P Square Kuachia Nyimbo Tatu Leo Ndani Ya Saa 48, Moja Ni Kolabo Na TI

P Square Kuachia Nyimbo Tatu Leo Ndani Ya Saa 48, Moja Ni Kolabo Na TI

Like
605
0
Thursday, 28 August 2014
Entertanment

Kundi la muziki la Mapacha wawili wa Ki Nigeria P Square kuanzia Alhamisi ya leo na ndani ya masaa 48 wanategemewa kuachia nyimbo tatu mfululizo moja kati ya hizo ikiwa collabo kali ya kimataifa.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa meneja wa wasanii hao Jude Okoye ambaye pia ni kaka yao wasanii hao wataachia nyimbo hizo kupitia record lebo yao ya Square Music. Wasanii hao ambao wamejijengea sifa kubwa ulimwenguni kote kwa sasa wanatamba na kibao cha “Taste The Money”.
Nyimbo hizo ni pamoja na “Ejeajo” waliyomshirikisha rapa wa Ki Marekani TI ambayo itatoka na Video yake inayosemekana kuwa kali sana ikifuatiwa na wimbo “Shekini “ kabla ya kuhitimisha na wimbo wa tatu “Bring it On” waliomshirikisha Dave Sott.

Comments are closed.