Tetemeko la ardhi Indonesia: Idadi ya waliofariki dunia yafika takriban watu 832

Written by

in

,

Takriban watu 832 wameuawa baada ya tetemeko kubwa la ardhi na tsunami kupiga kisiwa cha Indonesia cha Sulawezi, kwa mujibu wa shirika la majanga la kitaifa.

Juhudi za kuwatafuta manusura zinaendelea na idadi ya waliofariki inatarajiwa kupanda pakubwa maeneo mengi ambayo kufikia sasa hayajafikiwa na waokoaji yakifikiwa.
Shirika hilo liloongeza kuwa eneo lililoathiriwa lilikuwa kubwa kuliko iliyodhaniwa.
Watu wengine waliripotiwa kukwama kwenye vifusi vya majengo yaliyoporomka siku ya Ijumaa.

 

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *