MWANZA: WANANCHI WATAHADHARISHWA JUU YA WEZI WANAOTUMIA BODABODA

MWANZA: WANANCHI WATAHADHARISHWA JUU YA WEZI WANAOTUMIA BODABODA

Like
259
0
Wednesday, 17 February 2016
Local News

MWENYEKITI wa chama cha waendesha pikipiki Mkoa wa Mwanza, Makoye Kayanda, amewatahadharisha wakazi wa jiji hilo kuwa makini wawapo barabarani ili kuepukana na vitendo vya ukwapuaji  mikoba na mabegi vinavyofanywa na baadhi ya wahalifu kwakutumia pikipiki maarufu Boda boda.

Kayanda ametoa tahadhari hiyo jijini Mwanza baada ya kupokea malalamiko ya kukithiri kwa vitendo hivyo vinavyofanywa na baadhi ya watu wanaojifanya waendesha pikipiki  jambo linalochafua taswira ya waendesha pikipiki wa Mwanza.

Comments are closed.