP

    APR ya Rwanda Yaomba Kubadiishiwa Ratiba Mashindano ya Kagame CUP

    Baada ya kuthibitisha rasmi kuwa watashiriki michuano ya KAGAME CUP inayotaraji kuanza Juni 28 2018, uongozi wa klabu ya APR umeomba kubalidishwa ratiba.

    Hatua hii imekuja mara baada ya CECAFA kuwapangia APR kucheza na Singida United Juni 29 itakayokuwa Ijumaa ya wiki lijalo.

    Taarifa kutoka Rwanda zinaeleza kuwa APR wamesema uchovu wa safari kwa wachezaji wao unaweza ukachangia wasioneshe kiwango kizuri hivyo ni vema wakapata muda kidogo wa kupumzika.

    Kutokana na tarehe 29 iliyopangwa, viongozi wa klabu hiyo wameomba iwe siku tofauti, ikiwezekana isogezwe mbele.

    Ikumbukwe APR walipewa mwaliko wa kushiriki mashindano haya kutokana na baadhi ya timu kujiondoa kwa madai ya kuwa hayakuwa yanaendana na ratiba.

    Tayari Singida nao wamethibitisha kupokea barua ya CECAFA jana na wamesema wako tayari kushiriki na wanaisubiri APR kwenye mchezo wao wa kwanza.

     

  • Hatima  ya Nigeria Kuvuka Hatua ya  Makundi  Kujulikana Leo Dhidi ya Iceland

    Hatima ya Nigeria Kuvuka Hatua ya Makundi Kujulikana Leo Dhidi ya Iceland

    Michuano ya Kombe la Dunia huko Urusi inaendelea kushika kasi tena ambapo Afrika itakuwa inawakilishwa na Nigeria itakayokuwa kibaruani dhidi ya Iceland.
    Matumaini pekee ya Nigeria kuendelea kusalia kwenye michuano hiyo yataonekana leo endapo itaibuka na ushindi wa mabao mengi huku ikitegemea matokeo ya mechi zingine zilizosalia.
    Timu hiyo ilipoteza mechi yake ya kwanza ilipocheza dhidi ya Croatia kwa kufungwa mabao 2-0.
    Msimamo kundi D unaonesha imeshikilia mkia namba 4 ikiwa haina alama yoyote huku Iceland na Argentina wakiwa na pointi moja kwa kila timu wakati Croatia wakiwa na 6.
    Mechi hii itaanza majira ya saa 12 kamili jioni huku mapema saa 9 Brazil wataanza kukipiga na Costa Rica na saa 3 usiku Serbia watakuwa wanacheza na Switzerland.
  • Kimahesabu Argentina Ishatoka kwenye Hatua ya Makundi Kombe la Dunia

    Kimahesabu Argentina Ishatoka kwenye Hatua ya Makundi Kombe la Dunia

    Kikosi cha timu ya taifa ya Argentina kimeshindwa kutamba mbele ya Croatia baada ya kukumbana na kichapo cha mabao 3-0.

    Mabao ya mchezo huo wa kundi D yaliwekwa kimiani na Luca Modric, Ivan Rakitic na Ante Rebic.

    Kufuatia kichapo hicho walichokipata Argentina kinawafanya wasalie na alama moja waliyoipata dhidi ya Iceland baada ya kwenda sare ya 1-1 wakiwa nafasi ya 3.

    Nyota wa timu hiyo, Lionel Messi alionekana kuwa na machungu kufuatia kichapo hicho ambacho ni kama dhamaha kubwa kwake.

    Messi ambaye amepewa nafasi kubwa zaidi ya kuisaidia Argentina ameshindwa kufunga bao lolote mpaka sasa katika michezo miwili ambayo timu hiyo imeshacheza.