Author: E-FM CO LTD

  • Korea Kaskazini yadai kufanyia majaribio ‘silaha mpya’

    Korea Kaskazini yadai kufanyia majaribio ‘silaha mpya’

    Korea Kaskazini imesema kuwa imefanyia majaribio silaha yenye kombora kali , ikiwa ni mara ya kwanza tangu mazungumzo kati ya rais Donald Trump na Kim Jong un kugonga mwamba.

    Vyombo vya habari vya serikali vilitoa maelezo , lakini wachanganuzi wanansema kuwa jaribio hilo halionekani kuwa lile la kombora la masafa marefu ambalo ni tishio kwa Marekani.

    Jaribio jingine kama hilo mnamo mwezi Novemba lilionekana kama hatua ya kuishinikiza Marekani kurudi katika meza ya mazungumzo.

    Kumekuwa na hatua chache zilizopigwa tangu mazungumzo ya kinyuklia yaanze msimu wa joto uliopita.

    Mnamo mwezi Februari , Donald Trump na Kim Jong Un walikutana katika mji mkuu wa Vietnam Hanoi kuzungumzia usitihswaji wa umiliki wa silaha za kinyuklia , lakini mazungumzo yalivunjika huku viongozi wote wawili wakiondoka ghafla.

    Wiki iliopita bwana Kim alisema kuwa rais Trump alifaa kuwa na tabia nzuri ili ,mazungumzo kuendelea.

    Kulingana na chombo cha habari cha Korea KCNA jaribio hilo lilisimamiwa na bwana Kim mwenyewe.

    KCNA iliripoti kwamba jaribio hilo lilifanywa katika awamu kadhaa za kulirusha , ambapo wachanganuzi wanaamini huenda silaha hiyo ilijaribiwa kutoka katika ardhi, baharini ama angani.

    Bwana Kim alisema kuwa hatua hiyo ilikuwa na uzito mkubwa katika kuimarisha jeshi lake.

    Ripoti hiyo ilitoa maelezo machache hivyobasi haijulikani iwapo lilikuwa kombora , lakini wadadisi wanasema kuwa huenda ilikuwa silha ya masafa mafupi.

    Mwaka uliopita , kiongozi huyo wa Korea alisema kuwa atasitisha majaribio ya silaha za kinyuklia na kwamba hatofanyia majaribio makombora ya masafa marefu huku uwezo wa Kinyuklia wa Pyonyang ukibainika.

    Vitendo vya kinyuklia vilionekana vikiendelea, hatahivyo picha za Setlaiti katika kiwanda kikubwa cha kinyuklia cha taifa hilo wiki ilioipita zilionyesha kulikuwa na vitendo vilivyokuwa vikifanyika-zikidai kwamba huenda Korea kaskazini inatengeneza mionzi kuwa mafuta ya bomu.

    Taifa hilo linadai kwamba limetenegeza bomu la kinyuklia ambalo linaweza kuingia katika kichwa cha silaha ya masafa marefu pamoja na kombora ambalo linaweza kufika Marekani,

    Mchanganuzi wa Korea Kaskazini Ankit Panda alisema kwamba tangazo hilo la mwisho lilifuatia zoezi la kijeshi lililofanyika kati ya Marekani na Korea kusini na kusema kuwa jaribio hilo lilipanga kulipza kisasi.

    Ni hatua chache zilizopigwa tangu mazungumzo kati ya Marekani na Korea Kaskazini kuvunjika mjini Hanoi.

    Marekani ilisema kuwa mazungumzo hayo yalivunjika baada ya Korea Kaskazini kutaka vikwazo vyote kuondolewa ili kuweza kupunguza uwezo wake wa utenegenezaji wa silaha za kinyuklia , lakini Pyongyang imepinga hilo.

    Katika matamshi yake ya hivi karibuni , bwana Kim alimtaka Trump kutafuta makubaliano ambayo yatakubaliwa na pande zote mbili lakini pia akazungumzia kuhusu uhusiano wake mzuri na rais Trump.

    Naye bwana Trump alijibu kupitia mtandao wake wa Twitter kwa kumsifu bwana Kim na kukubali wazo jingine la mkutano mwengine.

    Mapema wiki hii wizara ya maswala ya kigeni ya Marekani ilitangaza kuwa Stephen Biegun , mjumbe maalum wa Korea Kaskazini alikuwa anaelekea Moscow kwa mikutano na maafisa wa Urusi ili kuzungumzia kuhusu hatua ya mwisho ya kuangamiza silaha za kinyuklia nchini Korea Kaskazini.

    Ziara hiyo ilijiri huku kukiwa na uvumi kuhusu mkutano wa Kim Jong Un na Vladmir Putin.

    cc;BBCswahili

  • Kanisa kongwe la Notre-Dame lateketea Ufaransa

    Kanisa kongwe la Notre-Dame lateketea Ufaransa

    Moto mkubwa umezuka katika kanisa kongwe la Notre-Dame mjini Paris Ufaransa ambalo ni moja ya makanisa maarufu na linalotembelewa na idadi kubwa ya watalii kutoka pande mbali mbali duniani kila mwaka.

    Vikosi vya zima moto vinaendelea kuzima moto huo katika kanisa hilo lililodumu kwa takriban miaka 850.

    Sehemu kubwa ya paa la majengo ya kanisa hilo yameteketezwa na mto huo huku moto katika minara miwili ya kengele umefanikiwa kuzimwa.

    Chanzo cha moto huo hakijajulikana, lakini maafisa maafisa wanauhusisha mkasa huo na shughuli ya ukarabati inayoendelea.

    Wazima moto wanafanya kila juhudi kuokoa vito vya thamani vilivyoko ndani kanisa hilo na pia kuzuia mnara wa upande wa kasskazini kutoporomoka.

    Maelfu ya watu wamekusanyika katika barabara zilizo karibu na kanisa hilo kushuhudia mkasa huo wakiwa kimya.

    Baadhi yao walionekana wakidondokwa na machozi, huku wengine wakiimba nyimbo za sifa na kuomomba Mungu.

    Makanisa kadha nchini Ufarasa yamekua yakipiga kengele kuashiria uharibifu wa moto huo.

    Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron,ambaye alifika katika eneo la tukio amesema mawazo yake yako na “waumini wote wa kanisa katoliki na wafaransa wote kwa ujumla.”

    “Sawa na watu wengine nchini , nimesikitika sana kuona sehemu ya maisha yetu ya kila siku ikiteketea.”

    Bw. Macron awali alifutilia mbali hutuba mmuhimu kwa taifa kufuatia moto huo, alisema afisa wa Élysée Palace.

    Msemaji wa kanisa hilo pia amekiri kuwa sehemu kubwa imeteketea na bado inaendelea “kuteketea”.

    Mwanhistoria Camille Pascalameliambia shirika la habari lla Ufaransa BFMTV kwamba moto umeharibu ”turathi ya kitaifa”

    “Kanisa hili limedumu Paris kwa takribani miaka 800 “, alisema.

    “Matukio ya furaha na ya kusikitisha kwa karne kadhaa yamekua yakiadhimishwa kupitia mlio wa kengele za Notre Dame.

    “Tunasikitishwa na kile kilichotokea na kile tunachojionea”.

    Meya wa jiji la Paris, Anne Hidalgo ametoa wito kwa wakaazi kuheshimu mipaka iliyowekwa na maafisa wa zima motoili kuwahakikishia usalam wao.

    “Kuna kazi nyingi inayoendelea ndani …hili ni janga kubwa,” aliwaambia wanahabari.

    The Notre-Dame cathedral, ambalo umaarufu wake huwavuvia maelfu ya watalii kila mwaka, lilikua likifanyiwa ukarabati baada ya nyufa zake kupasuka na kuzua hofu huenda jengo hilo likawa dhaifu.

    Mwak jana, kanisa katoliki liliomba msaada Ufaransa kufanyia ukarabati jengo la kanisa hilo la zamani.

    Maelezo kuhusu Notre-Dame

    • Kanisa hilo hupokea karibu wageni milioni 13 kila mwaka, idadi ambao ni kubwa kuliko watalii wanaozuru Eiffel Tower
    • Lilijengwa katika karne ya 12 na 13 na limekuwa likifanyiwa ukarabati mkubwa.
    • Sanamu kadhaa ziliondolewa kanisani hapo ili kuruhusu ukarabati wake.
    • Palaa la lanisa hilo lililoteketezwa na moto lilikua limetengenezwa kwa kiasi kikubwa kutokana na mbao

     

  • Maambukizi ya Ukimwi yapungua nchini

    Maambukizi ya Ukimwi yapungua nchini

     Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Sera, Bunge, Uratibu, Ajira, Kazi, Vijana na Wenye Ulemavu, Jenista Mhagama amesema kuwa utafiti wa viashiria na matokeo ya Ukimwi wa mwaka 2016/17 unaonyesha kwamba kiwango cha maambukizi ya VVU yamepungua kwa asilimia moja kutoka asilimia 5.1 mwaka  2011/2012 mpaka asilimia 5.0 kwa mwaka 2016/17.

    Waziri Mhagama amesema hayo wakati akizindua utafiti huo ambapo ameeleza kuwa unaonyesha kwamba kiwango cha maambukizi ya VVU kwa watu wenye umri wa miaka 15-64 umepungua kwa asilimia moja kutoka asilimia 5.1 mwaka 2011/2012 na kufikia  asilimia 5.0 kwa mwaka 2016-2017 ambapo wanawake ni asilimia 6.5 na wanaume ni asilimia 3.5.

    Amesema asilimia 60.9 ya watu wanaoishi na VVU ndio wanaofahamu hali zao ikiwa ni chini ya kiwango cha lengo ambapo amedai wamaofahamu hali zao asilimia 93.6 ndio wanaopatiwa dawa  za kufubaza makali ya VVU (ARV) ambao miongoni mwao asilimia 87.0 virusi vyao vimefubazwa.

    Ameongeza kuwa utafiti huo unaonesha zaidi ya nusu milioni ya watu wanaoishi na VVU Tanzania hawajui hali yao ya maambukizi.

    “Juhudi za pamoja za wenye wigo mpana zinahitajika kuwafikia watu wanaishi na VVU ambao bado hawajapima na kujua hali zao  nakuanza dawa,” alisema.

    Amesema takribani watu 72,000 wanapata maambukizi mapya huku kiwango cha wanaume kujua maambukizi kikiwa kipo chini kuliko wanawake.

  • Mwanafunzi Chuo Kikuu amchoma visu mpenzi wake

    Mwanafunzi Chuo Kikuu amchoma visu mpenzi wake

    Mwanafunzi wa kike wa mwaka wa tatu katika Chuo Kikuu cha Pwani kilichoko Kaunti ya Kilifi nchini Kenya, jana alichomwa visu mara kadhaa na mwanafunzi mwenzake anayedaiwa kuwa alikuwa mpenzi wake.

    Mwanafunzi huyo aliyetajwa kwa jina la Naomi Chepkemboi, alichomwa visu mara kadhaa kifuani na alikimbizwa katika hospitali ya Kaunti ya Kilifi anakoendelea kupatiwa matibabu.

    Kwa mujibu wa Jeshi la polisi, mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kenyatta aliyetambulika kwa jina la Henry Kipkoech, ambaye alikuwa mpenzi wake anashikiliwa na jeshi hilo kwa tuhuma la kumchoma kisu Naomi.

    Ripoti ya awali ya Polisi imeeleza kuwa Henry alifika kwenye nyumba ya Naomi jana asubuhi akiwa na begi lenye visu vitatu. Aliingia ndani na kufunga mlango kisha kuanza kumshambulia msichana huyo ambaye alipiga kelele za kuomba msaada. Wanafunzi wenzake ndio waliofanikiwa kumuokoa.

    Mtuhumiwa huyo alikamatwa na kupelekwa kwenye kituo cha polisi cha Kilifi ambako anashikiliwa kwa ajili ya hatua zaidi za kisheria, kwa mujibu wa Citizen.

     

  • Maafisa wa zamani wa serikali matatani Sudan

    Maafisa wa zamani wa serikali matatani Sudan

    Baraza la mpito la kijeshi nchini Sudan limewakamata waliokuwa maafisa wa serikali na kuahidi kutowatawanya waandamanaji.

    Msemaji mmoja pia ameuomba upinzani kumchagua waziri mkuu mpya na kuahidi kumuidhinisha watakayemchagua.

    Maandamano ya miezi kadhaa nchni Sudan yamechangia kutimuliwa kwa kiongozi wa muda mrefu nchini Sudan Omar al-Bashir Alhamisi wiki iliyopita

    Waandamanaji wameapa kusalia mitaani mpaka itakapoundwa serikali ya kiraia

    Raia wanaendelea kuandamana na wamekita kambi nje ya makao makuu ya wizara ya ulinzi katika mji mkuu Khartoum.

    Katika mkutano na waandishi habari siku ya Jumapili, msemaji Meja Jenerali Shams Ad-din Shanto ameeleza kwamba baraza la kijeshi lipo “tayari kuidhinisha” serikali yoyote ya kiraia itakayoidhinishwa na vyama vya upinzani.

    “Hatutomteua waziri mkuu. Watamchagua,” alisema akimaanisha upinzani na makundi yanayoandamana.

    Ameeleza pia kwamba jeshi halitowaondoa waaandamanaji kwa lazima lakini ametoa wito kwa waandamanaji hao “kuruhusu maisha yaendelee kama kawaida” na waache kuweka vizuzi kinyume cha sheria.

    “Kushika silaha hakutoruhusiwa,” aliongeza

    Maandamano ya kupinga kupanda gharama ya maisha yalianza Desemba mwaka jana lakini punde tu yakageuka kuwa wito mkubwa wa kumpinga rais bashir na utawala wake.

    Aliyeongoza mapinduzi hayo, waziri wa ulizni Awad Ibn Auf, alitangaza kwamba jeshi litasimamia serikali ya mpito kwa kipindi cha miaka miwili kitakachofuatwa kwa uchaguzi na akaidhinisha miezi mitatu ya hali ya dharura.

    Lakini wandamanji waliapa kusalia mitaani hata baada ya hatua hiyo, wakitaka maguezi na kuidhinishwa kwa serikali ya kiraia mara moja.

    A Sudanese girl flashes the victory sign and holds the national flag during a rally near the military headquarters in the capital Khartoum on April 11, 2019. – The Sudanese army is planning to make “an important announcement”, state media said today, after months of protests demanding the resignation of longtime leader President Omar al-Bashir. Thousands of Khartoum residents chanted “the regime has fallen” as they flooded the area around army headquarters where protesters have held an unprecedented sit-in now in its sixth day. (Photo by – / AFP)-/AFP/Getty Images

    Ibn Auf himself alijiuzuliu ziku ya pili , kama alivyojiuzulu mkuu wa usalama anayeogopwa na wengi Jenerali Salah Gosh.

    Luteni Jenerali Abdel Fattah Abdelrahman Burhan baada ya hapo alitajwa kuwa kiongozi wa baraza la mpito la kijeshi, kuwa kiongozi wa tatu kuwahi kushuhudiwa katika kipindi cha siku nyingi.

    Lakini muungano wa wataalamu Sudan (SPA), ambao umekuwa ukiongoza maandamano hayo umesema muitikio wa baraza hilo “haukudhihirisha matakwa yoyote ya raia” na ametaka maandamano yaendelee.

    Miongoni mwa matakwa yao ni kutaka idara ya ulinzi ifanyiwe mageuzi, “viongozi wafisadi” wakamatwe na kuvunjiliwa mbali makundi ya sungusungu yaliohudumu chini ya rais wa zamani Bashir.

    Kiongozi huyo wa zamani hajulikani yuko wpai, lakini viongozi wa mapinduzi hayo wanasem ayumpo mahali salama.

    Bashir ameshtakiwa kwa mashtaka ya uhalifu wa vita na uhalifu dhidi ya binaadamu huko Darfur na mahakama ya kimatiafa ya jinai ICC.

     

  • Polisi wakatazwa kuwashambulia waandamanaji Sudan

    Polisi wakatazwa kuwashambulia waandamanaji Sudan

    Polisi nchini sudan imewaamuru maafisa wake kutowashambulia maelfu ya waandamanaji waliopiga kambi nje ya makao makuu wa jeshi mjini Khartoum tangu Ijumaa.

    Waandamanaji hao wanamtaka rais Omar al-Bashir ajiuzulu.

    Awali milio ya risasi ilisikika nje ya makao ya jeshi na ripoti zinasema kuwa maaskari wanaotoa ulinzi kwa waandamanaji wamepigwa risasi na maajenti wa serikali.

     

    Katika taarifa yake msemaji wa polisi aliandika”Tunatoa amri kwa vikosi vyote” visiingilie “maandamano ya amani aukuwashambulia wananchi”.

    “Tunamuomba Mungu asaidie kuleta utulivu nchini mwetu… na kuwaunganisha Wasudan… na kufikiwa kwa makubaliano yatakayosaidia kupokezana madaraka kwa amani,” iliendelea kusema taarifa hiyo.

    Waziri wa mambo ua ndani wa nchi hiyo amesema waandamanaji saba waliuawa siku ya Jumatatu na wengine 15 kujeruhiwa, huku maafisa 42 wa vikosi vya usalama nao wakijeruhiwa pia.

    Ameongeza kuwa karibu watu 2,500 wamekamtwa.

    Mmoja wa wandamanani hao, Ahmed Mahmoud, ameimbia BBC kuwa maajenti wa kitaifa wa upelelezi walitumia mabomu ya kutoza machozi na risasi halisi dhidi ya waandamanaji.

    Amesema maaskari wamewatengea eneo salama waandamanaji karibu na makao makuu ya jeshi la taifa.

    “Hakuna haja ya Omar al-Bashir kutumumia majangili wake kutuondoa barabarani, hatuendi popote,” alisema.

    Mwandamanaji mwingine ameiambia BBC kuwa sio kila mwanajeshi ana unga mkono vugu vugu la maandamano; Maafisa wa ngazi ya juu jeshini wanaunga mkono serikali iliyopo madarakani, huku wale wa ngazi ya chini wakiunga mkono waandamanaji.

    Siku ya Jumatatu kuliibuka video inayowaonesha maafisa wakifyatua risasi kuelekea sehemu ambayo haikubainika huku waandamanaji wakijificha nyuma yao.

     

    Waandamanaji walisema kuwa maafisa hao walikuwa wanajibu mashambulio kutoka kwa maajenti wa NISS.

    Kumekuwa na miito ya kuitaka serikali ya Sudan kutotumia nguvu kupita kiasi dhidi ya raia.

    Marekani, Uingereza na Norway yametoa wito kwa serikali kutoa suluhisho la mpito la kisiasa.

    ”Ni vyema serikali ishughulikie matakwa ya wandamanaji kwa njia “ya uwazi na uwajibikaji”, ilisema taarifa yao.

    “Kutofanya hivyo kutasababisha machafuko. Mamlaka nchini Sudan ina jukumu la kuzua matukio kama hayo,” iliendelea kusema taarifa yao..

    Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito kwa pande zote mbili “kuwa na subira ili kuzuia kuzuka kwa machafuka”.

    Mwandishi habari Mohamed Ali Fazari, aliyekuwepo katika umati wa waandamanaji mjini Khartoum, anasema waanadamanaji hao wanaliomba jeshi lishirikiane na raia dhidi ya serikali.

    Umati ulipiga kelele ukisema “uhuru, uhuru, haki – jeshi moja, watu wamoja”, ameiambia BBC.

    Kiini cha maandamano hayo awali kilitokana na gharama kubwa ya maisha lakini sasa ni ya kumshinikiza rais Bashir ambaye amekuwa madarakani kwa takriban miaka 30 sasa, ajiuzulu.

    Uchumi wa Sudan umeathirika kwa muda mrefu na vikwazo vya Marekani kwa zaidi ya miaka 20 iliyopita inayoishutumu Khartoum kwa kufadhili makundi ya kigaidi.

    Utawala wake umegubikwa kwa shutuma za uikukaji wa haki za binaadamu.

    Mnamo 2009 na 2010, mahakama ya kimataifa ya jinai (ICC) ilimshtaki kwa makosa ya uhalifu wa kivita, mauaji ya kimbari na uhalifu dhidi ya binaadamu.

    Marekani iliiwekea vikwazo Sudan kwa zaidi ya miaka 20 iliyopita kwa tuhuma za kufadhili makundi ya kigaidi.

    Mnamo Desemba mwaka jana serikali ya Sudan ilitangaza kwamba bei ya mafuta na mkate itapanda.

    Katika mwaka uliofuata uamuzi huu, gharama ya maisha ilipanda huku pauni ya Sudan ikashuka thamani kwa kiasi kikubwa.

    Tangazo la kupanda kwa bei ya bidhaa hizo ilichangia kuzuka maandamano, yaliogeuka kuwa shinikizo dhidi ya Bashir ajiuzulu.

    Mwezi Februari kulikuwana fununu rais Omar al Bashiri atajiuzulu lakini katika hotuba yake kwa taifa rais huyo alitangaza hali ya hatari kote nchini humo

    Maandamano ya hivi punde yanajiri huku taifa hilo likiadhimisha ukumbusho wa 34 wa mapinduzi yaliyoondoa madarakani utawala wa rais wa zamani wa Sudan Jaafar Nimeiri.

    cc;-BBCswahili

  • Wanasayansi wagundua mti mrefu zaidi duniani

    Wanasayansi wagundua mti mrefu zaidi duniani

    Wanasayansi nchini Uingereza na Malaysia wanasema kuwa wamegundua mti mrefu zaidi duniani wenye urefu wa zaidi ya mita 100.

    Mti huo wa kitropiki aina ya meranti ulipatikana katika msitu wa Borneo na kundi moja kutoka chuo kikuu cha Nottingham mwaka uliopita.

    Watafiti kutoka katika chuo kikuu cha Oxford walifanya utafiti huo kwa kutumia kamera zisizokuwa na rubani kuthibitisha rekodi hio.

    Mti huo uliopatikana katika eneo la uhifadhi la Danum Valley huko Sabah umepewa jina Menara ambalo linamaanisha jumba refu.

    Mkweaji miti kutoka eneo hilo, jami ambaye aliupima mti huo kwa kutumia kamba alisema alliogopa kuupanda mti huo

    ”Lakini kwa kweli picha kutoka juu ilikuwa nzuri mno. Sijui cha kusema isipokuwa tu ulikuwa uzoefu mzuri sana”, aliongezea.

    Daktari Doreen Boyd, kutoka chuo kikuu cha Nottingham, alisema kuwa ugunduzi huo ulikuwa muhimu kwa kuwa ni sayansi inayosema miti kama hii inapatikana , ni mirefu hali ya kwamba hatukuwahi kudhania na huenda kuna miti mirefu zaidi ambayo haijagunduliwa.

    ”Inatuambia kwamba tunahitaji kuilinda miti”, alisema.

    Daktari Alexander Shenkin , kutoka chuo kikuu cha Oxford , alisema baada ya kusikia ugunduzi huo walitembea kwa muda wa saa tatu hadi Menara.

    Alisema: Nimeona kile ambacho wanasema ni miti mingi , lakini nilipotembea hadi katika mti huu, kichwa changu kilizidi kuangalia juu unapokaribia kileleni.

    Sijawahi kuona mti mrefu kama huu.

  • Waandamanaji katika makao makuu ya jeshi waongeza shinikizo dhidi ya rais Omar al-Bashir ajiuzulu

    Waandamanaji katika makao makuu ya jeshi waongeza shinikizo dhidi ya rais Omar al-Bashir ajiuzulu

    Maelfu ya waandamanaji wamekita kambi nje ya makao makuu ya jeshi nchini Sudan, wakimtaka rais Omar al-Bashir ajiuzulu.

    Inavyoonekana wanatarajia mapinduzi ya ndani ya nchi, wakiliomba jeshi kumtimua Bashir na kufungua njia ya kupatikana serikali ya mpito.

    Ni maandamano makubwa dhidi ya Bashir tangu kuzuka ghasia mnamo Desemba mwaka jana.

    Bashir amekataa kuondoka, akieleza kwamba wapinzani wake wanastahili kutafuta uongozi kupitia uchaguzi. Jeshi halijaingilia kati.

    Maafisa wa usalama wamefyetua gesi ya kutoa machozi kuwatimua wandamanaji nje ya makao hayo makuu katika mji mkuu, Khartoum.

    Maandamano haya yanaadhimisha miaka 34 ya mapinduzi yaliouondoa utawala wa rais Jaafar Nimeiri.

    Katika maandamano ya nyuma, wamettumia pia guruneti na silaha za moto zikiwemo risasi. waandamanaji kadhaa wameuawa .

    Siku ya Jumamosi, mwandamanaji mmoja alifariki katika mji wa Omdurman, polisi wanasema.

    Waziri wa habari nchini Sudan amethibitisha mipnago ya serikali kutatua mzozo kupitia mazungumzo na kupongeza vikosi vya usalama.

    Ni wazi kwamba yanayodhihirika katika mji mkuu Khartoum yanardhirisha. Umati kama huuu haujawahi kushuhudiwa kwa miongo kadhaa.

    Lakini kumeshuhudiwa vifo kadhaa na kuna uwezekano wa kuwepo msako mkali kwa hivi sasa.

    Na hata iwapo rais Bashir atajiuzulu hakuna uhakika kwamba nafasi yake itachukuliwa na serikali itakayokuwa na uwakilishi wa wengi kama wanavyotaka waandamanaji.

    Serikali za utawala wa nguvu katika karne ya 21 barani Afrika zimeadimika na kutoa taswira ya mabadiliko lakini inayotoa maana finyu.

    Kinachofichuka sasa huenda ni sehemu ya ushindani wa kisiasa usiotarajiwa wa muda mrefu zaidi.

    Mwandishi habari Mohamed Ali Fazari, aliyekuwepo katika umati wa waandamanaji mjini Khartoum, anasema waanadamanaji hao wanaliomba jeshi lishirikiane na raia dhidi ya serikali.

    Umati ulipiga kelele ukisema “uhuru, uhuru, haki – jeshi moja, watu wamoja”,

    Kiini cha maandamano hayo awali kilitokana na gharama kubwa ya maisha lakini sasa ni ya kumshinikiza rais Bashir ambaye amekuwa madarakani kwa takriban miaka 30 sasa, ajiuzulu.

    Uchumi wa Sudan umeathirika kwa muda mrefu na vikwazo vya Marekani kwa zaidi ya miaka 20 iliyopita inayoishutumu Khartoum kwa kufadhili makundi ya kigaidi.

    Mnamo Desemba mwaka jana serikali ya Sudan ilitangaza kwamba bei ya mafuta na mkate itapanda

    Katika mwaka uliofuata uamuzi huu, gharama ya maisha ilipanda huku pauni ya Sudan ikashuka thamani kwa kiasi kikubwa.

    Tangazo la kupanda kwa bei ya bidhaa hizo ilichangia kuzuka maandamano, yaliogeuka kuwa shinikizo dhidi ya Bashir ajiuzulu.

     

    Utawala wake umegubikwa kwa shutuma za uikukaji wa haki za binaadamu.

    Mnamo 2009 na 2010, mahakama ya kimataifa ya jinai (ICC) ilimshtaki kwa makosa ya uhalifu wa kivita, mauaji ya kimbari na uhalifu dhidi ya binaadamu. Waranti wa kumkamata umetolewa.

    Usalama umeimarishwa pakubwa mitaani huku gesi za kutoa machozi zikitumika kiholela na ripoti za kuwepo ghasia zikiwa ni jambo la kawaida.

    Maafisa nchini humo wameshutumiwa kwa kuwakamata wanaharakati maarufu na kuwalenga matabibu , jambo ambalo idara ya ujasusi inakana.

    Maafisa wanasema watu 32 wamefariki katika ghasia zinazohusiana na maandamano kufikia sasa, lakini shirika la Human Rights Watch linasema huenda idadi hiyo ni 51.

    Kundi la kutetea haki za binaadamu Physicians for Human Rights linasema lina ushahidi wa mauaji, na unyanyasaji wa waandamanaji wa amani na matabibu waliokuwa wakiwashughulikia.

     

    cc;BBCswahili

  • ‘Licha ya juhudi zao marubani walishindwa kuidhibiti ndege hiyo”

    ‘Licha ya juhudi zao marubani walishindwa kuidhibiti ndege hiyo”

    Ripoti ya uchunguzi kuhusu kuanguka kwa ndege ya Ethiopia Airlines mwezi uliopita inasema kuwa ndege hiyo ilitaka kuangukia pua yake mara kadhaa kabla ya ajali hiyo.

    Marubani walifuata maagizo yaliopendekezwa na Boeing kabla ya ajali hiyo kulingana na ripoti ya kwanza ya ajali hiyo.

    ”Licha ya juhudi zao , marubani walishindwa kuidhibiti ndege hiyo” , alisema waziri wa uchukuzi Dagmawit Moges.

    Ndege hiyo aina ya ET302 ilianguka baada ya kupaa kutoka mji wa Adis Ababa , na hivyobasi kuwaua watu 157.

    Ilikuwa ndege ya pili aina ya Boeing 737 kuanguka katika kipindi cha miezi mitano.

    Mwezi Oktoba mwaka uliopita , ndege aina ya Lion Airflight JT610 ilianguka baharini karibu na Indonesia na kuwaua watu wote waliokuwa wameabiri.

    ”Wafanyikazi wa ndege hiyo walijaribu kila mbinu walizoelezewa na mtengenezaji wa ndege hiyo lakini walishindwa kuidhibiti” , bi Moges alisema katika mkutano na wanahabari mjini Adis Ababa.

    Katika taarifa , afisa mkuu wa Ethiopia Airlines , Tewolde GebreMariam alisema kuwa alifurahishwa na kazi ya marubani hao kujaribu kuidhibiti ndege hiyo.

    ”Ni bahati mbaya kwamba walishindwa kuidhibiti ndege hiyo kutoangukia pua yake”, ilisema kampuni hiyo ya ndege katika taarifa yake.

    Mkurugenzi mtendaji wa Ethiopian Airlines CEO Tewolde Gebremariam ameuambia mkutano wa waandishi wa habari kwamba miongoni mwa waliokuwemo kwenye ndege hiyo ni pamoja na :

    Wakenya 32 Kenyans, raia wa Canada 18 raia tisa wa Ethiopia , wataliano wanane , Wachina wanane, wamarekani wanane , waingereza saba , Wafaransa saba , Wamisri sita, Wajerumani watano , Wahindi wanne na wanne kutoka Slovakia.

    Waaustralia watatu, Waswizi watatu, Warusi watatu , Warusi 3, Wakomoro wawili, Wahispania wawili, Wapoland wawili, Waisraeli wawili.

    Kulikuwa pia na abiria mmoja kutoka nchi za Ubelgiji, Indonesia, Somalia, Norway, Serbia, Togo, Msumbiji, Rwanda, Sudan, Uganda na Yemen.

    Boeing ambayo ni kampuni ambayo iliitengeneza ndege iliyoanguka , imesema kwenye ukurasa wake wa Twitter kwamba ‘inafuatilia kwa karibu hali’ ya mambo.

    Ndege ya 737 Max-8 ni mpya angani , ikiwa ilizinduliwa kwa mara ya kwanza 2016. Iliongezwa kwenye safari za ndege za Ethiopian Airlines Julai mwaka jana.

    Boeing imesema ”imesikitishwa sana” na ajali na imejitolea kutuma kikosi cha wahandisi wake kutoa usaidizi wa kiufundi.

    Afisa wa itifaki wa Somalia ameripotiwa kuwa mmoja wa watu waliokufa kwenye ajali hiyo , kulingana na kituo cha kibinafsi cha Radio Dalsan, kinachomilikiwa na redio ya Somalia.

  • Kenyatta amekuwa gumzo kuu katika mitandao ya kijamii nchini Kenya wakati akitarajiwa kulihotubia taifa leo.

    Kenyatta amekuwa gumzo kuu katika mitandao ya kijamii nchini Kenya wakati akitarajiwa kulihotubia taifa leo.

    Uhuru Kenyatta amekuwa gumzo kuu katika mitandao ya kijamii nchini Kenya wakati akitarajiwa kulihotubia taifa leo.

     

    Kiongozi huyo mkuu nchini Kenya anatarajiwa kuizungumzia hali ya mambo nchini katika hotuba anayotarajiwa kuitoa bungeni leo mchana.

    Na hili linatarajiwa kufanyika wakati ufisadi, deni kubwa la taifa na suala la ukosefu wa ajira na mishahara yakizungumziwa pakubwa na wakenya ambao wametumia fursa kumshinikiza kiongozi huyo kuyazungumzia leo.

    Swali kuu ni je, Rais Uhuru Kenyatta atasema nini leo kipya katika hotuba yake ya taifa?

    Baadhi ya Wakenya wanauliza, ‘Ni kipi kipya atakachotuambia ambacho hatujakisikia?’

    Baadhi wamegusia kwamba wangependa sana rais Kenyatta aangazie kuhusu matumizi ya fedha serikalini na uhaba wake unaochangia kuongezeka kwa mikopo – jambo linalowatia wasiwasi raia wengi.

    Uchumi wa Kenya umekuwa ukikua kwa kiwango cha wastani kila mwaka tangu kiongozi huyo aingie madarakani, lakini baadhi ya Wakenya wanasema hawajahisi manufaa ya ukuaji huo.

    Serikali imeshutumiwa kuchukua mikopo kwa wingi, baadhi wakikadiria kwamba serikali hiyo imepitisha viwango vya ukopaji vya serikali zote za awali tangu uhuru.

    Mchambuzi wa kisiasa nchini Kenya na Mhadhiri, katika Chuo Kikuu cha Nairobi Hezron Mogambi anahoji, swali ambalo limekuwa likiibuka miaka ya hivi karibuni ni iwapo Kenya itaweza kujimudu kulipa madeni ambayo yamekuwa yakijilimbikiza.

    Wakopaji wa kimataifa kupitia shirika la Moody’s katika siku za nyuma wameishusha Kenya daraja katika masuala ya ukopaji.

    Sababu zilizotolewa kwa hatua hiyo ni pamoja na hali ya kiuchimi isiyoonyesha matumaini kutokana na kulimbikizwa kwa madeni, kutegemea sana madeni ya kibishara na mahitaji ya kifedha mengi katika uchumi wa Kenya kutokana na miradi.

    ‘Hali hii ambayo inaonyesha ishara ya Kenya kutoweza kuyalipa madeni, ni suala linalotatiza na kuzua changamoto kwa serikali na wananchi kwa jumla,’ anasema Mogambi katika makala aliyoiandika kwenye BBC Swahili.

    Bw Kenyatta, hata hivyo amekuwa akisema kuwa uwekezaji wa pesa hizo katika miradi ya miundo mbinu, mfano reli ya kisasa kutoka Mombasa hadi Nairobi iliyogharimu $3.2bn (£2.5bn), itasisimua ukuaji wa uchumi nchini.

    Jambo jingine ambalo baadhi ya wakenya katika mitandao ya kijamii waliloinuka nalo moyoni na wanalotaka hatua madhubuti kuchukuliwa kulihusu ni ufisadi.

    Limekuwa donda sugu kwa miaka kadhaa nchini.

    Wakenya wanataka rais atoe muongozo au muelekeo thabiti katika kukabiliana na matatizo ya kiuchumi.

    Kumekuwa na kilio cha umma nchini Kenya kufuatia kashfa mbali mbali za rushwa ambazo hazijatatuliwa.

    Baadhi wamekuwa wakieleza kwamba wanahisi Rais hajachukua hatua stahiki na kwa muda mrefu kufikia sasa amewaendekeza ‘wahalifu’ katika serikali.

    Rais Kenyatta amekuwa akisema juhudi zake za kukabiliana na ufisadi zimehujumiwa na idara mbali mbali.

    Mwaka 2015, Kenyatta aliwasimamisha kazi na kisha akawafuta mawaziri watano na maafisa wengine wa ngazi ya juu serikali waliotuhumiwa kujihusisha katika ufisadi.

    Waziri mwingine alijiuzulu kutokana na shinikizo la umma.

    Katika orodha ya mataifa yanayoshuhudia ufisadi Kenya ipo katika nafasi ya 144 chini ya mataifa 180 kwa mujibu wa utafiti wa shirika la kimataifa la Transaparency International mnamo 2018.

    Kwa miaka mingi, kumekuwa na wito wa kwamba ufisadi unastahili kutangazwa janga la kitaifa nchini Kenya.

    Shinikizo limeongezeka kwa rais Uhuru Kenyatta asiteteleke katika vita dhidi ya ufisadi.

    Raia wanamtaka kiongozi huyo pia aidhinishe hatua zitakazohakikisha kwamba vita hivyo vinaendelezwa hata kwa uongozi ujao na wahalifu wachukuliwe hatua za kisheria.

    Kimsingi wanashinikiza kwamba vitendo vidhihirike zaidi ya maneno ‘matupu’.

    Kuna waliochukua fursa hii kumsifia rais kwa jitihada zake katika kuimarisha nchi na kufikia malengo manne makuu aliyoahidi katika kampeni ya kuchaguliwa kwake uongozini.

    Ajenda hizo kuu ambazo kiongozi wa Kenya ametilia maanani ni pamoja na kuimarisha sekta ya viwanda, afya, makaazi kwa bei nafuu na chakula.

    Tayari Hazina ya kitaifa ya matibabu nchini Kenya (National Hospital Insurance Fund) imeshaanza kutekeleza afya kwa umma.

    Lakini pia kuna wanaopigia upatu sekta ya usalama kwa mahali ambapo taifa limefika kwa sasa.

    Ijapo ni suala linalojadiliwa, kuna wanaosifia hatua angalau ndogo katika sekta hiyo.

    Kwa mfano wa hivi karibuni, muitikio ulioshuhudiwa katika shambulio lililotekelezwa na wapiganaji wenye itikadi kali za dini ya kiislamu jijini Nairobi tarehe 15 Januari umeonekana kama mapinduzi makubwa ya Propaganda kwa upande wa wapiganaji hao na kudhihirisha uwezo wa Kenya kukabiliana na ugaidi.

  • Rais Abdelaziz Bouteflika ajiuzulu

    Rais Abdelaziz Bouteflika ajiuzulu

    Rais wa Algeria, Abdelaziz Bouteflika amejiuzulu wadhifa wake baada ya miaka 20 kufuatia wiki kadhaa za maandamano nchini mwake.

    Bouteflika amekuwa madarakani kama rais kwa muda wa miaka 20 , tayari alikuwa amefutilia mbali mpango wa kugombea muhula mwingine kutawala kutokana na kukuwa kwa upinzani.

    Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na Shirika la Habari la nchi hiyo, kiongozi huyo tayari aliondoa mipango yake ya kusaka awamu ya tano madarakani, wakati upinzani dhidi ya serikali yake ukiongezeka.

    Jeshi la Algeria ambalo lina nguvu, lilimtaka kiongozi huyo mwenye umri wa miaka 82 kutangaza kuwa hana uwezo wa kutekeleza majukumu yake ya uongozi.

    Abdelaziz Bouteflika alikuwa akisumbuliwa na ugonjwa wa Kiharusi, miaka sita iliyopita na tangu hapo mara chache amekuwa akionekana katika sehemu za umma.

    Kujiuzulu kwake kulitangazwa kwa namna gani?

    Rais Abdelaziz Bouteflika,aliweza kutoa taarifa hizo rasmi kwa mujibu wa katiba inayoruhusu rais kusitisha muda wake wa kutawala”

    Uamuzi huo wa Rais Bouteflika ulitangazwa pia na Televisheni ya Taifa ya nchi hiyo.

    Kwa nini amejiuzulu?

    Msukumo wa wananchi kutaka ajiuzulu ulianza kujijenga tangu mwezi Frebruari, na kusitishwa na tangazo la rais Bouteflika baada ya kutangazwa kuwa hatawania tena nafasi ya uraisi.

    Maelfu waliandamana nchini kote tarehe 1 Machi.

    Bouteflika amehaidi kuhudumia kama watateuliwa katika awamu ya tano, pamoja na mabadiliko kwa waziri mkuu ambaye alishinwa kuondoka.

    ” Rais wa Jamhuri Bwana Abdelaziz Bouteflika, ametangaza rasmi uamuzi wake wa kumaliza kazi yake kama Rais wa Jamhuri ya Algeria, katika Baraza la Katiba. Uamuzi huo unaanza mara moja kuanzia leo..”

    Kuondoka madarakani kwa kiongozi huyo pia kumekuja baada ya kiongozi wa maandamano kukataa ahadi iliyotolewa na Rais Bouteflika wiki hii kwamba atajiuzulu madarakani ifikapo Aprili 28.

    Kwa nini maandamano yalikuwa?

    Waandamanaji wengi ambao ni vijina wanadai kuwa wanataka mfumo mpya wa serikali.

    Kuna madai kuwa Bouteflika alikuwa anatumika katika vikundi vya kisiasa , biashara na maafisa wa jeshi,

    Watu wamepokeaje uamuzi wa rais huyo?

    Mamia ya watu wanasheherekea katika mji mkuu wa Algiers, huku wakiwa wanapepea bendera ikiwa ishara ya furaha ya ushindi.

    Selmaoui Seddik moja ya waliojitokeza barabarani kushangilia anasema ingawa amepokea kwa furaha kujiuzulu kwa Rais Bouteflika, serikali nzima inabidi kuondoka madarakani.

    ”… Niko nje kusherehekea kujiuzulu kwa Rais Bouteflika. Tumeondoa kisiki madarakani. Kwa mapenzi ya Mungu, tutakuwa na asilimia mia moja ya demokrasia ya mpito. Hilo ni jambo muhimu. Tunahitaji kuondoa utawala wote madarakani na hili ni jambo gumu.

    Ni vigumu kulifanya kwa amani, lakini nina imani na watu wa Algeria kulifanya jambo hilo kwa amani na tukaelekea katika taasisi za uongozi na sio magenge ya wahuni, kila kitun kitakuwa sawa. Mungu atasaidia”, Selmaoui.

    Abdelaziz Bouteflika ni nani?

    Bouteflika aliingia madarakani mwaka 1999 na kusifiwa kwa kutokomeza vita ya wenyewe kwa wenyewe ambayo ilikadiriwa kuuwa watu zaidi ya 100,000.

    Waandamanaji dhidi ya ongezeko la gharama ya chakula na ukosefu wa ajira mwaka 2011 wakati wa utawala wa kiarabu , rais huyo aliweza kutatua tatizo hilo kwa haraka.

    Mara baada ya kupooza , aliweza kushinda tena uchaguzi licha ya kuwa na upinzani mkali kutoka kwa vyama vya upinzani kwa kudaiwa kuwa afya yake itamfanya ashindwe kutimiza majukumu yake.

    Pamoja na ukosoaji huo bwana Bouteflika bado ana nafasi kubwa ya kushinda mwaka huu.

    Upinzani nchini Algeria umegawanyika na Bouteflika alishinda uchaguzi wa awali wa urais wa mwaka 2014 pamoja na kutofanya kampeni mwenyewe