Tag: bbcswahili

  • Rangi ya ngozi yako yaweza kukupa uraia nchini Liberia

    Rangi ya ngozi yako yaweza kukupa uraia nchini Liberia

    Tony Hage ameishi Liberia kwa zaidi ya miaka hamsini.
    Na ndipo mahali alipo kutana na mke wake kisha kuanzisha biashara yake yenye mafanikio.
    Aliendelea kuishi Liberia katika kipindi ambacho raia wengi wa nchi hiyo wali kimbia ili kuepuka machafuko akilenga kuiona nchi anayoipenda ikipata mafanikio.
    Mpaka sasa bwana Hage si raia wa Liberia, amezuiwa kupata uraia wa kudumu wa nchi hiyo kwa sababu ya rangi ya ngozi yake na asili ya familia yake kutoka huko Lebanon.
    ‘Tutakuwa watumwa’
    Nchi ya Liberia iliyoko mashariki mwa Afrika, ilianzishwa kama makazi ya watumwa wanaorejea Afrika kutoka huko Marekani sehemu ambayo walikuwa wakinyanyasika.
    Lakini cha ajabu tangu ilipo tengenezwa katiba mpya kiliwekwa kipengele cha kutoa uraia kwa watu wenye asili ya Afrika tu na kutoa kizuizi kwa watu weupe.
    Miaka mingi baadae, rais mpya wa Liberia na mchezaji wa zamani wa mpira wa miguu George Weah anapingana na kipengele hicho na kusema ni kitu kisicho cha lazina lakini pia ni ubaguzi.
    Anaongeza kuwa ubaguzi wa rangi unaondoa kabisa tafsiri ya Liberia, neno ambalo linamaanisha uhuru.
    Msimamo huo wa Rais wa Liberia umezua tafrani katika maeneo mbali mbali ya nchi hiyo.
    “Watu weupe watawatawala wa Liberia weusi” mfanyabiashara Rufus amesema.

    Anaamini kuwa mpango wowote ule wa kutoa nafasi za uraia kwa watu tofauti na wenye asili ya Afrika utaharibu nafasi ya wa Liberia kuendeleza nchi yao.
    Pia anasema ni hatari kuruhusu watu wa nchi nyingine kuwa na umiliki wa mali huko Liberia.
    Bwana Oulagbo sio mtu pekee kuweka wazi hofu yake, kundi jipya la utetezi wa raia ‘Citizen’s Action Against Non-Negro Citizenship and Land Ownership’ limejipanga kupambana na mipango ya Rais.
    Kila nchi imejengwa kwa misingi maalumu, kama ukii shusha thamani misingi hiyo nchi lazima iyumbe, kiongozi wa kundi hilo Fubbi Henries ameiambia BBC.
    Anaongeza kuwa Bwana Weah anatakiwa kushughulikia sera sahihi kwa wa Liberia.
    “Tunahitaji kuweka biashara zetu sawa, sekta ya elimu na kilimo na si uraia au umiliki wa ardhi kwa watu weupe” amesema.
    Licha ya utajiri wake wa mali asili, linapo kuja swala la wastani wa mapato kwa kila mtu Liberia ni nchi ya 225 kati ya 228 ambapo kwa mwaka 2017 pekee mtu mmoja alipata dola za kimarekani 900 tu.
    Hata hivyo asilimia tatu ya pato la taifa la Liberia inatokana na wale wanaoishi nje ya nchi – na baadhi ya familia hutegemea fedha kutoka Marekani.
    Lakini Bwana Weah anashutumiwa kwa kutoitathimini vyema hali hiyo anasema liberia ina hali mbaya kiuchumi na yeye anakwenda kutatua hilo.
    Baada ya miaka mingi ya vita vya kiraia na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola mwaka 2014 ahadi za George Weah zimekuwa kama muziki masikioni mwa raia wa Liberia.
    Kubadilishwa kwa sheria sasa ni sawa na kumweka mtoto wa miaka miwili na mtu wa miaka 45 katika ulingo wa ngumi kuona kama wanaweza pigana kwa haki. Anasema Fubbi Henries kiongozi wa kundi la kiraia.
    Anasisitiza kuwa lazima mtoto wa miaka miwili ataonewa hivyo basi wa Liberia bado hawana nguvu hiyo.
    Usikizano
    Hofu ya watu kutoka mataifa mengine sio kitu kipya, jamii ya wa lebanoni wameizoe sasa.” Baadhi ya watu wanaweza chukulia hii kama kitisho, kwamba wageni wanakuja kuchukua fursa zetu lakini si hivyo, bwana Hage anaiambia BBC akiwa nyumbani kwake Monrovia.
    Hata hivyo kuna kipindi familia za Kilebanoni zilikuwa na biashara katika maeneo mengi ya nchi, na mpaka sasa wanamiliki baadhi ya hoteli na biashara kubwa katika nchi hiyo lakini hii isiwatie hofu majirani zetu wazaliwa wa Liberia.

    Hage anaamini kuwa kama pendekezo la Rais litapia, hii itafungua njia ya ushirikiano zaidi. Sasa anasherekea sikukuu yake ya kuzaliwa ya 15 akiwa ndani ya Liberia, na haja wahi kujuta kuishi Liberia.
    “Nina furaha si kwa sababu sina uraia wa Liberia, ninafuraha kwa sababu Rais Weah anatazamia mwelekeo wa nchi hii”

  • Miguna atarajiwa kuwasili Nairobi Jumatatu

    Miguna atarajiwa kuwasili Nairobi Jumatatu

    Miguna

    Wakili na mwanaharakati mzaliwa wa Kenya ambaye alilazimishwa kwenda uhamishoni nchini Canada mwezi Februari mwaka huu alitarajiwa kurejea mjini Nairobi siku ya Jumatatu Machi 26, 2018 huku kukiwa na wasiwasi kwamba huenda asiruhusiwe na serikali ya Kenya kuingia nchini.
    Katika taarifa aliyoituma kwa idhaa ya Kiswahili ya Sauti ya Amerika siku ya Jumapili akiwa mjini London Uingereza, Miguna Miguna alisema kuwa ataingia Kenya hata bila pasipoti au viza kumruhusu kufanya hivyo.

    “Ndege yetu itatua Nairobi Jumatatu saa nane na dakika kumi na tano alasiri,” alisema Miguna.

    Wakati wa kuchapisha ripoti hii, serikali ya Kenya haikuwa imetekeleza maagizo ya mahakama kuu, kuitaka imrejeshee hati yake ya kusafiria.

    Miguna, ambaye amejitangaza kuwa kiongozi wa vuguvugu la National Resistance Movement (NRM- Kenya), amekuwa akiishi uhamishoni tangu maafisa wa polisi walipomlazimisha kuabiri ndege katika uwanja wa kimataifa wa Jomo Kenyatta mjini Nairobi mapema mwezi Februari, kwa madai kwamba yeye si raia wa Kenya.

    Mapema mwezi Februari, serikali ya Kenya iliwasilisha hoja mahakamani na kudai kuwa Miguna aliukana rasmi uraia wake na kwa hivyo hastaili kudai kuwa Mkenya.

    Lakini mwanasiasa huyo mwenye utata ameshikilia kwamba katiba ya Kenya inaeleza bayana kuwa mtu aliyezaliwa katika nchi hiyo hawezi kupoteza uraia wake.

    Akizungumza na Sauti ya Amerika kwa njia ya simu siku ya Jumapili kabla ya kuabiri ndege mjini London akiwa njiani kwelekea Kenya, Miguna alisema hakuna mtu yeyote aliye na nguvu kuliko amri ya mahakama, na kupuzilia mbali kauli zilizokuwa zikitolewa kwamba huenda seriakli isimruhusu kuingia nchini Kenya, licha ya mahakama kuamuru asizuiliwe kuingia na kwamba arejeshewe hati yake ya kusafiria.

    “Ninasafiri na pasipoti yangu ya Canada kwa sababu mahakama iliamuru iwapo watakataa kurudisha cheti cha kusafiria, nina uhuru wa kutumia pasipoti ya Canada kusafiria. Nitaenda huko na sitaomba viza kwa sababu mahakama ilisema hivyo,” alisema Miguna.

    Serikali ya Kenya haijatoa kauli yoyote hadharani kuhusu kurudi kwa mwanasiasa huyo ambaye aliwania nafasi ya gavana wa Nairobi kwenye uchaguzi wa mwaka jana.

    Safari yake inajiri chini ya wiki tatu baada ya rais wa nchi hiyo Uhuru Kenyatta Kukutana na kiongozi wa upinzani Raila Odinga na kukubaliana kushirikiana pamoja kutafuta uwianio wa kitaifa.

    Miguna alikuwa amekamatwa na kuzuiliwa na polisi kwa takriban siku tano kwa tuhuma kwamba alitoa kiapo – kinyume na sheria – kwa kiongozi wa upinzani, Raila Odinga, mbali na kuwa mwanachama wa vuguvugu la NRM lililopigwa marufuku.

    Lakini licha ya mahakama moja mjini Nairobi kumtaka afikishwe mbele ya jaji, polisi walimuwasilisha mbele ya hakimu katika mji ulio mbali na mji mkuu wa Kenya, na baadaye wakampeleka moja kwa moja hadi kwenye uwanja wa ndege, na kuwondosha nchini.

    Tangu wakati huo, Miguna amekuwa akishiriki mahojiano na vyombo mbalimbali vya habari na kufanya mikutano na Wakenya wanaoishi nje ya nchi, ikiwa ni pamoja na kutembelea miji kadhaa ya Canada, Marekani na Uingereza.

    Tangu Miguna aondoke nchini, mgawanyiko mkubwa ndani ya muungano wa National Alliance Super Alliance (NASA) umejidhihirisha huku baadhi ya vinara wakuu wakisema kuwa Odinga aliwasaliti na kuashiria kwamba huenda muungano huo unaelekea kusambaratika.

    Moses Wetangula, ambaye ni mmoja wa vinara wanne wa muungano huo, alisema yafuatayo siku ya Jumamosi: “Kile walizungumza, hakutuambia. Kile alipewa hakutuambia.”

    Wetangula tayari amevuliwa madaraka ya kiongozi wa walio wachache kwenye seneti ya Kenya, na wadhifa huo ukachukuliwa na wakili wa chama cha Raila Odinga, ODM, ambaye pia ni seneta wa kaunti ya Siaya, James Orengo.

    “Wanachama wa NRM wako tayari kuhakikisha kwamba hakuna shughuli zitakazoendelea katika mji wa Nairobi hadi pale wanyanyasaji wa raia walionykua madaraka kwa nguvu waachie mamlaka na kukubali kufanyika kwa uchaguzi huru na wa haki nchini Kenya,” Miguna aliuambia mkutano aliohutubia mjini London siku ya Ijumaa.

    Hata hivyo, baadhi ya wachambuzi wa masuala ya sisasa wanasema hata ikiwa Miguna Miguna hatazuiliwa kuingia nchini Kenya, huenda ikawa vigumu kwake kutimiza malengo ya vuguvugu la NRM, hususan kufuatia mabadiliko makubwa ya Kisiasa yaliyotokea tangu aende uhamishoni.

    Tayari Miguna amemkosoa vikali Raila Odinga kwa kukubali kushirikiana na rais Kenyatta huku akidai kwamba itakuwa vigumu mno kwa masuala waliokuwa wakipigania kama upinzani kutekelezwa.

  • Watu 37 wafariki katika mkasa wa moto jumba la Kemerovo, Urusi

    Watu 37 wafariki katika mkasa wa moto jumba la Kemerovo, Urusi

    Kemerovo

    Watu 37 wamethibitishwa kufariki baada ya moto kuzuka katika jumba moja kubwa la kibiashara katika mji maarufu kwa uchimbaji wa mkaa wa mawe wa Kemerovo, eneo la Siberia nchini urusi.
    Watu zaidi ya 64 hawajulikani walipo, wakiwemo watoto 41.
    Baadhi ya maeneo ya jumba hilo kubwa yanadaiwa kuwa kwenye hatari ya kuporomoka.
    Moto huo ulianza katika ghorofa ya juu katika jumba Winter Cherry.
    Inadaiwa wengi wa waliofariki walikuwa kwenye kumbi za sinema.
    Video zilizopakiwa mitandao ya kijamii zinawaonesha watu wakiruka nje kupitia madirisha kujaribu kujinusuru kutoka kwa moto huo uliozuka Jumapili.
    Wazima moto zaidi ya 660 wametumwa kusaidia juhudi za uokoaji.
    Chanzo cha moto huo hakijabainika lakini maafisa wameanzisha uchunguzi.
    Kemerovo, ni eneo maarufu sana kwa uchimbaji wa mkaa wa mawe.
    Ni mji unaopatikana takriban kilomita 3,600 mashariki mwa mji mkuu Moscow.
    Kansela wa Austria Sebastian Kurz ametuma salamu zake za rambirambi kwa jamaa na marafiki wa waathiriwa, sawa na Waziri wa mambo ya nje wa Latvia Edgars Rinkēvičs.

  • Ahed Tamimi: Binti Mpalestina aliyemzaba kofi mwanajeshi wa Israel afungwa jela

    Ahed Tamimi: Binti Mpalestina aliyemzaba kofi mwanajeshi wa Israel afungwa jela

    Binti mmoja wa Kipalestina aliyekamatwa baada ya kumchapa kofi mwanajeshi, Msichana huyo Ahed Tamimi alikiri kuwa na hatia kwa makosa manne aliyokuwa akishtakiwa kati ya 12 yaliyokuwa yakimkabili, ikiwemo shambulio la mwili, wakili wake ameeleza.


    Kadhalika, atalipa faini ya shekeli 5,000 sawa na dola 1,440 .
    Binti huyo mwenye miaka 17 alikamatwa baada ya kunaswa kwenye picha ya video akiwakabili wanajeshi wawili nje ya nyumba yake mwezi Desemba.
    Uamuzi wa mahakama unamaanisha kuwa ataachiwa huru kipindi cha majira ya joto kwa sababu hukumu yake imehesabu siku alizokaa korokoroni, mwanasheria wake Gaby Lasky amenukuliwa na shirika la habari la AFP.eshi wa Israel amekiri kosa na atatumikia kifungo cha miezi minane gerezani kufuatia maafikiano kati yake na upande wa mashtaka.