Tag: zimbabwe

  • Uchaguzi Zimbabwe: Ghasia zazuka kati ya upinzani na maafisa wa usalama

    Uchaguzi Zimbabwe: Ghasia zazuka kati ya upinzani na maafisa wa usalama

    Ghasia zimezuka nchini Zimbabwe kati ya wafuasi wa upinzani na vikosi vya
    usalama katika mji mkuu wa Zimbabwe huku kukiwa na maandamano dhidi
    ya kucheleweshwa kwa matokeo ya uchaguzi
    Magari yaliobeba maji ya kuwatawanya waandamanaji na vitoa machozi
    yalitumiwa katika barabara muhimu za mji wa Harare baada ya wafuasi wa
    chama cha upinzani cha MDC Alliance kuweka vizuizi katikati ya mji huo.
    Mtu mmoja aliyekuwa miongoni mwa waandamanaji ameuawa kwa kupigwa
    risasi na polisi. Muungano wa Ulaya umeonyesha wasiwasi wake kuhusu
    kucheleweshwa kwa matokeo.
    Maandamano hayo ya wafuasi wa chama cha upizani cha MDC mjini Harare
    yalibadilika na kuwa mabaya nyakati za mchana.
    Makundi ya waandamanaji yalikuwa katikati ya mji huo tangu alfajiri lakini
    habari zilipozuka kwamba Zanu Pf imeshinda viti vingi katika bunge na
    kwamba matokeo ya urais hayakuwa tayari , hali ilibadilika.
    Walifanya maandamano katika barabara muhimu mjini Harare na kuelekea
    katika ofisi za zamani za chama cha Zanu Pf wakibeba mawe makubwa , fimbo
    na chochote kila ambacho wangeweza kubeba.
    Kundi hilo lilisema 'tunamtaka Chamisa', wanaamini kwamba uchaguzi huo
    umekumbwa na udanganyifu na sasa wanataka mgombea wa MDC
    kutangazwa mshindi.
    Matokeo yanaonyesha kwamba Zanu-PF inashinda viti vingi vya ubunge
    katika uchaguzi huo tangu kung'atuliwa madarakani kwa Robert Mugabe
    Matokeo ya kura ya urais yanatarajiwa baadaye siku ya Jumatano.
    Mapema , chama cha upinzani cha MDC Alliance kilikuwa kimesema kwamba
    kura hiyo ilifanyiwa udanganyifu na kwamba mgombea wake Nelson Chamisa
    alikuwa ameibuka mshindi.

    Tume ya uchaguzi nchini Zimbabwe Zec imetangaza kwamba Zanu Pf kufikia
    sasa imejishindia viti 110 huku MDC ikijipatia viti 41 kulingana na chombo
    cha habari cha ZBC.
    Kuna viti 210 katika bunge la taifa hilo.
    Uchaguzi wa Jumatatu ulivutia asilimia 71 ya wapiga kura. Chombo cha habari
    cha ZBC kimesema kuwa Zec itatangaza matokeo ya uchaguzi wa urais
    mwendo wa 12.30 za Zimbabwe.

  • Wengi Wajitokeza Kwnye Vimbabwe

    Wengi Wajitokeza Kwnye Vimbabwe