Tanzania Waomba Kuandaa AFCON 2017

Tanzania Waomba Kuandaa AFCON 2017

Like
284
0
Monday, 25 August 2014
Slider

Jamal malinzi caf

Shirikisho la Soka Tanzania TFF leo lilikuwa linatarajiwa kutuma rasmi maombi ya kuandaa michuano hiyo inayotakiwa kufanyika mwaka 2017, baada ya Libya kujitoa.

Akizungumza leo mbele ya waandishi wa habari katika ofisi za shirikisho hilo Karume Ilala jijini Dar-Es-Salaam, katibu mkuu wa TFF Selestine Mwesigwa, amewaambia waandishi wa habari kuwa, baada ya kupata taarifa za libya kujitoa, wajumbe wa kamati ya utendaji ya TFF  jana walikutana kujadili na kupitisha uamuzi wa kutuma maombi rasmi ambapo kwanza watapeleka taarifa rasmi serikalini kupitia wizara ya habari vijana, utamaduni na michezo na kupata baraka za Serikali kabla ya kutuma maombi hivi karibuni.

Comments are closed.