Category: Global News

  • Ugonjwa wa Virusi vya corona Kuvuruga utaratibu wa chanjo kwa watoto .

    Ugonjwa wa Virusi vya corona Kuvuruga utaratibu wa chanjo kwa watoto .

    Mamilioni ya watoto wanaweza kupoteza maisha kutokana na maradhi yanayoweza kuzulika kwa sababu ya kukatizwa kwa programu za chanjo kutokana na virusi vya corona ambapo wataalam wametahadharisha.

    Shirika la Afya duniani limeshauri nchi nyingi kusitisha chanjo ili kusaidia kudhibiti kuenea kwa virusi vya corona ambapo takribani nchi 68 zimeathirika na  baadhi zikisitisha kabisa kampeni za chanjo.

    Lakini sasa makundi kadhaa ya wataalamu wanaona kuwa kutakuwa na madhara ya muda mrefu kutokana na hali hii Mfuko wa Umoja wa Mataifa unaoshughulikia watoto (Unicef), Taasisi ya chanjo, Sabin na Shirika la Chanjo la Gavi pia yameonesha wasiwasi kuwa maelfu ya watoto watapoteza maisha kwa sababu zinazoweza kuzuilika.

    Wahudumu wa afya wakielekeza nguvu yao kuhudumia matatizo mengine kama kupata vifaa vya chanjo hospitalini Lakini Polio, ambayo inaweza kusababisha kupooza au hata kifo, pia inarejea- wagonjwa wanne wapya wa polio wameripotiwa tangu mwezi Februari.

  • Maandamano yaendelea usiku kucha Marekani kufuatia kifo cha George Floyd

    Maandamano yaendelea usiku kucha Marekani kufuatia kifo cha George Floyd

    Kimataifa

    Maandamano juu ya kifo cha raia mweusi wa Marekani George Floyd bado yanaendelea kwa usiku wa nane mfululizo.

    Kifo cha Floyd kilichotokea Mei 25, mikononi mwa polisi huko Minneapolis kimesababisha maandamano makubwa katika maeneo mbalimbali nchini huko.

    Waandamanaji wameamua kukiuka hatua ya kusalia ndani iliyowekwa katika miji mbalimbali.

    Katika eneo la Fort Worth, Texas, inasemekana kundi dogo la watu lilisalia nje hata baada ya kuanza kwa muda wa kutoka nje saa mbili usiku.

    Waandamanaji katika mji wa New York pia nao walikiuka hatua ya kutoka nje iliyowekwa kuanzia saa mbili usiku.

    Meya wa mji alisongeza mbele muda huo kwa usiku wa pili mfululizo baada ya waandamanaji kupora eneo la kibiashara la Manhattan Jumatatu.

  • Waafrika wenye rangi nyeusi huwa na wakati mgumu pale wanapohitaji tiba ya dawa

    Waafrika wenye rangi nyeusi huwa na wakati mgumu pale wanapohitaji tiba ya dawa

    Waafrika wenye rangi nyeusi huwa na wakati mgumu pale wanapohitaji tiba ya dawa kwa sababu wanawakilisha asilimia mbili tu ya sampuli ya vina saba iliyotumika na utafiti wa kutengeneza dawa, lakini kampuni mpya ya Nigeria inataka kubadili mumo huo.

    Uhaba wa tafiti kuhusu watu wa aina fulani unahatarisha kuenea kwa magonjwa duniani kote.

    Kwa mujibu wa muasisi na mkurugenzi wa kampuni inayoangazia biolojia ya vina saba ‘ 54gene’ , Dkt. Ene-Obong, watu wenye rangi nyeusi wako na utofauti wa kimaumbile ofauti na watu wengine duniani , na kutengeneza taarifa zao za vina saba kuna uhitaji wa raslimali kubwa zaidi kupatikana.

    Amefanya utafiti wa vinasaba katika maabara ya nchini Nigeria katika mji wa Lagos , ambapo timu yake ina mpango wa kufanyia utafiti vinasaba 4000 vya sampuli zitakazokusanywa kwa mwaka 2019, kwa malengo ya kuwafikia watu laki moja ifikapo miezi 12 ijayo.

    Abasi Ene-Obong ameiongoza timu ya utafiti wa dawa ambazo zinaweza kutumika duniani kote

    Dkt. Ene-Obong anasema kuwa ufahamu wa jukumu la vina saba katika magonjwa litasaidia katika uhusiano wa tiba .

    “Dawa hazitengenezwi hata kwa kuwafikiria kuwa kuna waafrika wapo, idadi ya waafrika haifanyiwi majaribio ya kitabibu kulingana na mahitaji yao , kile kilichopo ni dawa ambazo hazina uwezo wa kutibu kiufanisi ,” alisema.

    Dawa mpya pia inachukua muda mrefu kufika Afrika – mara nyingine ni kati ya miaka 15 mpaka 20 , alisema Dkt. Ene-Obong.

    Watengenezaji wakubwa wa dawa huwa wanaangalia soko la mataifa ya magharibi, na aina ya vina saba vinavyopatikana barani Afrika baada ya makampuni hayo kupoteza wagonjwa wao.

    Dkt Ene-Obong anasema kwamba anadhamiria kutatua tatizo hili kwa kuongeza upatikanaji wa takwimu za vina saba kutoka Afrika ili kuhamasisha utafiti wa kisayansi kufanyika zaidi kwa kuwaangazia watu hao.

    “Mpango huo utatoa mwanya wa upatikanaji wa matokea ambayo yatawafanya waafrika wapate tiba kulingana nao lakini pia tiba ya kila mmoja ipatikane,” alisema.

    Kampuni yake ina mpango wa kufanyia utafiti magonjwa kama ya selimundu(sickle cell), ugonjwa ambao unawaathiri waafrika zaidi.

    Licha ya kuwa Dkt. Ene-Obong anasema kuwa ’54gene’ itaweza kubainisha namna ambavyo jenetiki inafanya kazi katika magonjwa ya muda mrefu na yasioambukiza kama saratani ,shinikizo la damu, ugonjwa wa kupoteza kumbukukumbu na mengineyo.

    Kwa sasa wameanza katika hospitali za Nigeria ili kukusanya sampuli za DNA.

    “Hatutaingilia huduma ambayo wagonjwa wanapata, lakini kwa ruhusa yao tutawaomba kupata damu au tishu za mwilini kwa ajili ya utafiti, alisema Dkt. Ene-Obong .

    Vilevile amesema kampuni haina nia ya kuhifadhi tu lakini kuboresha huduma ya afya katika jamii inazozifanyia kazi.

    Kampuni hiyo ilipokea ufadhili wa dola milioni 4.5 kutoka kwa wafadhili wakati ilipozindua mradi huo mwezi januari.

    Fedha nyingi zilitumika kuongeza maabara zilizopo mjini Lagos, kukodisha wafanyakazi na kutengeneza mfumo wa kusambaza umeme kwa sababu Nigeria inakabiliwa na tatizo kubwa la kukatika umeme.

    Presentational white space

    Dkt. Ene-Obong aliacha kazi yake ya ushauri wa viongozi wa sekta ya dawa na kuanzisha kampuni yake ya 54gene, ambayo sasa imeweza kutengeza watafiti zaidi ya 30 ambao wamefanya kazi katika taasisi za tiba nchini Marekani na Uingereza.

    Lengo letu ni kuhakikisha kuwa watu wanatibiwa kiwango kisichokua na utofauti na Marekani au Uingereza.

    Jina la kampuni hiyo imetokana na majina ya nchi 54 za Afrika .

    “Hatutakikuwa kampuni ya wanaijeria peke yake bali tuko na mazungumzo na nchi za Afrika mashariki, magharibi na kusini mwa Afrika”.

    Ingawa alikuwa na hofu kuhusu miongozo iliyopo katika baadhi ya mataifa ya Afrika na kutokuepo na utayari.

    “Tunafuatilia sheria muhimu za kuzifuata katika nchi husika ,kwa sababu baadhi ya nchi miongozo haiko wazi.Hivyo lazima kujiandaa kufuata sheria husika na kufuata utaratibu wa taifa husika.”

    Kampuni hiyo itatunza taarifa iliyozipata kwa kufuata utaratibu.

    Kuna baadhi ya serikali za Afrika kama Kenya na Uganda,mamlaka imependekeza kuwa wakusanye taarifa za vina saba ambazo zitasaidia kupambana na uhalifu

    Lakini Dk Ene anasema kuwa kampuni yake haina nia ya kuzigawa taarifa wanazozitafuta ingawa kampuni hiyo iko radhi kutoa picha kubwa ya takwimu ili serikali kuweza kuelewa hali ya afya ya watu.

     

     

     

    cc;BBCswahili

  • Japan yazindua kifaa maalum cha kuwatambua wanyanyasaji wa kingono

    Japan yazindua kifaa maalum cha kuwatambua wanyanyasaji wa kingono

    Kifaa kilicho na muhuri maalum wa kuwatambua wanyanyasaji wa kingono katika magari ya usafiri wa umma kimezinduliwa nchini Japan.

    Kifaa hicho kinamfahamisha muathiriwa kuwa kuna mtu anampapasa na kuwawekea alama ya wino ambayo hauonekani.

    Watu wanaweza kuwatambua wanyanayasaji wa kingono waliowekwa alama hiyo kwa kutumia taa nyeusi kuwabaini.

    Wasafiri wakiwa ndani treni

    Shirika la kiteknolojia lililobuni kifaa hicho linasema kiitasaidia kukabiliana na uhalifu wa kingono.

    Hata hivyo shirika moja lisilokuwa na kiserikali linanahofia kifaa hicho kinaweza kutumika vibaya na watu wenye chuki dhidi ya watu fulani.

    Kampuni Japani linalofahamika kama hachihata linasema liliamua kutengeza muhuri huo ili kuwadhibiti watu wanaowanyanyasa kingono abiria katika vituo vya treni.

    Kampuni hiyo ilitangaza wazo la kubuni muhuri huo mara ya kwanza mwezi wa tano baada ya video inayowaonesha wasichana wawili wa Japan wakimkimbiza mshukiwa wa unyanyasaji wa kingono katika kituo cha usafiri wa treni iliyosambazwa katika mitandao ya kijamii kupata umaarufu.

    Msemaji wa kapuni ya Shachihata aliandika katika mtandao wake wa Twitter kuwa kifaa hicho”ni hatua moja kuelekea ulimwengu usiokuwa na uhalifu wa kingono”.

    Wasafiri wakiingia ndani treni mjini Tokyo

    Lakini msemaji wa kitengo ckinachoshughulikia masuala ya ubakaji England na Wales ameiambia BBC huenda kifaa hicho kikatumiwa kibiasha na kufanya kuwa rasmi masuala ya ubakaji na unyanyasaji wa kingono na kuwaeka hatarini wale wanaomiliki kifaa hicho.

    “Japo waliobuni kifaa hicho wamekitengeza kwa nia njema nahofia pia kunawatu watakaotumia kujifaidi- kutokana na waathiriwa wa ubakaji’,” anasema Katie Russell.

    Hii ndiyo hatua ya hivi karibuni zaidi kufikiwa katika majaribio ya kukabiliana na visa vya upapasaji nchini humo, ikiwa ni miezi michache tu baada ya kuzinduliwa kwa programu inayojulikana kama Digi Police, inayolinda waathirika dhidi ya visa vya unyanyasaji katika maeneo yenye msongamano wa watu.

    Kifaa hicho kinawafahamisha abiria wengine kwamba wako hatarini kwa kuonyesha ujumbe unaosema: “Kuna mtu anayepapasa watu hapa. Tafadhali nisaidie.” Kamera za kukabiliana na visa vya upapasaji ziliwekwa kwenye treni za jiji la Tokyo mwaka 2009 kusaidia kukabiliana na malalamiko ya unyanyasaji wa kingono.

    Zaidi ya watu 6,000 walikamatwa kwa kushukiwa kutekeleza vitendo hivyo mwaka huohuo.

    Harakati zinazoendeshwa na vuguvugu la #MeToo bado hazijafanikiwa nchini Japani ambayo inaorodheshwa kuwa nambari 110 katika nchini 149 kwenye suala la usawa wa kijinsia katika kipimo cha Kongamano la Kiuchumi Duniani.

     

     

     

    cc:BBCswahili

  • Vita vya wenyewe kwa wenyewe Syria: ‘Watu watatu’ wauawa katika shambulio la msafara wa magari ya kijeshi ya Uturuki

    Vita vya wenyewe kwa wenyewe Syria: ‘Watu watatu’ wauawa katika shambulio la msafara wa magari ya kijeshi ya Uturuki

    Shambulio la angani la serikali ya Syria uliolenga msafara wa kijeshi wa Uturuki uliokuwa ukielekea katika eneo linalotawaliwa na waasi kaskazini mwa Syria limesababisha vifo vya raia watatu, Uturuki imedai.

    Watu wengine 12 walijeruhiwa katika shambulio hilo katika mkoa wa Idlib siku ya Jumatatu kulingana na wizara ya ulinzi ya Uturuki.

    Idlib ambayo ni mojawapo ya maeneo machache yasiodhibitiwa na serikali, ilitarajiwa kulindwa na kuwa eneo huru linalotenganisha majeshi pinzani lililoafikiwa na Uturuki inayowaunga mkono waasi mwaka uliopita.

    Lakini mashambulizi ya serikali yamekuwa yakiongezeka tangu mwezi Aprili.

    Mamia ya raia wameuawa kutokana na hilo na kuna hofu kwamba wengi watafariki iwapo hali itaendelea kuwa mbaya.

    ”Hii ndio hatari inayotukabili kwa sasa”, alisema Jan Egeland kutoka baraza la wakimbizi la Norway akizungumza na BBC.

    Kwa miaka kadhaa sasa tumeonya kuhusu hatari inayoikabilia Idlib , ambapo hakuna mahala pa kutorokea kwa raia milioni 3.

    Kuna wapiganaji wabaya mjini humo. Lakini shambulio la jumla katika eneo hilo pamoja na lile lililomkabala la kaskazini mwa Hama litamaanisha kwamba watoto milioni moja wataathiriwa na vita hivyo na hicho ndicho tunakiona kikifanyika

    Uturuki inayounga mkono baadhi ya waasi na sio wote ina majeshi yake Idlib kama mojawapo ya makubaliano na Urusi mwaka uliopita.

    Kulingana na Naji Mustafa , msemaji wa waasi wa National Liberation Front msafara huo ulikuwa ukielekea katika mojawapo ya vituo vyake vya uchunguzi na walinzi wakati shambulio hilo lilipotokea,

    Mwandishi wa AFP ambaye aliuona msafara huo anasema ulishirikisha magari 50 ya kijeshi , matano kati yao yakiwa vifaru.

    Lakini Syria imesema kuwasili kwa msafara huo katika eneo hilo ni kitendo cha uchokozi . Imesema kuwa silaha hizo hazitasitisha harakati za wanajeshi wa Syria kukabili kile ilichokitaja kuwa magaidi.

    Kulingana na Shirika la haki za kibinadamu la Syrian Observatory for Human Rights (SOHR), lililo na makao yake nchini Uingereza , ndege ya kijeshi ya Urusi ilitekeleza mashambulio karibu na msafara huo tarehe 19 Agosti.

    Uturuki imesema kuwa shambulio hilo linakiuka makubaliano ya mwaka uliopita huku kisa hicho kikizua hofu kuhusu makubiiano ya moja kwa moja kati ya mataifa hayo mawili.

    Kwa nini shambulio hilo lifanyike?

    Baada ya miaka minane ya vita , serikali ya Syria inajaribu kuyakomboa maeneo yanayodhibitiwa na waasi.

    Vikosi vya serikali vinavyoungwa mkono na Urusi , viliripotiwa kuingia eneo la kaskazini magharibi la Khan Sheikhoun siku ya Jumapili.

    Eneo la Khan Sheikhoun ambalo lilishambuliwa na gesi aina ya sarin mwaka 2017 lipo katika barabara kuu inayounganisha Damascus na Aleppo na ni eneo muhimu la kimkakati kusini mwa mkoa huo.

    Iwapo litakombolewa , itamaanisha kwamba utawala wa Syria umefanikiwa kulizunguka eneo linalodhibitiwa na waasi upande wa kusini ambalo linashirikisha kituo cha uchunguzi cha Uturuki katika mji wa Morek.

    Bwana Mustafa alisema kwamba msafara huo ulikuwa unaelekea Morek.

    cc;BBCswahili

  • Korea kaskazini yasusia mazungumzo ya amani na Korea kusini kuhusu mazoezi ya vita

    Korea kaskazini yasusia mazungumzo ya amani na Korea kusini kuhusu mazoezi ya vita

    Korea kaskazini imepinga mazungmzo ya ziada ya Korea kusini, na kusema uamuzi huo ni “makosa ya hatua za Korea kusini”.

    Imetoa taarifa kufuatia hotuba ya rais wa Korea kusini Moon Jae-in hapo jana Alhamisi.

    Wakati huo huo, mapema leo Ijumaa Korea kaskazini imefyetua makombora mawili baharini kutoka pwani ya mashariki, jeshi la Korea kusini limearifu.

    Likiwa ni jaribio la sita la aina hiyo, na linafanyika chini ya mwezi mmoja.

    Makombora hayo mawili “ambayo hayakutambuliwa ” yalifyetuliwa mwendo wa saa mbili asubuhi Alhamisi na kusafiri umbali wa kilomita 230 kufika ujuu wa 30km, Afisa wa vikosi jumla Korea kusini amesema.

    Msururu wa majaribio hayo yanajiri baada ya rais wa Marekani Donald Trump na mwenzake wa Korea kaskazini Kim Jong-un kukubaliana katika mkutano mnamo Juni kuanza upya majadiliano ya jitihada za kusitisha matumizi ya silaha za nyuklia.

    Korea kaskazini imekabiliwa na vikwazo vya kimataifa kwa kutengeneza silaha za nyuklia.

    Korea kusini imesema nini?

    Katika hotuba hiyo, ya kuadhimisha uhuru wa Korea dhidi ya utawala wa Japan, rais Moon aliapa kuiunganisha rasi ya Korea kufikia mwaka 2045.

    Korea iligawanyika na kuwa mataifa mawili mwishoni mwa vita vya pili vya dunia.

    Rais Moon amesema lengo la kufanikiwa kuacha matumizi ya silaha za nyuklia katika rasi ya Korea ni jambo muhimu zaidi wakati mazungumzo kati ya Kaskazini na Kusini yakionekana kukwama.

    “Rasi mpya ya Korea, ambayo italeta amani na ustawi kwayo, na mashariki mwa Asia, pamoja na katika dunia nzima, inatusubiri,” alisema katika hotuba hiyo aliyoitoa kwenye televisheni.

    Korea kaskazini imelipokea vipi?

    Katika taarifa yake, Korea kaskazini imehoji maana ya mazungumzo wakati “hata katika wakati huu Korea Kusini inaendeleea kufanya mazoezi ya kijeshi ya pamoja na kuzungumzia suala la uchumi wa amani na utawala wa amani. Haina haki ya kufanya hivyo.”

    Katika linaloonekana kuwa ni shambulio dhidi ya rais Moon, taarifa hiyo imeendelea kusema “Tunajiuliza pia iwapo yupo timamu katika fikra zake wakati anapotaja ‘mazungumzo’ baina ya Kaskazini na Kusini wakati anaendeleza taswira ya vita inayopanga kuangamiza vikosi vyetu katika siku 90.

    “Ni mwanamume aliyekosa haya.”

    Korea kaskazini imekasirishwa na mazoezi ya kijeshi baina ya Korea kusini na Marekani , ikieleza kuwa yanakiuka makubaliano yaliofikiwa baina ya rais Donald Trump na rais Moon.

    Imewahi kuyataja mazoezi hayo kuwa “mazoezi ya vita”.

    Katika barua ya hivi karibuni kwa Trump, kiongozi wa Korea kaskazini Kim Jong-un anaarifiwa kuwa alilalamika “kuhusu gharama kubwa na kichekesho” cha mazoezi hayo.

    Mkwamo uliopo katika mazunguzo ya kuistisha matumizi ya silaha za nyuklia ni makosa ya uamuzi wa Korea kusini kufanya mazoezi ya kijeshi, msemaji wa utengamano kutoka Korea kaskazini amesema.

    “Hatuna maneno ya ziada kuzungumza na maafisa wa Korea kusini,” afisa huyo amesema katika taarifa iliyopeperushwa kwenye televisheni ya taifa ya Korean Central News Agency.

    cc;BBCswahili

  • Ni hatari kwa wanawake kufukiza  sehemu zao za siri.

    Ni hatari kwa wanawake kufukiza sehemu zao za siri.

    Madaktari wa magonjwa ya wanawake wameonya kuhusu hatari inayotokana na kutumia mvuke wa moto kwenye sehemu za siri, baada ya kutokea kuwa mwanamke mmoja alijiunguza sehemu zake za siri baada ya kutumia mvuke wa maji kufusha sehemu za siri.

    Mwanamke huyo alikuwa na tatizo la kubadilika muundo wa maumbile ya sehemu zake za siri (prolapsed vagina) kitaalamu, na kuamini kuwa tiba hiyo itamfanya akwepe kufanyiwa upasuaji.

    Kufusha kwa mvuke sehemu za siri, kitendo ambacho uhusisha kukaa kwenye chombo chenye maji ya moto chenye mchanganyiko wa maji na dawa, kimekuwa maarufu sana hivi sasa.

    Tiba hiyo na tiba nyingine kwenye maeneo nyeti, imekuwa ikifanyika kwenye saluni na nyumba za Spa kwenye maeneo mbalimbali ya miji.

    Nyumba za Spa zimekuwa zikitangaza kutoa huduma hiyo iitwayo ”v-steaming” ikidaiwa kuwa imekuwa maarufu miaka mingi barani Afrika na Asia. Wanasema tiba hiyo, ambayo wakati mwingine huitwa Yoni steaming hufanyika ”kuondoa uchafu” kwenye sehemu za siri.

    Wataalamu hata hivyo, wanaasa kuwa ni hatari sana na hakuna uthibitisho wowote kisayansi kuwa ni tiba yenye kufanya kazi kiafya, ikiwemo kupunguza maumivu wakati wa hedhi au kusaidia kupata watoto.

    Dokta Vanessa Mackay, msemaji wa shule ya wataalamu wa magonjwa ya wanawake, anasema ni ”imani” kuwa sehemu za siri zinahitaji usafi wa hali ya juu kiasi hicho au tiba ya namna hiyo.

    Amesema inashauriwa kutumia sabuni zisizo na manukato kwenye eneo la nje la maungo hayo pekee.

    ”Sehemu za siri za mwanamke zina vijidudu vizuri, ambavyo husaidia kulinda maungo hayo,” alieleza katika taarifa yake.

    Kuzifusha sehemu za siri kunaweza kuathiri vijidudu hivyo na kusababisha kuwashwa, na athari nyingine kama maumivu mithili ya kuwaka moto, pia ngozi laini pembezoni mwa sehemu za siri inaweza kuungua au kubabuka

    Madaktari kadhaa wameeleza hadithi kuhusu mwanamke aliyepata madhara kutokana na kufusha sehemu zake.

    Dokta Magali Robert, aliyeandika taarifa ya mwanamama huyo mwa miaka 60 wa huko Canada, alisema mwanamke huyo alijaribu kufukiza sehemu zake za siri kwa ushauri wa daktari wa tiba za kienyeji wa kichina.

    Mwanamke huyo alikaa kwenye maji yaliyokuwa yamechemka kwa dakika 20 kwa siku mbili mfululizo kabla ya kujisalimisha kwa dharura baada ya kupata majeraha.

    Alilazimika kuahirisha upasuaji ili kuuguza majeraha aliyoyapata.

    Doka Robert anasema taarifa hizi za kupotosha huwafikia watu kwa wingi kwenye mitandao na taarifa kutoka kwa watu.

    ”Watu wanaotoa huduma kwa wanawake wanapaswa kufahamu tiba mbadala ili waweze kuepuka madhara.”Alieleza kwenye makala yake.

    cc;BBCswahili

  • Korea kaskazini imefyatua ”kombora” la tatu ndani ya siku 8

    Korea kaskazini imefyatua ”kombora” la tatu ndani ya siku 8

    Korea kaskazini imefyatua kombora la masafa mafupi ambalo halijabainika mara mbili , kwa mujibu wa maafisa wa Korea Kusini , katika jaribio la tatu la silaha hizo katika kipindi cha wiki moja pekee.

    Ufyatuaji wa makombora hayo ulifanyika katika eneo la mwambao wa mashariki mwa taifa hilo mapema Ijumaa.

    hatua hiyo inaonekana kama hatua ya taifa hilo inayolenga kujibu mazoezi ya kijeshi ya baina ya Korea Kusini na Marekani yanayotarajiwa kuanza mwezi huu.

    Wakati huo huo Uingereza, Ufaransa na Ujerumani zimeitaka Korea kaskazini kushiriki maungumzo ya “maana ” na Marekani.

    baada ya mkutano wa faragha katika baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa , mataifa yalisema kuwa vikwazo vya kimataifa vinapaswa kuimarishwa hadi utawala wa Pyongyang utakapoangamiza mipango yake ya nyuklia makombora ya masafa.

    Ufyatuaji wa makombora hayo ulifanyika katika eneo la Yonghung katika jimbo la South Hamgyong katika bahari ya Japan, inayofahamika pia kama Bahari ya Masharik , kwamujibu wa Mkuu wa kikosi cha pamoja cha Korea kaskazini na Korea Kusini (JCS)

    Eneo hilo linaonekana kama kituo cha kufyatulia makombora ambacho hakijawahi kutumiwa awali , amesema Ankit Panda, afisa katika shirikisho la wanasayansi wa Marekani – Federation of American Scientists.

    “Hiki ni kielelezo kingine cha enzi ya Kim Jong-un zaidi ya ufyatuaji wa makombora ya usiku : kufyatua kutoka vituo ambavyo havikuwahi kutumiwa awali au ambavyo havitumiwi .”

    Akizungumza katika ikulu ya White House, rais wa Marekani Donald Trump amesema kuwa hana hofu na ufyatuaji wa hivi karibuni w amakombora kwasababu ni ya masafa mafupi na “ni ya kiwango cha kawaida “.

    Vipi kuhusu majaribio mengine?

    Jumatano , Korea Kaskazini ilirusha makombora mawili ya masafa yanayopaa kilomita 250 (maili 155 ) na kufikia urefu wa kilomita 30 kabla ya kutua kwenye bahari ya Japan, inayofahamika a Bahari ya mashariki , k wamujibu wa Korea Kusini.

    Korea Kusini iliyatambua makombora hayo ya masafa kuwa yalikuwa ni aina tofauti na yaliyofyatuliwa awali . Lakini Alhamisi , Pyongyang ilitoa kauli tofauti , ikisema kuwa ilifanya majaribio ya mfump mpya wa ufyatuzi wa roketi, lakini haikutoa maelezo.

    Mnamo Julai 25, Korea kaskazini ilifyatua makombora mengine mawili, moja likiwa na uwezo wa kusafiri takriban kilomita 690.

    Ufyatuaji huo wa makombora ulikuwa ni wa kwanza kufanyika tangu Bwana Trump na kiongozi wa korea Kim Jong-un wafanye mkutano ambao haukupangwa mwezi Juni katika eneo lisilokuwa na silaha ,, ambalo linatenganisha Korea mbili , ambako walikubaliana kuanzisha mazungumzo ya kuacha matumizi ya nyuklia.

    Ni nini kinachoendelea sasa?

    Korea kaskazini hivi karibuni ilipaza sauti ya hasira yake dhidi ya mazoezi yaliyopangwa kufanyika baina ya Marekani na Korea Kusini, tukio la mwaka ambalo washirika wamekataa kuachana nalo ,lakini limeleta athari kubwa.

    Korea kaskazini inayaona mazoezi hayo ya kijeshi lama maandalizi ya vita na iliyaita “uvuriugaji wa roho ” wa kauli ya pamoja aliyoisaini Bwana Trump na Kim katika kikao chao cha kwanza cha ana kwa ana cha mwaka jana cha Singapore.

    Pyongyang ilikuwa imeonya kwamba mazoezi hayo yanaweza kuathiri kufufuliwa kwa mazungumzo ya kuanchana na nyuklia.

    Jumatatu waziri wa mambo ya kigeni wa Marekani Mike Pompeo alisema kwamba anatumaini mazungumzo haya yanaweza kuanza “haraka sana ”, lakini hakuna mkutano uliopangwa.

    Mwaka jana , Bwana Kim alisema Korea Kaskazini ingesitisha majaribio ya nuklia, na ingeacha kufyatua tena makombora ya masafa marefu yanayoweza kuvuka mipaka ya mabara.

    Shughuli za nyuklia zinaelekea kuendelea, hata hivyo , na picha za setilaiti za kituo kikuu cha nyuklia cha Korea Kaskazini mwezi uliopita zilionyesha kuwa taifa hilo huenda linatengeneza mionzi ya inayochochea makombora.

    Serikali ya Pyongyangpia inaendelea kuonyesha uwezo wake wa kutengeneza silaha mpya licha ya kuwekewa vikwazo vikali vya kiuchumi.

    Ilifyatua kombora la masafa mafupi la aina hiyo mapema mwezi Mei ,likiwa ni kombora la kwanza la aina yake tangu iliporusha kombora la ballistic mnamo mwaka 2017.

    Korea Kaskazini pia ilionyesha manuwari yake ya kijeshi wiki iliyopita, ambayo maafisa wa Korea Kusini wamesema ina uwezo wa kubeba makombora hadi matatu ya masafa ya ballistic.

    cc;BBCswahili

  • Mtoto wa kiume wa Bin Laden ”amefariki”

    Mtoto wa kiume wa Bin Laden ”amefariki”

    Mwana wa kiume wa muasisi wa al-Qaeda Osama Bin Laden, Hamza,amefariki , kwa mujibu wa maafisa wa ujasusi wa Marekani.

    Taarifa kuhusu mahala au tarehe ya kifo cha Hamza Bin Laden bado haijawa wazi katika ripoti ya chanzo hicho cha habari.

    Mwezi Februari, Serikali ya Marekani iliahidi kutoa dola milioni 1 kwa ajili ya yeyote atakayetoa taarifa zitakazosaidia kutambua ni wapi alipo.

    Hamza Bin Laden, anayedhaniwa kuwa na umri wa miaka 30, alikuwa ametoa ujumbe mbalimbali wa sauti na video akitoa wito wa kufanya mashambulio dhidi ya Marekani na nchi nyingine.

    Ripoti zilitolewa kwanza na mashirika ya habari ya NBC na New York Times.

    Hamza Bin Laden aliwatolea wito wapiganaji wa jihadi kulipiza kisasi mauaji ya baba yake aliyeuliwa na kikosi maalum cha Marekani nchini Pakistan mnamo mwezi Mei 2011.

    Kadhalika alikuwa amewatolea wito watu wa rasi ya Arabia kulipiza kisasi. Saudi Arabia ilimyang’anya uraia mwezi Machi.

    Aliaminika kuwa katika kifungo cha nyumbani nchini Iran lakini ripoti nyingine zilisema kuwa huenda alikuwa akiishi katika mataifa ya Afghanistan, Pakistan na Syria.

    Wizara ya mambo ya nje ya Marekani ilisema kuwa nyaraka zilizokamatwa katika uvamizi wa mwaka 2011 katika nyumba ya baba yake ya Abbottabad, Pakistan, zinaonyesha kuwa Hamza Bin Laden alikuwa anaandaliwa kuchukua utawala wa al-Qaeda.

    Vikosi vya Marekani pia viliripotiwa kubaini video hii ya harusi yake akimuoa binti wa afisa mwingine wa ngazi ya juu wa al-Qaeda ambayo ilidhaniwa kufanyika nchini Iran

    Baba mkwe wake alikuwa ni Abdullah Ahmed Abdullah au Abu Muhammad al-Masri, ambaye anatafutwa kwa madai ya kuhusika katika mashambulio ya ugaidi ya mwaka 1998 dhidi ya balozi za Tanzania na Kenya.

    Al-Qaeda lilikuwa ni kundi lililotekeleza mashambulio mabaya ya ugaidi ya Septemba 11, 2001 dhidi ya Marekani, lakini hadhi yake kwa sasa imeshuka katika kipindi cha miongo kadhaa iliyopita baada ya kuibuka kwa umaarufu wa kundi la Islamic State.

    Ni ishara ya jinsi taarifa chache kumuhusu Hamza Bin Laden kiasi kwamba maafisa hawakuweza kuthibitisha umri wake.

    Katika miezi ya hivi karibuni walisema kuwa huenda alikuwa nchini Afghanistan, Pakistan au Iran. lakini hawakuweza hata kusema ukweli hasa ni nchi gani mmoja wa watu ambao Marekani ”inawatafuta sana” anaishi.

    Zawadi ya dola milioni moja kwa yeyote atakayetoa taarifa kumuhusu ilikuwa ni hatua si tu ya uwezekano wa hatari anayoweza kusababisha lakini pia ilikuwa ni ishara ya umuhimu kwa al-Qaeda na propaganda yao.

    Hamza alikuwa ni mtoto pekee aliyekuwepo wakati baba yake aliposaidia kupanga njama za mashambulio ya Septemba 11 lakini, kwa mujibu wa wakuu wa kundi hilo lenye itikadi kali, alikuwa pamoja naye wakati wa mashambulio hayo.

    Kwa mtoto wa kiume ambaye alikuwa akifundishwa kuichukia Marekani, kukwepa mauaji ya ulipizaji kisasi mikononi mwa kikosi maalumu lingekuwa ni jambo ambalo lingesalia akilini mwa watu.

    Katika miaka ya hivi karibuni alituma ujumbe mtandaoni akitoa wito kwa mashambulio dhidi ya Marekani na washirika wake.

    Al-Qaeda: Taarifa muhimu

    • Alifahamika nchini Afghanistan katika miaka ya mwisho ya 1980, kama mwarabu aliyejitolea kujiunga na kikosi cha Afghanstan kilichoungwa mkono na mujahideen kilichopigana kuvifukuza vikosi vilivyoteka eneo la Usovieti
    • Osama Bin Laden alianzisha shirika la kusaidia wahudumu wa kujitolea ambalo lilikuja kutambuliwa kama al-Qaeda, au “ngome”
    • Aliondoka Afghanistan mnamo mwaka 1989, na kurejea tena mwaka 1996 kuongoza makambi ya mafunzo ya kijeshi ya maelfu ya waislamu kutoka mataifa ya kigeni.
    • Al-Qaeda ilitangaza “vita vitakatifu ” dhidi ya Wamarekani,wayahudi na washirika wao.

    cc;BBCswahili

  • Mamilioni ya watu bado wanakabiliwa na njaa Afrika

    Mamilioni ya watu bado wanakabiliwa na njaa Afrika

    Zaidi ya watu milioni 820 au 10.8% duniani bado wanakabiliwa na njaa, inasema ripoti ya Umoja wa Mataifa wakati dunia ikiadhimisha siku ya njaa siku ya njaa.

    Kiwango cha njaa kimepanda karibu katika maeneo yote ya Afrika, na kulifanya bara la Afrika kuwa kanda yenye idadi kubwa ya watu wenye utapiamlo, kwa takriban asilimia 20, ikifuatiwa na Asia ambako zaidi ya asilimia 12 ya wakazi wa bara hilo wana tatizo hilo.

    Asilimia 7 ya watu wa Amerika Kusini na Caribbean pia wameathiriwa na utapiamlo. Kuna watoto zaidi ya milioni 40 wenye uzito wa mwili wa kupindukia duniani ,hili kikiwa ni ongezeko la watoto milioni 10 wenye tatizo hilo tangu mwaka 2000.

    Japo idadi ya watoto idadi ya watoto walio chini ya umri wa miaka 5 waliodumaa, imepungua kwa ujumla duniani, bado watoto milioni 149 au asilimia 21.9 ya watoto walio chini ya umri wa miaka 5 wamedumaa. Hata hivyo Afrika bado ina kiwango cha juu kuliko mabara mengine cha watoto waliodumaa katika ukuaji.

    Mnamo mwaka 2018, mabara ya Africa na Asia ayalikuwa na kiwango cha tisa kwa kumi cha watoto wote waliodumaa duniani (sawa na asilimia 54.9 kwa Afrika na asilimia 39.5 kwa Asia).

    Kiwango hicho kinafanya idadi ya waathiriwa wa ukosefu wa usalama wa chakula kufikia zaidi ya watu bilioni mbili.

    Tathmini ya kipekee kuhusu kuongezeka kwa uzito wa mwili inaonyesha kwamba kuna ongezeko la haraka la uzito wa mwili miongoni mwa watoto wa shule na watu wazima katika maeneo yote ya Afrika.

    Kulingana na Umoja wa Mataifa watoto wa shule hawali matunda na mboga za kutosha, mara kwa mara hula vyakula vyenye kutia nguvu na joto mwilini , na mara nyingi hula vyakula vinavyotengenezwa haraka kama vile vibanzi na vinywaji vya sukari nyingi kama vile soda, na hawafanyi mazoezi ya mwili.

    Mazowea haya mabaya , yanaweza kuwa yanachangia kwa sehemu fulani, kuongezeka kwa uzito wa mwili miongoni mwa watoto wa shule, inasema ripoti.

    Tatizo hilo linachangiwa, kwa sehemu moja na kuongezeka kwa masoko ya vyakula vilivyopitia mchakato wa viwandani na upatikanaji wake, pamoja na viwango vya chini vya mazoezi ya mwili.

    Kudorola wa chumi za dunia pamoja na kufungwa kwa biashara kuu za dunia kumeelezewa kuchangia kwa ukosefu wa hivi karibuni wa usalama wa chakula pamoja na ukosefu wa virutubisho vya mwili unaoendelea, pamoja na na ukosefu wa sera za muda mfupi na mrefu ambazo ni muhimu katika kulinda usalama wa chakula, iwe nyakati za matatizo ya kiuchumi au katika kuandaa sera hizo.

    Mabadiliko ya hali ya hewa pia yamechangia kuathiri kilimo na kusababisha kupungua kwa idadi ya wakulimana shughuli za kilimo . “haya yote yamesababisha mabadiliko ya namna chakula kinavyozalishwa, kugawanywa na kuliwa kote duniani – na kujitokeza kwa changamoto mpya za usalama wa chakula na afya .” wanasema wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa.

    Wakizungumza kuhusiana na baa la njaa, wakuu hao wa mashirika ya Umoja wa Mataifa wameapa kuandaa mikakati ya kukabiliana na baa la njaa duniani.

    ” Matendo yetu ya kukabilana na hali ya njaa inayotatiza dunia yatakuwa thabiti,” Walisema viongozi hao wa Umoja wa Maraifa. na kuongeza kuwa: “Lazima tukabiliane na umaskini na kuandaa muundo wa mikakati ya mabadiliko inayoshirikisha ikiwalenga watu na kushirikisha jamii zilizozo katika hatari ya kuathirika kiuchumi na kujipanga wenyewe ili kumaliza njaa, kuweka usalama wa chakula na kukabiliana na aina zote za utapiamlo.” Wanasema maafisa wa Umoja wa mataifa.

    Umoja wa mataifa unasema kuwa kasi ya mafanikio katika kukabiliana na kudumaa kwa mtoto na kupungua kwa idadi ya watoto wachanga wanaozaliwa na uzito wa chini wa mwili ni ya kiwango cha chini sana, na hivyo kupunguza fursa za kufikia mafanikio malengo mengine ya kudumu.

    Umoja wa Mataifa unasema kuwa licha ya kwamba kiwango cha kudumaa kwa watoto kimepungua duniani kwa asilimia 10 katika kipindi cha miaka sita, bado mafanikio ni ya taratibu sana kulingana na malengo ya 2030 ambapo kiwango cha watoto wanaodumaa katika ukuaji kinatarajiwa kupunguzwa kwa asilimia 50.

     

  • Wabunge Kenya watofautiana kuhusu matamshi ya ‘chuki’ ya Charles Kanyi ‘Jaguar’

    Wabunge Kenya watofautiana kuhusu matamshi ya ‘chuki’ ya Charles Kanyi ‘Jaguar’

    Matamshi ya mbunge wa Starehe nchini Kenya Charles ‘Jaguar’ Kanyi kuhusu kuwatishia raia wa kigeni wanaofanya kazi nchini Kenya yaliwasilishwa mbele ya kikao cha bunge ili kujadiliwa.

    Hatua hiyo inajiri huku Mbunge huyo akizuiliwa katika kituo cha polisi usiku kucha ambapo anasubiri kuwasilishwa mahakamani siku ya Alhamisi.

    Kulingana na mtandao wa runinga ya Citizen nchini Kenya, licha ya wabunge wengi kushutumu jinsi ambavyo bwana Jaguar alitoa hoja yake , baadhi yao walikubaliana kwamba kuna swala tata kuhusiana na raia wa kigeni ambalo lilihitaji kuangaziwa.

    Kulingana na mtandao huo swala hilo liliwasilishwa na mwenyekiti wa kamati ya Ulinzi na Uhusiano wa kigeni Katoo Ole Metito katika taarifa yake, akithibitisha kwamba raia wa kigeni hususan kutoka Jumuiya ya Afrika mashariki wana uhuru wa kufanya biashara nchini Kenya.

    ”Tunashutumu sana matamshi yoyote ya chuki yanayokiuka msimamo huu unaotuleta sisi pamoja kama taifa na kuthibitisha sera ya kuwakaribisha raia wote wa kigeni”, alisema mbunge huyo wa Kajiado kusini.

    Matamshi yake yaliungwa mkono na mbunge wa Suba Kaskazini John Mbadi ambaye aliwarai wabunge wenzake kutotoa matamshi mbele ya umma kwa lengo la kujitafutia umaarufu na badala yake kuchukua tahadhari.

    ”Kama bara, tunahitaji kukuza uwiano katika mipaka yetu ili kutafuta ajira; Wakenya wako huru kwenda Tanzania kufanya biashara iwapo biashara hiyo ni halali”, alisema Mbadi.

    Hatahivyo kiongozi wa walio wengi bungeni Aden Duale, ambaye pia alishutumu matamshi hayo ya mbunge huyo wa Starehe alisema kwamba Kenya sio jaa la raia wa kigeni na bidhaa zao, kulingana na mtandao wa Citizen kenya.

    Kulingana na mbunge huyo wa Garissa mjini, Bunge pamoja na serikali zinafaa kuwalinda wananchi wa kawaida kutopoteza kazi kwa idadi kubwa ya raia wa kigeni waliomo nchini.

    Mbunge huyo alitaja mfano ambapo wataalam kutoka Kenya kama vile afisa wa kampuni ya Safaricom Sylvia Mulinge alinyimwa fursa ya kufanya kazi katika taifa jirani la Tanzania, akiongezea kuwa Kenya pia inafaa kutokubali maswala mengine.

    “Lazima ukweli usemwe; Unapoona biashara ya uchuuzi ikichukuliwa na raia wa taifa jingine tuna jukumu la kuwalinda watu wetu. Hawa wabunge hawafai kusahau kwamba kuku wetu walichomwa Tanzania , ng’ombe wetu walipigwa mnada Tanzania”, alisema Duale.

    ”Leo chini ya utawala uliopo Tanzania Wakenya hawawezi kufanya biashara, kwa nini bidhaa zetu haziingi Tanzania? Kwa sababu wametuwekea kodi ya juu”.

    Duale aliwataka wabunge kutolichukulia swala hilo na hisia, bali kuchukua tahadhari wanapochukua jukumu lao la kuwalinda raia wa kawaida.

    ”Kama bunge ni lazima tuamue na kuleta sheria zitakazolinda biashara zetu. Munaweza kumshutumu Jaguar, lakini leo ndiye mbunge maarufu zaidi katika eneo bunge lake”, aliongezea Duale.

    Nae mbunge wa Ugenya David Ochieng, kwa upande wake aliilaumu idadi kuu ya raia wa kigeni wanaofanya biashara nchini Kenya kwa kushindwa kwa serikali kuidhinisha sera yake.

    ”Katika uchumi wa leo , ni rahisi kununua bidhaa kutoka mataifa jirani kama vile Tanzania na Uganda na kuleta Kenya. Sio kwamba hatuna sheria, ni swala la utekelezwaji na ufisadi. Tunwaruhusu watu kuingia nchini na kuanza kuuza vitu barabarani. Huwezi kuwalaumu Watanzania kwa kufanya hivyo ni kwa sababu ya mfumo wetu ambao ni dhaifu”, alisema Ochieng’.

    ”Hatuwakagui watu wanaoingia nchini. Watanzania wanafanya kazi yao, ndio sababu wanaweza kujua kwamba Mulinge hakuhitimu kufanya kazi Tanzania.

    Hatahivyo Mbunge huyo alishutumu matamshi ya Jaguar , huku akilitaka bunge hilo kuchukua hatua za kinidhamu dhidi ya wabunge wanaoharibu jina la taifa hilo katika ulingo wa kimataifa.

    Tayari ofisi ya Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai kupitia ukurasa wake wa Twitter imesema mbunge huyo anashikiliwa kwa tuhuma za kuchochea ghasia.

    Katika kanda ya video iliosambazwa pakubwa nchini Kenya na katika nchi jirani Tanzania, mbunge huyo alisema hawatokubali watu wa nje waje kuendesha biashara nchini humo.