Tumieni Vizuri Tabiri Za Hali Ya Hewa

Tumieni Vizuri Tabiri Za Hali Ya Hewa

Like
517
0
Wednesday, 03 September 2014
Local News

joel bendera

Jamii imetakiwa kufuata na kutumia vema utabiri wa Hali ya Hewa unaotolewa kwa muda muafaka na mamlaka ya hali ya hewaTanzania -TMA ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi pamoja na kuepuka madhara ikiwemo mafuriko.
Wito huo umetolewa leo na Mkuu wa wa Mkoa Morogoro JOEL BENDERA wakati akifungua Warsha juu ya umuhimu wa huduma za ushirikishwaji na usambazaji wa taarifa za hali ya hewa kwa Umma.
Wakati huo huo Mkurugenzi wa Mamlaka hiyo Dokta AGNES KIJAZI amewasisitiza wananchi kutopuuza taarifa za mabadiliko ya hali ya hewa ili kujipatia manufaa katika sekta mbali mbali ikiwemo Kilimo na Afya katika jamii inayowazunguka.

 

Comments are closed.