Author: E-FM CO LTD

  • Nigeria yasuburia matokeo ya uchaguzi

    Nigeria yasuburia matokeo ya uchaguzi

    Kura zinaendelea kuhesabiwa nchini Nigeria kufuatia uchaguzi mkuu wa nchi hiyo,Hata hivyo upigaji kura ulisogezwa kufikia siku ya pili katika maeneo machache

    Kutokana na hitilafu ya mambo,kutokukamilika kwa mipango na vurugu katika baadhi ya maeneo uchaguzi umesogezwa mpaka hapo baadae.

    Raisi Muhamadu Buhari mwenye miaka 76 anatetea kiti chake kwa awamu ya pili .Mpinzani wake mkuu ni Makamu wa Rais wa zamani Atiku Abubakar, 72.

    Uchaguzi ulitakiwa kufanyika juma moja lililopita na baadae kuahirishwa katika dakika za lala salama

    Kwa yeyote atakeshinda na kukikalia kiti hicho katika taifa hilo lenye watu wengi zaidi Barani Afrika na uchumi mkubwa atakabiliwa na suala la ukosefu nishati ya uhakika,Rushwa ,tishio la kiusalama na kuporomoka kwa uchumi.

    Rais Buhari alipiga kura yake katika mji wa Daura kaskazini mwa mkoa wa Katsina.Alipoulizwa kama atampongeza mpinzani wake pale atakapoangushwa kwenye uchaguzi huo alisema. ”Nitajipongeza Mwenyewe”

    karatasi ya majina ilikua ndefu ili kuweka wagombea wote 73

    Bwana Abubakar,Mfanyabiashara Mkubwa ,Amesema ana Imani ya kushinda uchaguzi.

    Huenda matokeo yakatangwazwa siku ya Jumatatu

    Uchaguzi ulikua wa Amani?

    Sehemu kubwa ya nchi hiyo ilionekana kua katika utulivu lakini kumekua na taarifa za uwepo wa Kundi la wapiganaji la Boko Haram eneo la kaskazini,Wapiga kura walitishwa huku wakijaribu kutaka kuiba masanduku ya kura katika sehemu ya vituo Hasa katika mikoa ya Kaskazini , Lagos na Anambra.

    Muungano wa makundi ya asasi za kiraia umeripoti kua jumla ya watu 16 waliuawa -Idadi mbayo ni ndogo ikilinganiswa na uchaguzi Uliopita

    Watu wawili walitiwa kizuizini katika mkoa wa Surulere eneo la mji mkubwa wa kibiashara Lagos , baada ya wapiga kura kuvamiwa na kundi la vijana wadogo Wakiwa na silaha kama jambia,shoka na Vitu vyenye ncha kali.

    Maboxi ya kupigia kura yaliteketezwa katika Wilaya Isolo huko Lagos.

    Tume ya Uchaguzi yenyewe inasema kua uchaguzi haukuwezekana katika vituo 8,500 kati ya vile 120,000 katika eneo lote la nchi ,Shirika la Habari la AFP Limeripoti.

    Mgombea atakayepata kura nyingi atatangazwa kua mshindi katika duru ya kwanza ya uchaguzi ,Hii ikiwa atapata asilimia 25% ya kura katika mbili ya tatu ya majimbo 36

    Wagombea wa nafasi ya uraisi walikua 73 ,lakini ushindani mzito Zaidi ulishuhudiwa kati ya raisi wa sasa Muhamadu Buhari na mfanyabiashara mkubwa Nchini Humo Atiku Aboubakar

    Takwimu za Uchaguzi

    73 million waliojiandikisha kupiga kura

    51% wapiga kura chini ya mika

    73 Wagombea wa nafasi ya Uraisi

    120,000 Vituo vya kupigia kura

     

    cc;BBCswahili

     

  • alinusurika kunyongwa mara tatu

    alinusurika kunyongwa mara tatu

    Katika hukumu ya kifo nchini Malawi,Byson Kaula alikuwa karibu anyongwe mara tatu lakini kila zamu yake ilipofika, mnyogaji aliacha kunyonga na kudai kuwa amechoka kabla hajamaliza watu wote ambao waliokuwa kwenye orodha yake.

    Hivyo kutokana na kuhairishwa huko Kaula aliweza kunusurika kifo mpaka taifa hilo lilipoacha kutoa adhabu ya kunyonga.

    Byson Kaula anasema kuwa ni jirani zake wenye wivu ndio walihusika kusababisha yeye apatikane na hatia ya uuaji.

    Ilikuwa mwaka 1992, wakati aambapo mtu akiua hukumu ya kunyongwa ilikuwa ni lazima.

    Byson alikulia katika kijiji kidogo kusini mwa Malawi na baadae aliweza kupata kipato akilichomtosha kwa kufanya kazi katika kiwanda cha gesi kilichopo Johannesburg, Afrika kusini.

    Na aliporudi nyumbani aliweza kununua ardhi na kuajiriwi watu watato ambao walikuwa wanamlimia mazao ya chakula na matunda.

    “Niliporudi nyumbani baada ya mafanikio ndio wakati wa huzuni ulipoanza,”Byson alisema.

    Majirani walimvamia mmoja wa wafanyakazi wangu na kumuacha akiwa amejeruhiwa, Byson alisema.

    Mwanaume huyo alivyoumizwa alishindwa kutembea bila msaada na wakati alipoenda kumsaidia kwenda maliwatoni, kwa bahati mbaya alianguka chooni.

    Mwanaume huyo alikufa mara baada ya kufikishwa hospitalini, na wakati huo Byson alikuwa na umri wa miaka 40 alishitakiwa kwa mauaji.

    Majirani zake Byson walitoa ushaidi dhidi yake mahakamani.

    Mama yake aitwaye Lucy hakusikia kile ambacho kilikuwa kinaendelea mahakamani kwa sababu alikuwa amekaa nyuma na alipouliza nini kilichoendelea aliambwa kuwa mwanae amehukumiwa kunyongwa, machozi yalimmiminika tu mpaka kifuani.

    Kipindi hicho kilikuwa wakati wa utawala wa serikali ya Banda, mwaka 1964.

    Byson anakumbuka vyema mateso yote ambayo aliyapitia wakati anasubiri kunyongwa kwa mashine.

    “Nilipoambiwa kuwa ninaweza kwenda niko huru na muda wangu wa kusubiri kunyongwa umeisha’ -yani nilijihisi kwanza kuwa nilishakufa tayari.”

    Byson anakumbuka siku moja aliambiwa kuwa jina lake lipo kati ya watu 21 ambao watanyongwa ndani ya saa chache. Walinzi walimwambia kuwa awe tayari kunyongwa majira ya saa saba, hivyo inabidi asali maombi yake ya mwisho.


    Watu waliendelea kunyongwa mpaka saa tisa, ndipo mnyongaji akaacha kufanya kazi hiyo wakati alikuwa hajamaliza watu ambao alikuwa nao katika orodha.

    Watu watatu walinusurika, Byson akiwemo katika majina hayo.

    “Alikuwa mtu mmoja tu ndio anaiendesha mashine hiyo. Na siku hiyo nilielewa kuwa alikuwa amechoka na alikuwa anatokea Afrika kusini, hivyo alivyoghairi alidai kurudi tena mwezi ujao”,Byson alisema.


    Jambo hilohilo la mnyongaji kuchoka kabla hajamaliza orodha yake lilijirudia mara mbili zaidi na Byson akaachwa hai.

    Kuna wakati ambapo wengine wote waliohukumiwa kunyongwa walinyongwa bali alibaki yeye tu”. Byson alisema.

    Kwa namna ambavyo alikuwa na bahati ya kupona kunyongwa, yeye mwenyewe alijaribu kujiua mara mbili na kupona pia.

    Baada ya vyama vingi kuanzishwa nchini Malawi mwaka 1994 , unyongwaji ulisitishwa na hukumu hiyo ikawa inatolewa tu pale ambapo rais atasaini lakini kwa miaka 25, hakuna rais aliyesaini ili wafungwa wanyongwe au wafungwe maisha.

    Muda ulivyoendelea kusogea, Byson alipata elimu ya gerezani na kuondolewa hukumu ya kifo kuwa kifungo cha maisha.

    Mwaka 2007, karibu nusu karne tangu Byson afungwe, kesi moja ya kihistoria ilibadili kila kitu.

    Mtumia madawa ya kulevya ambaye alikiri kumuua mama yake wa kambo, lakini alidaiwa kuwa hana akili vizuri alipoenda mahakamani na kuhoji juu ya hukumu ya kifo.Alitaka hukumu hiyo iangaliwe vizuri katika katiba ya nchi hiyo ili hukumu hiyo iweze kutolewa kwa haki.

    Na mara baada ya hukumu za kifo za wafungwa 170 kuhakikiwa, wafungwa 139 waliachiwa huru.

    Ingawa kwa mujibu wa kituo cha sheria cha kujitolea alidai kuwa wengi walioachiwa huru walipatwa na matatizo ya akili na wengine walipata ulimavu.

    Zaidi ya nusu ya wafungwa waliachiwa huru walikuwa hawamo hata kwenye rekodi ya mahakama, na wengine ilikuwa haieleweki kwa nini walikuwa geezani.

    “Ilikuwa kama ninaota -sikuamini kile ambacho jaji alikisema” Byson alisema.

    Byson aliachiwa huru aliwa na miaka 60, na sasa anajitolea kwenda gerezani mwishoni mwa wiki ili kutoa ushauri kwa wafungwa kwa kueleza kile alichopitia.

    Mke wake alifariki dunia wakati yeye yuko gerezani na kuwaacha watoto sita ambao aliwakuta wamekuwa tayari baada ya kukaa muda mrefu gerezani.

    Byson anaishi mwenyewe ila anamtunza mama yake ambaye ana umri wa miaka 80.

    Hukumu ya kifo imesalia kuwa ni ya lazima kwa baadhi ya visa vya uhalifu – na kubaki kuwa miongoni mwa hukumu yenye utata duniani.

    Kwa sehemu kubwa, imekuwa ikipingwa mahakamani, huku baadhi ya nchi ikiiondoa katika katiba yake, baada ya kugundua inakinzana na haki za binadamu.

     

    cc: BBCswahili

  • Serikali yakerwa na vitendo vya mauaji na unyang’anyi mipakani

    Serikali yakerwa na vitendo vya mauaji na unyang’anyi mipakani

    Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameviagiza vyombo vya ulinzi na usalama kuongeza ulinzi na doria katika maeneo ya mipaka kutokana na ongezeko la vitendo vya mauaji, unyang’anyi wa kutumia silaha na vitisho kwa wananchi.

    Ametoa agizo hilo alipokuwa akizungumza na wananchi katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye Uwanja wa Taifa wilayani Kibondo wakati akihitimisha ziara yake mkoani Kigoma.

    Pia, Waziri Mkuu ameagiza wakimbizi wote watakaobainika kutoroka kwenye makambi wanayohifadhiwa na kuingia uraiani wakamatwe na wachukuliwe hatua kwa mujibu wa sheria za Tanzania, kwani wanachokifanya ni ukiukwaji wa sheria.

    Aidha, maeneo yaliyo katika hali mbaya ni Kibondo, Buhigwe, Kasulu, Ngara, Biharamulo, Uvinza, Kakonko na Kigoma Vijijini, ambako wananchi hususani wafanyabiashara wameingiwa na hofu kutokana na vitendo hivyo.

    ”Kulinda usalama wa nchi ni jukumu letu sote na si la vyombo vya ulinzi na usalama pekee, kila mmoja anapaswa kushiriki. Kwa upande wa majirani zetu wanaotaka kuja nchini ni lazima wafuate taratibu kwa kuomba vibali.”amesema Majaliwa

    Hata hivyo, Majaliwa ameongeza kuwa watu wote wanaoingia bila ya kufuata sheria na taratibu ndio hao wanashiriki katika vitendo vya uhalifu yakiwemo mauaji ya raia wasiokuwa na hatia, unyang’ani wa kutumia silaha za kivita pamoja na utekaji wa watoto.

     

  • Meneja afia kwenye kiti akizungumza na waandishi wa habari

    Meneja afia kwenye kiti akizungumza na waandishi wa habari

    Meneja wa Wakala wa Huduma za Misitu, Glory Mziray amefariki dunia jana majira ya mchana akiwa ofisini kwake jengo la Mpingo wakati akifanya mkutano na waandishi wa habari juu ya kupandishwa hadhi kwa misitu 7.

    Meneja huyo alishikwa na umauti wakati akijibu maswali ya waandishi wa habari yaliyotokana na kile alichokuwa akiwasilisha.

    Hapa ndipo ule msemo usemao hakuna ajuaye siku wala saa unavyotimia kwa meneja huyu kijana, ambaye dakika chache zilizopita hakuwa mgonjwa wala hakuonesha kupata shida yeyote kwani alijiandaa vyema kuiwakilisha wizara yake.

    Glory alikutwa na mauti mara baada ya mmoja ya mwandishi wa habari kumtaka ajitambulishe kwa majina na cheo chake kwani hakufanya hivyo mwanzoni wakati akitoa hotuba yake.

    Ambapo dakika kadhaa baada ya kusimama kujibu swali hilo, Glory alianza kubadilika gafla na kuanza kupoteza sauti na kupoteza fahamu kabisa.

    Wanahabari walimpa huduma ya kwanza bila mafanikio, ndipo wakaamua kumkimbiza hospitali ya TMJ chang’ombe ambapo madaktari walimfanyia uchunguzi na kubaini kuwa alipoteza maisha kabla ya kufika hospitali hapo.

    Aidha, Daktari Chris Peterson ameeleza kuwa familia yake imesema Glory alikuwa na tatizo la Shinikizo la damu.

     

  • Atapokonywa uraia kwa kuwa mfuasi wa Islamic State

    Atapokonywa uraia kwa kuwa mfuasi wa Islamic State

    Shamima Begum, aliyejiunga na kundi la wapiganaji wa Islamic State nchini Syria akiwa na miaka 15, atapoteza uraia wake Uingereza.

    Shamima Begum ametafuta hifadhi katika kambi ya wakimbizi Syria

    Duru kutoka serikalini zilisema inawezekana kumvua uraia msichana huyo mwenye umri wa miaka 19 raia wa Uingereza kwasababu ana nafasi ya kupata uraia wa nchi nyingine.

    Wakili wa familia yake, kwa uamuzi huo na wanatathmini ‘njia zote kisheria’ kukabiliana na hatua hiyo.

    Begum, aliyeondoka London mnamo 2015, alisema anataka kurudi nyumbani.

    Alipatikana katika kambi ya wakimbizi nchini Syria wiki iliyopita baada ya kuondoka Baghuz, inaarifiwa – ngome ya wapiganaji wa IS – na kwamba alijifungua mtoto wa kiume mwishoni mwa juma.

    Katika mahojiano na BBC Jumatatu, Begum amesema hakutaka kuwa ‘sura ya wasichana’ wa IS na kwamba anachotaka sasa ni kumlea mtoto wake kwa umakini nchini Uingereza.

    Inaaminika ana asili ya Bangladeshi lakini alipoulizwa na BBC, ameeleza kwamba hana pasipoti ya Bangladesh na kwamba hajawahi kwenda katika nchi hiyo.

    Lakini vipi kuhusu mwanawe aliyemzaa? mtoto aliyezaliwa na mzazi aliye na uraia wa Uingereza kabla ya kupokonywa uraia, bado anatizamwa kuwa raia wa Uingereza.

    Wakati inawezekana kimsingi kumpokonya mtoto uraia , maafisa watahitaji kupima sawa haki zao dhidi ya tishio walilonalo.

    Presentational white space

    Islamic State limepoteza sehemu kubwa ya maeneo ambayo yalidhibiti , lakini kati ya wapiganaji 1000 na 1500 inaaminika wamesalia katika eneo la kilomita 50 kwa mraba karibu na mpaka wa Syria na Iraq.

     

     

  • Mbunge ajiuzulu baada ya kuiba mkate

    Mbunge ajiuzulu baada ya kuiba mkate

    Mbunge mmoja nchini Slovenia amejiuzulu baada ya kuiba mkate maarufu ”sandwich” katika duka moja kwa madai kuwa wahudumu wa sehemu hiyo walimpuuzia.

    Darij Krajcic ameviambia vyombo vya habari vya ndani kuwa alipuuzwa na wafanyakazi wa duka hilo na walikua wakiendelea na shuguli zao.

    Hakujilakana kama ameiba lakini baadae baadhi ya wanachama walisisitiza arudi kulipa pesa ya mkate huo.

    Krajcic ameomba msamaha na kusema kuwa anajutia kitendo alichokifanya.

    Suala lake la kuiba lilisambaa baada ya kuwaambia wabunge wengine wakati wa mkutano wa kamati siku ya Jumatano.

    ”Nilisimama pale kwa dakika tatu, kabla wanihudumie,” mbunge huyo mwenye miaka 54 alisimulia katika kituo cha runinga cha mtu binafsi.

    Wafanyakazi watatu wa duka hilo hawakugundua kama yupo baada ya kuwa walikua na mazungumzo baina yao hali iliyosabisha profesa huyo wa zamani kujaribu bahati yake.

    ”Hakuna mtu yoyote aliyepiga kelele, wala kunifuata.”

    Wabunge wenzake walicheka baada ya kusikia kisa hicho.

    Lakini siku ya Alhamisi spika wa bunge hilo Brane Golubovic, alikemea vikali kitendo cha mbunge kuiba, na kusema kuwa ni kitendo kisichokubalika.

    ”Amechukua hatua za kuwajibika na kujiuzulu yeye mwenyewe,” Golubovic aliviambia vyombo vya habari.

  • Polisi Kenya wadai kifo cha mwanaharakati maarufu Caroline Mwatha huenda kimesababishwa na kutoa mimba

    Polisi Kenya wadai kifo cha mwanaharakati maarufu Caroline Mwatha huenda kimesababishwa na kutoa mimba

    Polisi nchini Kenya wamesema kuwa uchunguzi wa awali uanaonesha kuwa kifo cha mwanaharakati maarufu Caroline Mwatha kimetokana na kutoa ujauzito wa miezi mitano.

    Mara ya mwisho kwa mawanaharakati huyo kuonekana hai ilikuwa Jumatano ya wiki iliyopita kabla ya mwili wake kugunduliwa kwenye chumba cha kuhifadia maiti cha City Mortuary mjini Nairobi.

    Caroline Mwatha ni mwanaharakati aliyefanya kazi katika shirika la haki la kijamii katika kitongoji cha Dandora mjini Nairobi, shirika linalonakili visa vya mauaji ya kiholela yaliotekelezwa na maafisa wa polisi hususan katika vitongoji vinavyoshuhudia uhalifu mkubwa Nairobi.

    Kumekuwa na hofu kuwa kifo hicho kimetokana na kazi zake ambazo jamii inaziona ni hatarishi kwa usalama na maisha.

    Lakini taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Upelelezi wa Makosa ya Jinai George Kinoti inasema kuwa makachero wanaamini mwanaharakati huyo alifariki wakati alipokuwa akitoa ujauzito Jumatano ya wiki iliyopita, (Februari, 6), siku ambayo alionekana kwa mara ya mwisho akiwa hai.

    Caroline inaarifiwa ni mke na mama wa watoto wawili.

    Hata hivyo, kwa mujibu wa taarifa ya wapelelezi, kuwa marehemu alikuwa kwenye mazungumzo ya simu ya mara kwa mara na mwanaume mwengine ambaye si mumewe kuhusu ujauzito huo. Plisi wanadai alikuwa ni mpenzi wake.

    Mwanaume huyo, wapelelezi wanadai ndiye aliyefanya mazungumzo na kituo cha kutolea mimba kilichopo eneo la Dandora Phase I, Nairobi na kutoa kima cha Sh6,000 ili kazi hiyo ifanyike.

    Baada ya kufikwa na umauti, polisi wanasema mwili wa Croline ulipelekwa Nairobi City Mortuary saa 10 usiku ya Februari 7.

    Watu sita, ikiwemo bwana huyo aliyekuwa akiwasiliana na marehemu, mmiliki wa kituo cha afya inachodaiwa alifariki ndani yake na dereva wa gari ya kukodi (Uber) wanashikiliwa na polisi mpaka sasa huku uchunguzi zaidi wa mkasa huo ukiendelea.

     

  • Urusi ‘kuzima intaneti ili kujilinda na maadui’

    Urusi ‘kuzima intaneti ili kujilinda na maadui’

    Urusi inajipanga kuzima mtandao wa intaneti kwa muda, na hivyo kujitoa kwenye mawasiliano na dunia kama sehemu ya majaribio yake ya kujikinga dhidi ya mashambulio ya kimtandao.

    Zoezi hilo litafanya mawasiliano baina ya raia na mashirika ya Urusi kubaki ndani ya nchi badala ya ya kupitia njia za kawaida za kimtandao kimataifa.

    Rasimu ya sheria ya kuruhusu mabadiliko ya kiufundi ili kuiwezesha nchi hiyo kuendesha mtandao wake wenyewe iliwasilishwa bungeni mwaka jana.

    Jaribio hilo linatarajiwa kufanyika kabla ya tarehe mosi Aprili, lakini siku rasmi ya kuzimwa mtandao haijatajwa.

    Rasimu hiyo ya sheria, iliyopewa jina la Programu ya Taifa ya Uchumi wa Kidijiti, inawataka watoa huduma za intaneti nchini Urusi kuwa na uwezo wa kuendelea na huduma zao hata pale ikitokea nchi za kigeni zikiamua kuitenga Urusi.

    Nchi wanachama wa Nato na washirika wake wamekuwa wakitishia kuiwekea vikwazo vya kimtandao Urusi ambayo wanaituhumu kwa kufanya mashambulio ya kimtandao.

    Njia mojawapo inayopangwa na Urusi katika kujilinda huko ni kutengeneza mfumo wake binafsi wa anuani za kimtandao ufahamikao kama DNS, waweze kupata mawasiliano hata pale watakapotengwa ama kujitenga.

    Kwa sasa, kuna taasisi 12 zinzoshughulikia suala la utolewaj na matumizi ya anuani hizo na hakuna hata moja iliyopo Urusi.

    Hata hivyo tayari kuna chapa nyingi za mfumo huo wa DNS nchini Urusi hali inayoonesha kuwa nchi hiyo inaweza kuendelea na shughuli zake za kimtandao hata ikitokea imetengwa leo.

    Watoa huduma za intaneti wanatarajiwa kuelekeza mawasiliano yote yanayopita kwao kwenye vituo vya serikali kwenye zoezi hilo. Mawasiliano yote ya ndani ya Urusi yataruhusiwa kuendelea lakini yale yatokayo nje ya nci yataminywa.

    Mwishowe, serikali ya Urusi itakuwa na ubavu kama wa China wa kupanga mawasiliano gani raia wake wapate kutoka nje ya nchi.

    Vyombo vya habari nchini humo vinadai kuwa watoa huduma za intaneti nchini humo wanakubaliana na mabadiliko hayo lakini wanatofautiana kwenye namna gani utekelzwaji wake uwe. Wanaamini jaribio hilo litazaa “mvurugano mkubwa” kwa matumizi ya mtandao ya nchi hiyo, umeandika mtandao wa ZDNet.

    Serikali ya Urusi inawapa fedha watoa huduma ya intaneti nchini humo ili kuboresha miundombinu yao kuendana na mipango yake ya baadae.

    Hata hivyo, kuna uwezekano wa watu kuchupa mazuio hayo ya serikali kwa kutumia mitandao binafsi (VPNs) – ambayo hudanganya mahala kompyuta ama simu janja ilipo na hivyo vidhibiti kushindwa kuzizui kupata mawasiliano yaliyokatazwa.

    Hata hivyo, baadhi ya nchi kama China zimekuwa wakali kwa wale wanaotumia tenkolojia hiyo. Ukikutwa unatumia ama kusambaza bila kibali teknolijia hiyo nchini China unaweza kutupwa jela.

    Mara chache, nchi hujikuta zimejitoa kwenye mawasiliano ya intaneti kwa bahati mabaya – ilitokea hivyo mwaka 2018 nchini Mauritania kwa siku mbili baada ya nyaya ya chini ya bahari inayopeleka mawasiliano hayo kukatika. Meli ya kuvua samaki inasadikiwa kusababisha ajali hiyo.

     

  • Wananchi Njombe waipigia magoti Serikali, ‘Tusaidieni Jamani’

    Wananchi Njombe waipigia magoti Serikali, ‘Tusaidieni Jamani’

    Wananchi takribani 285 wa Kijiji cha Utelingolo halmashari ya wa Mji wa Njombe mkoani humo wamesema kuwa hali ya uchumi itashuka kijijini hapo kwa sababu wamekuwa wakitumia muda mwingi kupeleka na kurudisha watoto shule badala ya kufanya shughuli za kuwapatia kipato.
     
    Hali hiyo imepelekea serikali ya kijiji hicho kuweka utaratibu wa kuwa na daftari maalumu la kusaini pindi unapopeleka na kuchukua mtoto katika shule husika wanayo soma.
     
    ‘’Sisi wanawake ndo tunateseka, kama mimi nina watoto watatu wanasoma madarasa tofauti na muda wa kutoka hivyo sasa asilimia kubwa nashinda na kazi ya kwenda kuwachukua kwa hiyo muda wa kufanya maendeleo unakua hamna,’’ amesema Mary Mlawa.
     
    ‘Aidha, wananchi hao wameiomba serikali kusema kitu kwani sasa hivi wanashindwa kufanya maendeleo ya kujenga nchi kwa sababu hakuna anayeruhusiwa kuchukua mtoto wa mwenzake mpaka umfuate yeye mwenyewe.
     
    Kwa upande wa Chris Msigwa amesema kuwa kila kitu kimesimama na kuna hatari kubwa hapo baadae kushindwa kusomesha watoto.
  • Trump atangaza mkutano mwingine na rais Kim Jong-un wa Korea kaskazini

    Trump atangaza mkutano mwingine na rais Kim Jong-un wa Korea kaskazini

    Rais wa Marekani Donald Trump ametangaza katika hotuba yake kwamba ataanda mkutano wa pili kujadili masuala ya nyuklia na kiongozi wa Korea kaskazini mwezi huu.

    Katika hotuba kwa taifa iliyoambatana na kauli mbiu “Choosing Greatness”, aliapa kwa mara nyingine kujenga ukuta mpakani.

    Huku akihimiza umoja, kiongozi huyo wa Republican pia amesema jitihada za ‘uchunguzi ulio na upendeleo’ wa Democratic huenda ukaathiri ustawi wa Marekani.

    Kwa ukali, wanachama wa Democrat wamemshutumu Trump kwa kupuuza maadili ya Marekani.

    Hotuba hiyo kuu ya rais Trump imejiri baada ya pengo la muda mrefu kuwahi kushuhudiwa katika historia, la kusitishwa ufadhili kutoka kwa serikali ya nchi hiyo.

    Alichochea kufungwa kwa mashirika ya serikali kwa kuitisha ufadhili wa ukuta wa mpakani kati ya Marekani na Mexico na kuishia kubadili kauli hiyo baada ya wanachama wa Democrat kukataa wazi.

    Amesema nini kuhusu Korea kaskazini?

    Trump amesema atakuna na Kim Jong-un huko Vietnam kuanzia Febrauri 27-28.

    Mipango ya mkutano wa pili imekuwa ikipangwa tangu mwaka jana.

    Mnamo Jumanne usiku, Trump alisema: “Mateka wetu wamerudi nyumbani, majaribio ya nyuklia yamesitishwa na hakujakuwa na shambulio la makombora kwa miezi 15.

    “Kama sikuchaguliwa rais wa Marekani, kwa maoni yangu tungekuwa katika vita vikubwa na Korea kaskazini hivi sasa.

    “Bado kazi kubwa imesalia, lakini uhusiano wangu na Kim Jong-un ni mzuri.”

    Amesema nini kuhusu umoja wa kisiasa?

    Baada ya miaka miwili ya ufuasi wenye uhasama, Trump ameregelea wito wa umoja wa kisiasa ambao ameutoa katika hotuba zake mbili zilizopita za kila mwaka bungeni.

    “Pamoja tunaweza kuvunja mkwamo wa kisiasa wa miongo kadhaa,” amesema.

    “Tunaweza kuziba migawanyiko ya siku za nyuma, tukaponya vidonda vya jadi, na kujenga muungano mpya.”

    Trump ameelezea maeneo ambayo yanaweza kufikiwa makubaliano, kama kuimarisha miundo mbinu, kupunguza bei za dawa na kupambana na saratani kwa watoto.

    Lakini saa chache kabla ya hotuba hiyo, Chuck Schumer, kiongozi wa Seneti wa chama cha Democratic amemshutumu Trump kwa “kuidhinisha taifa lenye mgawanyiko” kwa sehemu kubwa ya mwaka.

    Katika chakula cha mchana na waandishi habari kwenye ikulu ya White House Jumanne, Trump alimuita Schumer “muovu”, na kutumia tusi, New York Times inaripoti.

    Wakati Trump akitoa hotuba yake kwa taifa Jumanne usiku, mpinzani wake mkuu alikuwa amekaa nyuma yake.

    Kiongozi wa Democrats katika bunge la wawakilishi, Spika Nancy Pelosi, aliidhinisha upinzani kwa matakwa ya rais kuhusu ufadhili wa ujenzi wa ukutana mara nyingi humkebehi.

    Democrats wamejibu nini?

    Stacey Abrams, aliyepoteza kiti chake kuwania Ugavana wa jimbo la Georgia, aliwasilisha ujumbe wa Democrats kwa Trump.

    Alikuwa mwanamke wa kwanza Mmarekani mweusi aliyejibu kwa upinzani mkali.

    Bi Abrams amesema: ” hatua ya serikali kusitisha ufadhili ni njama iliyopangwa na rais, na ambayo imekiuka kila ncha ya usawa na ambayo sio tu ambayo haikuwajali raia – lakini pia maadili.”

    Wakati wa hotuba ya Trump wabunge kadhaa wanawake wa Democratic walivaa nguo nyeupe, rangi iliyoidhinishwa na kundi la wanawake katika karne ya 20 waliokuwa wakidai haki ya kupiga kura.

    Walikaa kimya pasi kucheka wakati wenzao wa Republican walipoinuka wakipiga makofi kushangilia aliyoyasema rais.

    Lakini wanachama wa Democrats walimshangaza Trump kwa kumsimamia kwaheshima kiongozi huyo aliposema kwamba kuna wanawake zaidi wanofanya kazi bungeni, kuliko ilivyowahi kushuhudiwa katika siku za nyuma.

    “Vizuri sana!” alisema rais baada ya muitikio huo. “Vizuri sana”

     

     

  • Maisha yaliobadilika kwa mwanamke aliyeugua saratani kwa miaka 9

    Maisha yaliobadilika kwa mwanamke aliyeugua saratani kwa miaka 9

    Millicent Kagonga, ameugua saratani ya mlango wa uzazi kwa miaka 9, na anasema maisha yake hayajakuwa rahisi.

    Saratani ya mlango wa uzazi inaweza kusababishwa kwa maambukizi ya virusi vya Human Papillomavirus au HPV, na aina hii ya virusi huambukizwa kwa njia ya kujamiiana.

    Alianza kuhisi kwamba ana tatizo alipojifungua mtoto wake wa tatu akiwa na miaka 20, ambapo alianza kutokwa na uchafu katika sehemu za siri lakini hakujua ulikuwa ni ugonjwa gani.

    “Baada ya muda nikaanza kuvuja damu na hapo nilikwenda hospitalini na daktari akasema ”Dada pole unaugua satarani na iko katika kiwango cha nne.”

    ”Nilipoteza fahamu na hata wakati huo nilitaka kujitoa uhai na hata watoto wangu wawili kwa sababu ya maisha niliyoyapitia, singependa mtoto wangu apitie hayo”.

    Bi, Milicent anazungumza akiwa amelala kwenye sakafu kwani hawezi kuketi kwa muda mrefu kutokana na shida ya mgongo na hata kusumbuliwa na misuli.

    ”Wakati nilipokuwa nimekaa na saratani hiyo kwa muda sikuweza kuzuia haja ndogo au kubwa, nilikuwa navuja damu mara mbili kwa siku kwa dakika tano na nilikuwa nikipoteza zaidi ya lita nne za damu asubuhi na nne jioni”.

    ”Lakini siwezi kusahau ile siku nilivuja damu kwa siku mbili”.

    ‘Nilitokwa na uchafu ulionuka kutoka sehemu zangu za siri kwa miaka sita, kwa sababu sikujua naugua ugonjwa gani? Nilivumilia kwa sababu niliogopa kubaguliwa na ndoa yangu kuvunjika,”Millicent anasema.

    Kwa kupitia matibabu haya ya saratani Millicent anasema kwa hivi sasa hawezi kukaa kwenye kiti kwa muda mrefu au hata kulala kitandani. Iliyobaki analala sakafuni kwa sababu ya maumivu makali mgongoni mwake.

    Millicent ameongeza kwamba alifika ukomo wa uzazi wa mapema, na hata kuwa mnene kutokana na matibabu hayo.

    Safari yake ya ugonjwa huo haikukomea hapo, alianza kutengwa akabaki na watoto wake pekee, na hakuna mtu aliyetaka kujihusishwa naye.

    Jamii yake ilisema kwamba amerogwa, wenine wakasema ni kiboko anachochapwa kutoka kwa maulana na hata wengine wakisema ni laana ya kuzaliwa nayo, kwa jinsi alivyokuwa akivuja damu.

    ”Kama si matibabu ya kuchomwa na miale ya moto, basi leo hii singekuwa hai,” Millicent anasema.

    Saratani hii haina dalili hadi inapofika kiwango kikuu. Mara nyingi wanawake hudhani dalili wanazopata ni za kitu kingine, kama vile hedhi ya kila mwezi, maambukizi katika kibofu cha mkojo, au kuvu.

    Kwa mujibu wa shirika la afya duniani, WHO, hizi ndizo baadhi ya dalili zinazojitokeza kwa muathiriwa:

    • Kuvuja damu kupita kiasi, ima ni kati kati ya muda wa hedhi, baada ya tendo la ndoa, au hata kuanza kuvuja damu baada ya ukomo wa uzazi.
    • Kutokwa na uchafu na harufu kupita kiasi kutoka sehemu za siri.
    • Kwenda haja ndogo kupita kiasi, na kupata maumivu wakati unapata haja.
    • Kupata maumivu kiunoni, na kwenye fupa la uzazi.
    • Figo kuacha kufanya kazi baada ya maambukizi katika kibofu cha mkojo, au kuziba kwa njia ya kwenda haja kubwa.

    Ni muhimu kwa wanawake wote kufanyiwa ukaguzi wa fuko, au mlango wa uzazi na kupata ushauri wa daktari iwapo baadhi ya dalili zitajitokeza.

    Kuna saabu nyingi za kukufanya ukavuja damu kupita kiasi na huenda sio saratani ya mlango wa uzazi. Na mambo mengi huzingatiwa katika kulibaini hilo, mfano umri, uzazi, iwapo umejifungua na pia historia ya familia.

    Kadhalika kuvuja damu baada ya ukomo wa uzazi ni jambo la kawaida, hatahivyo ni vyema kupata ushauri wa daktari wako.