Rais Kikwete Aipa Halmashauri Ya Kilosa Wiki Moja Kuwapatia Wahanga Wa Mafuriko Viwanja

Rais Kikwete Aipa Halmashauri Ya Kilosa Wiki Moja Kuwapatia Wahanga Wa Mafuriko Viwanja

Like
333
0
Monday, 25 August 2014
Local News

Jakaya-Kikwete

Rais JAKAYA KIKWETE ametoa wiki moja kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Mkoani Morogoro, kuwapatia viwanja vya kujenga nyumba wahanga wa mafuriko ya kiasi cha miaka minne iliyopita mjini Kilosa.Rais KIKWETE ametoa agizo hilo mkoani Morogoro alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kilosa katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Kilosa baada ya kutembelea Wilaya hiyo kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo.Agizo hilo limekuja kufuatia malalamiko yaliyotolewa na wahanga hao kwa njia ya maneno na mabango baada ya kuwa wameahidiwa viwanja hivyo na Rais KIKWETE mwenyewe wakati alipowatembelea kufuatia mafuriko ya Mto Mkondoa miaka minne iliyopita.

Comments are closed.