ZLATAN IBRAHIMOVIC AITWA NA KLABU YA UINGEREZA

ZLATAN IBRAHIMOVIC AITWA NA KLABU YA UINGEREZA

Like
271
0
Thursday, 26 May 2016
Slider

Aliyekuwa mshambuliaji wa klabu ya PSG nchini Ufaransa Zlatan Ibrahimovic amesema kuwa alipokea ombi la kujiunga na kilabu moja ya ligi ya Uingereza lakini akakataa kuthibitisha iwapo klabu hiyo ni Manchester United au la.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 34 yuko huru baada ya kuondoka PSG na amehusishwa na uhamisho wa United.

Alipoulizwa iwapo ombi hilo linatoka Old Trafford ,alisema :Wacha tuone kitakachofanyika.

Aliyekuwa kocha wa Chelsea Jose Mourinho anatarajiwa kutangazwa mkufunzi wa Manchester United na alifanya kazi na Ibrahimovic alipkuwa katika kilabu ya Inter Milan.

Comments are closed.