KUWAIT YAMUONDOA BALOZI WAKE IRAN

KUWAIT YAMUONDOA BALOZI WAKE IRAN

Like
149
0
Tuesday, 05 January 2016
Global News

Kuwait imetangaza kwamba inamuondoa balozi wake kutoka Iran huku mvutano kuhusu kuuawa kwa mhubiri wa Saudi Arabia nchini Saudi Arabia ukizidi.

 

Ubalozi wa Saudi Arabia nchini Tehran ulivamiwa na kuchomwa moto na waandamanaji waliokuwa wakilalamikia kuuawa kwa mhubiri wa madhehebu ya Shia Sheikh Nimr al-Nimr na watu wengine 46 nchini Saudia Jumamosi.

 

Saudi Arabia ilivunja uhusiano na Iran baada ya tukio hilo, na washirika wake wa karibu Bahrain na Sudan wakafuata.

 

Comments are closed.