Tetemeko la ardhi Indonesia: Indonesia yaomba msaada wa kimataifa, Thailand na Australia zapeleka vifaa vya usaidizi

Written by

in

 

Indonesia imeomba msaada wa jumuiya za kimatafa wakati huu ikihangaika kupata chakula sambamba na vifaa vya uokoaji katika kisiwa cha Sulawesi, ambacho kimeharibiwa vibaya kwa kimbunga na tsunami mwishoni mwa juma lililopita.

Thailand na Australia ni miongoni mwa nchi ambazo tiyari zimetoa misaada yao.

Vikosi vya uokoaji vinaendelea na juhudi za kutafuta watu waliokwama katika majumba makubwa kwenye mji wa Palu huku uwezekano wa kuwakuta wakiwa hai ukiendelea kupungua.

 

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *