Rais Dkt Magufuli afanya uteuzi wa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TPB

Written by

in

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amemteua Dkt. Edmund Bernard Mndolwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki ya Posta Tanzania (TPB).

Uteuzi wa Dkt. Mndolwa umeanza leo tarehe 23 Aprili, 2018.

Dkt. Mndolwa anachukua nafasi ya Prof. Lettice Rutashobya ambaye amemaliza muda wake.

Gerson Msigwa

Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU

Dodoma

23 Aprili, 2018

 

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *