NIGERIA: MHUBIRI WA KIISLAM AHUKUMIWA KIFO

NIGERIA: MHUBIRI WA KIISLAM AHUKUMIWA KIFO

Like
191
0
Wednesday, 06 January 2016
Global News

MAHAKAMA moja ya Kiislamu nchini Nigeria imemhukumu kifo mhubiri anayetuhumiwa kukufuru kwa kumtukana Mtume  Muhammad.

 

Abdul Inyass amehukumiwa katika kikao cha faragha cha mahakama katika mji wa Kano, kaskazini mwa Nigeria.

 

Afisa wa mashtaka Lamido Abba Soron-Dinki ameliambia shirika la AFP kuwa Kikao hicho kimefanyika faraghani kuzuia “fujo kutoka kwa umma” sawa na ilivyoshuhudiwa wakati wa kikao cha awali.

Comments are closed.