Global News

Iran imefanya kosa  kubwa sana
Global News

Rais wa Marekani aliidhinisha majeshi ya Marekani kuishambulia siku ya Alhamisi na kisha kubadili msimamo, vyombo vya habari vya nchi hiyo viaripoti. Mashambulizi hayo ilikuwa yawe ya kulipiza kisasi baada ya Iran kuitungua ndege isiy na rubani ya Marekani. Kwa mujibu wa gazeti mashuhuri la The New York Times, tayari matayarisho ya awali ya mashambulizi hayo yalikuwa yakiendelea wakati Trump alipobadili mawazo na kuamuru yasitishwe. Gazeti hilo linamnukuu afisa mmoja mwanandamizi wa Ikulu ya White House. Hata hivyo bado hakuna...

Like
475
0
Friday, 21 June 2019
Morsi Azikwa saa chache baada ya kifo
Global News

Rais wa zamani wa Misri, Mohamed Morsi amezikwa saa chache baada ya kufariki dunia akiwa mahakamani siku ya Jumatatu. Wakili wake ameliambia shirika la habari la Ufaransa, AFP kiongozi huyo wa zamani alizikwa Mashariki mwa jiji la Cairo asubuhi ya Jumanne familia yake ikiwepo Morsi,aliyekuwa na miaka 67, alikuwa kizuizini tangu alipoondolewa madarakani mwaka 2013. Makundi ya watetezi wa haki za binaadamu , ambayo yalikosoa mazingira ambayo Morsi aliwekwa,wametoa wito wa kufanyika uchunguzi kuhusu kifo chake. Familia yake na wanaharakati...

Like
472
0
Tuesday, 18 June 2019
Omar All bashir ashtakiwa kwa Ufisadi
Global News

Rais aliyeng’olewa madarakani nchini Sudan Omar al-Bashir ameshtakiwa kwa kosa la ufisadi. Mashtaka yanahusiana na sheria zinazohusu “utajiri haramu na maagizo ya dharura “,imesema ofisi ya mwendesha mashtaka, ambayo haikutoa taarifa zaidi. Jeshi lilimuondoa madarakani rais huyo wa muda mrefu mwezi April kufuatia miezi ya maandamano dhidi yake. Msemaji wa jeshi aliesma Alhamisi kuwa makosa yalifanyika wakati majeneraliwalipoamrisha kumalizika kwa mhgomo wa kukaa mbele ya makao makuu ya jeshi ambapo waandamanaji wanadai...

Like
523
0
Friday, 14 June 2019
wanne waripotiwa kuuawa nchini Sudan
Global News

Watu wanne wameripotiwa kuuawa nchini Sudan katika siku ya kwanza ya maandamano ya kitaifa ya kupinga utawala wa Kijeshi nchini humo. Vikosi vya Usalama nchini Sudan viliwarushia mabomu ya machozi baridi na kutumia risasi halisi kuwatawanya waandamanaji hao katika mkuu wa nchi hiyo Khartoum. Wanaharakati wameitisha maandamano ya kupinga utawala huo kuanzia Jumapili, siku kadhaa baada ya msako wa kijeshi uliosababisha vifo vya mamia ya watu katika mji mkuu wa Khartoum. Aidha, Wafanyikazi kadhaa wa benki, Viwanja wa Ndege pamoja...

Like
495
0
Monday, 10 June 2019
Njiwa amuepusha dereva  na faini
Global News

Dereva aliyekua akiendesha Gari kwa kasi nchini Ujerumani alinusurika kulipa faini ya pauni 93 baada ya njiwa mweupe kumuepusha kutambulika sura yake. Dereva alinaswa kwenye kamera za mwendo kasi lakini sura yake ilifichwa na mabawa ya ndege huyo alipokua akiruka mbele ya kioo cha gari. Taarifa ya polisi inasema pengine ”Roho mtakatifu” aliingilia kati- ishara ya njiwa mweupe kama alama ya uwepo wa Mungu katika imani ya dini ya kikristo. ”Tumeelewa ishara hiyo na kumuacha dereva kwa amani wakati huu.”...

Like
644
0
Wednesday, 29 May 2019
Brexit ilivyomuondoa madarakani Theresa May
Global News

Waziri mkuu wa pili mwanamke Uingereza, kama ilivyo kwa wa kwanza, mwishowe ameondolewa madarakani kutokana na mvutano wa ndani ya chama cha Conservative kuhusu Ulaya.   Angalau sio kwa namna ambavyo angetamani wakati alipoingia Downing Street mnamo Julai 2016. Maazimio aliyokuwa nayo – kufikia maenoe yaliosahauliwa katika taifa hilo, au kusahihisha masuala nyeti ya dhulma katika jamii ya Uingereza – yaligubikwa kwa neno moja: Brexit. Takriban muda wa miaka mitatu aliyohudumu yote yalifafanuliwa kwa uamuzi wa kujiondoa katika...

Like
425
0
Saturday, 25 May 2019
Cardi B amehairisha tamasha kisa upasuaji
Global News

Kutokana na upasuaji wa kuongeza mwili unaojulikana kama (liposuction) alioufanya  rappa Cardi B umesababisha kujitoa kutumbuiza kwenye tamasha la 92Q Spring Bling lilipangwa kufanyika ijumaa hii mjini Maryland. Kwa mujibu wa mtandao wa TMZ rapa Cardi b amejitoa baaada ya kupata tatizo mara tu baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuongea baadhi ya sehemu za mwili wake. kwa mujibu wa vyanzo vya karibu vya rapa huyo vimeeleza kuwa kwa sasa yupo kwenye mchakato wa kupona baada ya kufanya pia upasuaji wa maziwa yake. Hata...

Like
409
0
Thursday, 23 May 2019
Kundi la IS kuvamia Mashariki mwa DRC
Global News

Wakuu wa vyombo vya usalama katika kanda ya Maziwa Makuu wanakutana nchini Uganda kupanga mikakati ya kukabiliana na tishio la kundi la Islamic State ambalo linasemekana limeanza kuendesha harakati zake katika maeneo ya Mashariki na Kaskazini mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Hayo ni kwa mujibu wa upelelezi wa chombo cha usalama kinachowaleta pamoja wakuu wa usalama katika kanda ya maziwa makuu, kuna uwezekano wa eneo hilo kuingiliwa kirahisi na wanamgambo wa kundi hilo kutokana na ukosefu wa usalama na...

Like
548
0
Thursday, 23 May 2019
Mfalme  amgeuza mlinzi  kuwa  Malkia wake
Global News

Mfalme wa Thailand amemuoa Naibu mkuu wa kikosi cha walinzi wake , na kumpa cheo cha malkia, imesema taarifa ya ufalme huo. Tangazo hilo la kushitukiza limetolewa huku sherehe za kutawazwa kwake zikitarajiwa kuanza Jumamosi, wakati atakapochukua wadhfa wake. Mfalme Maha Vajiralongkorn, mwenye umri wa miaka 66, alikuwa mfalme kikatiba baada ya kifo cha baba yake aliyependwa sana kilichotokea mwaka 2016. Amekwisha wataliki wanawake mara tatu na ana watoto saba. Ufalme ulisema kuwa: Mfalme Vajiralongkorn “ameamua kumpandisha cheo Generali...

Like
521
0
Thursday, 02 May 2019
Maisha ya wengi yako hatarini kutokana na maafa ya kimbunga
Global News

Msumbiji inahitaji misaada ya haraka kuokoa maisha ya walioathirika na kimbunga Kenneth, shirika la msaada limesema. Huku shirika la ‘Save the Children’ limesema hali waliokuwa nayo watu wa Msumbiji inatishia usalama wa maisha yao hivyo ni muhimu misaada zaidi itolewe. Umoja wa mataifa umetoa kiasi cha fedha cha dola milioni 13 ili ziweze kuwasaidia wahanga wa kimbunga wa Msumbiji na Comoro kwa ajili ya chakula, maji na kurekebisha miundo mbinu. Idadi ya vifo vilivyosababishwa na kimbunga , magharibi mwa Msumbiji...

Like
657
0
Tuesday, 30 April 2019
‘Hali ni mbaya kuliko ilivyodhaniwa’ Msumbiji
Global News

Hali kaskazini mwa Msumbiji ni mbaya kuliko ilivyodhaniwa, msemaji wa Umoja wa mataifa ameeleza, siku chache baada ya kimbunga Kenneth kutuwa nchini humo.   Kimbunga hicho kilituwa siku ya Alhamisi kwa upepo mkali wenye kasi ya 220km/h (140mph) kilichoviangamiza vijiji. Takriban watu 700,000 sasa wanadhaniwa kuwa katika hatari katika eneo hilo wakati mvua kubwa ikiendelea kunyesha. Pemba, mji mkubwa wa jimbo la Cabo Delgado kumeshuhudiwa mvua yenye kina cha mita mbili na mafuriko. Msemaji katika ofisi ya uratibu wa masuala...

Like
610
0
Monday, 29 April 2019