Category: Local News

  • Aliyekuwa Mkurugenzi TBS Ekelege Apatikana Na Hatia Afungwa Mwaka

    Aliyekuwa Mkurugenzi TBS Ekelege Apatikana Na Hatia Afungwa Mwaka

    ekelege

    Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jana imemhukumu kifungo cha mwaka mmoja jela Mkurugenzi Mkuu wa zamani wa Shirika la Viwango Tanzania (TBS), Charles Ekelege na kumwamuru kurejesha Dola za Marekani 42,543 (Sh68,068,800).
    Akisoma hukumu hiyo jana, Hakimu Mkazi, Augustina Mmbando alimtia hatiani Ekelege baada ya kupitia ushahidi uliotolewa na mashahidi saba wa upande wa mashtaka, vielelezo na ushahidi wa utetezi uliotolewa na mshtakiwa.
    Hakimu Mmbando alisema katika kesi hiyo, upande wa mashtaka ulithibitisha mashtaka yote yanayomkabili Ekelege pasipo kuacha shaka na kumhukumu kifungo hicho.
    Mmbando alisema viongozi wapo kwa ajili ya kulinda masilahi na rasilimali za nchi ili wananchi waweze kuifurahia keki ya Taifa na siyo kufuata matakwa yao.
    Alisema kiongozi kama Ekelege aliaminiwa na kuteuliwa na Rais ili aweze kuiongoza TBS ambayo ni sehemu ya chanzo cha mapato ya nchi, hivyo kuzembea kwake na kusababisha hasara ya kiasi hicho cha fedha, hapaswi kuonewa huruma ili iwe fundisho kwa viongozi wengine.
    Katika shtaka la kwanza la kutumia madaraka yake vibaya kwa kuziondolea asilimia 50 ya ada ya utawala, Kampuni za Jaffar Mohamed Ali na Quality Motors, Ekelege alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela.
    Katika shtaka la pili la kuondoa ada za kampuni hizo bila idhini ya Baraza la Utendaji kinyume na utaratibu wa TBS pia alihukumiwa kifungo cha mwaka mmoja jela na katika shtaka la tatu la kusababisha hasara ya kiasi hicho cha fedha alifungwa tena kifungo kingine cha mwaka mmoja jela.
    Hakimu Mmbando alisema vifungo hivyo vitakwenda pamoja, hivyo mshtakiwa huyo atatumikia kifungo cha mwaka mmoja jela na kurejesha Sh68,068,800 anazodaiwa kulisababishia shirika hilo hasara kwa uzembe.
    Kabla ya kutolewa kwa hukumu hiyo, Mwendesha Mashtaka wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Janeth Machulya alisema kwa kuzingatia uzito wa mashtaka aliyotenda Ekelege na alivyoshindwa kuitumikia dhamana aliyopewa, anastahili adhabu kali ili iwe fundisho kwa viongozi wanapokuwa wakitekeleza majukumu yao.
    Machulya aliiomba mahakama wakati ikifikiria kutoa adhabu kwa Ekelege izingatie sheria ya uhujumu uchumi.
    Wakili aliyekuwa akimtetea Ekelege, Majura Magafu aliiomba Mahakama impunguzie adhabu mteja wake kwa kuwa ni kosa lake la kwanza, ana familia ya mke, watoto na wazee wanaomtegemea.
    Katika utetezi wake, Ekelege alikana kusababisha hasara kwa kutoa msamaha, akisema hali hiyo ilitokana na udanganyifu uliofanywa na kampuni husika.
    Alidai kuwa kampuni hizo zilidanganya na kusababisha kutoa uamuzi mwingine ambao haukuwa sahihi na bodi ya wakurugenzi ya TBS ilipoitishwa iliridhia kuwa msamaha huo haukutolewa kwa makusudi.
    Alisema kwa kuwa TBS haikuwa na historia ya kutoa msamaha hiyo na kwa kuwa ilikuwa mara ya kwanza na kampuni hizo hazikuwa na uaminifu, aliiomba Mahakama imwachie huru.
    Akijitetea, alisema kampuni ya Jaffar Mohamed Ali ilipata msamaha baada ya kuwasilisha maombi yake ikidai kuwapo kwa ushindani uliotokana na wakala mwenzake, Total Otomotive Services, aliyekuwa akifanya mchezo mchafu wa kuvuta wateja kwa kutokagua viwango vya ubora wa magari yao na kuwapa vyeti vya ubora.
    Alidai kuwa menejimenti ya TBS iliijadili na kukubaliana na matatizo hayo na ikatoa msamaha kwa kipindi cha Oktoba 2007 na Machi 2008 na alitakiwa kuanza kulipa tozo na gharama zake ifikapo Aprili Mosi, 2008.

     

  • HALIMA MDEE AMWAGA MACHOZI BAADA YA KUKABIDHIWA FOMU YA KUGOMBEA UENYEKITI!

    HALIMA MDEE AMWAGA MACHOZI BAADA YA KUKABIDHIWA FOMU YA KUGOMBEA UENYEKITI!

    Halima Mdee

    Vigogo wa Baraza la Wanawake la Chadema (Bawacha), watachuana katika kinyang’anyiro cha kuwania uenyekiti wa baraza hilo baada ya jana baadhi ya wanawake kujitokeza kumchukulia fomu Mbunge wa Kawe, Halima Mdee.Mbunge huyo anaungana na Mbunge wa Viti Maalumu, Chiku Abwao na wanachama wengine, Lilian Wasira na Sophia Mwakagenda ambao nao wamesharejesha fomu kuwania nafasi hiyo inayoshikiliwa na Suzan Lyimo. Mwisho wa kuchukua na kurejesha fomu ni Agosti 30 na uchaguzi unatarajiwa kufanyika Septemba 11, mwaka huu.
    Wanawake zaidi ya 30 kutoka Kinondoni, Kawe, Pwani na Ubungo jana saa 5.20 asubuhi, walifika katika ofisi za Bawacha jijini Dar es Salaam kumchukulia fomu Mdee wanayedai kuwa ndiye anayestahiki kuliongoza baraza hilo kutokana na msimamo wake wa uongozi wa kutotaka kuyumbishwa.
    “Tumekaa na kutafakari ili kumpata mwanamke atakayeweza kuliongoza baraza hili kwa kututoa hapa tulipo na kutupeleka mbele zaidi, tumeona Halima Mdee anatufaa zaidi ndiyo maana tumeamua kuja kumchukulia fomu,” alisema Felister Njau, Katibu Mwenezi wa Jimbo la Kawe.
    Huku akishangiliwa na wenzake alisema, “Tunakwenda kumtafuta sehemu yoyote alipo ili tukamkabidhi hii fomu na tutamwomba akubali ombi letu.”
    Msafara wa wanawake hao wakiwa na fomu yao mkononi ukiongozwa na Mwenyekiti wa Wazee Kata ya Kunduchi, Elefedina Mali ulikwenda makao makuu ya chama hicho ambako walimkuta Mdee na kumkabidhi fomu hiyo.
    Huku akibubujikwa na machozi, Mdee (pichani) alisema; “Nimewaelewa naombeni nikajitafakari kwanza, nitawaeleza nitakachoamua.” Wanawake hao pia walichangishana fedha Sh53,000 walizomkabidhi Mdee kwa ajili ya kurejeshea fomu hiyo.Aliwashukuru na kuwaomba wamvumilie kwani anahitaji muda wa kulitafakari ombi hilo.

     

  • Serikali Yaridhishwa Na Maendelea Ya Mradi Wa Mabasi Yaendayo kasi

    Serikali Yaridhishwa Na Maendelea Ya Mradi Wa Mabasi Yaendayo kasi

    Hawa Ghasia

    Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI), Bi. Hawa Ghasia ameridhishwa na tathimini ya mkutano wa mashauriaono wa awamu ya kwanza wa Mradi wa Mabasi yaendeyo Haraka (DART) uliofanyika hivi karibuni ukiwemo pia na wa kampuni ya Simon Group inayomiliki mabasi ya UDA na wamiliki wa usafirishaji jijini Dar es Salaam.

  • Arsenal Yaifunga 1-0 Besiktas Na Kufuzu UEFA Kwa Msimu Wa 17 Mfululizo

    Arsenal Yaifunga 1-0 Besiktas Na Kufuzu UEFA Kwa Msimu Wa 17 Mfululizo

    Arsenal

    Timu Ya Arsenal ya nchini Uingereza jana usiku iliweza kufuzu kucheza mashindano ya kombe la UEFA kwa msimu wa 17  mfululizo kwa timu za Ulaya baada ya kuichapa timu ya Besiktas ya Uturuki kwa bao 1-0.

    Katika mchezo wa awali wiki mbili zilizopita timu hizo zilitoka sare ya bila kufungana na hivyo kusubiri uamuzi wa nani atavuka katika mechi ya pili ya marudiano ambayo ilichezwa jana usiku. Alikuwa ni mchezaji mpya wa timu ya Arsenal aliyejiunga msumu huu akitokea timu ya FC Barcelona Alex  Sanchez, ambaye ndiye aliyeiwezesha Arsenal kusonga mbele baada ya kuipatia timu yake bao hilo pekee la ushindi kwa timu yake katika dakika ya 46 ya kipindi cha kwanza.

    Arsenal ilipata nafasi ya kumaliza mchezo huo mapema lakini washambuliaji wake Santi Cazorla na Alex Chamberlain walipoteza nafasi nyingi za wazi walizopata.

    Timu ya Arsenal ilipata pigo la kupungukiwa na mchezaji mmoja uwanjani, zikiwa zimesalia dakika 15 kabla ya kumalizika kwa mchezo,  baada ya mchezaji wake Mathieu De Buchy kutolewa nje ya mchezo kwa kadi mbili za njano na kufanikiwa kupambana wakilinda ushindi wao kiduchu hadi mwisho wa mchezo.

    Timu nyingine zilizofuzu pamoja na Arsenal katika kinyang’anyiro cha kufuzu jana usiku ni pamoja na Atletico Bilbao 3-1 dhidi ya Napoli,  Bayer 04 Leverkusen 4-0 dhidi ya FC Copenhagen, Ludogorets Razgrad 1-0 dhidi ya Steau Bucharest na Malmo FF – 3-0 dhidi ya Fc Red Bull Salzburg.

     

     

     

     

  • P Square Kuachia Nyimbo Tatu Leo Ndani Ya Saa 48, Moja Ni Kolabo Na TI

    P Square Kuachia Nyimbo Tatu Leo Ndani Ya Saa 48, Moja Ni Kolabo Na TI

    Kundi la muziki la Mapacha wawili wa Ki Nigeria P Square kuanzia Alhamisi ya leo na ndani ya masaa 48 wanategemewa kuachia nyimbo tatu mfululizo moja kati ya hizo ikiwa collabo kali ya kimataifa.
    Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa meneja wa wasanii hao Jude Okoye ambaye pia ni kaka yao wasanii hao wataachia nyimbo hizo kupitia record lebo yao ya Square Music. Wasanii hao ambao wamejijengea sifa kubwa ulimwenguni kote kwa sasa wanatamba na kibao cha “Taste The Money”.
    Nyimbo hizo ni pamoja na “Ejeajo” waliyomshirikisha rapa wa Ki Marekani TI ambayo itatoka na Video yake inayosemekana kuwa kali sana ikifuatiwa na wimbo “Shekini “ kabla ya kuhitimisha na wimbo wa tatu “Bring it On” waliomshirikisha Dave Sott.

  • Man UTD Yachapwa 4-0. Van Gaal Alaumu Wachezaji Wake

    Man UTD Yachapwa 4-0. Van Gaal Alaumu Wachezaji Wake

    Van GaalBaada ya kipigo cha magoli 4-0 dhidi ya timu yake,  Meneja wa klabu ya Man Utd Van Gaal amelia na kikosi chake ambacho jana usiku kiliendelea kupata matokeo mabaya tangu kuanza kwa msimu mpya wa soka huko nchini Uingereza Agosti 16.
    Kocha Van Gaal amesema kikosi chake hakikucheza vizuri wakati wa mchezo wa michuano ya kombe la ligi dhidi ya klabu ya Milton Keynes Dons ambao waliibuka na ushindi wa mabao manne kwa sifuri na kuwatupa nje ya michuano hiyo mashetani wekundu.
    Pia Van Gaal amesema makosa madogo madogo yaliyofanywa na wachezaji wake wa safu ya ulinzi yalitoa mwanya mkubwa kwa wapinzani wao kupata mabao kwa urahisi. Akiendelea kulalamika kocha huyo alisema hana budi kuwasilisha lawama zake kwa wachezaji aliokuwa amewapa jukumu la kucheza mechi ya jana usiku.

  • Mapigano Baina Ya Israel Na Wapalestina Yasimama Gaza

    Mapigano Baina Ya Israel Na Wapalestina Yasimama Gaza

    Gaza

    Israel na wapiganaji wa Ki Palestina wamekubaliana kusitisha mapigano kwa muda mrefu katika ukanda wa Gaza.
    Kusitishwa kwa mapigano hayo, kumehitimisha wiki saba za vita vilivyosababisha vifo vya watu zaidi ya 2,200, wengi wao wakiwa Wapalestina. Mazungumzo hayo yalisimamiwa na Misri na yalianza kutekelezwa jana kuanzia majira ya saa moja usiku.
    Hamas wamesema mpango huo unawakilisha “ushindi wa upinzani wao”.Maafisa wa Israel wamesema Israel italegeza vikwazo ilivyoiwekea Gaza ili kuruhusu misaada na vifaa vya ujenzi kuingia Gaza.
    Rais wa Wapalestina Mahmoud Abbas ametangaza kukubaliana na mpango wa kusitisha mapigano.Msemaji wa serikali ya Israeli, Mark Regev amesema: “hebu tuwe na matumaini kwamba mpango huu wa kusitisha mapigano utaheshimika”
    Mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja katika masuala yenye utata, ikiwa ni pamoja na wito wa Israel wa kuyataka makundi ya wapiganaji yanapokonywa silaha, yataanza mjini Cairo katika kipindi cha mwezi mmoja.
    Marekani imeunga mkono kikamilifu mpango huu, kwa msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani Jen Psaki kusema: “tunaunga mkono kikamilifu tangazo la kusitisha mapigano.”
    Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon pia amepongeza mpango huo wa kusitisha mapigano. Lakini katika taarifa kupitia kwa msemaji wake, Bwana Ban ameonya kuwa “jitihada yoyote ya amani ambayo haishughulikii chanzo halisi cha mgogoro, itafanya kazi kidogo kuliko kutengeneza mzunguko mwingine wa ghasia”.
    Hatua ya kusitisha mapigano imekuja huku Israel na Wapalestina wakiendelea kushambuliana.
    Kombora la dakika ya mwisho ya makabiliano kutoka Gaza limemuua raia wa Israel na kuwajeruhi wengine sita katika Barazala la Jimbo la Eshkol.
    Mapema Jumanne, Wapalestina wapatao sita waliuawa katika mfululizo wa mashambulio ya anga ya Israel huko in Gaza, Wamesema maofisa wa Palestina.
    Maofisa wa Palestina wamesema pendekezo la Misri la kusitisha mapigano linataka kumalizwa kwa uhasama kusiko na kikomo, kufunguliwa haraka kwa mipaka ya Gaza na Israel na Misri na kuongezewa ukanda wa uvuvi katika bahari ya Mediterani..
    Tangazo la kusitisha mapigano lilishangiliwa na Wapalestina katika mji wa Gaza.
    Kabla ya kuanza utekelezaji wa mpango huo, majengo marefu mjini Gaza yalishambuliwa na makombora zaidi yalipiga Israel.
    Mwezi mmoja baadaye Israel na vikundi vya Wapalestina vitajadili ujenzi wa bandari na uwanja wa ndege huko Gaza na kuwaachilia huru wafungwa 100
    Israel na Misri pia zimesemekana kutaka kuhakikishiwa kuwa silaha hazitaingizwa Gaza kwa njia ya magendo.

     

  • Rais Kikwete Kukutana Na Ukawa Hivi Karibuni

    Rais Kikwete Kukutana Na Ukawa Hivi Karibuni

    Jakaya-Kikwete

    Rais Jakaya Kikwete anatarajia kukutana na viongozi wa Vyama vya Siasa vinavyounda Kituo cha Demokrasia Tanzania (TCD) ili kuzungumzia mchakato wa Katiba wakati wowote wiki hii.
    Katika mkutano huo, ambao unasubiriwa kwa hamu, Rais Kikwete atakutaka na wajumbe wa Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ambao unaundwa na vyama vya NCCR-Mageuzi, Chadema na CUF.
    Aprili 16, mwaka huu wajumbe wa Ukawa na baadhi kutoka Kundi la 201, walisusia vikao vya Bunge hilo wakitaka msingi wa mapendekezo ya Rasimu ya Katiba usibadilishwe, wakipinga uamuzi wa CCM kutaka kuingiza mfumo wa serikali mbili badala ya tatu zilizopendekezwa katika Rasimu.
    TCD inaundwa na vyama vya siasa vyenye uwakilishi bungeni ambavyo ni CCM, CUF, Chadema, NCCR-Mageuzi, UDP na TLP, huku vyama visivyo na uwakilishi bungeni vikiwakilishwa na UPDP kinachoongozwa na Fahmi Dovutwa.
    Jana, kwa nyakati tofauti wenyeviti wenza wa Ukawa, Freeman Mbowe (Chadema) na Profesa Ibrahim Lipumba (CUF) na James Mbatia (NCCR Mageuzi), walisema wako tayari kukutana na Rais, ila msimamo wao wa kutaka ijadiliwe rasimu iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
    Kimekuwa ni kilio cha muda mrefu kwa Ukawa kuomba wakutane na Rais Kikwete kwa ajili ya kujadiliana namna bora ya kuendesha mchakato wa kupata Katiba Mpya.
    Akizungumza na waandishi wa habari bungeni Dodoma jana, Mwenyekiti wa TCD, John Cheyo alisema Rais atafanya kikao hicho wakati wowote ndani ya wiki hii na kwamba viongozi wa vyama wakiwamo wa Ukawa, wamethibitisha kushiriki.
    Cheyo alisema, katika kikao walichokutana Dar es Salaam Agosti 23, wanachama wa TCD walikubaliana kwamba upo umuhimu wa kukutana na Rais Kikwete kwa mazungumzo na maridhiano.
    Kukutana kwa viongozi hao, kunakuja huku wajumbe wa Bunge Maalumu wakiwa wamemaliza kujadili sura zote 15 zilizokuwa zimesalia na tayari baadhi ya kamati zimemaliza kupiga kura wakisubiri kuingia bungeni Septemba 2 kwa kazi ya kupigia kura sura kwa sura.
    Kuhusu viongozi wa Ukawa, alisema wanazo taarifa na baadhi yao walikuwapo katika kikao cha kujadili kukutana na kiongozi huyo wa nchi, hivyo akasema lazima watashiriki wakati wowote wakiitwa.
    Lipumba
    Akizungumzia mkutano huo na Rais, Profesa Lipumba alisema: “Tunakutana na Rais Kikwete kwa sababu sisi ni wanachama wa TCD.” Alipoulizwa juu ya msimamo wa Ukawa, alisema lengo ni kutafuta mwafaka ili mchakato wa kupata Katiba Mpya uendeshwe kwa kufuata sheria, kanuni na taratibu.
    “Kikubwa tunachokitaka ni maoni ya wananchi yaliyokusanywa na Tume ya Katiba iliyokuwa ikiongozwa na Jaji Warioba kuheshimiwa na siyo kuchukuliwa maoni mengine kama inavyofanyika sasa huko bungeni,” alisema Profesa Lipumba.

    Mbowe
    Mbowe alisema Katiba Mpya ni kwa masilahi ya Watanzania wote na Taifa lao, hivyo inapotokea mikutano kama hiyo na kwa hali ilivyo sasa, hakuna mtu mwenye nia njema atakayekataa kushiriki. Kikubwa ni kwamba hatuwezi kubadili msimamo wetu na huo ndiyo ukweli,” alisema.
    Kuhusu Bunge hilo kupokea maoni ya makundi mbalimbali wakati tayari ukusanyaji wa maoni umeshafanywa na Tume ya Jaji Warioba, Mbowe alisema, “Ndiyo maana tulisusia vikao vya Bunge la Katiba, nadhani sasa Watanzania wamejua kwa nini tulitoka nje.”
    Mbowe alisema kuwa mchakato wa Katiba unaendeshwa kwa mujibu wa sheria, lakini hivi sasa Mwenyekiti wa Bunge hilo, Samwel Sitta analiendesha Bunge hilo kinyume na sheria hiyo… “Ukusanyaji wa maoni unaofanyika sasa ni fedheha kwa CCM na Serikali, ni utoto na aibu wa CCM. Kwa sasa Ukawa tumetulia tunatazama hali inavyokwenda na tuna mipango yetu ambayo tunapanga. Kama hali ikiendelea kuwa hivi tutachukua uamuzi mgumu ili dunia nzima ijue.”

    James Mbatia
    Alisema wako tayari kukutana na Rais Kikwete kwa ushauriano kwa sababu suala la maridhiano ni la msingi na viongozi wote wa TCD walikubaliana Agosti 23.
    “Mwaliko tumeupata na tutashiriki. Bunge linaweza kuendelea kwa taratibu zake za kisheria, lakini suala la mashauriano, lazima tukae tuangalie ni jinsi gani Taifa letu linaweza likavuka kwa maridhiano kwa amani na utulivu,” alisema.
    Kauli ya Ikulu
    Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, Salva Rweyemamu alisema Rais Kikwete yuko tayari kukutana na viongozi wa vyama vya siasa muda wowote… “Wao wafuate utaratibu tu, Rais hawezi kukataa kukutana nao na hilo amekuwa akilisema mara nyingi tu.”

     

     

  • Bunge Latuhumiwa Kufanya Kazi Ya Kukusanya Maoni Upya

    Bunge Latuhumiwa Kufanya Kazi Ya Kukusanya Maoni Upya

    BUNGE_SITTA

    Kitendo cha Bunge Maalumu la Katiba kukusanya maoni ya makundi na wananchi mbalimbali, kimepokewa kwa hisia tofauti, baadhi ya wasomi wakisema ni kinyume cha sheria na kuonyesha kutapatapa huku Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba akisema linafanya kazi ambayo tayari tume yake ilishaifanya.
    Hata hivyo, Katibu wa Bunge hilo, Yahya Khamis Hamad amesema litaendelea kupokea mapendekezo kutoka kwa watu na makundi mbalimbali hadi hapo litakapohitimisha kazi yake.
    Kwa muda sasa, wawakilishi wa taasisi mbalimbali wamekuwa wakifika Dodoma kuwasilisha mapendekezo yao wakitaka yazingatiwe kwenye Katiba Mpya kwa maelezo ya kutoonekana katika rasimu ya Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
    Suala hilo limezua mjadala hasa katika mitandao ya kijamii ambako watu mbalimbali wamekuwa wakihoji sababu za Bunge hilo kufanya kile kinachotafsiriwa kuwa ni ‘kukusanya maoni’, kazi ambayo tayari ilishafanywa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba.
    Akitetea hoja hiyo, Hamad alitetea akisema wananchi, watu au taasisi zinazotoa mapendekezo yao zinashirikiana na wabunge katika mchakato wa kile kinachoendelea bungeni hivi sasa.
    “Tutaendelea kupokea maoni ya wananchi kwa sababu na sisi tunaendelea kujadili, kwa hiyo kadri makundi yatakavyoleta maoni yao, tutayapokea na kuyapitisha kwenye mchakato wa kuyawezesha kuzingatiwa kama yataonekana yanafaa,” alisema Hamad.
    Warioba na wasomi
    Akizungumzia hatua hiyo, Jaji Warioba aliponda kitendo cha kukusanywa upya kwa maoni hayo akisema yalishachukuliwa na Tume yake na kuingizwa katika Rasimu ya Katiba.
    “Nyaraka zote za maoni, yakiwamo ya makundi hayo tuliziwasilisha, sasa wanakusanya maoni mapya ili iweje? Wanatakiwa kufuata maoni ya wananchi na si ya makundi na kama wanafanya hivyo basi maoni ya makundi hayo yakusanywe hadharani ili wananchi wayasikie ili nao waweze kuchangia,” alisema jana.
    Alitolea mfano wa maoni yaliyotolewa na Jumuiya ya Serikali za Mitaa Tanzania (ALAT), kwamba ni makosa kuchukua maoni hayo na kuyaacha yaliyotolewa nawananchi.
    “Naona kuhusu ardhi eti wamechukua maoni ya Wizara ya Ardhi na Maendeleo ya Makazi, hii si sahihi kabisa. Kama wanajadili suala la serikali za mitaa, ardhi na maliasili wanatakiwa kuyaongeza mambo hayo katika mambo ya muungano kwa sababu hivi sasa mambo hayo si ya muungano na ndiyo maana Tume hatukuyaingiza katika Rasimu ya Katiba,” alisema.
    aji Warioba alilitaka Bunge hilo kutochakachua maoni kuhusu ardhi, maliasili na ardhi ambayo Tume yake iliyawasilisha serikalini ili baadaye yaingizwe katika Katiba ya Tanganyika, “Wakiyaingiza mambo hayo katika Katiba ya Muungano, yatapingana na Katiba ya Zanzibar na kuleta shida.”
    Mtaalamu wa lugha na falsafa, Faraja Christoms alisema, “Kinachofanyika Dodoma ni dalili ya kutapatapa. Wanatakiwa kukumbushwa kuwa wanachokifanya si sahihi na ni kinyume na sheria, kifupi ni kwamba Bunge la Katiba limepoteza mwelekeo.”
    Mhadhiri wa Idara ya Sayansi za kwenye Maji na Uvuvi Chuo Kikuu Dar es Salaam (UDSM),Dk Charles Lugomela alisema: “Bunge limekosa mwelekeo kwa sababu Katiba ni suala la maridhiano ya kisiasa na linatakiwa kuendeshwa kwa nguvu ya hoja na si hoja ya nguvu.”
    Mwenyekiti wa Jukwaa la Katiba Tanzania (Jukata), Deus Kibamba alisema Bunge hilo sasa linakwenda mwendo wa gari bovu, huku akimtuhumu Mwenyekiti wake, Samuel Sitta kuwa analiendesha kwa mtindo wa comedy (vichekesho) na si kufuata kanuni na sheria.
    “Ndiyo maana tulimtaka Sitta aliahirishe Bunge kwa sababu anaweza kwa mujibu wa Kifungu cha 28(4) ambacho walikibadili na kujipa mamlaka ya kulifanya Bunge hilo kuendelea mpaka pale itakapoonekana inafaa,” alisema Kibamba.
    Mtaalamu wa lugha ya Kiswahili, Dk Aldin Mutembei alisema: “Kinachofanyika Dodoma ni makosa na wajumbe wanafanya mambo ambayo hayakutakiwa kufanyika, kifupi ni kwamba wanakwenda kinyume na utaratibu.”
    Mutembei alisema kitendo hicho kinastaajabisha na ni matokeo ya kutofuatwa kwa sheria zilizozalisha Bunge hilo na mchakato wote wa kuandika Katiba Mpya.
    Maoni ya Takukuru
    Miongoni mwa makundi yaliyowasilisha maoni ni Taasisi ya Kuzuia na Kupamba na Rushwa (Takukuru) ambayo imependekeza kuanzishwa kwa divisheni katika Mahakama Kuu ya Tanzania itakayokuwa na wajibu wa kusikiliza kesi zote zinazopelelezwa na kufikishwa mahakamani na taasisi hiyo.
    Pia, inashauri kuanzishwa kwa ‘Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa na Uhujumu Uchumi’ ambayo itakuwa moja ya taasisi za uwajibikaji zinazotajwa katika sura ya 13 ya Rasimu ya Katiba.
    Katika Rasimu iliyotolewa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Takukuru haikutajwa kwani ilipaswa kuwa kwenye Katiba ya Tanganyika.
    Mapendekezo ya Takukuru ni miongoni mwa mengine saba ambayo uongozi wa Bunge Maalumu umeyapeleka katika kamati zote 12 ili kubaini iwapo yanafaa kuingizwa kwenye Rasimu ya Katiba kabla ya kamati hizo kuwasilisha taarifa zake za uchambuzi bungeni kuanzia wiki ijayo.
    “Si kwamba yote ni sura mpya, mengine ni nyongeza katika ibara sura zilizopo kwenye Rasimu ya Katiba, kwa hiyo kwa sababu wajumbe walishafanya uchambuzi wa sura zote, itakuwa rahisi kwao kujua wapi waingize kipi,” alisema Hamad.

    Mapendekezo mengine
    Mapendekezo mengine yaliyofanyiwa uchambuzi ni yale yanayohusu muundo wa serikali ambayo yamewasilishwa na mwanasheria na mwalimu, Onesmo Kyauke ambaye katika mapendekezo yake, ametaka muundo wa muungano usizingatie idadi ya Serikali, bali mgawanyo wa madaraka wa nguzo tatu za dola ambazo ni Mahakama, Bunge na Serikali.
    Pia yapo mapendekezo yanayohusu masuala ya ardhi, mazingira na rasilimali za Taifa, kutoka Tume ya Mabadiliko ya Katiba ambayo ni mapya kwani hayamo kwenye rasimu ya sasa.
    Taasisi nyingine zilizowasilisha mapendekezo ya sura inayohusu masuala ya ardhi, mazingira na rasilimali za Taifa ni Wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, pamoja na wajumbe wa Bunge Maalumu wanaotetea wakulima, wafugaji na wavuvi.
    Pendekezo jingine ni lile la sura mpya ya Serikali za Mitaa na ugatuaji wa madaraka kwa wananchi yaliyowasilishwa na Tume ya Mabadiliko ya Katiba pamoja na Alat.
    Pia yapo mapendekezo kuhusu haki za wakulima kutoka Chama cha Wakulima wa Pamba Tanzania (TACOGA), ambayo uongozi wa Bunge umeelekeza yajadiliwe pamoja na yale yanayohusu ardhi bila kusahau mapendekezo ya Shirikisho la Wasanii (Taff).

     

     

     

  • Rais Kikwete Aipa Halmashauri Ya Kilosa Wiki Moja Kuwapatia Wahanga Wa Mafuriko Viwanja

    Rais Kikwete Aipa Halmashauri Ya Kilosa Wiki Moja Kuwapatia Wahanga Wa Mafuriko Viwanja

    Jakaya-Kikwete

    Rais JAKAYA KIKWETE ametoa wiki moja kwa uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa, Mkoani Morogoro, kuwapatia viwanja vya kujenga nyumba wahanga wa mafuriko ya kiasi cha miaka minne iliyopita mjini Kilosa.Rais KIKWETE ametoa agizo hilo mkoani Morogoro alipokuwa akizungumza na wananchi wa Kilosa katika mkutano wa hadhara uliofanyika mjini Kilosa baada ya kutembelea Wilaya hiyo kukagua na kuzindua miradi ya maendeleo.Agizo hilo limekuja kufuatia malalamiko yaliyotolewa na wahanga hao kwa njia ya maneno na mabango baada ya kuwa wameahidiwa viwanja hivyo na Rais KIKWETE mwenyewe wakati alipowatembelea kufuatia mafuriko ya Mto Mkondoa miaka minne iliyopita.

  • Dar es Salaam ikinyesha mvua kidogo tu basi NI SHIDAAAA

    Dar es Salaam ikinyesha mvua kidogo tu basi NI SHIDAAAA

    20140327_065455

    Haya ni maeneo ya Mikocheni Tanesco ambapo huwaga hivi kama siku itanyesha mvua kubwa…husababisha foleni kubwa ya magari kwa wafanyakazi waendao makazini nyakati za asubuhi.

    20140327_06562720140327_06570520140327_065722