WAPIGA KURA ZAMBIA WACHAGUA VIONGOZI

WAPIGA KURA ZAMBIA WACHAGUA VIONGOZI

Like
254
0
Thursday, 11 August 2016
Slider

Wapiga kura nchini Zambia wameanza kufika katika vituo vya kupigia kura kushiriki uchaguzi wa urais na wabunge.

Kumekuwa na ushindani mkali na kipindi cha kampeni kilikumbwa na vurugu.

Ushindani mkubwa unatarajiwa kuwa kati ya Rais Edgar Lungu wa chama cha PF na mgombea wa upinzani wa chama cha UPND Hakainde Hichilema.

Kuna jumla ya wapiga kura 6.7 milioni waliojiandikisha kupiga kura.

Kwa mara ya kwanza, mgombea urais anatakiwa kupata asilimia 50 ya kura zitakazopigwa pamoja na kura moja zaidi ili kuepusha awamu ya pili ya uchaguzi.

Bw Lungu alishinda uchaguzi mkuu uliopita kwa kupata 48% ya kura.

Waangalizi wa uchaguzi huo wanasema suala ya kudorora kwa uchumi litakuwa muhimu katika uamuzi wa wapiga kura.

Kuporomoka kwa bei ya shaba nyekundi, tegemeo kuu la uchumi wa taifa hilo, kumesababisha kufungwa kwa migodi na maelfu ya watu kupoteza kazi.

Ukuaji wa uchumi umepungua kwa nusu na serikali ya nchi hiyo iliomba usaidizi wa kifedha kutoka kwa Shirika la Fedha Duniani (IMF).

Isitoshe, sawa na nchi nyingine za kusini mwa Afrika, Zambia imekumbwa na ukame mbaya zaidi katika kipindi cha miaka 35.

Edgar Lungu alishinda uchaguzi uliofanyika kufuatia kifo cha rais Michael Sata

Chama cha UPND (United Party for National Development) kimemtuhumu Rais Lungu kwa kusimamia “kusambaratika” kwa uchumi.

Comments are closed.