RAIS MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA SPIKA WA BUNGE KUFUATIA KIFO CHA SPIKA MSTAAFU, SAMWEL SITTA

RAIS MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KWA SPIKA WA BUNGE KUFUATIA KIFO CHA SPIKA MSTAAFU, SAMWEL SITTA

Like
441
0
Monday, 07 November 2016
Slider

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa dokta John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Spika wa Bunge la Tanzania Mheshimiwa Job Ndugai kufuatia kifo cha Spika mstaafu na Mbunge Mstaafu wa Jimbo la Urambo mkoani Tabora
Samwel Sitta.
Samwel Sitta amefariki dunia usiku wa kuamkia leo katika hospitali ya Technical University of Munich nchini Ujeruman alikokuwa akipatiwa matibabu tangu mwezi uliopita.

Katika salamu hizo Rais Magufuli amesema amepokea kwa mshituko na masikitiko taarifa hizo na kwamba Taifa limempoteza mtu muhimu aliyetoa mchango mkubwa katika uongozi na maendeleo.

Comments are closed.