Author: E-FM CO LTD

  • Majambazi wachomoa mashine ya ATM ukutani

    Majambazi wachomoa mashine ya ATM ukutani

    Majambazi wamenyofoa na kutokomea na mashine ya kielektroniki ya kutolea pesa nchini Ireland ya Kaskazini.

    Majambazi hao walitumia tingatinga ambalo pia waliliiba katika kunyofoa ATM hiyo kutoka kwenye ukuta wa duka moja katika Kaunti ya Antrim.

    Tukio hilo limetokea saa tisa ya usiku wa Jumatatu. Polisi wamethibitisha kuwa jengo hilo limeharibiwa vibaya.

    Majambazi wamenyofoa na kutokomea na mashine ya kielektroniki ya kutolea pesa nchini Ireland ya Kaskazini.

    Majambazi hao walitumia tingatinga ambalo pia waliliiba katika kunyofoa ATM hiyo kutoka kwenye ukuta wa duka moja katika Kaunti ya Antrim.

    Tukio hilo limetokea saa tisa ya usiku wa Jumatatu. Polisi wamethibitisha kuwa jengo hilo limeharibiwa vibaya.

    Majambazi wa ATM

    “Tulipokea simu kuhusu tukio hilo mishale ya saa 9:25 usiku kuwa tingatinga linaungua moto nje ya duka ambalo ATM imechomolewa,” Inspekta wa Polisi Richard Thornton amesema.

    “ATM imenyofolewa ukutani na kuharibu jengo ilipokuwa imewekwa…tunawataka mashuhuda wajitokeze, hususan walioiona gari ya rangi ya fedha.”

    Mwezi uliopita, polisi walitangaza kuundwa kwa kikosi kipya cha kupambana na wizi wa mashine za ATM.

    Toka ulipoanza mwaka 2019, mashine saba za ATM zimeibiwa. Polisi pia wanaamini kuna makundi kadhaa ya majambazi ambayo yanajihusisha na wizi wa mashine hizo.

    Wamiliki wa maduka sasa wanaonesha uoga wao juu ya kuweka mashine hizo kwenye maeneo yao ya biashara na tayari watu kadhaa wametahadharisha endapo wizi huo utaendelea basi watalazimika kuzitoa mashine hizo.

  • Maandamano yakumba mpaka wa Kenya na Tanzania, kunani?

    Maandamano yakumba mpaka wa Kenya na Tanzania, kunani?

    Maandamano yamekumba mji wa mpakani wa Namanga uliopo kati ya kenya na Tanzania.

    Kulingana na maafisa wa polisi maandamano hayo yalizuka kufuatia kutekwa nyara kwa mfanyibishara mmoja wa Kenya ambaye waandamanji hao wanasema alipelkekwa nchini Tanzania.

    Mfanyikazi wa ofisi ya serikali katika mji huo ambaye hakutaka jina lake litajwe amesema kuwa waandamanaji hao waliojawa na ghadhabu walifunga barabara inayoelekea Tanzania na hivyobasi kukatiza uchukuzi kutoka na kuelekea nchini humo.

    Anasema hali ilibadilika na kuwa mbaya zaidi wakati maafisa wa polisi wa Tanzania walipowasili karibu na ukuta unaogawanya Kenya na Tanzania ambapo waandamanaji waliingiwa na mori na kuanza kukabiliana na maafisa hao ambapo walirusha vitoa machozi .

    Anasema kuwa Wakenya walitumia fursa ya upepo mkali uliokuwa ukielekea upande wa Tanzania ambapo waliokota na kurudisha vitoa machozi hivyo .

    Wakati hali hiyo iliposhindwa kudhibitika , anasema, maafisa wa polisi walipiga risasi hewani kwa lengo la kuwatawanya waandamanaji hao kutoka Kenya.

    Kulingana na afisa huyo maafisa wa Polisi wa Kenya wamekuwa wakipiga doria katika eneo hilo huku wakiwaomba waandamanaji hao kuwa watulivu.

    Wakaazi waombwa kuwa watulivu

    Mfanyibiashara huyo anayejulikana kwa jina Moha alidaiwa kuchukuliwa kutoka eneo analofanya kazi na gari lenya sajili za Tanzania.

    ”Tangu alipochukuliwa usiku uliopita hajaonekana”, alisema mmoja wa wakaazi wa eneo hilo Odinga Nguduu.

    Akizungumzia kuhusu ufungaji wa barabara mkuu wa wilaya ya Longido Frank Mwaisumbe alisema kuwa ni makosa kwa kundi lolote kusimamisha magari yanayovuka mpaka.

    ”Hiyo ni kinyume na sheria hivyobasi tutalazimika kutumia uwezo wa serikali kusitisha wazimu huu”, alisema.

    Mwaisumbe aliwashauri wakaazi wa namanga kuwa watulivu huku serikali ikichunguza swala hilo.

    ”Hakuna haja ya vurugu kwa kuwa sasa tunachunguza swala hili tujue ni akina nani waliotekeleza kitendo hicho kwa lengo la kuweza kuwachukulia hatua kali za kisheria”, aliongezea.

    Gazeti la The Citizen nchini Tanzania limeelezwa kwamba kamishna wa jimbo la Arusha Jonathan Shanni alizuru mji wa Namanga ili kuchunguza hali ilivyo.

  • uongozi wa klabu ya Yanga waachia ngazi

    uongozi wa klabu ya Yanga waachia ngazi

    Aliyekuwa Kaimu Mwenyekiti wa Yanga Samwel Lukumay na aliyekuwa mjumbe wa kamati ya utendaji, akishikilia nyadhifa za Mwenyekiti wa Kamati ya mashindano na Mwenyekiti wa Kamati ya usajili, Hussein Nyika, wamejiuzulu nafasi zao leo Machi 27, 2019.

    Nyika na Lukumay wametangaza hilo, kwenye makao makuu ya klabu hiyo ambapo wamesema kuwa wamefanya hivyo ili kupisha uchaguzi utaowezesha klabu hiyo kupata viongozi wapya.

    Aidha, viongozi hao ndio waliokuwa wamebaki kwenye uongozi wa Yanga ambao uliingia madarakani mwaka 2016 baada ya wengine kujizulu, hivyo sasa timu hiyo inabaki bila uongozi mpaka pale uchaguzi mkuu utakapofanyika.

    ”Ninajiuzulu nafasi zangu zote nikiwa kama Mjumbe wa kamati ya utendaji lakini pia Mwenyekiti wa kamati ya usajili na kamati ya mashindano na niombe msamaha kwa wale niliowakosea katika utekelezaji wangu wa majukumu,” amesema Nyika.

    Kwa upande wake Lukumay amesema kuwa wameamua kufanya hivyo ili kutoa nafasi kwa uchaguzi mkuu kupata viongozi wote tofauti na awali ambavyo ilikuwa ni uchaguzi mdogo wa kuziba nafasi.

    Hata hivyo, siku za hivi karibuni Baraza la wadhamini la Yanga liliweka wazi kuwa, badala ya kufanya uchaguzi mdogo wa kuziba nafasi zilizowazi ikiwemo ile ya Mwenyekiti, utafanyika uchaguzi mkuu kwaajili ya kupata viongozi.

  • Afariki dunia kwa kuchomwa mkuki mbavuni

    Afariki dunia kwa kuchomwa mkuki mbavuni

    Mzee mmoja aliyetambulika kwa jina la Visu Urembo (80) amefariki dunia baada ya kuchomwa mkuki sehemu ya ubavuni mwa mwili wake, katika mgogoro wa wakulima na wafugaji uliotokea Lukenge, Tarafa ya Ruvu, Kibaha Vijijini mkoani Pwani.
     
    Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani, ACP Wankyo Nyigesa amethibitisha kutokea kwa tukio hilo, ambapo amesema tukio hilo limetokea machi 26 mwaka huu baada ya kutokea tafrani kati ya wakulima na wafugaji.
     
    Amesema kuwa mzee Urembo kabla ya kufikwa na umauti alikimbizwa kituo cha afya Mlandizi, ambapo baadaye alikimbizwa katika hospital ya Tumbi kwa matibabu zaidi lakini kabla ya kupatiwa matibabu madaktari waligundua kuwa tayari ameshafariki.
     
    Aidha, Wankyo amesema kuwa wafugaji hao waliingiza mifugo yao (Ng’ombe) kwenye bwawa linalotumika katika shughuli za kibinadamu ikiwemo kunywa, kufulia, kupikia, kwa kuona hivyo wakulima walienda na mihemko kuwazuia wafugaji hao, ndipo wafugaji hao walipoanza kurusha mikuki na vitu vyenye ncha kali na kusababisha kifo cha mzee huyo na wengine watatu kujeruhiwa vibaya.
     
    “Polisi tulifika eneo la tukio alfajiri Machi 27 mwaka huu ,na kutuliza tafrani hiyo na sasa hali ni shwarii,”amesema kamanda Wankyo
     
    Hata hivyo, amewataja waliojeruhiwa kuwa ni pamoja na John Kisukari Urembo (50) ambaye ni mwenyekiti wa serikali ya kijiji cha Lukenge. Maximilian Evarist (34) mtendaji wa kijiji cha Lukenge na Adam Onesha ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya maji kijijini hapo .
     
    Kwa upande wake, mkuu wa wilaya ya Kibaha Assumpter Mshama ameyataka makundi hayo yaheshimiane na kujenga upendo badala ya kujiona kundi moja ni zaidi ya kundi jingine.
  • Bosi ashtakiwa kwa ‘Kujamba’ ofisini

    Bosi ashtakiwa kwa ‘Kujamba’ ofisini

    Mfanyakazi mmoja nchini Australia amefungua mashtaka kwenye mahakama ya rufaa ya nchi hiyo akidai bosi wake alikuwa akimbughudhi ofisini kwa kujamba sana.

    Awali, mahakama moja ya chini ilifikia uamuzi kuwa hakukuwa na bughudha yeyote katika suala hilo.

    Hata hivyo, David Hingst anadai kuwa bosi wake wa zamani Greg Short alikuwa “akinyanyuka na kumjambia” karibu mara sita kwa siku.

    Mwaka jana mashtaka dhidi ya kampuni yake ya zamani na kudai dola milioni 1.28 yalitupiliwa mbali na Mahakama Kuu ya Victoria iliyohukumu kuwa hakukuwa na bughudha.

    Bwana Hingst mwenye miaka 56, amedai kuwa mashuzi hayo yamemsababishia “msongo mkubwa”.

    Aalikuwa akijamba na kwenda zake

    Hingst, ambaye alikuwa afisa utawala katika mji wa Melbourne, ameishtaki kampuni ya Construction Engineering mwaka 2017 lakini kesi hiyo ilitupwa Aprili 2018.

    Amekata rufaa dhidi ya uamuzi huo na Jumatatu, Novemba 25 alisikilizwa na Mahakama ya Rufaa.

    “Nilikuwa nikikaa kwenye chumba kidogo ambacho hakina madirisha, alikuwa akiingia na kujamba nyuma yangu na kisha kwenda zake. Alikuwa akifanya hivyo mara tano mpaka sita kwa siku,” Hingst ameliambia Shirika la Habari la nchi hiyo, Australian Associated Press (APP).

    Katika kesi ya awali mwaka jana, bwana Short alidai kuwa hakumbuki kujamba akiwa karibu na Hingst lakini “yawezekana ilitokea mara moja ama mbili hivi, yawezekana.”

    Hata hivyo, alikanusha kuwa alifanya vitendo hivyo “kwa madhumuni ya kumkera na kumbughudhi” Hingst.

    Hingst alikuwa akimuita Short “Bwana Mnukaji” na alikuwa akipuliza uturi kila aliposogea karibu yake, korti iliambiwa.

    Kwa mujibu wa mitandao ya Australia, Hingst amedai kuwa, tabia ya Short ilikuwa ni sehemu ya mpango wa kumng’oa kazini na muda aliofanya kazi na Construction Engineering kulimsababishia majeraha ya kiakili. Pia amedai kuwa Short alikuwa akimkejeli kutokana na ufanisi wake na kumpachika jina la “bwege”.

    Hingst amesema kesi yake ya kwanza haikuamuliwa kwa usawa, kudai jaji alimbagua.

    Mahakama ya Rufaa itatoa hukumu yake Ijumaa, Machi 29.

     

  • Trump ‘hakusuka njama na Urusi’ kushinda uchaguzi

    Trump ‘hakusuka njama na Urusi’ kushinda uchaguzi

    Kampeni iliyoendeswa na rais wa Marekani Donald Trump ‘haikushirikiana na Urusi wakati wa uchaguzi wa 2016, kwa mujibu wa muhtasari wa ripoti ya ya mwanasheria mahususi Robert Mueller iliyowasilishwa kwenye bunge la Congress ,Jumapili.

    Muhtasari wa ripoti haukuelezea ikiwa Bwana Trump alizuia utekelezwaji wa sheria – lakini pia haikumuhusisha rais na madai hayo.

    Ripoti hiyo iliwekwa kwa muhtasari kwa ajili ya Congresi na Mwanasheria Mkuu, William Barr.

    Trump alituma ujumbe wa twitter kujibu muhtasari wa ripoti yake akisema: ” hakuna ushirikiano, hakuna kuzuia sheria.”

    Rais Trump, ambaye mara kwa mara aliuelezea uchunguzi kama ”uwindaji wa kichawi”, alisema Jumapili kwamba “ni aibu kwamba nchi ililazimika kupitia hili”, akiuelezea uchunguzi dhidi yake kuwa “kuangushwa kwa jambo lililo kinyume cha sheria “.

    Ripoti hiyo inakamilisha uchunguzi wa miaka miwili wa Bwana Mueller, ambapo wakati wa uchunguzi huu washirika wa karibu wa rais walishitakiwa, na wakati mwingine hata kufungwa.

    “Japo ripoti hii haionyeshi kuwa rais alifanya uhalifu, haimuweki huru ,”Bwana Mueller aliandika katika ripoti yake.

    Kile kilichomo kwatika muhtasari wa ripoti

    Barua ya muhtasari wa ripoti hiyo ya Bwana Barr inaainisha matokeo ya uchunguzi unaohusiana na juhudi za Urusi za kushawishi matokeo ya uchaguzi wa 2016.

    Bwana Barr alihitimisha ripoti yake kwa kusema: “Mchunguzi maalum hakumpata Trump, mtu yeyote wa Marekani au afisa wa kampeni ya Trump na hatia ya kushirikiana au kwa kufahamu kuratibu ushirikiano wowote na Urusi .”

    Sehemu ya pili ya barua hiyo ilizungumzia suala la kuzuwia utendaji wa sheria . Muhtasari wa Bwana Barr unasema ripoti wa mchunguzi mkuu “Hatimae haimuweki katika nafasi ya kushtakiwa “.

    Uchunguzi wa Robert Mueller umechukua takribani miaka miwili

    “Kwa hiyo baraza la uchunguzi halikutoa hitimisho – kwa njia moja au nyingine- juu ya ikiwa mienendo iliyochunguzwa ilikuwa ni ya kuzuwia utendaji wa kisheria ,”ilielezea barua hiyo.

    Bwana Barr anasema kuwa ushahidi haukutosha “kubaini kwamba rais alitenda kosa la kuzuwia utendaji wa washeria “.

    Bwana Barr alikamilisha barua yake kwa Congresi kwa kusema kuwa atafichua mengi zaidi katika ripoti kamili , lakini akasema baadhi ya yanazuwiwa kutangazwa.

    “Kutokana na masharti hayo , mpango wa mchakato wa ripoti hiyo utategemea kwa upande mmoja juu ya namna wizara ya mambo ya nje itakavyoweza haraka kubaini yaliyopendekezwa na jopo kuu la mahakama ambayo kw amujibu wa sheria hayapaswi kutangazwa kwa umma ,” aliandika.

    ” Nimeomba msaada wa mchunguzi mkuu katika kutambua taarifa zote zilizomo kwenye ripoti haraka iwezekanavyo .”

    Walichosema wanasiasa wa marekani kuhusu Muhutasari wa ripoti

    Mjumbe wa Congresi Jerry Nadler, ambaye ni mwenyekiti wa tume ya sheria wa Democratic katika bunge la wawailishi, alisisitiza kuwa mwanasheria mkuu hakusema moja kw amoja kwamba Trump alizuwia utendaji wa sheria .

    “Barr anasema kwamba rais huenda alizuwia uutekelezwaji wa sheria, lakini kupatikana na hatia hiyo , ‘serikali itahitaji kutoa ushahidi wa kutosha kwamba mtu alifanya hivyo kwa kukusudia, au kuhusika katika mwenendo wa kuzuwia utekelezwaji wa sheria’.”

    Seneta wa Democratic Richard Blumenthal, ambaye ni mjumbe wa kamati ya Seneti ya sheria, alisema kwamba japo ushahidi ulikosa wa “kushtakiwa kwa uhalifu wa kushirikiana “, bado maswali yanabakia juu ya ikiwa Bwana Trump alihusika.

    Katika taarifa ya pamoja , Spika wa bunge kutoka chama cha Democratic Nancy Pelosi na kiongozi wa wabunge wa Democratic katika seneti Chuck Schumer walisema barua ya Bwana Barr ” inaibua maswali mengi kama inavyoyajibu” na wakatoa wito wa ripoti kamili kutolewa.

    “kwa rais kusema yuko huru kabisa inakwenda kinyume kabisa na maneno ya Bwana Mueller na maneno yake hayapaswa kuchukuliwa kuwa ni ya kuaminika ,” ilisema taarifa yao.

    Afisa habari wa ikulu ya White House Sarah Sanders alielezea matokeo ya uchunguzi huo kuwa “ya kumuweka huru kwa jumla rais”.

    Wakili wa Trump, Rudy Giuliani, alisema ripoti “ilikuwa bora kuliko nilivyotarajia “. Nae Seneta wa Republican Mitt Romney aliafiki “habari njema “, akituma ujumbe wake wa twitter kwamba ”Ni wakati wa taifa kusonga mbele “.

  • Basi la shule latekwa na kuteketezwa kwa moto

    Basi la shule latekwa na kuteketezwa kwa moto

    Basi lililokuwa limebeba watoto wa shule wapatao 51 lilitekwa na dereva wake na kisha kutiwa moto karibu na Milan nchini Italia.

    Watoto hao wa shule, baadhi yao walifungwa kamba, waliokolewa baada ya kuvunjwa vioo vywa basi hilo upande wa nyuma na hakuna hata mmoja aliyejeruhiwa vibaya.Watu kumi na wanne waliathiriwa na moshi uliotokana na kuteketea kwa basi hilo.

    Dereva wa basi hilo alikuwa na umri wa miaka arobaini na saba mwenye uraia wa nchini Italia ingawa ana asili ya kutoka nchini Senegal, inaarifiwa kwamba ametiwa nguvuni.

    Dereva huyo alisikika akitamba, akiwaambia waliokuwemo katika basi hilo kwamba hakuna hata mtu mmoja atakaye nusurika.Ulikuwa ni muujiza, vinginevyo yangekuwa ni mauaji ya halaiki, alinukuliwa akisema hayo mwendesha mashtaa mkuu wa mjini Milan, Francesco Greco.

    Mwalimu mmoja wapo alikuwa ndani ya basi wakati tukio hilo likitekelezwa, alimuelezea mtuhumiwa huyo kuwa alikuwa na silika ya hasira mara kwa mara na kubwa hasa ni juu ya sera za wahamiaji nchini Italia .Taarifa zingine zinaarifu kuwa dereva huyo alisikika akibwata sitisheni mauaji katika bahari ya Mediterranean”.

    ukio hilo lilikuwaje?

    Makundi mawili ya wanafunzi waliokuwa wakisindikizwa na waalimu wao , walikuwa wameyatoka mazingira ya shuleni iitwayo Vailati di Crema , wakielekea kwenye mazoezi lakini baadaye gari ikachukua muelekeo tofauti na safari yao na kuelekezwa kwenye barabara kuu ya mkoa na kufuata njia inayoelekea katika uwanja wa ndege wa Milan Linate, ripoti za mashuhuda zinaarifu .

    Suala hilo liling’amuliwa dakika arobaini baadaye , wakati dereva alipowaelekezea abiria wake kisu huku akizungumza, mvulana mmoja aliwapigia wazazi wake kwa siri, ambao nao waliwafahamisha polisi juu ya tukio hilo.

    Ilichukua muda kidogo kabla polisi hawajalifikia basi lililotekwa na kujaribu kulifanya lisimame,na mara basi hilo lilianza kubamiza gari la polisi kabla ya kupunguza mwendo na kusimama kabisa.

    Taarifa kutoka nchini Italia zinaarifu kuwa mafuta ya petroli yalinyunyizwa kulizunguuka basi hilo la shule , lakini polisi walitumia mbinu ya kuvunja mairisha ya nyuma ya basi hilo na hivyo kuwaruhusu abiria kushuka kwa haraka kabla basi hilo halijalipuka moto.

    Waendesha mashitaka wa Milan waliarifu kuwa wanafanya uchunguzi wa kina kuchunguza ikiwa kulikuwa na nia zozote mbaya ikiwa ni pamoja na ugaidi.Waziri wa Mambo ya Ndani wa Italia, Matteo Salvini, alizungumza kwa hasira kwamba dereva huyo alikuwa na rekodi ya uhalifu.

    Msimamo mkali wa Italia kwa wahamiaji

    Tangu alipoingia madarakani mwezi wa sita mwaka jana, uongozi wa Italia wa chama cha mrengo kulia na harakati za umoja wa Wanawake wenye hadhi ya nyota tano wameanzisha harakati zenye msimamo mkali wa kupambana na uhamiaji nchini humo.

    Harakati hizo zimepamba moto na kuwa za mstari wa mbele dhidi ya wahamiaji wanaovuka Bahari ya Mediteranean kwenda Ulaya, nayo Italia imejaribu kufunga bandari zake kwa kutumia boti.

    Mapema wiki hii, watu karibu hamsini waliokolewa na meli ya wasamaria wema ambapo wahamiaji walikuwa wakisafiri kwenye boti iliyotengenezwa kwa plastiki ikielea katika pwani ya Libya na kuchukuliwa hadi katika pwani ya Sicilia ya Lampedusa.

    Mamlaka nchini Italia iliamuru kukamatwa kwa meli hiyo na kuanzisha uchunguzi juu ya madai ya kuhamia uhamiaji wa siri

    cc;BBCswahili
  • Janga kubwa’ Msumbiji na Zimbabwe kuathiri Afrika mashariki

    Janga kubwa’ Msumbiji na Zimbabwe kuathiri Afrika mashariki

    Kimbunga Idai kimesababisha “janga kubwa” katika mataifa ya kusini mwa Afrika na kuathiri laki kadhaa za watu kama sio mamilioni, Umoja wa mataifa unasema.

    Eneo hilo limekabiliwa na mafuriko katika sehemu nyingi na uharibifu katika nchi za Musmbiji Zimbabwe na Malawi.

    Huku kukiwa na ripoti kwamba takriban angalau watu 400,000 wameachwa bila ya makaazi Msumbiji ya kati, shirika la kimataifa la msalaba mwekundu linaonya kwamba huenda ikachukua siku kadhaa kabla ya athari kamili ya “janga la kibinaadamu” kujulikana dhahiri.

    Maafisa kutoka kitengo cha utabiri wa hali ya hewa nchini Kenya wanaonya kwamba athari ya kimbunga hicho itashuhudiwa katika baadhi ya maeneo ya Afrika mashariki.

    Benard Chanzu, naibu mkurugenzi katika idara ya utabiri wa hali ya hewa Kenya anasema kimbunga hicho huenda kikaathiri msimu wa mvua kwenye eneo hili.

    ‘Mara nyingi upepo unapovuma, kila mahali huwa unaeleka katika eneo ambapo kunashuhudiwa kimbunga kile, pahali kulipo na hewa nyepesi, upepo unapovuma unakwenda ukielekea kwenye hicho kimbunga.

    ‘Wakati kimbunga kimeelekea kikaja mpaka kikaktua Msumbiji, kilitunyanganya upepo wote kutoka sehemu ya Afrika mashariki, kwa hivyo inanyang’anya uwezekano wa kuwepo mvua katika sehemu hii yetu’ameeleza bwana Chanzu.

    Rais wa Msumbiji Filipe Nyusi ameliita “janga la kibinaadamu lenye kiwango kikubwa”.

    Amesema Idadi ya watu waliofariki kutokana na kimbunga Idai nchini Msumbiji sasa huenda ikawa ya juu na kufikia watu 1000.

    Kimbunga hicho kilishuka katika mji wa bandari wa Beira siku ya Alhamisi kikiwa na upepo wenye kasi ya hadi kilomita 177 kwa saa, lakini mashirika ya misaada yalifika katika eneo hilo siku ya Jumapili.

    Serikali ya Msumbiji imesema watu 84 wamefariki na wengine takriban 100,000 wanahitaji kuokolewa kwa dharura karibu na mji wa Beira.

    Picha ya kutoka juu ya jimbo hilo imeonyesha kiasi cha 50km ya ardhi imezikwa chini ya maji baada ya mto Buzi kuvunja kingo zake , shirika la misaada la Save The Children limesema.

    Juhudi za uokoaji zinaendeleaje?

    Nchini Msumbiji, mashirika kadhaa ya misaada yanasaidia jitihada za serikali katika kuwatafuta na kuwaokoa watu na katika kutoa misaada ya chakula pia, mtandao wa ReliefWeb unaripoti.

    Shirika la Telecoms Sans Frontiers limetuma maafisa mjini Beira kusaida kuidhinisha mawasiliano – ambayo yamekatizwa kutokana na mafuriko hayo – katika kusaidia kuendeleza operesheni za usaidizi.

  • Watu 1000 wahofiwa kufariki kutokana na kimbuga Msumbiji

    Watu 1000 wahofiwa kufariki kutokana na kimbuga Msumbiji

    Idadi ya watu waliofariki kutokana na kimbunga Idai nchini Msumbiji sasa huenda ikawa ya juu na kufikia watu 1000 rais Filipe Nyusi amesema.

    Bwana Nyusi alisafiri kwa ndege katika maeneo yalioathirika zaidi siku ya Jumatatu. Alielezea kuona miili ikielea juu ya mito.

    Tayari kuna hatari ya maisha ya zaidi ya watoto 100,000 na watu wazima kufuatia kikmbunga hicho huku mito katika maeneo yaliothirika zaidi ikivunja kingo zake , kulingana na shirika la Save the Children.

    Mafuriko yaliofanyika mapema mwezi huu yamezidishwa na kimbunga Idai ambacho kilikumba eneo la kaskazini mwa Msumbiji mnamo tarehe 15 mwezi Machi 2019 na kusababisha unahiribifu mkubwa wa nyumba , shule, hospitali na miundo mbinu.

    Kulingana na serikali ya Msumbiji takriban watu 600,000 wameathiriwa , huku maisha ya zaidi ya watu 1000 yakidaiwa kupotea huku yale ya watu 100,000 yakihitaji msaada wa dharura mjini Beira.

    Kiwango cha janga hilo kinazidi kuongezeka kila dakika na shirika la Save the Children lina wasiwasi mkubwa kuhusu watoto na familia walio katika hatari huku viwango vya mafuriko vikizidi kuongezeka anasema Machel Pouw mkuu wa operesheni ya shirika hilo nchini Msumbiji.

    Save the Children ni mwanachama wa COSACA wakishirikiana na shirika la OXFAM pamoja na lile la CARE na linafanya kazi kwa ushirikiano wa karibu na serikali pamoja na taasisi za usimamizi wa majanga ili kuwasaidia watoto walioathirika

    Kimbunga hicho kilishuka katika mji wa bandari wa Beira siku ya Alhamisi kikiwa na upepo wenye kasi ya hadi kilomita 177 kwa saa , lakini mashirika ya misaada yalifika katika eneo hilo siku ya Jumapili.

    Mfanyikazi mmoja wa Umoja wa mataifa aliambia BBC kwamba kila nyumba mjini Beira- ambapo ni mji wenye makaazi ya watu nusu milioni iliharibiwa.

    Gerald Bourke, kutoka kwa shirika la chakula duniani , alisema: Hakuna nyumba ambayo haikuathiriwa . hakuna Umeme, hakuna mawasiliano.

    Barabara zimejaa magogo ya nyaya za umeme. Paa za nyumba zimeanguka pamoja na nyuta zake. raia wengi wa mji huo wamepoteza makaazi yao.

    Idadi rasmi ya watu waliofariki nchini Msumbiji inadaiwa kuwa watu 84 kufuatia mafuriko na upepo mkali.

    Kimbunga hicho kimewaua takriban watu 180 katika eneo lote la Afrika Kusini.

    Shirika la msalaba mwekundu limeelezea uharibifu huo kuwa mbaya zaidi na wa kutisha. Watu wamelazimika kuokolewa wakiwa juu ya miti , Jamie LeSeur mkuu wa IFRC aliambia BBC.

    Nchini Zimbabwe takriban watu 98 wamefariki huku 217 wakiwa hawajulikani waliko mashariki na kusini serikali imesema.

    Idadi ya watu waliofariki inashirikisha wanafunzi wawili wa shule ya St Charles Lwanga katika wilaya ya Chimanimani, ambao walifariki baaada ya bweni lao kuathiriwa kutokana na mawe yaliosombwa na maji hayo katika mlima.

    Malawi pia nayo iliathiriwa vibaya . Mafuriko nchini humo yaliosababishwa na mvua kabla ya kimbunga hicho kuwasili yalisababisha mauaji ya vifo 122 kulingana na mitandao ya mashirika ya misaada.

    Serikali ya Uingereza inasema kuwa itatoa msaada wa kibinaadamu wenye thamani ya £6m kwa Msumbiji na Malawi.

    Pia imesema kuwa itatuma mahema pamoja na maelefu ya mahema nchini Msumbiji.

    Uharibifu wa Beira ni mkubwa kiasi gani?

    Wengi wa wale wanaojulikana kufariki waliuawa karibu na mji wa Beira , ambao ndio mji mku wa nne kwa ukubwa ukiwa na idadi ya watu isiopungua nusu milioni kulingana na mamlaka.

    Zaidi ya watu 1500 walijeruhiwa na miti pamoja na vifusi vilivyoanguka ikiwemo paa , kulingana na maafisa katika mji mkuu wa Maputo waliozunguzma na BBC.

    ”Karibu kila kitu kimeathiriwa na janga hili” , Alberto Mondlane , gavana wa mkoa wa Sofala unaoshirikisha Beira alisema siku ya Jumapili. Tuna watu wanaotaabika kwa sasa , wengine juu ya miti na wanahitaji sana msaada.

    Barabara inayounganisha Beira na maeneo mengine ya taifa hilo iliharibiwa vibaya, lakini usafiri wa ndege hadi maeneo yalioathirika pakubwa umeanzishwa.

    Rais Filipe Nyusi alikata ziara yake ya Swaziland ili kutembelea maeneo yalioathirika.

    Manusura katika hospitali moja katika wilaya ya Chimanimani walizungumza kuhusu vile mafuriko hayo yalivyoharibu nyumba zao na kuwasomba wapendwa wao.

    ”Hadi sasa sijui ni wapi mwangu yupo” , Jane Chitsuro aliambia shirika la habari la AFP . ”hakuna samani , hakuna nguo ni vifusi na mawe pekee’.

    Nyumba ya Praise Chipore pia nayo iliharibiwa .

    ”Mwanangu alikuwa nami kitandani akasombwa na mafuriko huku mafuriko makubwa yakinisomba mie pia”, alisema.

     

  • Utepe mweupe watoa ujumbe kwa jamii

    Utepe mweupe watoa ujumbe kwa jamii

    Wadau wa sekta ya Afya wameazimisha siku ya Muungano wa Utepe mweupe wa uzazi salama katika mkoa wa Kagera kwa kuhimiza jamii kuzuia ukatili wa kijinsia kwa wanawake na wasichana

    Maazimisho hayo yamefanyika katika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera yakiwa na kauli mbiu ‘komesha  unyanyasaji kwa wanawake na wasichana, okoa maisha wakati wa uzazi’.

    Meneja Mawasiliano wa Muungano wa Utepe mweupe wa uzazi salama, Anna sawaki amesema kuwa lengo la kufanya maazimisho ni kuweza kupunguza vifo kwa wanawake wakati wa kujifungua.

    Amesema kuwa takwimu zinaonyesha vifo vitokanavyo na uzazi vinaongezeka badala ya kupungua kutokana na unyanyasaji wanaoupata akina mama pindi wawapo wajawazito na wakati wa kujifungua.

    Kwa upande wake mratibu wa taifa wa muungano wa utepe mweupe wa uzazi salama, Rose Mlayi ameiomba jamii  kukomesha ukatili kwa wanawake na wasichana, ili kuokoa maisha yao wakati wa uzazi.

    Katika hotuba ya Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu iliyosomwa kwa niaba yake na Mkuu wa wilaya ya Bukoba, Deodatus Kinawilo amesisitiza kuwa serikali kupitia idara zake inaendelea kukomesha vitendo hivyo, ikiwemo kuendelea na mikakati yake ya kutokomeza vifo vitokanavyo na uzazi pingamizi.

    Waziri ummy ameongeza kuwa wizara yake inaendelea kuboresha sekta ya afya hasa upande wa vituo vya afya pamoja na vifaa tiba ambapo pia ameeleza mkakati wa kuanzisha vituo vya huduma jumuishi kwa kila kituo cha afya.

  • Watu 10 wamefariki kutokana na uhaba wa chakula

    Watu 10 wamefariki kutokana na uhaba wa chakula

    Zaidi ya watu 10 wameripotiwa kufariki kutokana na ukame katika kaunti ya Turkana nchini Kenya,

    Wengine zaidi ya 800,000 wakiendelea kuumia kwa makali ya njaa na kiu kwa mujibu wa wizara ya kudhibiti majanga na utumishi wa umma ya kaunti ya Turkana.

    Mariam Loolio ni ajuza mwenye umri was miaka 85. Kwa siku tano anasema hajala chochote

    Serikali ya kaunti hiyo wiki iliyopita ilitoa hakikisho kwamba imeidhinisha mpango wa usaidizi kuwakinga wakaazi kutokana na madhara ya ukame uliopo.

    Katika kijiji cha Kakwanyang’ Turkana ya Kati, mizoga ya wanyama iliyotapakaa, na miti yaliyokauka inaashiria hali inayoshuhudiwa katika eneo hilo kutokana na na ukame.

    Wakaazi wengi katika kijiji hiki hawajatia chakula chochote mdomoni kwa muda wa karibu siku 5 zilizopita.

    Kwa sasa wakaazi hawa wanalazimika kutuliza makali ya njaa kwa kula matunda ya mwituni yajulikanayo kama Mkoma.

    Moru Lomutan ni mzazi wa watoto sita na nilipofika nyumbani kwake nilimkuta akiwa analigonga gonga tunda la Mkoma ili kulifanya liwe laini kwake kutafuna.

    “Najaribu kuligonga hili tunda kwa mawe ili nile kwa sababu sina hata nguvu ya kuliuma mdomoni”

    Katika bwawa la maji, watu walikuwa wamejaa, kina mama na watoto.

    Miale ya jua sio kizuizi kwa wanakijiji hao kusimama kwenye foleni kwa muda mrefu ili kuweza kujipatia maji.

    Karibu na bwawa hilo mizoga ya mbuzi na kondoo imetapakaa. Wakaazi wanadai kuwa mifugo hao walifariki baada ya kukosa chakula na maji.

    Anna Emaret amepoteza mifugo wake 20. Anasema amekuwa akigawana chakula na mifugo wake, lakini chakula kilipoisha, wakafa.

    “Kondoo wangu wote wamekufa, mbuzi pia wamekufa. Sasa sina mifugo, sina chakula, serikali isipotusaidia, tutakufa tu kama mifugo wetu”

    Mariam Loolio ni ajuza mwenye umri was miaka 85. Kwa siku tano hajala chochote .

    “Nimekaa hapa kungoja serikali ituletee chakula. Munavyoniona mimi ni mzee, tena kipofu. Hakuna jinsi ninavyoweza kutafuta chakula, hakuna kabisa. Kwa hivyo nasubiri tu serikali ije iniokoe ili nisife njaa. Sina namna”

    Nancy Alimlim alimzika kakake siku ya Jumamosi. Anaelezea kwa uchungu huku akibubujikwa na machozi.

    Maji yamekuaka katika visima na mabwawa ya maji

    Ukame umekuwa ukishuhudiwa kwa miaka mingi katika kaunti hii.

    Kila mara ukame unapobisha hodi, maisha ya wakaazi na mifugo wao huwa hatarini.

    Nchini Uganda katika Jimbo la Karamoja karibu na eneo hili la Turkana, Rais Museveni alijenga bwawa ambalo hutumiwa na jamii ya Karamoja ambayo ni jamii ya wafugaji.

    “Kwanini serikali ya Kaunti na ile serikali kuu zisiungane pamoja na kutafutia wananchi suluhisho mwafaka na la kudumu kama ilivyofanywa na Rais Museveni upande ule mwingine?…” anauliza Paul Jaling’a, kiongozi wa vijana katika Kaunti ya Turkana.

    Anna Emaret anasema amekuwa akigawana chakula na mifugo wake, lakini chakula kilipoisha, wakafa.

    “Inapaswa sisi kama vijana tuelimishwe jinsi ya kufuga mifugo kwa manufaa ya biashara. Isiwe tu kwamba tunafuga mifugo kisha kiangazi kikianza, tunarudi kuwa masikini.

    “Kuuza mifugo wakati wa mvua na kuwekeza fedha ili kujinusuru wakati wa kiangazi itasaidia pakubwa katika kuhakikisha kwamba ukame unasalia kuwa historia”.

    baadhi ya maeneo ya mashariki, kaskazini na kaskazini magharibi mwa Kenya ambapo kuna jamii za wafugaji, huenda zikakabiliwa na mzozo wa uhaba wa chakula.