Slider

WABUNGE WAWILI WA CHADEMA WASIMAMISHWA KUHUDHURIA VIKAO VYA BUNGE KUANZIA LEO
Local News

Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi amesimamishwa kuhudhuria vikao kumi vya bunge kuanzia leo June 30 mwaka huu baada ya kubainika kunyosha kidole cha kati kwa wabunge baada ya kukiri mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka kwamba alifanya kitendo hicho. Hata baada ya kuhojiwa Mbunge Mbilinyi alishindwa kumtaja Mbunge wa CCM aliyedaiwa kumtukana ili nae achukuliwe hatua na kamati hiyo. Bunge limeridhia adhabu hiyo iliyotolewa na kamati. Nae Mbunge wa Ubungo Chadema Saed Kubenea amesimamishwa kuhudhuria...

Like
388
0
Thursday, 30 June 2016
TUZO ZA OSCAR: BAADA YA KULAUMIWA SANA WAANDAJI WAJA NA MAAMUZI HAYA
Entertanment

Waandalizi wa tuzo za Oscar wametangaza kuwa wamewaalika wanachama wapya zaidi kupiga kura ya maamuzi ya washindi wa mwaka huu, baada ya malalamishi makubwa ya mwaka uliopita ambapo walilaumiwa kwa kuyabagua makundi mengine ya watu. Waandalizi hao wa The Academy of Motion Picture Arts and Sciences wanasema wamewaalika karibu watu 700, wakiwalenga hasa wanawake na watu kutoka jamii za watu wachache. Miongoni mwa wale ambao wamealikwa kushiriki katika uteuzi wa washindi wa tuzo hizo ni wacheza filamu weusi, na vilevile...

Like
253
0
Thursday, 30 June 2016
UINGEREZAYAZUIWA KUHUDHURIA MKUTANO WA EU
Global News

Uingereza imezuia kuhudhuria mkutano wa viongozi wa Jumuiya ya Ulaya ambapo itakuwa mara ya kwanza kufanyiwa hivyo kwa miaka 40. Waziri Mkuu, David Cameron, hatakuwa mezani wakati viongozi wengine 27 wa mataifa wanachama wa Jumuiya ya Ulaya watakuwa wakihudhuria mkutano usio rasmi juu ya hatma ya muungano huo baada ya kuondoka kwa Uingereza. Uingereza imeambiwa ianzishe mpango wake wa kuondoka katika jumuiya hiyo bila kuchelewa. Rais wa Jumuiya ya Ulaya, Jean-Claude Junker, amesema kuwa shughuli za kutegua kujiondoa kwa Uingereza...

Like
257
0
Wednesday, 29 June 2016
PROFESA ALIEMBEBA MTOTO WA MWANAFUNZI WAKATI WA MTIHANI AJIZOLEA UJIKO
Global News

Profesa mmoja wa chuo kikuu amesifiwa nchini Ivory Coast kwa kumbeba mtoto wa mmoja wa wanafunzi wake mgongoni wakati wa masomo. Picha za Honore Kahi wa chuo cha Bouake, zimesambaa pakubwa kwenye mitandao ya kijamii. Alisema aliamua kumsaidia mwanamke katika darasa lake wakati mtoto alianza kulia. Picha zilizochukuliwa na mwanafunzi mwingine zinamuonyesha, bwana Kahi akifunza huku mtoto akiwa...

Like
389
0
Wednesday, 29 June 2016
SUGE KNIGHT AMSHITAKI CRIS BROWN
Entertanment

Suge Knight anamshtaki mwanamuzki mwenza wa R& B Chris Brown mahakamani pamoja na mmiliki wa kilabu moja ya usiku nchini Marekani kufuatia ufyatulianaji wa risasi uliotokea katika kilabu hiyo mwaka 2014. Mwanamuziki huyo wa zamani alipigwa risasi mara saba katika hafla ya Chris Brown. Kesi hiyo iliowasilishwa katika mahakama ya Los Angeles inamshtaki Chris Brown na kilabu ya West Hollywood Ckub 1 Oak kwa kushindwa kuweka usalama wa kutosha na kumruhusu mtu mmoja aliyejihami kuingia katika kilabu hiyo. Suge Knight...

Like
337
0
Wednesday, 29 June 2016
KOREA KUSINI, JAPAN NA MAREKANI ZAFANYA ZOEZI LA KIJESHI
Global News

Korea Kusini, Marekani na Japan zimefanya zoezi la ushirikiano la kukabiliana na makombora katika maji ya jimbo la Hawaii. Hatua hiyo inajiri kufuatia msururu wa majiribio ya makombora ya masafa mafupi katika miezi ya hivi karibuni inayofanywa na Korea kaskazini. Majaribio mengi hatahivyo hayakufanikiwa lakini ufanisi wa kombora la sita hivi majuzi ulilishangaza eneo hilo. Korea Kaskazini ambayo imefanya majaribio manne ya mokombora ya kinuklia imesema kuwa zoezi hilo ni la uchokozi wa kijeshi. Vyombo vya habari vimesema kuwa Marekani...

Like
347
0
Wednesday, 29 June 2016
HIFADHI KUBWA ZAIDI YA GESI ILIYOTOWEKA DUNIANI YAGUNDULIWA TANZANIA
Local News

Tanzania ni miongoni mwa mataifa chache duniani yaliyojaliwa kuwa na rasilimali na madini mengi. Na baada ya kugunduliwa kwa gesi asili huko Mtwara na dhahabu sasa watafiti kutoka Uingereza wamegundua hifadhi kubwa zaidi duniani ya gesi adimu zaidi ya Helium nchini Tanzania. Watafiti kutoka chuo kikuu cha Oxford na kile cha Durham kwa ushirikiano na wataalumu wa madini kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya barafu kama inavyofahamika. Ugunduzi huo umefanyika katika eneo la...

Like
416
0
Tuesday, 28 June 2016
KOCHA WA UINGEREZA ROY HODGSON AJIUZULU
Slider

Saa chache tu baada ya timu ya kandanda ya Uingereza kubanduliwa nje ya mashindano ya mwaka huu ya Euro 2016, Kocha wa Uingereza Roy Hodgson amejiuzulu wadhfa wake. Hodgson alikuwa ameshuhudiwa uingereza ikiambulia kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Iceland katika mkumbo wa 16 bora huko ufransa. Kocha huyo mwenye umri wamiak 68 amekiongoza kikosi hicho cha Uingereza kwa miaka 4 sasa. Hodgson alichukuwa wadhfa huo kutoka kwa kocha muitaliano Fabio Capello aliyetimuliwa kufuatia matokeo duni. Hata hivyo kocha huyo...

Like
225
0
Tuesday, 28 June 2016
RAIS WA ARGENTINA AMSIHI MESSI ASIJIUZULU
Slider

Rais wa Argentina Mauricio Macri amemwita nyota wa soka wa nchi hiyo Lionel Messi kwa lengo la kumuomba atengue maamuzi yake ya kujiuzulu kucheza soka la kimataifa. Messi alifikia maamuzi hayo baada ya timu yake kushindwa kwa mara ya pili mfululizo katika fainali za Copa America huku akiwa miongoni mwa wachezaji waliokosa mikwaju ya penalti. ”Amemwita na kumueleza namna anavyoona fahari kwa kiwango kizuri kilichoonyeshwa na timu yake katika michuano hiyo huku akimtaka asisikilize maneno ya watu” alisema msemaji wa...

Like
211
0
Tuesday, 28 June 2016
VARDY AKUBALI KUMWAGA WINO NA KUITUMIKIA TENA LEICESTER
Slider

Mshambuliaji wa Uingereza na Leicester Jamie Vardy amekubali kuweka kandarasi mpya na viongozi wa ligi ya Uingereza Leicester. Leicester imesema kuwa mchezaji huyo wa miaka 29 ambaye mabao yake yameisaidia klabu hiyo kushinda taji la ligi ya Uingereza msimu uliopita ameongeza kandarasi yake hadi miake minne na klabu hiyo. ”Pande zote mbili zinatumai tangazo hilo litamaliza uvumi wa hivi karibuni kuhusu hatma ya Jamie”,taarifa ya klabu imesema. Vardy alitarajiwa kununuliwa na klabu ya Arsenal kwa kitita cha pauni milioni 20...

Like
281
0
Thursday, 23 June 2016
CHINA KUWATEMBEZA RAIA WAKE KWENYE VISIWA VYENYE UTATA
Global News

Uchina inasema kuwa itaanza kuwatembeza kwa meli raia wanaotaka kuzuru visiwa vinavyozozaniwa vilivyoko kusini mwa bahari ya China. Vyombo vya habari vya serikali vinasema kuwa miaka minne ijayo, ziara hizo zitakuwa zikitoka kisiwa cha Hainan kabla ya kuelekea katika kisiwa chengine cha Nansha na kisha Spratley. Mapema juma hili, kampuni kubwa ya meli, Cosco, ilitangaza kuwa itaanzisha ziara za meli katika visiwa vingine vilivyoko katika eneo la kusini mwa bahari ya China, Paracels. Kutokana na shughuli kadhaa za kijeshi na...

Like
297
0
Wednesday, 22 June 2016