NEW ZEALAND WAPIGA KURA KUCHAGUA BENDERA YA TAIFA

NEW ZEALAND WAPIGA KURA KUCHAGUA BENDERA YA TAIFA

Like
188
0
Friday, 20 November 2015
Global News

RAIA nchini New Zealand leo wanapiga kura kuchagua bendera ya Taifa ambayo huenda ikachukua nafasi ya bendera ya sasa.

Kura hiyo ya maamuzi inapigwa kuanzia leo hadi Desemba 11 kupitia posta kuamua bendera moja kati ya tano zilizopendekezwa ambayo ni bora zaidi.

Waziri Mkuu wa nchi hiyo John Key amesema bendera ya sasa haiakisi hali halisi ya New Zealand na kuamini kuwa bendera hiyo inafanana na bendera ya Australia.

Comments are closed.