RAIA WA CUBA KUANZA  KUINGIA MAREKANI KWA VIZA

RAIA WA CUBA KUANZA KUINGIA MAREKANI KWA VIZA

Like
461
0
Friday, 13 January 2017
Slider

Marekani imesitisha sera ya muda mrefu ambayo ilikuwa inawapa raia wa Cuba hadhi maalumu ya kuingia na kuishi nchini Marekani bila ya visa.

Serikali ya Cuba imekuwa ikilalamika kwamba, sera hiyo, ijulikanayo kama “wet foot, dry foot,” imewafanya maelfu ya raia wa Cuba kukimbia nchini humo kila mwaka.

Rais Obama amesema hatua ya kuondolewa kwa sera hiyo, ni hatua muhimu katika kurudisha uhusiano na Cuba.

Mahasimu hao wa muda mrefu wamerudisha uhusiano wa kidiplomasia mnamo mwaka 2015 baada ya karne ya uhasama.

Comments are closed.