Category: Music

  • Miaka 9 tokea kifo cha Michael Jackson, kuna haya ya kuyafahamu

    Miaka 9 tokea kifo cha Michael Jackson, kuna haya ya kuyafahamu

    Miaka tisa tokea dunia ipate taarifa za kifo cha mfalme wa muziki wa
    Pop duniani Marehemu Michael Jackson ambaye alifahamika
    duniani kote kutokana na upekee aliokuwa nao katika uchezaji
    pamoja na nyimbo zake ambazo zilipendwa na watu wengi
    ulimwenguni.
    Marehemu Michael Jackson alipendwa zaidi na watoto kutokana na
    upendo na ukaribu aliokuwa nao kwa watoto wote ambapo hakujali
    rangi na enzi za uhai wake Michael Jackson aliwahi pia kutembelea
    Tanzania na kukutana na Rais wa awamu ya pili wa Tanzania
    mstaafu Ali Hassan Mwinyi.
    Marehemu Michael Jackson alifariki June 25,2009 akiwa nyumbani
    kwake Holmby Hills, Los Angeles nchini Marekani ambapo alikutwa
    chumbani kwake na mmoja wa madaktari wake Conrad
    Murray akiwa hapumui na kukimbizwa hospitali ya Ronald
    Reagan UCLA Medical Centre.
    Marehemu Michael Jackson aliwahi kushinda tuzo ya Grammy
    Awards katika wimbo bora wa RnB mwaka 1984, Grammy Award
    wimbo bora wa mwaka 1986, MTV video music award 1995,Billboard
    Music Award for spotlight 1989 na nyingine nyingi.
    Marehemu Michael Jackson alitamba na ngoma kali ikiwemo
    Thriller, Bill Jean, We are the World, The way you make me feel, Beat
    It, You Rock My World, Earth song, Dirty Diana na nyingine nyingi
    ambazo bado zinaheshimika duniani kote mpaka leo.

  • Nyota Ndogo alizwa na historia ya mama yake, Aomba msaada kwa Watanzania

    Nyota Ndogo alizwa na historia ya mama yake, Aomba msaada kwa Watanzania

    Nyota Ndogo
    Nyota Ndogo

    Msanii wa muziki kutoka Kenya, Nyota Ndogo amewaomba wana Afrika Mashariki kumsaidia kutafuta ndugu wa mama yake mzazi ambao hadi leo hii hawajui walipo.

    Nyota Ndogo amesema kuwa mama yake mzazi alifika nchini Kenya akitokea Zambia akiwa na miaka 14 akisafirishwa na rafiki na baba yake (Babu wa Nyota Ndogo) kwa lengo la kwenda kusoma.

    Nyota Ndogo amesema kuwa mama yake hakufanikiwa kwenda shule kama alivyoahidiwa bali aliishia kuwa kijakazi wa nyumbani.

    Baadaye Mama yake alipata bahati ya kuolewa na mwanaume kutoka Tanzania ambaye ndio baba yake mzazi, na kwa maelezo ya mama yake kwenye familia yao walizaliwa watoto 15 na mama yake alikuwa ndiye mtoto wa mwisho.

    “Anatokea Zambia kisha baba anatokea Tanzania lakini sisi tumezaliwa pale makadara hospital. Mimi ni 001 damu kisha my mum alitoka kwao akiwa 14 years but kasahau kikwao. hatujui mtu hata mmoja wakutoka upande wa mama, anasema kwa wapo kumi na tano na yeye ndio alikua wa mwisho hajui kama babake yupo au hayupo anasema anatokea Tunduma.“ameandika Nyota Ndogo kwenye ukurasa wake wa Instagram.

    Kwa upande mwingine Nyota Ndogo amesema kuwa kwa sasa anahitaji kufanya ziara nchini Tanzania maeneo ya Tunduma, ambapo amesema kuwa anachohitaji kutoka kwa watu wa Afrika Mashariki ni kumsaidia kutambua lugha anayozungumza mama yake ili apate wepesi wa kutafuta ndugu wa mama yake.

    “Nataka kufanya tour ya kumtafutia familia yake alikuja vipi Kenya? Rafiki ya babake alikwenda kumchukua kwa wazazi wake nakusema anakuja kumsomesha badala yake akamgeuza kijakazi,” ameeleza Nyota Ndogo.

    Baba mzazi wa Nyota Ndogo ni Mtanzania lakini kwa upande wa mama yake bado haijajulikana asili yake ingawaje wameishi Kenya kwa muda mrefu.

     

  • LADHANI LEO, 26 March

    LADHANI LEO, 26 March

    Professor Jay ndani ya Nyumba

    Professor Jay: Naamini basata ni wazazi na walezi wa muziki

    Professor Jay: Niliposikia nyimbo zinafungiwa nilishtuka, nafikili basata wanatakiwa kukaa na vijana kuweza kuwaelekeza

    Professor Jay: Kwa dunia ilivyo sasa sidhani hizi contents za kawaida sana sioni kama shida

    Professor Jay: Kweli tunaitji kujitune kufuata utamaduni wetu lakini tuliangalie hili

    Professor Jay: Unapoongelea serikali ni chombo kikubwa sana, na hata baraza la sanaa ni kama mzazi.

    Professor Jay: Kulidharau baraza la Sanaa si vizuri, kinachotakiwa ni kukaa na baraza na kuongea nayo

    Professor Jay:Yaha ni kweli vijana  wanakosea, na sisi ni kama kolodoza, tumechonga barabara haawa madogo wanapita kwenye njia imenyooshwa

    Professor Jay: Pagamisa ni neno la kizuru maana yake pukutisha, au usikate tamaa

    Professor Jay: Lengo la huu wimo ni kuwapa funzo vijana, wasikate tamaa, wapambane mpaka kieleweke

    Professor Jay: Unajua mimi  sasa ni mwanasiasa so siku hizi nikishasema wadau watasema mimi nasema kwa ajili ya upande wa chama

    Professor Jay: wimbo huu target yangu ni kuwini market ya umri wote, wale kitambo, na wasasa

    Professor Jay:  Video ya Pagamisa imeshatoka inapatika kwenye chanel yangu ya Youtube

     

     

  • JE NINI KIMEBADILIKA WAKATI HUU HADI WASANI KUFUNGIWA NYIMBO ZAO: NIKKI WA PILI LADHANI

    JE NINI KIMEBADILIKA WAKATI HUU HADI WASANI KUFUNGIWA NYIMBO ZAO: NIKKI WA PILI LADHANI

    • Tukirudi miaka 5 nyuma na kuendelea hakukua na kufungiwa sana kwa nyimbo za Bongofleva. Je nini hasa kimebadilika wakati huu.. Ladhani leo tutakuwa na Inspector Haroin Babu na  Nikki wa Pili  kuliangalia hili na mengineyo Saa 9 kamili hadi saa 10 jioni #Efmtanzania
  • LADHANI LEO CHIN BEEZ ANA REVIEW ALBUM YAKE LIVE

    LADHANI LEO CHIN BEEZ ANA REVIEW ALBUM YAKE LIVE

    CHIN BEEZ akiwa ndani ya kipindi cha Ladha 3600
    CHIN BEEZ kulia akiwa na mtangazaji wa kipindi cha Ladha 3600, Jabiri Salehe kushoto wakionesha cover ya cd ya Album yake
    CHIN BEEZ akikamua

     

    CHIN BEEZ: unajua ukizungumzia swala la Albam, tukiziweka ndani hatuwatendei haki mashabiki wetu

    CHIN BEEZ: Hii ni kama zawadi nimewapa mashabiki wangu

    CHIN BEEZ: Hii albam ni bure kabisa una weza kudownload kupitia wanene

    CHIN BEEZ: Na sisitiza usiuziwe hii Albam, ni bure ni zawadi kwamashabiki wangu

    CHIN BEEZ: Sometie kila msanii ana stayle yake unajua ehe

    CHIN BEEZ: Mimi sio mkorofi ila unajua mtu ukiwa na modi furani hivi ndio unaonekana hivyo

    CHIN BEEZ: Sasa mimi nafikiria maisha, yale mambo ya zamani sinaga tena meen

    CHIN BEEZ: Kwa Bongo hii ndio album ya kwanza ambayo haina korabo

    CHIN BEEZ: Nimeimba mwenyewe Album nzima kwa sababu nyimbo nyingi nilikuwaga nazo

    CHIN BEEZ: Toka niachane Mpenzi wangu, now Sina Perment love (Nipo Single)

    CHIN BEEZ: Mimi sio mtu wa starehe, mimi ni mtu wa studio

    CHIN BEEZ: Hii album ina nyimbo 11 na ni bure kabisa, unaweza kuipata youtube, au unaweza ukagoogle

    BOFYA HA KU DOWANLOAD NYIMBO YA MY BABY YA CHIN BEEZ

  • NEW MUSIC: DREAM – NIMESHAZAMA

    NEW MUSIC: DREAM – NIMESHAZAMA

    Baada ya kufnya vizuri na track yake ya kwanza kama  solo artist, Dream ameachia wimbo mpya unaweza kuusikiliza na kuupakua hapa

    Wimbo umetayarishwa na Abbah katika studio za Vipaji TZ

    pakua hapa https://mkito.com/song/nimeshazama/18065

  • UFISADI: MAJAJI 7 WASIMAMISHWA KAZI GHANA

    UFISADI: MAJAJI 7 WASIMAMISHWA KAZI GHANA

    JUMLA ya Majaji saba kati ya 12 wa mahakama ya juu nchini Ghana wamesimamishwa kazi kwa muda kufuatia madai ya kuhusika katika ufisadi.

    Mwezi uliopita majaji wengine 22 wa ngazi za chini walisimamishwa kazi baada ya filamu moja kuwaonesha wakipokea rushwa kutoka kwa wateja ili wapate kupendelewa katika kesi zilizowakabili.

    Hata hivyo Majaji wengine kadhaa wamekana kuhusika na madai hayo hali iliyowapeleka mahakamani kupinga kitendo cha wao kusimamishwa kazi.

  • GHANA YATANGAZA SIKU TATU ZA MAOMBOLEZO KUFUATIA VIFO VYA WATU 150

    GHANA YATANGAZA SIKU TATU ZA MAOMBOLEZO KUFUATIA VIFO VYA WATU 150

    GHANA imetangaza siku tatu za maombolezo ya kitaifa kufuatia vifo vya watu mia na hamsini vilivyotokana na mafuriko na mlipuko kwenye kituo kimoja cha mafuta.

     

    Mlipuko huo ulitokea hapo jana wakati mamia ya watu walipokuwa wamejihifadhi katika kituo hicho cha mafuta kutokana na mvua kubwa zinazonyesha.

     

    Rais wa Ghana,John Mahama amesema janga kama hilo halitajirudia tena. Rais Mahama amesema hayo wakati akizungumza na waandishi wa habari katika mji mkuu ,Accra alipotembelea eneo la tukio.

    baadhi ya picha za ajali ya moto Ghana

    150604093627_ghana_fire_640x360_bbc_nocredit

     

     

    150604092839_ghana_floods_accar_640x360_bbc_nocredit

     

     

    150604131908_ghana_fire_640x360_epa

     

  • NEW AUDIO: MUZYD FT RICH MAVOKO

    NEW AUDIO: MUZYD FT RICH MAVOKO

    Huu ni wimbo uliyotayarishwa katika studio za Vipaji Tz chini ya Producer Abba

    Artist : Muzdy ft Rich Mavoko

    Song: Mboni yangu

    unaweza kuusikiliza na kudonwload hapa

     

     

  • UINGEREZA YATARAJIWA KUANZA KAMPENI ZA UCHAGUZI MKUU

    UINGEREZA YATARAJIWA KUANZA KAMPENI ZA UCHAGUZI MKUU

    Waziri Mkuu wa Uingereza DAVID CAMERON akutana na Malkia ELIZABETH kumuarifu kuwa Bunge limevunjwa, hatua inayofungua mlango wa kuanza Kampeni kwa uchaguzi Mkuu May 7 mwaka huu.tarehe 7 Mei.

    Bwana CAMERON anaiongoza Serikali ya Mseto  kati ya Chama chake cha Conservative na  kile cha Liberal Democrats tangu mwaka 2010.

    Utafiti wa maoni ya Wapiga kura unaonyesha matokeo yanayotafautiana.