Man UTD Yachapwa 4-0. Van Gaal Alaumu Wachezaji Wake

Man UTD Yachapwa 4-0. Van Gaal Alaumu Wachezaji Wake

Like
370
0
Wednesday, 27 August 2014
Local News

Van GaalBaada ya kipigo cha magoli 4-0 dhidi ya timu yake,  Meneja wa klabu ya Man Utd Van Gaal amelia na kikosi chake ambacho jana usiku kiliendelea kupata matokeo mabaya tangu kuanza kwa msimu mpya wa soka huko nchini Uingereza Agosti 16.
Kocha Van Gaal amesema kikosi chake hakikucheza vizuri wakati wa mchezo wa michuano ya kombe la ligi dhidi ya klabu ya Milton Keynes Dons ambao waliibuka na ushindi wa mabao manne kwa sifuri na kuwatupa nje ya michuano hiyo mashetani wekundu.
Pia Van Gaal amesema makosa madogo madogo yaliyofanywa na wachezaji wake wa safu ya ulinzi yalitoa mwanya mkubwa kwa wapinzani wao kupata mabao kwa urahisi. Akiendelea kulalamika kocha huyo alisema hana budi kuwasilisha lawama zake kwa wachezaji aliokuwa amewapa jukumu la kucheza mechi ya jana usiku.

Comments are closed.