MFALME MTEULE WA THAILAND KUTHIBITISHWA DECEMBER

MFALME MTEULE WA THAILAND KUTHIBITISHWA DECEMBER

Like
201
0
Wednesday, 02 November 2016
Slider

imetaarifiwa kwamba mfalme mteule mtarajiwa wa Thailand Vajiralongkorn atathibitishwa rasmi kama mfalme ajaye mnamo Desemba mosi.

Mwana wa mfalme huyo ambaye pia ni mfalme mtarajiwa alitarajiwa kupakwa mafuta na kutawazwa katika kipindi ama baada ya maziko ya babake , mfalme King Bhumibol Adulyadej, aliyefariki wiki tatu zilizopita, kutokana na yeye mwenyewe kuomba muda wa kumuomboleza babake.

Mpaka sasa haijafahamika wazi, ni uhusiano wa namna gani mfalme huyo mtarajiwa atakuwa nao baina yake na vikosi vya jeshi la serikali ambavyo hivi karibuni vilikuwa vinaiongoza Thailand, ama ni namna gani atapokelewa na raia wake.

Comments are closed.