TYRESE: WAZUNGU NI WABAGUZI HAWATOPIGA WIMBO WANGU

TYRESE: WAZUNGU NI WABAGUZI HAWATOPIGA WIMBO WANGU

Like
298
0
Tuesday, 28 July 2015
Entertanment

Mkali wa r&b kutoka Marekani ambae pia ni muigizaji wa wa movie ya Fast and Furious Tyrese amevifungukia vyombo vya habari vinavyomilikiwa na watu weupe nchini humo kuwa na ubaguzi wa rangi.

 

Tyres amesema kuwa redio hizo zinapiga nyimbo za R&B/Soul ambazo zimeibwa na watu weupe tu lakini sio watu weusi ambao kimsingi ndio wanafanya vizuri kwenye chart za muziki huo akiwemo yeye mwenyewe ambae albamu yake imeshika namba moja kwenye chart za muziki wa R&B/Soul album.

 

Tyrese amefunguka kuwa hawezi kuupeleka wimbo wake wake mpya “Shame” kwenye vituo vya watu hao kwani hawatoucheza labda  angeimbwa na Justin Timberlake, Sam Smith ama Robin Thicke.

Comments are closed.