Author: E-FM CO LTD

  • Kafulila autaka mpango kazi wa kisheria kukamilika mapema

    Kafulila autaka mpango kazi wa kisheria kukamilika mapema

    Katibu Tawala Mkoa wa Songwe, David Kafulila ameutaka mpango kazi wa kuratibu taasisi na mashirika yanayotoa msaada wa kisheria kwa wananchi ukamailike haraka ili wananchi wapate huduma ya usaidizi wa kisheria kwa ufanisi.

    Ameyasema hayo wakati akifungua kikao cha wadau wa msaada wa kisheria kwa Mikoa ya Nyanda za juu Kusini inayojumuisha mikoa ya Njombe, Iringa, Mbeya, Rukwa na Songwe.

    “Watu wengi wamepoteza haki zao kwa kutokujua sheria au kutokuwa na fedha za kumudu gharama za mawakili lakini serikali imetengeneza utaratibu wa kuratibu taasisi ambazo zinatoa msaada wa kisheria bila malipo ili wananchi wengi zaidi wasiojiweza waweze kupata msaada wa kisheria na wasikose haki zao,” amesema Kafulila.

    Amesema kuwa mpango kazi wa kuziratibu taasisi zinazotoa msaada wa kisheria uwe unapimika na hasa uwe na lengo la kutoa elimu kwa wananchi ili wajue kuwa hata kama hawana fedha za kugharimia mawakili wa kuwatetea ili wapate haki zao.

    Naye Msajili wa Mashirika na taasisi zinazotoa Msaada wa Kisheria kutoka Wizara ya Katiba na Sheria, Felista Joseph amesema kuwa elimu kwa umma itapewa kipaumbele katika mpango kazi huo na ni jambo la msingi ili wananchi wafahamu uwepo wa taasisi hizo

    Kwa upande wake Mratibu wa shirika la Gender and Social Reform, Steward Shiwuga amesema shirika lake limekuwa likipata vikwazo katika kutoa msaada wa kisheria bila gharama yoyote na pia baadhi ya watendaji wamekuwa hawatoi ushirikiano kwao.

    Msajili Msaidizi wa Taasisi za Msaada wa kisheria kwa Wilaya ya Ileje, Rodrick Sengela amesema kuwa hapo awali taasisi hizo zilijiendesha bila kuratibiwa pia baadhi ya watu wasio waaminifu walikuwa wakiwarubuni wananchi na kuwatoza fedha nyingi pale wanapohitaji msaada wa kisheria lakini kwa sasa wananchi wataelimisha mahali sahihi pa kupata msaada wa kisheria bila malipo

  • Cardi B amehairisha tamasha kisa upasuaji

    Cardi B amehairisha tamasha kisa upasuaji

    Kutokana na upasuaji wa kuongeza mwili unaojulikana kama (liposuction) alioufanya  rappa Cardi B umesababisha kujitoa kutumbuiza kwenye tamasha la 92Q Spring Bling lilipangwa kufanyika ijumaa hii mjini Maryland.

    Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ rapa Cardi b amejitoa baaada ya kupata tatizo mara tu baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuongea baadhi ya sehemu za mwili wake.

    kwa mujibu wa vyanzo vya karibu vya rapa huyo vimeeleza kuwa kwa sasa yupo kwenye mchakato wa kupona baada ya kufanya pia upasuaji wa maziwa yake.

    Hata hivyo Madaktari wameshauri kuwa Cardi B anahitaji mapumziko ya muda mrefu ili mwili wake urudi kama zamani kutokana na baadhi ya sehemu alizofanyiwa upasuaji kuwa hazijapona vizuri.

    Imeelezwa kuwa Cardi B alifanya upasuaji huo mara tu baada ya kumpata mtoto wake wa kwanza Kulture, May 5,2019

    Aidha Cardi B alisikika akiwaambia mashabiki zake katika tamasha lilofanyika Memphis kuwa alitaka kuahirisha tamasha hilo kwasababu kucheza sana kunaweza kumsababishia matatizo.

     

  • Kundi la IS kuvamia Mashariki mwa DRC

    Kundi la IS kuvamia Mashariki mwa DRC

    Wakuu wa vyombo vya usalama katika kanda ya Maziwa Makuu wanakutana nchini Uganda kupanga mikakati ya kukabiliana na tishio la kundi la Islamic State ambalo linasemekana limeanza kuendesha harakati zake katika maeneo ya Mashariki na Kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.

    Hayo ni kwa mujibu wa upelelezi wa chombo cha usalama kinachowaleta pamoja wakuu wa usalama katika kanda ya maziwa makuu, kuna uwezekano wa eneo hilo kuingiliwa kirahisi na wanamgambo wa kundi hilo kutokana na ukosefu wa usalama na mlipuko wa ugonjwa wa Ebola ambao unatatiza juhudi za kukabiliana nao.

    Vyombo vya usalama katika eneo hilo sasa vinataka kuhakikisha kuwa kundi hilo halipati nafasi kuendesha shughuli zake katika matatifa ya eneo hilo baada ya kutimuliwa mashariki ya kati.

    ”Kuna vitisho kwa hivyo ni onyo kwetu kulishughulika mapema kabla halijawa tatiza kubwa katika kanda ya maziwa makuu” alisema Mkuu wa Jeshi la Uganda, Jenerali David Muhoozi’

    Kulingana na wakuu hao wa usalama kuna haja ya wao kushirikiana na majeshi ya mataifa ya kigeni yaliyochangia katika juhudi za kuvunja kundi hilo mashariki ya kati.

    ”Tishio la kundi hilo la kigaidi ni kubwa kiasi ya kuhamasisha Serikali za eneo hili lote la Maziwa Makuu, kuona ya kwamba zinaongeza juhudi za kukabiliana masuala ya kigaidi iwe ni kutoka kwa kundi la al-Shabab, ISIS, Boko Haram au Al-Qaeda”, alisema katibu mtendaji wa mataifa ya maziwa makuu, Zakaria Mubuli Mwita.

    Aliongeza kuwa wamepokea ripoti kutoka kwa serikali za eneo hilo kwamba kundi la kigaidi la ADF linashirikiana na na makundi hayo ya kigaidi.

    Hivi karibuni kundi la kigaidi la Islamic State lililo na chimbuko lake nchini Iraq, lilidai kufanya mashambulizi katika kijiji cha Kamango mkoani Kivu Kaskazini.

    Maafisa wa kanda hiyo walisema hapakuwa na ushahidi wa IS kuhusika na shambulio hilo japo waliyoshuhudia walilaumu kundi la Allied Democratic Forces (ADF) ambalo wanadai limekuwa likishirikiana na IS.

    Shambulio hilo la mwezi Aprili lilizua taharuki kuhusu hali ya usalama katika Mataifa ya Kanda ya Maziwa Makuu.

    Bw. Zakaria Mwita ambaye ni Katibu Mkuu Mtendaji wa Mataifa ya Maziwa Makuu amesema kuwa wanapania kushirikiana na vikosi vya Umoja wa Mataifa kame vile MONUSC, Serikali na Jeshi la DRC pamoja na nchi zote za Maziwa Makuu ili kuona kuwa wanakabiliana vilivyo na makundi hayo ya kigaidi yasitie fora katika eneo hilo.

    Ingawa maeneo karibu yote ya DRC yamekuwa yakikumbwa na changamoto za usalama kama vita ama kushambuliwa na waasi mara kwa mara, eneo la mashariki ya nchi hiyo ndiyo lililoathirika zaidi.

     

    Usalama mashariki ya DRC

    Akiongea na BBC siku chache kabla ya kuondoka madarakani mwishoni mwa maka 2018, rais mataafu wa nchi hiyo, Joseph Kabila alisema katika mambo ambayo angekuwa na muda zaidi kuyashughulikia ni kurudisha amani kwa taifa hilo.

    Mashariki mwa DRC kuna makundi ya kijeshi ya waasi na ya kikabila.

    Baadhi ya makundi yanaondwa na raia wa nchi hiyo, lakini kuna amakundi mengine makubwa ambayo yanafadhiliwa ama kupambana za serikali za nchi jirani.

    Makundi ya waasi yanayotokea nchi jirani ni FDLR ambalo lilitekeleza mauaji ya kimbari nchini Rwanda mwaka 1994 na wapiganaji wake wakakimbilia DRC.

    Waasi wa ADF wanatokea nchini Uganda.

    Makundi hayo ya waasi yanatumia misitu mizito iliyopo kwenye eneo hilo kujificha na kuendesha shughuli zao huku wakitangaza nia ya kushambulia nchi zao walizozikimbia.

    Uganda na Rwanda zimeshavamia DRC mara mbili kwa lengo la kusambaratisha makundi hayo na vita hizo kupelekea mamilioni ya watu kufariki.

     

     

     

    cc;BBCswahili

  • Serikali haijasema mradi wa Bandari ya Bagamoyo ni hatari

    Serikali haijasema mradi wa Bandari ya Bagamoyo ni hatari

    Mkurugenzi na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas amesema kuwa Serikali inaendelea na majadiliano kuhusu kuendelea na ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo Mkoani Pwani ili kuona kama inaweza kuwa na tija kiuchumi kwa upande wa Tanzania.

    Mkurugenzi na Msemaji Mkuu wa Serikali, Dkt. Hassan Abbas

    Amesema kuwa Serikali ina uwezo wa kujenga bandari nyingi na kwa kuwa Tanzania ina ukanda mkubwa wa ufukwe wa bahari na kwamba bado majadiliano yenye tija kwa Taifa yanaendelea kufanywa baina ya Serikali ya Tanzania na wawekezaji wa mradi huo.

    “Serikali haijasema kuwa Mradi wa Bandari ya Bagamoyo ni hatari, tunaendelea na majadiliano ya utekelezaji wa mradi huo, nchi yetu imejaliwa ukanda mkubwa wa ufukwe wa bahari kwa hiyo tuna uwezo wa kujenga Bandari nyingi tu, hii ya Bagamoyo si kweli kuwa imeachwa kuna mambo ya msingi tunayajadili na tusipofikia maamuzi tutaachana nayo,”amesema Dkt. Abbas

    Aidha, kuhusu uhuru wa habari na kufungia magazeti yasiyofuata sheria za uchapishaji Msemaji huyo wa Serikali amesema kuwa ofisi yake haikurupuki kufungia magazeti, na kusema kuwa ni magazeti matatu tu yalifungiwa kati ya 266 yaliyosajiliwa nchini na kuwataka wamiliki wa magazeti hayo kufuata sheria.

    Hata hivyo, kuhusu malamiko ya wafanyabiashara kwenye maeneo mbalimbali nchini ya kufunga biashara hizo kwa kisingizio cha kodi na tozo mbalimbali, amesema kuwa ni muhimu wakaelewa kwamba kwa sasa Serikali inapita katika kipindi cha mabadiliko na hakuna siku serikali haitadai kodi huku akieleza kuwa kodi nyingi zimepunguzwa hususani kwenye sekta za Kilimo, Mifugo na uvuvi.

    “kwanza tukubali tunapita kwenye kipindi cha mabadiliko, hakuna siku serikali haitadai kodi kwa sababu ndio msingi wa maendeleo ya nchi hii, kuna dhana ilijengeka kuwa unaweza kufanya biashara bila kulipa kodi hiyo sasa haipo, lazima tuangalie changamoto ambazo zinakumba sekta mbalimbali mfano sekta ya kilimo, miufgo na uvubvi kulikuwa na kodi zaidi ya 150, serikali imefuta zaidi ya kodi 80 hadi 100” alisema Dkt Abbas

  • Berahino apatikana na hatia ya kuendesha gari akiwa mlevi

    Berahino apatikana na hatia ya kuendesha gari akiwa mlevi

    Mchezaji soka Saido Berahino amepatikana na hatia ya kuendesha gari huku akiwa amekunywa pombe.

    Mshambuliaji wa Stoke City alikuwa amezidisha takriban mara tatu ya kiwango cha kileo wakati wakati gari lake aina ya Range Rover liliposimamishwa katika eneo la West End jijini London majira ya saa tisa usiku tarehe 18 Februari.

    Mahakama ya Highbury Corner ilisikiliza kesi ya kijana huyo mwenye umri wa miaka 25-ambaye alikamatwa dakika chache baada ya kuibiwa.

    Mahakimu walisema”hakuwa na uoga wa kifo wala wa kujeruhiwa vibaya ” kabla ya kumpiga faini ya £75,000 na kumzuwia kuendesha gari kwa kipindi cha miezi 30.

    mahakama iliambiwa kuwa “hapakuwa na mzozo ” juu ya wizi , ulionaswa na kamera za CCTV, lakini wakili wa Berahino Garry Green alidai kuwa muhimu katika kesi ilikuwa ni “ikiwa mteja ilikuwa ni muhimu kwa mteja kuendesha gari lake au la “.

    Jaji mkuu Mark Oxenham alisema kuwa rafiki wa kike wa Berahino alikuwa meendesha gari hilo kabla na “angeweza kuendelea na safari kutoka kwenye eneo la tukio “.

    Mahakama iliambiwa kuwa mchezaji huyo wa kimataoifa wa Burundi awali alipatikana na hatia ya kuendesha akiwa amelewa mnamo mwaka 2015 na ya kuwa mmiliki wa gari lililoendeshwa na mlevi being mwaka 2012.

    Katika usiku alipokamatwa, polisi waliitwa kutokana na ripoti ya uwezekano wa tukio la kudungwa kisu kwa watu saba nje ya mgahawa wa VQ Cafe, katika mtaa wa Great Russell.

    Berahino,ambaye ni mkaazi wa Old Penkridge Road, Staffordshire alikuwa anaendesha gari ya Range Rover wakati polisi walipolisimamisha katika eneo la Bedford Square.

    Aliulizwa kuhusu mapigano, lakini hakuwa ameona chochote, alisema mwendesha mashtaka Katie Weiss.

    Kamishna wa polisi Stephen Luu alisema kuwa dereva alionekana “muoga” na alikuwa ” alikuwa anapumua hewa yenye harufu ya pombe.

    Berahino alipatikana amekunywa mililita103 za pombe mililita 100 za hewa, iliambiwa mahakama . Kiwango kinachokubalika kisheria ni miligramu 35.

    Aliwaambia polisi kuwa aliibiwa, huku rafiki yake wa kike akisema anaamini rafiki yake wa zamani wa kiume alikuwa amepanga Berahino asha,mbuliwe, iliambiwa mahakama.

    Mahakama iliambiwa kiuwa Berahino kwa sasa hana kipato, kwasababu amesimamishwa kucheza na Stoke bila malipo na ana gharama za malipo ya £20,000 kila mwezi.

    Mzaliwa huyo wa Burundi aloiyejiunga na Stoke kutoka West Brom kwa mkataba wa awali wa £12m mwezi Januari January 2017, anatarajiwa kushiriki katika michuano ya Kombe la Mataifa barani Afrika linaloanza mwezi Juni.

    “Nilikuwa naogopa . nilikuwa tu ndio nimeshambuliwa na mpwa wangu alikuwepo pale na nilipaswa kuchukua hatua. ilinibidi niendeshe haraka kutoka eneo la tukio ,”alisema.

    “Walikuwa na kisu na bunduki pia .”

    Alisema hakuwaarifu polisi mara moja juu ya wizi baada ya kuitwa .

    “Siku za nyuma nimekuwa katika vyombo vya habari na sikutaka lolote litangazwe kunihusu ,” alisema.

    “Ineharibu taaluma yangu nilikuwa naogopa hilo.

    “Hicho hi kitu ambacho sikukitaka kabisa.”

  • marufuku ya vipodozi vinavyobadili rangi ya mwili

    marufuku ya vipodozi vinavyobadili rangi ya mwili

    Bunge la Afrika Mashariki (EALA) limepitisha azimio linalotoa wito wa kuwekwa kwa marufuku dhidi ya watengenezaji na waagizaji wa bidhaa zenye kemikali ya hydroquinone.

    Bidhaa hizo ni pamoja na sabuni, mafuta na urembo wenye kemikali ya hydroquinone inayobadilisha ngozi kuwa nyeupe.

    Hydroquinone ni kemikali inayopatikana katika aina mbali mbali za bidhaa mbali mbali za mwili ambayo kwa kawaida imetengenezwa kwa ajili ya kuifanya ngozi kuwa nyeupe.

    “Athari za vipodozi vyenye hydroquinone zinaonekanana zimesambaa katika jumuiya nzima ya Afrika mashariki ,” alisema Gideon Gatpan, mwanasheria kutoka Sudan Kusini.

    Chini ya kipengele 81(2) cha mkataba ulioanzishwa na Jumuiya ya Afrika Mashrariki ,unaotambua umuhimu wa nchi wanachama katika kuweka viwango, na vipimo, wabunge wamependekeza Baraza la Mawaziri liundwe kwa ajili ya kuchunguza aina za kemikali zilizopo ndani yabidhaa za urembo kama moja ya viwango vya lazima katika kanda ya Afrika Mashariki.

    “Baadhi ya bidhaa hizi huwa zina hadi 6% ya kemikali ya hydroquinone,”alisema mbunge kutoka Uganda Suzan Nakawuki.

    Jane Ndagire alitumia mafuta yanayochubua mwili kwenye uso wake kwa miaka kadhaa

    Kenya na Rwanda, sawa na Afrika Kusini , Ghana na Ivory Coast , zimekwishaweka hatua za sheria za udhibiti au marufuku ya uagizwaji wa bidhaa zenye kemikali ya hydroquinone.

    Wataalamu wa masuala ya ngozi wanasema Kemikali ya hydroquinone inaweza kusababisha muwasho wa ngozi, mzio wa ngozi, kuchubuka kwa ngozi na kusababisha mabaka meusi na meupe na hata saratani ya ngozi.

    Namna hydroquinone inavyobadili ngozi:

    • Katika ngozi ya mwanadamu kuna chembechembe ambazo huitwa melanin.
    • Kemikali ya Hydroquinone inakwenda kuzuia utengenezaji wa melanin.
    • kwenye mwili wako hivyo ngozi kupoteza rangi yake ya asili na ulinzi kutokana na miale ya jua yenye madhara Kazi ya chembe chembe hizi ni kuipa Rangi ngozi yako na kuilinda kutokana ni miale ya jua yenye madhara.
    • Kemikali ya Hydroquinone inakwenda kuzuia utengenezaji wa melanin kwenye mwili wako hivyo ngozi kupoteza Rangi yake ya asili na ulinzi kutokana na miale ya jua yenye madhara.
  • Mfalme  amgeuza mlinzi  kuwa  Malkia wake

    Mfalme amgeuza mlinzi kuwa Malkia wake

    Mfalme wa Thailand amemuoa Naibu mkuu wa kikosi cha walinzi wake , na kumpa cheo cha malkia, imesema taarifa ya ufalme huo.

    Tangazo hilo la kushitukiza limetolewa huku sherehe za kutawazwa kwake zikitarajiwa kuanza Jumamosi, wakati atakapochukua wadhfa wake.

    Mfalme Maha Vajiralongkorn, mwenye umri wa miaka 66, alikuwa mfalme kikatiba baada ya kifo cha baba yake aliyependwa sana kilichotokea mwaka 2016.

    Amekwisha wataliki wanawake mara tatu na ana watoto saba.

    Ufalme ulisema kuwa: Mfalme Vajiralongkorn “ameamua kumpandisha cheo Generali Suthida Vajiralongkorn Na Ayudhya, na kuwa Malkia Suthida na atakuwa na cheo cha kifalme na hadhi kama sehemu ya sfamilia ya kifalme”.

    Malkia Suthida ni mpenzi wa muda mrefu wa Mfalme Vajiralongkorn na amekuwa akionekana hadharani pamoja nae kw amiaka mingi, ingawa mahusiano yao haukuwahi kukubalika rasmi.

    Picha kutoka kutoka katika sherehe za harusi zilionyeshwa moja kwa moja kwenye vituo vya televisheni vya Thailand Jumatano, ambapo watu wa wengine wa familia ya ufalme na washauri wa ufalme walihudhuria.

    Mfalme alionekana akimwagia maji ya baraka Malkia Queen Suthida kichwani. Baadae wawiloi hao walisaini cheti cha ndoa.

    Mnamo mwaka 2014 Vajiralongkorn alimteua Suthida Tidjai, ambaye ni mhudumu wa zamani wa Thai Airways,kama naibu kamanda wa kikosi cha walinzi wake. Alimpandisha cheo na kuwa Generali kamili jeshini Disemba 2016.

    Mfalme aliyetangulia Bhumibol Adulyadej, alitawala kwa miaka 70 na kuwa ndiye mfalme aliyetawala kwa muda mrefu zaidi duniani na alifariki dunia mwaka 2016

  • Maisha ya wengi yako hatarini kutokana na maafa ya kimbunga

    Maisha ya wengi yako hatarini kutokana na maafa ya kimbunga

    Msumbiji inahitaji misaada ya haraka kuokoa maisha ya walioathirika na kimbunga Kenneth, shirika la msaada limesema.

    Huku shirika la ‘Save the Children’ limesema hali waliokuwa nayo watu wa Msumbiji inatishia usalama wa maisha yao hivyo ni muhimu misaada zaidi itolewe.

    Umoja wa mataifa umetoa kiasi cha fedha cha dola milioni 13 ili ziweze kuwasaidia wahanga wa kimbunga wa Msumbiji na Comoro kwa ajili ya chakula, maji na kurekebisha miundo mbinu.

    Idadi ya vifo vilivyosababishwa na kimbunga , magharibi mwa Msumbiji vimefika 38 na vifo vingine vinatarajiwa kutokea, utawala umebainisha.

    Kwa sasa wafanyakazi wa mashirika ya msaada yanahangaika kufika katika maeneo ambayo yameathirika zaidi na kimbunga.

    Mvua kubwa ilipiga kusini mwa Afrika mwishoni mwa wiki iliyoambatana na upepo mkali uliovuma kwa kilomita 220 kwa saa, na kusababisha zaidi ya maelfu ya makazi ya watu kuharibika.

    Kwa sasa mvua si kubwa sana ingawa bado inaendelea kunyesha.

    Mamlaka ya hali ya hewa inatabiri kuwa mvua hizi zitapiga mara mbili kama ilivyotokea kwenye kimbunga cha Idai ambacho kilitokea mwezi uliopita na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 900 katika maeneo ya kusini mwa Msumbiji, Malawi na Zimbabwe.

    Afisa wa masuala ya misaada kwa binadamu kutoka Umoja wa mataifa anasema hatari za mafuriko ambayo yamesababishwa na kimbunga Kenneth zinatarajia kuendelea mpaka mwishoni mwa msimu wa mvua ambapo kiwango cha maji kwenye mito kitakuwa juu.

    Tayari mji wa Pemba na Cabo Delgado umeathirika na mvua kubwa na mafuriko.

    Kipi kipya?

    Wafanyakazi wa shirika la msaada wanajaribu kupeleka dawa na kusambaza chakula kabla mvua nyingine kubwa haijaja.

    Kwa mujibu wa taarifa kutoka kitengo cha taifa cha kukabiliana na majanga nchini humo, wamesema watu 38 wamefariki kutokana na kimbunga Keneth huku makazi 35,000 yameharibiwa na mvua.

    Mtandao wa kujitegemea wa ‘O Pais’ umeripiti kuwa watu wengine watano wamefariki baada ya nyumba za Pemba kuanguka siku ya jumapili ingawa bado serikali haijathibitisha idadi ya vifo hivyo.

    Watu laki mbili wapo hatarini Pemba peke yake, Ocha ilitoa angalizo.

    Lakini kufika katika maeneo hayo hatari imekuwa kazi ngumu kwa wasaidizi kufanikiwa kufikia.

    “Tumefanikiwa kutuma ndege moja kwa msaada wa shirika la chakula duniani ili kusambaza mchele na biskuti na vitu vingine ambavyo sio vyakula,

    Lakini hali ya hewa imekuwa ikibadilika haraka sana na kuathiri operesheni hiyo ya kutoa misaada. Mvua zinaendelea kunyesha na walishindwa kutuma ndege nyingine”, Bwana Abreu aliiambia AFP

    Kimbunga cha kitropiki huwa inatokea katika sehemu ya bahari ya hindi na huwa nadra kutokea.

    Hata hivyo kwa mujibu wa mwandishi wa mazingira wa BBC ,Matt McGrath,Kimbunga Idai kilikuwa cha saba kupiga katika bahari hindi msimu ambao kilikuwa kimepiga mwezi achi.

    Hii ni zaidi ya mara mbili ya kiwango cha kawaida kwa mwaka.

    Kitu ambacho sio cha kawaida, licha ya kuwa kimbunga Idai na Kenneth vimepiga kwa mfululizo.

    Kwa mujibu wa mamlaka ya hali ya hewa duniani imesema, kimbunga hiki kilichotokea Msumbiji kimevunja rekodi kwa sababu haijawahi kutokea kupiga mara mbili katika msimu mmoja.

    Si hali ya kawaida kimbunga kuonekana katika maeneo haya na vilipungua kutokea yapata miongo saba iliyopita.

    Lakini ni mapema sana au ni mfano mdogo kusema kuwa mabadiliko ya tabia nchi ndio yamesababisha mabadiliko haya.

    Wataalamu wameainisha kuwa dhoruba hii inahusishwa na mabadiliko ya tabia nchi.

    cc;BBSswahili

     

  • ‘Hali ni mbaya kuliko ilivyodhaniwa’ Msumbiji

    ‘Hali ni mbaya kuliko ilivyodhaniwa’ Msumbiji

    Hali kaskazini mwa Msumbiji ni mbaya kuliko ilivyodhaniwa, msemaji wa Umoja wa mataifa ameeleza, siku chache baada ya kimbunga Kenneth kutuwa nchini humo.

     

    Kimbunga hicho kilituwa siku ya Alhamisi kwa upepo mkali wenye kasi ya 220km/h (140mph) kilichoviangamiza vijiji.

    Takriban watu 700,000 sasa wanadhaniwa kuwa katika hatari katika eneo hilo wakati mvua kubwa ikiendelea kunyesha.

    Pemba, mji mkubwa wa jimbo la Cabo Delgado kumeshuhudiwa mvua yenye kina cha mita mbili na mafuriko.

    Msemaji katika ofisi ya uratibu wa masuala ya kibinaadamu (Ocha) Saviano Abreu ameeleza kwamba hali ni mbaya katika miji ya Macomia na Quissanga, akiongeza kwamba kuna wasiwasi pia kwa kisiwa kisichoweza kufikiwa cha Ibo.

    Mawimbi ya hadi mita 4 yanatarajiwa, na mashirika ya misaada yanahofia kwamba mvua itazidi kunyesha.

    “Tuna wasiwasi mkubwa kwasababu, kwa mujibu wa utabiri wa hali ya hewa, mvua nzito inatarajiwa kunyesha katika siku nne zijazo,” Deborah Nguyen, msemaji wa shirika la mpango wa chakula la Umoja wa mataifa , alieliambia shirika la habari la AFP.

    “Tunatarajia mvua iwe na ukubwa wa mara mbili zaidi ya ilioshuhudiwa wakati wa kimbunga Idai,” ameongeza.

    Kimbunga Idai kilisababisha vifo vya watu 900 katika nchi tatu mnamo Machi mwaka huu.

    Ni yapi yanayojiri?

    Inadhaniwa kwamba watu 400,000 wanaishi Pemba , na mvua kubwa imesababisha watu wengi kuwa katika hatari.

    Kuna wasiwasi unaotokana na maporomoko ya ardhi katika mtaa wa Mahate mjini humo, maafisa wa Ocha katika eneo hilo wanasema, na katika mtaa wa Natite, nyumba zimeanza kuporomoka.

    Shirika la mpango wa chakula duniani linaarifiwa kuanza kutoa misaada kwa watu waliokwama, lakini barabara zilizoharibika zimesababisha shughuli zisitishwe katika maeneo yaliotengwa sana.

    Takriban watu watano wamefariki kutokana na kimbunga hicho na takriban nyumba 35000 zimeharibika vibaya au kubomoka kabisa, maafisa wa kitaifa wanasema.

    Mashirika ya Umoja wa mataifa yanasaidia maafisa wa serikali na bwana Guterres ametoa wito wa “rasilmali za ziada” kutoka jumuiya ya kimataifa “kufadhili usaidizi wa sasa, wa siku zijazo na wa kipindi kirefu zaidi”.

    Eneo lililoathirika liko vipi?

    Jimbo la Cabo Delgado halina watu wengi kama eneo lililoathirika na kimbunga Idai na inavyoonekana sehemu kubwa iko katika ardhi ya juu.

    Hilo kwa pamoja na tahadhari za mapema kutoka kwa maafisa husika kabla ya kutokea kimbunga hicho huenda ikasaidia kuzuia hasara ikilinganishwa na wakati wa kimbunga Idai.

    Lakini taarifa zinasema maelfu ya makaazi yameharibiwa kutokana na upepo mkali, na ene hilo limekabiliwa na mashambulio ya wanamgambo wenye itikadi kali za dini ya kiislamu katika miezi ya hivi karibuni, jambo ambalo linaonekana huenda likatatiza utoaji wa msaada.

    Tayari maelfu ya watu walikuwa wametoroka makaazi yao kutokana na ghasia kutafuta hifadhi katika kambi za kuwahifadhi watu walioachwa bila ya makaazi.

  • Mnyeti awaonya wanasiasa, ‘Nitawashughulikia ipasavyo’

    Mnyeti awaonya wanasiasa, ‘Nitawashughulikia ipasavyo’

    Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Alexander Mnyeti amewashukia vikali wanasiasa nane wa Kata ya Kitwai Wilayani Simanjiro wanaorudisha nyuma maendeleo kwa kukataza wanafunzi wasisome kwenye madarasa ya shule ya msingi Kitwai B yaliyojengwa na mdau wa maendeleo hivyo kuyasusia.
     
    Ametoa onyo hilo mkoani humo wakati akizindua madarasa matatu mapya ya shule hiyo, ambapo amesema kuwa wanasiasa hao atawachukulia hatua kali wanaoshawishi wananchi kususia maendeleo.
     
    Amesema kuwa hatakubali kuona watu wachache wanaopinga maendeleo, hivyo serikali itamuunga mkono mdau huyo wa maendeleo, Sanare Mollel ambaye pia ana mpango wa kumalizia majengo ya Zahanati ya kijiji hicho.
     
    “Wanasiasa hao wanampinga mdau huyo kwa sababu ni mfugaji mkubwa ambaye amefuata taratibu na kanuni zote za kuingia ndani ya kijiji hicho lakini hajavunja sheria kwani Mtanzania anaruhusiwa kuishi popote,”amesema Mnyeti.
     
    Aidha, amesema kuwa haiwezekani mdau wa maendeleo ajitolee kujenga madarasa matatu kisha baadhi ya wanasiasa wanawaambia wananchi wasisomeshe watoto katika shule hiyo.
     
    Kwa upande wake Diwani wa kata hiyo, Nyika Shawishi amesema kuwa wapinzani wake wa kisiasa ndiyo wanaosababisha hali hiyo kwani wanaona maendeleo yakifanyika sifa zitakuwa kwake.
     
    Naye ofisa elimu ya msingi wa halmashauri ya wilaya ya Simanjiro, Silvanus Tairo amesema kuwa shule hiyo imegharimu sh. 47.3 milioni ambapo mdau wa maendeleo alijitolea sh30 milioni na nguvu za wananchi zimegharimu sh.12.3 milioni.
  • Msichana kiziwe aliyesikia sauti yake baada ya upasuaji wa ubongo

    Msichana kiziwe aliyesikia sauti yake baada ya upasuaji wa ubongo

    Msichana mwenye umri wa miaka saba Leia Armitage amekuwa akiishi katika maisha ya ukimya kutokana na kutosikia katika kipindi cha miaka miwili ya mwanzo ya masha yake , lakini upasuaji wa hivi karibuni wa ubongo na tiba vimeweza kubadili maisha yake na sasa anaweza kusikia sauti zake na hatimae anaweza kusikia sauti za wazazi wake na kuwambia kuwa anawapenda.

    “Tuliamboiwa kuwa unaweza kuweka bomu nyuma yake na asingeliweza kabiza kusikia sauti ya mlipuko wake ,” amesema baba yake Leia , Bob, huku akikumbuka namna walivyobaini kuwa mtoto wao mchanga wa kike alikuwa na aina ya nadra kabisa ya ulemavu wa kutosikia.

    Leia, ambaye anatoka katik eneo la Dagenham mashariki mwa London, hakuwa na sikio la ndani au mshipa wa kusikia, hii ikimaanisha kuwa mtambo wa kawaida wa kusaidia mlemavu wa kutosikia wala ule wa kupandikiziwa visingemsaidia lolote.

    Matokeo yake, hakutarajiwa kuzungumza- licha ya hatari hizo, wazazi wake walimpigania ili awe mmoja wa watoto wa kwanza nchini Uingereza kupewa kifaa kinachopandikizwa ndani ya ubongo kwa njia ya upasuaji mgumu alipokuw ana umri wa miaka miwili.

    Taasisi ya upasuaji huo ya nchini Uingereza NHS imeutaja kama “halisi uliobadilisha maisha ” na imesema kuwa itadhamini kifedha utapandikizaji huo kwa watoto wengine wasioweza kusikia wenye hali kama yake.

    Inakadiriwa kuwa watoto wapatao 15 kila mwaka watakiuwa wanachunguzwa kwa ajili ya kufanyikwa upasuaji huo na tisa miongoni mwao watakuwa wanajfanyiwa upasuaji huo

    Anasikia honi za magari

    Bob anasema kuchagua aina hii ya upasuaji wa wa ubongo ulikuwa ni uamuzi mkubwa kwao, lakini ”tulitaka Leia apate fursa hii muhimu maishani mwake “.

    yeye na mkewe Alison walitumai kwamba baada ya upasuaji katika hospitali ya wakfu wa Guy’s and St Thomas’ NHS ,ataweza kusikia kama vile honi za magari wakati atakapokuwa akivuka barabara ili kumfanya awe salama katika dunia hii.

    Hata hivyo katika kipindi cha miaka mitano baada ya upasuaji, mafanikio ni makubwa zaidi kuliko walivyotarajia .

    lianza polepole, Leia alipoanza kugeuza kichwa chake akisikia sauti ya mlango wa treni inapofungwa baada ya kufanyiwa upasuaji .

    Hatimae, alianza kuelewa dhana ya sauti huku wazazi wake wakiendelea kurudia rudia maneno, wakimtaka aigize sauti.

    Sasa baada ya matamshi mengi na tiba ya lugha, anaweza kutunga sentensi na kuizungumza ,akijaribu kuimba muziki unapopigwa na kusikia sauti kwenye simu

    “Tunaweza kumuita kwenye vyiumba vya juu tukiwa vyumba vya chini na akatusikia ,” Alieleza baba yake Bob.

    Nakupenda

    Lakini ilikuwa ni katika shule , katika darasa la watoto wanaosikia, ambapo Leia anafanya vizuri zaidi, hii ni kutokana na usaidizi wa kutumia alama za lugha na kumpatia muda wa kiujifunza nae peke yakei

    ” Anaendelea vizuri zaidi na zaidina hayuko nyuma sana ya wenzake wa umri wake kwa mambo mengi ,”anasema Bob

    Nyumbani, anapotumia sauti yake ndio jambo linalowaridhisha zaidi wazazi wake zaidi.

    “‘Nakupenda baba’ huenda ni kitu kizuri zaidi nilichowahi kusikia akisema ,” anasema Bob

    “Ninapomuweka kiytandani sasa anasema ‘usiku mwema mama’, maneno ambayo hatukutarajia kuyasikia kutoka kwake ,” Alison anasema.

    Upasuaji huo hufanyika kwa kuweka kifaa moja kwa moja kwenye ubongo kinachosaidia kuamsha njia za usikivu miongoni mwa watoto wanaozaliwabiola neva za kusikia.

    Kitengo cha kupaza sauti na utambuzi wake hufahamisha sehemu nyingine ya kichwa na baadae husafirisha sauti hadi kwenye kifaa na hivyo kumuwezesha mtumiaji kusikia.

    Uchochezi huu wa nkielektroniki unaweza kutoa hisia , lakini hauwezi kurejesha usikivu wa kawaida.

    Hata hivyo Profesa Dan Jiang, daktari wa masikio na Mkurugenzi wa kituo cha upandikizaji wa tiba katika kiliniki ya wakfu wa Guy’s and St Thomas anadsema baadhi ya watoto wanaweza kukuwa kwa kiwango cha matamshi.

    “Matokeo ni tofauti. Baadhi watafanya vema kuliko wengine ,” alisema.

    “Lazima wajifunze na watoto wadogo hufanya vizuri kwa hiyo tunapenda kuwawekea watoto vifaa vya kusikia mapema iwezekanavyo .”

    Watoto walio chini ya umei wa miaka mitano wako katika nafasi nzuri ya kujifunza kitu kipyana kupona kwa matibabu , alisema.

    Susan Daniels, Mkurugenzi mkuu wa Taasisi ya taifa ya watoto wasio sikia lisema: “Kila mtoto asiyesikia ni tofauti , na kwa baadhi teknolojia kama ya kifaa cha kushitua ubongo inaweza kuwafaa na kuleta tofauti kubwa katika maisha yao”.

    “Kwa usaidizi unaofaa, watoto wasiosikia wanaweza kusikia kama watoto wenzao wasio na ulemavu huu na uwekezaji huu ni hatua nyingine ya kuhakikisha kuwa watoto wasio sikia hawaachwi nyuma katika jamii” amesema Susan Daniels

    cc;BBCswahili