Category: Local News

  • KUPIGA KELELE NI UCHAFUZI WA MAZINGIRA

    KUPIGA KELELE NI UCHAFUZI WA MAZINGIRA

    Katika kukabiliana na uchafuzi wa mazingira unaosababishwa na kelele serikali imewaelekeza  wamiliki wa maeneo ya burudani na starehe kuzingatia matumizi ya vipima kelele na vizuia sauti kama inavyoelekezwa kwenye masharti ya leseni zao. Hili ni kwa sababu ya kulinda afya za wananchi kutokana na athari za kelele na mitetemo.

    Hayo yameelezwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais,Muungano na Mazingira Seleman Jaffo wakati akiongea na vyombo vya habari Juni 29 kuhusu udhibiti wa uchafuzi wa Mazingira unaosababishwa na vitu hivyo.

    “Kila mwananchi ahakikishe shughuli anazofanya haisababishi kero ya kelele na mitetemo, Wamiliki wa kumbi za starehe na burudani wahakikishe sauti zinazozalishwa katika shughuli zao hazizidi viwango vinavyokubalika kwa mujibu wa sheria. Hili tumeazimia wenye kumbi za starehe na burudani isiwe starehe ya kwako na watu wengine ikawa kero kwa watu wengine, Sauti zinazotoka zisidi viwango vilivyowekwa kwa mujibu wa sheria na kanuni”.- Amesema Jaffo

  • WATOTO WAELEKEZWE MATUMIZI SAHIHI YA BARAKOA

    WATOTO WAELEKEZWE MATUMIZI SAHIHI YA BARAKOA

    “Watoto waelekezwe kuhusu matumizi ya barakoa, wajue namna ya kuzivaa, waelekezwe na mahali pa kuzitupa” Dkt Ama.

    Dkt. Ama Kasangala, Kaimu Mkurugenzi wa kitengo cha Elimu ya Afya kutoka Wizara ya Afya

    Alikuwa anajibu maswali ya Dina Marious kuhusu madhaara ya Corona kwa watoto. Japo hawako kwenye hatari kubwa kama wazee, lakini mi muhimi walindwe.

    .

    Swebe alisema watoto kwa kutokuelezwa vizuri kuhusu Barakoa, wawapo shuleni wanaweza kuchangia, au kuokota na kuzivaa.

    .

    Hivyo wazazi wanasisitizwa kuwalinda watoto, lakini pia Wizara ya Afta kwa kushirikiana mamlaka nyingine na walimu wanahakikisha watoto wanaelezwa vyema na kulindwa.

    .

    #JikingeWakingeWengine #CoronaInazuilika

  • Hatma maombi ya kukamatwa Lissu Julai 14.

    Hatma maombi ya kukamatwa Lissu Julai 14.

    Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es salaam, inatarajia kuanza kusikiliza maombi ya wadhamini wa aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu ambao wanataka akamatwe ili wajitoe udhamini.

    Mahakama imetoa siku 7 kwa upande wa Jamhuri kuwasilisha majibu ya kiapo kinzani na maombi ya wadhamini, Ibrahim Ahmed na Robart Katula Julai 14, mwaka huu ambapo Wadhamini hao wamefungua maombi wakiiomba itoe hati ya kumkamata kwa kuwa wameshindwa kumpata na kumfikisha Mahakamani hapo.

    Maombi hayo namba 2/2020 yalipelekwa mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba ambapo upande wa Jumhuri uliomba kuongezwa muda wa kuwasilisha majibu ya kiapo kinzani.

    Hakimu Simba amesema Mahakama itasikiliza maombi hayo Julai 14, mwaka huu na kesi ya msingi itatajwa siku hiyo ikiwa Mbali na Lissu washtakiwa wengine ni Wahariri Simon Mkina, Jabir Idrisa na Mchapishaji wa Kampuni ya Jamana, Ismail Mehbooh.

    Katika kesi ya msingi kwa pamoja washtakiwa hao, wanakabiliwa na mashtaka matano ikiwamo kuandika habari za uchochezi kinyume na Sheria ya Magazeti ya Mwaka 2002 ambapo hii ilitokea Januari 12 na 14, 2016 Dar es salaam, washtakiwa waliandika na kuchapisha taarifa za uchochezi zenye kichwa cha habari ‘Machafuko yaja Zanzibar’

  • Rais Magufuli Atoa tamko la kutengewa eneo kwa Wafanyabiashara wadogo stendi mpya Dodoma.

    Rais Magufuli Atoa tamko la kutengewa eneo kwa Wafanyabiashara wadogo stendi mpya Dodoma.

    Rais Magufuli ametoa agizo kwa Mkurugenzi wa jiji la Dodoma, Godwin Kunambi, kuhakikisha wafanyabiashara ndogondogo (Machinga), mama lishe pamoja na magari ya mizunguko mifupi jijini, (Daladala) kutengewa maeneo ya kufanya kazi katika stendi mpya ya kisasa Dodoma.

    Ametoa agizo hilo Jun 18 kwa njia ya simu, baada ya Mkurugenzi kuwatembelea wafanyabiashara katika stendi hiyo na kusikiliza kero zao.

    Ameongeza kuwa Mama lishe lazima wawepo, ikiwa stendi hiyo imejengwa kwaajiri ya watanzania wote wakiwepo maskin ambapo Hakuna sababu ya kuwa na stendi ya watanzania wote wa maisha yote,.

    Usafiri mwingine wa daladala na pikipiki Rais amesema Nilazima jiji litengeneze mazingira, watu wa daladala wawe wanaweza kufika pale, wa bodaboda waweze kufika pale, wa pikipiki waweze kufika pale, ili kusudi hata mvua ikiwa inanyesha mtu asianze kutembea na mizigo yake, wapo wengine wagonjwa.

    Aidha ametoa onyo kwa walinzi waliopewa kazi kwenye stendi hiyo kutoka Suma JKT kuacha kuwarusha watu vichura na kufanya kazi ya kuwalinda, kama wanavyofanya mikoa mingine ikiwa hapo sio jeshini wanapaswa kuwalinda .

    Kwa upande wake Mkurugenzi, Kunambi ameahidi kufanyia kazi maelekezo yote yaliyotolewa ndani ya muda mfupi na kuwatafutia vijana mikopo kama ambavyo Rais ameagiza.

  • Msamaha wa Rais Magufuli kwa zimamoto watoka na onyo kali.

    Msamaha wa Rais Magufuli kwa zimamoto watoka na onyo kali.

    Rais Magufuli amesema amemsamehe aliyekuwa Kamishna wa Jenerali wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, Thobias Andengenye baada ya kumuomba msamaha kwa zaidi ya mara tatu na viongozi wengine katika jeshi hilo ambao ilitakiwa awafukuze.

    Amesema kwa upande wa Andengenye, hawezi kumrudisha katika Jeshi hilo ila ataonekana katika kazi nyingine kwani mtu akiomba msamaha na kuonesha kutubu inabidi asamehewe

    Rais Magufuli ametangaza msamaha huo huku akitoa onyo kwa askari wa Jeshi la Zimamoto juu ya uchukuaji wa rushwa na kuingia mikataba isiyo na tija kuacha mara moja ambapo amewaambia kuwa fedha za bure katika kipindi chake ni mbaya zitawaharibia maisha yao.

    Amesemahayo leo Juni 11 2020, alipokuwa  anazindua jengo la makao makuu ya jeshi hilo mjini Dodoma huku akiwasifia kuwa jeshi hilo ni sawa na malaika wa duniani hivyo hawapaswi kufanya mambo mabaya kwa kuanzisha moto.

    Aidha Rais magufuli ameongeza kuwa Fedha za bure kwenye kipindi chake ni mbaya na zinaweza kuwaharibia maisha ambapo ametaka fedha za walipakodi zikawaletee mabadiliko

    Ikumbukwe kuwa mapema January 23 2020, Rais John magufuli alitengua uteuzi wa aliyekuwa waziri wa mambo ya ndani Kangi Lugola na Andengenye kutokana na kuingia mkataba mbovu uliolengwa kusaidia jeshi la hilo.

  • Waziri Philip Mpango aishukuru IMF kuisamehe Tanzania deni la Bilioni 33.

    Waziri Philip Mpango aishukuru IMF kuisamehe Tanzania deni la Bilioni 33.

    Waziri wa Fedha, Dkt. Philip Mpango ametoa shukurani kwa shirika la fedha duniani, (IMF) kwa kusamehe deni ambalo walikuwa wanaidai Tanzania la takriban Bilioni 33.

    Ametoa shukurani hiyo leo Juni 11, Bungeni jijini Dodoma alipokuwa anawasilisha bajeti kuu ya Serikali kwa mwaka wa fedha 2020/21 na kusisitiza kuwa wanaendelea kuomba mashirika mengine yatoe msamaha wa madeni.

    Hii baada ya Shirika la Fedha Duniani (IMF) jana, kutangaza limeisamehe Tanzania deni lenye thamani ya Dola Milioni 14.3 (takriban Tsh. Bilioni 33) ambalo lilipaswa kulipwa ndani ya miezi minne ijayo, kuanzia Juni 10, 2020 hadi Oktoba 13, 2020.

    IMF imechukua hatua hiyo kupitia mfuko wake wa ‘Catastrophe Containment and Relief Trust (CCRT)’ ili kuiwezesha Tanzania kukabiliana na athari za virusi vya Corona katika nyanja za kijamii na kiuchumi.

    Taasisi hiyo imesema kutegemeana na uwepo wa fedha katika mfuko huo, huenda ikaongeza msamaha wa deni lenye thamani ya Dola Milioni 11.4 (takriban Tsh. Bilioni 26.4) ambalo linatakiwa kulipwa kati ya Oktoba 14, 2020 na Aprili 13, 2022.

    IMF imeeleza kuwa janga hili limesababisha athari mbalimbali nchini ikiwa ni pamoja na kupungua kwa watalii, changamoto za kibajeti na kupungua kwa makadirio ya ukuaji wa Pato la Taifa (GDP) kutoka 6% hadi 4% katika mwaka huu wa fedha, na 2.8% katika mwaka wa fedha ujao ambapo hatua hii imekuja ikiwa ni takribani miezi miwili tangu Rais wa Tanzania, Dkt Magufuli alipozitaka nchi zote za Afrika kuungana kuziomba taasisi za kifedha za kimataifa kutoa msamaha wa madeni.

  • Serikali kutoweka bei elekezi zao la Pamba

    Serikali kutoweka bei elekezi zao la Pamba

    Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga amesema msimu wa ununuzi wa pamba wa mwaka 2020/2021 utazinduliwa tarehe 15 Juni 2020, ambapo serikali imejiweka kando kutopanga bei elekezi katika zao hilo pamoja na mazao mengine badala yake bei za mazao zitatokana na soko.

    Ameyasema hayo, wakati akizungumza kwenye mkutano maalumu wa wadau wa tasnia ya Pamba uliofanyika katika Ukumbi wa mikutano wa Chuo cha Benki kuu Jijini Mwanza.

    Ameongeza kuwa kazi ya serikali ni kuhakikisha inasimamia uzalishaji bora wa mazao kadhalika kusimamia upatikanaji wa masoko ya mazao ili kuwa na bei nzuri yenye manufaa kwa wakulima ambapo Kutokana na usimamizi madhubuti wa serikali kupitia Wizara ya Kilimo, uzalishaji wa pamba umeongezeka kutoka tani 122,178 msimu wa ununuzi wa 2015/2016 hadi tani 348,910 msimu wa 2019/2020.

    Amezitaja Hatua zilizochukuliwa na serikali kuwa ni pamoja na kuhamisha makao makuu ya Bodi ya Pamba kutoka Dar es Salaam kwenda Mwanza ili kuwa karibu na maeneo yanayolima pamba na kuwahudumia wakulima kwa karibu zaidi ambapo Kutokana na hatua hiyo, ufanisi wa utendaji na huduma kwa wakulima umeongezeka.

    Aidha ameeleza kuwa zao la pamba ni mhimili wa uchumi wa wananchi wengi katika mikoa 17 na Wilaya 56 zinazozalisha zao hilo.

  • Ajali mbili za lori zatokea kwa mpigo na kusababisha vifo katika Daraja la Wami.

    Ajali mbili za lori zatokea kwa mpigo na kusababisha vifo katika Daraja la Wami.

    Daraja la Wami, ajali mbili tofauti zimetokea  kwa kufuatana mara baada ya malori hayo kufeli breki na kusababisha vifo ambapo Lori la kwanza limesababisha kifo cha mtu mmoja na majeruhi wawili, huku lori la pili likiwa limesababisha vifo vya watu wawili mama pamoja na mtoto mdogo.

    Katika ajali ya Lori la kwanza lililokuwa linatokea Dar es salaam kuelekea Arusha limepoteza mtu mmoja ambae alikuwa dereva aliyeshindikana kuokolewa kufuatia kushindwa kufungua mkanda wa gari hivyo amezama katika mto wami wenye kina kirefu pamoja na lori hilo.

    Ajali hizo zimetokea June 5, 2020, ambapo wakati watu wakiwa wamejaa kushuhudia ajali hiyo ya lori, ghafla lori lingine pia likafeli breki na kusababisha vifo vya watu wawili ambao ni mama na mtoto waliokuwa kwenye eneo la tukio wakishangaa ajali ya kwanza ya lori.

    Lakini pia Lori hilo limezoa magari zaidi ya saba ambayo yote yameharibiwa vibaya.

    Aidha, jeshi la Uokaaji kwa kushirikiana na timu ya Askari polisi Wilayani bado wapo kwenye jitihada za kuhakiksha wanaokoa mwili wa dereva uliozama pamoja na lori mtoni.

  • Vyuo vyapewa siku 3 kukamilisha mgao fedha za kujikimu kwa wanafunzi

    Vyuo vyapewa siku 3 kukamilisha mgao fedha za kujikimu kwa wanafunzi

    Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Joyce Ndalichako ameagiza vyuo vyote nchini kuhakikisha hadi kufikia ijumaa Juni 5, mwaka huu viwe vimeshawalipa wanafunzi wote fedha zao za kujikimu na ambao hawatafanya hivyo watachukuliwa hatua.

    Waziri Ndalichako ametoa agizo hilo leo Juni 3, jijini Dar es Salaam wakati akikabidhi magari manne kwa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) ambacho  ni miongoni mwa vyuo vinne vitakavyonufaika na mkopo wa Benki ya Dunia kupitia mradi wao wa Kuleta Mapinduzi kwenye elimu ya ufundi Afrika Mashariki (EASTRIP).

    Profesa Ndalichako amesema  kuna baadhi ya vyuo mpaka leo bado havijawapatia wanafunzi fedha hizo za kujikimu licha ya kwamba Serikali imeshazitoa hivyo anatoa siku tatu kuanzia leo kuhakikisha wanazitoa ili wanafunzi waendelee na masomo bila kupata usumbufu wowote.

  • Vijana wapewa siri ya ubunifu katika Biashara zao

    Vijana wapewa siri ya ubunifu katika Biashara zao

    Vijana nchini wametakiwa kuachana na biashara ambazo zimekuwa zikiwapotezea muda na badala yake wajikite katika ubunifu wa kazi wanazozifanya, ili kuweza kupata matokeo chanya yatakayobadilisha maisha yao.

    Hayo yamebainishwa na Katibu Mtendaji wa Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Beng’i Issa, katika uzinduzi wa shughuli za kiubunifu Kitaifa zilizofanyika jijini Dodoma, zilizoandaliwa na Tanzania Innovation Explore Gala.

    “Epukeni biashara zinazowapotezea muda, haiwezekani miaka mitano unafanya biashara isiyokupa faida, jitahidini katumia ubunifu wa kazi ambazo zitawafanya mfikie malengo yenu, maana kama utajibidiisha katika ubunifu ni lazima utayapata mafanikio,” ameongeza Beng’i.

    Amesema wengi wa Vijana wamekuwa hawana mawazo mbadala katika kujikwamua na hali ngumu ya kiuchumi inayowakabili kwa kuendelea kung’ang’ania mfumo mmoja wa mbinu za kibiashara ambazo haziwaingizii faida na mwisho huitupia lawama Serikali au mashirika ya utoaji mikopo.

    Beng’i ambaye alikuwa mgeni rasmi katika ufunguzi huo amebainisha kuwa uzoefu unaonesha baadhi ya watu wanaoendesha biashara kwa mikopo wamekuwa hawafikii malengo yao kutokana na faida kidogo wanayoipata huku wakitakiwa kufanya marejesho.

    “Mtu huna mbinu za biashara zilizo na mashiko halafu unachukua mkopo ni wazi kuwa utaanguka tu, hivyo ni lazima kuweka mawazo mbadala ambayo kibiashara yanaweza kukupa faida kwa kuwa mbunifu katika bidhaa zako,” ameongeza Beng’i.

    Kwa upande wake Afisa maendeleo ya jamii Idara kuu ya Vijana Jiji la Dodoma Mfungo Daniel Manyama, amesema ili kupata maendeleo yenye muonekano chanya maishani, Vijana hawana budi kutumia Elimu walizonazo kwa kuleta ubunifu na kujiajiri.

    Amesema utafutaji na uzalishaji wa mipango thabiti ikiwemo suala la ushirikishwaji wa mawazo ya Vijana kwa watu sahihi, utaleta utatuzi wa changamoto na kupata mafanikio kwa kila kijana mpambanaji, aliye na kiu ya maendeleo.

    “Elimu hii tuipatayo mashuleni inatakiwa itusaidie katika suala la ubunifu na kujiajiri maana kuwa na elimu halafu haitumiki katika kupata mbinu mpya za ubunifu inakua haina mantiki, sasa sisi kama eneo la uwezeshaji watu mbalimbali hasa vijana katika vikundi vyao tupo tayari kuunga mkono juhudi zenu,” amesema Manyama.

    Awali akiongea katika uzinduzi huo mwakilishi wa makundi ya Vijana toka chuo cha Mipango Dodoma (IRDP), Gabriel Muhuwa amesema uwezo wa kubuni na kuwa na vipaji mbalimbali utasaidia kuinua uchumi wa wajasiriamali wadogo ambao wamekuwa na kiu ya kupata mafanikio.

    Suala la kukuza mitaji inayotokana na ufanyaji wa biashara kwa wajasiriamali mbalimbali limekuwa likilalamikiwa katika maeneo mengi nchini kutokana na baadhi yao kukosa ubunifu, kuwa na uelewa mdogo wa mambo ya kibiashara, kutoitumia ipasavyo elimu waliyoipata katika ubunifu na kukosa maarifa mapya.

  • Wabunge Kenya watofautiana kuhusu matamshi ya ‘chuki’ ya Charles Kanyi ‘Jaguar’

    Wabunge Kenya watofautiana kuhusu matamshi ya ‘chuki’ ya Charles Kanyi ‘Jaguar’

    Matamshi ya mbunge wa Starehe nchini Kenya Charles ‘Jaguar’ Kanyi kuhusu kuwatishia raia wa kigeni wanaofanya kazi nchini Kenya yaliwasilishwa mbele ya kikao cha bunge ili kujadiliwa.

    Hatua hiyo inajiri huku Mbunge huyo akizuiliwa katika kituo cha polisi usiku kucha ambapo anasubiri kuwasilishwa mahakamani siku ya Alhamisi.

    Kulingana na mtandao wa runinga ya Citizen nchini Kenya, licha ya wabunge wengi kushutumu jinsi ambavyo bwana Jaguar alitoa hoja yake , baadhi yao walikubaliana kwamba kuna swala tata kuhusiana na raia wa kigeni ambalo lilihitaji kuangaziwa.

    Kulingana na mtandao huo swala hilo liliwasilishwa na mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Uhusiano wa kigeni Katoo Ole Metito katika taarifa yake, akithibitisha kwamba raia wa kigeni hususan kutoka Jumuiya ya Afrika mashariki wana uhuru wa kufanya biashara nchini Kenya.

    ”Tunashutumu sana matamshi yoyote ya chuki yanayokiuka msimamo huu unaotuleta sisi pamoja kama taifa na kuthibitisha sera ya kuwakaribisha raia wote wa kigeni”, alisema mbunge huyo wa Kajiado kusini.

    Matamshi yake yaliungwa mkono na mbunge wa Suba Kaskazini John Mbadi ambaye aliwarai wabunge wenzake kutotoa matamshi mbele ya umma kwa lengo la kujitafutia umaarufu na badala yake kuchukua tahadhari.

    ”Kama bara, tunahitaji kukuza uwiano katika mipaka yetu ili kutafuta ajira; Wakenya wako huru kwenda Tanzania kufanya biashara iwapo biashara hiyo ni halali”, alisema Mbadi.

    Hatahivyo kiongozi wa walio wengi bungeni Aden Duale, ambaye pia alishutumu matamshi hayo ya mbunge huyo wa Starehe alisema kwamba Kenya sio jaa la raia wa kigeni na bidhaa zao, kulingana na mtandao wa Citizen kenya.

    Kulingana na mbunge huyo wa Garissa mjini, Bunge pamoja na serikali zinafaa kuwalinda wananchi wa kawaida kutopoteza kazi kwa idadi kubwa ya raia wa kigeni waliomo nchini.

    Mbunge huyo alitaja mfano ambapo wataalam kutoka Kenya kama vile afisa wa kampuni ya Safaricom Sylvia Mulinge alinyimwa fursa ya kufanya kazi katika taifa jirani la Tanzania, akiongezea kuwa Kenya pia inafaa kutokubali maswala mengine.

    “Lazima ukweli usemwe; Unapoona biashara ya uchuuzi ikichukuliwa na raia wa taifa jingine tuna jukumu la kuwalinda watu wetu. Hawa wabunge hawafai kusahau kwamba kuku wetu walichomwa Tanzania , ng’ombe wetu walipigwa mnada Tanzania”, alisema Duale.

    ”Leo chini ya utawala uliopo Tanzania Wakenya hawawezi kufanya biashara, kwa nini bidhaa zetu haziingi Tanzania? Kwa sababu wametuwekea kodi ya juu”.

    Duale aliwataka wabunge kutolichukulia swala hilo na hisia, bali kuchukua tahadhari wanapochukua jukumu lao la kuwalinda raia wa kawaida.

    ”Kama bunge ni lazima tuamue na kuleta sheria zitakazolinda biashara zetu. Munaweza kumshutumu Jaguar, lakini leo ndiye mbunge maarufu zaidi katika eneo bunge lake”, aliongezea Duale.

    Nae mbunge wa Ugenya David Ochieng, kwa upande wake aliilaumu idadi kuu ya raia wa kigeni wanaofanya biashara nchini Kenya kwa kushindwa kwa serikali kuidhinisha sera yake.

    ”Katika uchumi wa leo , ni rahisi kununua bidhaa kutoka mataifa jirani kama vile Tanzania na Uganda na kuleta Kenya. Sio kwamba hatuna sheria, ni swala la utekelezwaji na ufisadi. Tunwaruhusu watu kuingia nchini na kuanza kuuza vitu barabarani. Huwezi kuwalaumu Watanzania kwa kufanya hivyo ni kwa sababu ya mfumo wetu ambao ni dhaifu”, alisema Ochieng’.

    ”Hatuwakagui watu wanaoingia nchini. Watanzania wanafanya kazi yao, ndio sababu wanaweza kujua kwamba Mulinge hakuhitimu kufanya kazi Tanzania.

    Hatahivyo Mbunge huyo alishutumu matamshi ya Jaguar , huku akilitaka bunge hilo kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya wabunge wanaoharibu jina la taifa hilo katika ulingo wa kimataifa.

    Tayari ofisi ya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai kupitia ukurasa wake wa Twitter imesema mbunge huyo anashikiliwa kwa tuhuma za kuchochea ghasia.

    Katika kanda ya video iliosambazwa pakubwa nchini Kenya na katika nchi jirani Tanzania, mbunge huyo alisema hawatokubali watu wa nje waje kuendesha biashara nchini humo.