UHONDO YAZINDUA SHINDANO LA KHANGA, MILIONI MOJA KUSHINDANIWA

UHONDO YAZINDUA SHINDANO LA KHANGA, MILIONI MOJA KUSHINDANIWA

Like
891
0
Monday, 14 September 2015
Entertanment

KATIKA kuhakikisha kuwa inamshirikisha msikilizaji wake kwenye kila jambo na hatua inayopiga  93.7 efm, kupitia kipindi chake kipya cha Uhondo ambacho huruka hewani kila siku za Jumatatu hadi Ijumaa kuanzia saa sita mchana hadi saa tisa Alasiri, Kikiwa na watangazaji mahiri Dina Marios na Swebe Santana (Rais wa Wanaume) kimeandaa shindano la Kanga kwa ajili ya wanawake wote wasikilizaji wa Efm.

 

Lengo la shindano hilo, linaloanza leo Septemba 14 na kuishia Oktoba 5 mwaka huu,  kwanza ni kuwahamasisha wanawake wote wakione Kipindi cha Uhondo kuwa kimekuja kwa ajili yao, pili kuinua uchumi wa mtu mmoja mmoja lakini pia tatu kumwonyesha njia nyingine mwanamke itakayomkomboa badala ya kukaa nyumbani mwisho wa siku atajifunza ujasiriamali kupitia biashara ya Kanga.

 

Mfumo wa shindano lenyewe utakuwa kama ifuatavyo:

 

Wasikilizaji wa  E fm  ambao ni wanawake wanakaribishwa kushiriki shindano la kubuni maneno ya Kanga kupitia kipindi cha UHONDO na maneno hayo yawe na neno UHONDO . “Mfano  Uhondo wa Ngoma uingie Ucheze” na Mshindi atajinyakulia kitita cha Shilingi za Kitanzania milioni moja.

Hata hivyo shindano hilo halitaishia hapo, kwani baada ya kupata mshindi neno lake la Ushindi zitatengenezwa  kanga zitakazoandikwa neno hilo ikiwa ni hatua ya pili sasa ya kumwezesha mwanamke kujikwamua kiuchumi.

 

Zikishatengenezwa kanga hizo, Efm kupitia kipindi hicho cha Uhondo, itatatoa nafasi kwa  wanawake kutengeneza pesa na kujikwamua kwa kuuza Kanga hizo na  Mwanamke yoyote hasa kwa Mkoa wa Dar es Salaam na Pwani atachukua kanga hizo na kuziuza ambapo kwa kila doti moja ya kanga atapata asilimia 30% ya pesa.

 

“ Ndugu zangu waandishi wa habari naomba kusisitiza tu hapa kuwa shindano hili  litashirikisha wanawake pekee”. Alisema Dina Marios

 

Asanteni sana kunisikiliza.

 

IMETOLEWA NA

 

DINA MARIOS

 

MTANGAZAJI  NA MTAYARISHAJI WA KIPINDI CH A UHONDO.

DU7C8467

kushoto ni Afisa habari wa E-fm Lydia Moyo akifungua mkutano na waandishi wa habari, katikati ni Mkuu wa idara ya mawasiliano na mahusiano Dennis Ssebo na kulia ni Dina Marious mtangazaji wa kipindi cha Uhondo

 

 

DU7C8485

Mkuu wa idara ya mawasiliano na mahusiano Dennis Ssebo akizungumza na waandishi wa habari, kushoto ni Afisa habari wa E-fm Lydia Moyo na kulia ni Dina Marious mtangazaji wa kipindi cha Uhondo

 

 

DU7C8491

Dina Marious mtangazaji wa kipindi cha Uhondo akizungumza na waandishi wa habari juu ya shindano la Khanga la kipindi cha Uhondo

 

 

DU7C8530

DU7C8601

Dina Marious akielezea jambo

 

 

 

 

 

Comments are closed.