Kim Jong-un kukutana na papa Francis

Written by

in

Ofisi ya rais wa Korea kusini imetangaza kuwa kiongozi wa Korea Kaskazini Kim Jong-un amemualika papa Francis kutembelea nchi hiyo.

Mualiko huo wa Pyongyang utawasilishwa na rais wa Korea kusini Moon Jae-in ambaye anatarajiwa kuwa Vatican wiki ijayo akiwa katika ziara zake barani ulaya.

Inaelezwa kuwa Papa Francis sio papa wa kwanza kualikwa kutembelea Korea kaskazini ,ingawa papa John Paul wa pili aliwahi kualikwa pia.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *