Category: Global News

  • RAIS MPYA WA AFGHANSTAN ASAINI MKATABA NA NATO

    RAIS MPYA WA AFGHANSTAN ASAINI MKATABA NA NATO

    afughan2
    Ashraf Ghani rais mpya wa Afghanstan

    Siku moja baada ya kuapishwa kuwa rais mpya wa Afghanistan Ashraf Ghani, serikali yake imetia saini mkataba mpya wa usalama na shirika la kujihami la NATO.

    Mkataba huo utaidhinisha zaidi ya wanajeshi elfu kumi na mbili, wengi wakiwa wamarekani, kusalia nchini Afghanistan hata baada ya kumalizika kwa kandarasi yao mwaka huu.

    Mkataba huo ulitiwa sahihi katika hafula iliyotangazwa moja kwa moja katika televisheni na mshauri wa maswala ya usalama wa kitaifa wa Afghanistan Hanif Atmar na balozi wa Marekani nchini humo Jim Cunningham, huku Rais mpya wa Afghanistan Ashraf Ghani akishuhudia.

     

    afughan

    Rais aliyeondoka Hamid Karzai alikataa kwa muda mrefu kusaini mkataba wa kuwaongezea wanajeshi wa Marekani muda wa kukaa huko, na hivyo kusababisha mvutano kati yake na Marekani.

    Bwana Karzai alikuwa anasisitiza kuwa la muhimu zaidi ni kuanzisha mpango wa amani na kusitisha mapigano na wanamgambo wa Taleban.

    Vikosi vya NATO vimekuwa vikipunguzwa nchini Afghanistan na taratibu kurudisha udhibiti wa usalama wa nchi hiyo kwa vikosi vya Afghanistan.

     

  • Je Mugabe atamrithisha mkewe mamlaka?

    Je Mugabe atamrithisha mkewe mamlaka?

     

     

     

     

     

     

    MUGABE
    Rais Mugabe akiwa na mkewe bi.Grace Mugabe

    Hivi karibuni kumekuwa na swali ambalo linawatatiza watu wengi hususani raia wa Zimbabwe kufuatia mtukio ya rais wa nchi hiyo kumkabidhi mkewe nyazfa mbalimbali za juu kiutawala.

    Kuzaliwa kwa utawala wa kinasaba sio jambo jepesi kubashiri.

    Lakini wananchi wengi wa Zimbabwe kwa sasa wanaonekana kushawishika kuwa kuna uwezekano wa familia ya Mugabe kuingia katika orodha hiyo ya kurithishana madaraka.

    Rais Mugabe ana umri wa miaka 90. Mke wake, Grace, ana umri wa miaka 49.

    Uvumi wa kurithishana madaraka umekuwa gumzo la kisiasa nchini Zimbabwe kwa miaka mingi, lakini Grace Mugabe katika miaka ya karibuni ameibuka kama mtu ambaye ataweza kumrithi mumuwe madaraka ya uongozi wa nchi ya Zimbabwe.

    Watu wa nje wamesikia tabia ya mke wa Rais Mugabe ambaye ni karani muhtasi wake wa zamani kutuhumiwa kufanya manunuzi yasiyo na mpangilio na katika tukio lingine kumpiga ngumi mwandishi wa habari wa Uingereza huko Hong Kong; na kufanya mambo mengine ambayo yanavuka mpaka kama mke wa kiongozi.

    Vyombo vya habari vya Zimbabwe, kwa kulinganisha vimedhamiria kumjenga Bi Grace Mugabe kuwa mtu wa kujitolea kwake katika kazi za kijamii.

     

    MUGABE2

    “Wakati mume wake akiondoka ndiyo mwisho wake wa kazi ya uanasiasa, kama kweli kuna kazi ya aina hiyo” anasema mchambuzi wa masuala ya siasa nchini Zimbabwe,anasema Ibbo Mandaza, akitupilia mbali wazo la kuendelea kuwa na utawala wa familia ya Mugabe.

    Nadharia nyingine ni kwamba Rais Mugabe anamjenga mke wake ili kuyayumbisha makundi yote ndani ya chama cha Zanu-PF, na kuimarisha nafasi yake ya urais.

    Dewa Mavhinga, kutoka Human Rights Watch, anaamini kuwa rais amefanya kosa kubwa kumleta mtu ambaye hana ujuzi wowote wa siasa.

    “Inaonyesha kuwa Rais Mugabe hamwaamini mtu yeyote karibu naye”Dewa Mavhinga.

     

     

     

  • CHINA YAONYA MATAIFA YA KIGENI KUTOINGILIA HONG KONG

    CHINA YAONYA MATAIFA YA KIGENI KUTOINGILIA HONG KONG

    china
    picha ni maelfu ya waandamanaji huko Hong kong nchini china

    Uchina imeonya kuwa  kuwa haitawavumilia wahaini kutoka nje ya nchi wanaounga mkono maandamano yasiyo halali nchini humo.

    Kundi lijulikanalo kama Occupy Central ndilo linalolengwa kwa sababu limekuwa likiunga mkono juhudi za maandamano ya maelfu ya watu wanaounga mkono kuimraishwa kwa Demokrasia nchini Uchina.

    Katika kile kinachoaminika kulenga maandamano yanayoendelea katika jimbo la Hong Kon, Uchina inaonya mataifa mengine yasijiingize kwa kila inachoamini na maswala ya ndani ya Uchina.Uchina mara kwa mara hutoa onyo kwa mataifa mengine yasijiingize katika jimbo hilo lake linalotaka kuendesha mambo yake kivyake.

    china
    polisi wakipambana na waandamanaji

    kauli hiyo ya serikali imekuja siku chache baada ya matamshi ya Chris Patten, aliyekuwa wakati mmoja Gavana wa Hong Kong, aliposema kwamba Uingereza ina wajibu wa kutoa taarifa kwa niaba ya wakazi wa Hong Kong, eneo lililokuwa koloni yake wakati mmoja.

    Baraza Kuu la Kitaifa la Uchina, ambalo ni kiungo muhimu katika Serikali, limesema kuwa lina imani kwamba Serikali ya Jimbo la Hong Kong, ina uwezo wa kukabiliana na maandamano hayo kibinafsi bila kuingiliwa na yeyote.

    Kuna hofu kuu Hong Kong kuwa huenda Serikali Kuu ikatumia polisi wenye silaha kuzima maandamano hayo.

    kumekuwa na mijadala mbalimbali duniani juu ya kauli hiyo ya serikali ya China na maoni tofauti yamekuwa yakitolewa na wasomi pamoja viongozi lakini pia watu mashuhuri duniani

     

     

  • Mapigano Baina Ya Israel Na Wapalestina Yasimama Gaza

    Mapigano Baina Ya Israel Na Wapalestina Yasimama Gaza

    Gaza

    Israel na wapiganaji wa Ki Palestina wamekubaliana kusitisha mapigano kwa muda mrefu katika ukanda wa Gaza.
    Kusitishwa kwa mapigano hayo, kumehitimisha wiki saba za vita vilivyosababisha vifo vya watu zaidi ya 2,200, wengi wao wakiwa Wapalestina. Mazungumzo hayo yalisimamiwa na Misri na yalianza kutekelezwa jana kuanzia majira ya saa moja usiku.
    Hamas wamesema mpango huo unawakilisha “ushindi wa upinzani wao”.Maafisa wa Israel wamesema Israel italegeza vikwazo ilivyoiwekea Gaza ili kuruhusu misaada na vifaa vya ujenzi kuingia Gaza.
    Rais wa Wapalestina Mahmoud Abbas ametangaza kukubaliana na mpango wa kusitisha mapigano.Msemaji wa serikali ya Israeli, Mark Regev amesema: “hebu tuwe na matumaini kwamba mpango huu wa kusitisha mapigano utaheshimika”
    Mazungumzo yasiyo ya moja kwa moja katika masuala yenye utata, ikiwa ni pamoja na wito wa Israel wa kuyataka makundi ya wapiganaji yanapokonywa silaha, yataanza mjini Cairo katika kipindi cha mwezi mmoja.
    Marekani imeunga mkono kikamilifu mpango huu, kwa msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani Jen Psaki kusema: “tunaunga mkono kikamilifu tangazo la kusitisha mapigano.”
    Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon pia amepongeza mpango huo wa kusitisha mapigano. Lakini katika taarifa kupitia kwa msemaji wake, Bwana Ban ameonya kuwa “jitihada yoyote ya amani ambayo haishughulikii chanzo halisi cha mgogoro, itafanya kazi kidogo kuliko kutengeneza mzunguko mwingine wa ghasia”.
    Hatua ya kusitisha mapigano imekuja huku Israel na Wapalestina wakiendelea kushambuliana.
    Kombora la dakika ya mwisho ya makabiliano kutoka Gaza limemuua raia wa Israel na kuwajeruhi wengine sita katika Barazala la Jimbo la Eshkol.
    Mapema Jumanne, Wapalestina wapatao sita waliuawa katika mfululizo wa mashambulio ya anga ya Israel huko in Gaza, Wamesema maofisa wa Palestina.
    Maofisa wa Palestina wamesema pendekezo la Misri la kusitisha mapigano linataka kumalizwa kwa uhasama kusiko na kikomo, kufunguliwa haraka kwa mipaka ya Gaza na Israel na Misri na kuongezewa ukanda wa uvuvi katika bahari ya Mediterani..
    Tangazo la kusitisha mapigano lilishangiliwa na Wapalestina katika mji wa Gaza.
    Kabla ya kuanza utekelezaji wa mpango huo, majengo marefu mjini Gaza yalishambuliwa na makombora zaidi yalipiga Israel.
    Mwezi mmoja baadaye Israel na vikundi vya Wapalestina vitajadili ujenzi wa bandari na uwanja wa ndege huko Gaza na kuwaachilia huru wafungwa 100
    Israel na Misri pia zimesemekana kutaka kuhakikishiwa kuwa silaha hazitaingizwa Gaza kwa njia ya magendo.

     

  • Habari Katika Picha; Tamasha mwembe yanga

    Habari Katika Picha; Tamasha mwembe yanga

     

     

    Hi ni baadhi ya Picha ya Matukio katika Tamasha Lilifanyika mwembe YangaIMG-20140602-WA0004

    IMG-20140602-WA0002

  • 93.7 E-FM Yaanza kurusha matangazo rasmi!!!

    93.7 E-FM Yaanza kurusha matangazo rasmi!!!

    93.7 E-FM radio Yaanza Rasmi Kurusha Matangazo Yake Toka Station Zake Zilizopo Kwenye Jengo La K-Net Kawe Dar es Salaam.

  • Mh. Lowassa akagua maandalizi ya Sokoine day Monduli Juu

    Mh. Lowassa akagua maandalizi ya Sokoine day Monduli Juu

    Waziri mkuu mstaafu na mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa akipata maelezo kutoka kwa watoto wa marehemu Edward Sokoine, Namelok Sokoine(mb) na Joseph Sokoine ambaye ni afisa katika balozi wa Taznania nchini Kanada, kuhusiana na maandalizi ya maadhimisho ya miaka 30 ya kifo Cha aliyekuwa waziri mkuu an mbunge wa Monduli Marehemu Edward moringe Sokoine, kesho April 12. Rais Jakaya Kikwete ataongoza maadhimisho hayo pamoja na marais na mawaziri wakuu wastaafu.

  • Msanii LADY JAY DEE (@jidejaydee) ameula katika michuano ya Kombe la Dunia 2014

    Msanii LADY JAY DEE (@jidejaydee) ameula katika michuano ya Kombe la Dunia 2014

    Msanii Judith Wambura ‘Lady Jaydee’ ameula katika michuano ya Kombe la Dunia 2014 baada ya kupata nafasi ya kuandaa wimbo kwa a jili ya michuano hiyo mikubwa zaidi ya soka duniani.

    Jaydee anayefahamika pia kama Komandoo au Anaconda, amepata fursa ya kuandaa wimbo maalum wa michuano hiyo ‘FIFA World Cup Anthem’ akishirikiana na wakali wawili David Correy wa Brazil na rapa Octopizzo wa Kenya.

    Katika wimbo huo, Lady Jaydee na Correy wameimba kwa lugha ya Kiingereza huku Octopizzo ‘akichana’ kwa Kiswahili.

    Wimbo huo ulipigwa kwa mara ya kwanza jana jijini Dar es Salaam wakati kampuni ya Coca-Cola ilipozindua promosheni yake mpya ya miezi miwili ya Kombe la FIFA la Dunia 2014 ambayo itawawezesha wateja wake kujishindia zawadi mbalimbali zikiwamo tiketi za kwenda kushuhudia mechi za robo fainali za Kombe la Dunia nchini Brazil.

    Meneja Mkazi wa Coca-Cola Tanzania, Yebeltal Getachew alisema hayo wakati wa hafla ya uzinduzi ya kampeni hiyo iliyofanyika jijini Dar es Salaam huku akizitaja zawadi nyingine kuwa luninga, mipira na fulana. Wakati huo huo, Jmosi tarehe 12 April Lady Jaydee anataraji kuachia wimbo wake na video mpya ‘Nasimama’.
    CHANZO: Nipashe

  • VODACOM YATEMBELEA VYOMBO VYA HABARI KUIMARISHA UHUSIANO

    VODACOM YATEMBELEA VYOMBO VYA HABARI KUIMARISHA UHUSIANO

    Waendeshaji wa kipindi cha Morning Choice kinachorushwa na kituo cha Radio cha Choice FM Baby Kabai (kulia) na Evans Bukuku wakionesha manjonjo kwa Mkuu wa Masoko wa Vodacom Kelvin Twissa na Mkuu wa Mawasiliano na Uhusiano wa Vodacom Rosalynn Mworia (hawapo pichani) walipotembelea vyombo vya habari vilivyo chini ya Clouds Media Group.

  • Matumaini Katiba Mpya arijojo

    Matumaini Katiba Mpya arijojo

    Ikulu imeeleza kuwa imeshindwa kutimiza ahadi yake kwa taifa ya kulipatia Katiba Mpya ifikapo Aprili 26, 2014.

    Katibu Mkuu Kiongozi (KMK), Balozi Ombeni Sefue alilieleza gazeti hili kuwa kwa hali ya mchakato huo ilivyo sasa, wameshindwa kufikia lengo hilo, lakini hawajakata tamaa kuhusu kupatikana Katiba Mpya ndani ya mwaka huu.

    “Kweli matarajio ya awali yalikuwa hayo, lakini kama unavyoona hali ilivyo, ni vigumu kusema matarajio mengine, ingawa majadiliano yaliyofanywa mwaka huu ni lazima Katiba inayopendekezwa iwasilishwe kwa wananchi na mwakani tutakuwa na Katiba Mpya,” alieleza Balozi Sefue.

    Katika hali isiyoeleweka Balozi Sefue alisisitiza msimamo wa awali wa Serikali kwamba Katiba itakayopatikana itatumika kwenye Uchaguzi Mkuu, unaotarajiwa kufanyika mwaka ujao.

    Dk Slaa

    Katibu Mkuu wa Chama cha Maendeleo na Demokrasia (Chadema), Dk. Willbroad Slaa, alisema hilo ni fundisho kwa Serikali kwamba kiburi na jeuri havitakiwi katika masuala yanayohusu umma.

    Alisema muda huo wa kupatikana Katiba Mpya ulipotangazwa, walioanzisha kilio cha kudai Katiba Mpya nchini ambao aliwataja kuwa ni vyama vya upinzani vya siasa, taasisi mbalimbali za kijamii walipinga na kutoa ushauri kwa Serikali, lakini walipuuzwa.

    Dk. Slaa alisema walipendekeza kwamba badala ya kupeleka mchakato wa Katiba mchakamchaka, warekebishe kwa mara ya 15 Katiba inayotumika, ili iende na wakati wa sasa ikiwamo Uchaguzi Mkuu ujao kwa lengo la kutoa muda wa kutosha kwa mchakato wa taifa kupata Katiba Mpya.

    “Lakini walitukebehi na kututukana sana, sasa kiko wapi Aprili 26 hiyo hapo na Katiba haijapatikana na kusema itapatikana mwaka huu na kutumika kwenye Uchaguzi Mkuu mwakani ni ndoto za mchana,” alieleza Dk. Slaa.

    Dk. Slaa alisema tukio hilo liwe fundisho kwa Serikali, wawe wakweli, wanyoofu na wafahamu kuwa nje ya Serikali kuna watu makini na wanaojua vilivyo mchakato wa Katiba.

    Alisema ana taarifa za Bunge Maalumu kuahirishwa Mei 9, 2014 ili kupisha Bunge la Bajeti. Hivyo mategemeo ya Katiba Mpya kwenye Uchaguzi Mkuu ujao, yanatia shaka.

    “Kwa akili ya kawaida tu isiyohitaji elimu ya chuo chochote, kutumia Katiba Mpya kwenye Uchaguzi Mkuu ujao ni jambo lisilowezekana kwa hiyo waache kutuletea matumaini yasiyokuwapo, sisi siyo watoto wadogo,” alieleza Dk. Slaa.

  • Mh. Edward Lowassa amuaga mkuu mkoa wa Mara

    Mh. Edward Lowassa amuaga mkuu mkoa wa Mara

    Waziri Mkuu mstaafu an mbunge wa Monduli Mh Edward Lowassa akiwasili katika viwanja vya Mwalimu Nyerere kumuaga mwili wa Mkuu wa Mkoa wa Mara marehemu John G Tuppa.Pembeni ni mbunge wa Mwibara Kangi Lugola