MCHUNGAJI AKATISHA HOTUBA YA TRUMP

MCHUNGAJI AKATISHA HOTUBA YA TRUMP

Like
291
0
Thursday, 15 September 2016
Slider

Mchungaji wa kanisa moja la watu weusi katika jimbo la Michigan, Marekani amemkatisha Donald Trump akihutubu alipoanza kumshutumu mpinzani wake Hillary Clinton.

Mchungaji Faith Green Timmons alimkatisha BwTrump alipomshutumu mgombea huyo wa chama cha Democratic kuhusu mikataba ya kibiashara duniani.

“Bw Trump, nilikualika hapa uje kutushukuru kwa juhudi ambazo tumefanya Flint, si kutoa hotuba ya kisiasa,” amesema pasta huyo wa kanisa la Bethel United Methodist.

“Aha, hilo ni jambo njema,” amemjibu mgombea huyo wa chama cha Republican huku akionekana kuanza kucheza na karatasi alizokuwa nazo jukwaani.

Bw Trump ameendelea na kuzungumzia kwa kifupi kuhusu kutatua matatizo ya maji safi Flint, lakini baadhi ya watu kwenye umati wakaanza kumzomea.

Comments are closed.