Tag: yanga

  • Yanga sc Kucheza na Timu ya Mchangani Leo

    Yanga sc Kucheza na Timu ya Mchangani Leo

    Baada ya siku takribani tano kupita tangu kikosi cha Yanga kiweke kambi mjini Morogoro, imeelezwa Kocha Mkuu, Mwinyi Zahera ameomba mechi moja kukipima kikosi chake.

    Taarifa kutoka Morogoro zinasema Zahera ameomba apatiwe timu moja ambayo haishiriki Ligi Kuu Bara ili aweze kukipima vizuri kikosi chake kabla ya kufikia hatua ya kucheza na timu za daraja la juu.

    Taarifa zinaeleza Yanga wametuma maombi kwa timu zaidi ya moja mjini humo na ambayo itakubali watakipiga nayo leo ikiwa ni sehemu ya maandalizi dhidi ya USM Alger.

    Ikumbukwe Yanga watakipiga na Alger Agosti 19 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, ukiwa ni mchezo wa mkondo wa pili wa Kombe la Shirikisho Afrika.

    Katika mechi ya mkondo wa kwanza, Yanga ililala kwa jumla ya mabao 4-0 jijini Algiers, Algeria ambapo sasa ipo mkiani kunako kundi D ikiwa na alama moja pekee.

  • BAADA YA MKWASA NA SANGA KUACHIA NGAZI, UONGOZI YANGA WATOA TAMKO JUU YA WATAKAORITHI NAFASI ZAO

    BAADA YA MKWASA NA SANGA KUACHIA NGAZI, UONGOZI YANGA WATOA TAMKO JUU YA WATAKAORITHI NAFASI ZAO

    Baada ya viongozi wa Yanga kuzidi kuachia ngazi akiwemo Kaimu Mwenyekiti wa klabu hiyo jana, Clement Sanga kutangaza kujiuzulu wadhifa wake, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Hussein Nyika, ameitisha kikao na wahabari leo.

    Nyika ameitisha kikao hicho kuzungumzia mustakabali mzima wa Yanga juu ya kujaza nafasi za viongozi wake walioachia ngazi namna utakavyokuwa.

    Ikumbukwe Yanga imekuwa haina Mwenyekiti kwa muda mrefu tangu kujiuzulu kwa Yusuf Manji akidai anahitaji kupumzika kutokana na kukabiliwa na majukumu mengi binafsi.

    Baada ya Manji, wajumbe kadhaa wa Kamati ya Utendaji akiwemo Salum Mkemi na Khalfan Hamis nao wameachia ngazi kutokana na kutokuwa na maelewano mazuri baina yao na uongozi wa juu wa klabu.

    Kutokana na kujizulu kwao, uongozi wa Yanga kupitia kwa Nyika utaeleza kiunagaubaga leo hatma ya nafasi zao ikiwemo suala la uchaguzi wa kujaza nafasi ya Mwenyikiti pamoja na ile ya Katibu Mkuu.

  • MAKAMU MWENYEKITI WA YANGA CLEMENT SANGA AJIUZULU NAFASI YAKE

    MAKAMU MWENYEKITI WA YANGA CLEMENT SANGA AJIUZULU NAFASI YAKE

    Makamu Mwenyekiti wa Yanga Clement  Sanga amejiuzulu nafasi yake katika klabu hiyo kuanzia leo hii.

    Amesisitiza kuendelea kuwa mwanachama na kuisaidia klabu ya Yanga katika kila hali.

    Kwa upande wa hela zinazozungumziwa za Milioni 240 za kutoka CAF, Sanga amesema Yanga imekuwa na changamoto nyingi sana katika upande wa fedha na wamekuwa wana madeni makubwa ambayo wanakatwa katika mapato ya mlangoni ikiwemo Deni la Ardhi na madeni mengine pia.