Mwanaharakati wa Rwanda awa mmoja kati ya wanawake 10 mashuhuri duniani
Global News

Mwanaharakati wa maswala ya wanawake nchini Rwanda Godelive Mukasarasi amewekwa kwenye orodha ya wanawake 10 mashuhuri duniani. Tuzo aliyopewa na Marekani Bi Godelive Mukasarasi inatokana na juhudi za shirika aliloanzisha nchini Rwanda la SEVOTA kusaidia wakinamama walionusurika na mauaji ya kimbari ya mwaka 1994. Amewekwa kwenye orodha hiyo na nchi ya Marekani ambao hivi karibuni walitunukiwa tuzo ijulikanayo kwa jina”International women of Courage ” kutokana na shughuli za shirika lake la SEVOTA ambalo husaidia wanawake...

Like
558
0
Thursday, 12 April 2018
Zuckerberg akiri kosa lake na kuomba radhi
Global News

Mkurugenzi Mtendaji wa Facebook Mark Zuckerberg ametoa maelezo katika Bunge la Marekani- Congress kwa mara ya kwanza Jumanne, akijibu wasiwasi ulioelezwa na wabunge juu ya kushindwa kwa mtandao wa jamii maarufu kulinda taarifa zao. Taarifa hizo za siri za watumiaji wanaofikia milioni 87 ulimwenguni zilizotumiwa na kampuni yenye kujishughulisha na siasa- Cambridge Analytica iliyokuwa na mafungamano na Trump. Mahojiano hayo yanaendelea Jumatano wakati Zuckerberg atakapokutana katika raundi ya pili kujibu maswali mbele ya jopo la Wabunge wa...

1
349
0
Thursday, 12 April 2018
Marekani inapima hatua za kujibu shambulio ‘kemikali nchini Syria
Global News

Marekani inasema kuwa “tayari ana maamuzi mengi” za kujibu shambulio linaloshukiwa kuwa la kikemikali nchini Syria, huku viongozi wa magharibi wakiendelea kupima hatua za kijeshi. Msemaji wa Ikulu ya White House Sarah Sanders amewaambia wandishi wa habari kuwa hakuna ushahidi wa mwisho uliokwisha chukuliwa juu ya mashambulio ya kijeshi. Lakini amesema Marekani inaziwajibisha Urusi na Syria kwa tukio hilo. Baraza la Kitaifa la Usalama la Marekani litakutana Alhamisi, huku waziri mkuu wa Uingereza PM Theresa May akiitisha mkutano wa...

1
1102
0
Thursday, 12 April 2018
Mfanyabiashara na Mmiliki wa mabasi ya HBS, Sultan Hemed amejiua kwa kujipiga risasi asubuhi ya leo Aprili 11, 2018 nyumbani kwake Sikonge mkoani Tabora.
Local News

Akithibitisha taarifa hizo mbele ya waandishi wa habari, Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora, Wilbroad Mutafungwa amesema kuwa marehemu amejipiga risasi mdomoni na kutokea nyuma ya kichwa. “Tumepokea taarifa za kifo cha mfanyabiashara ambaye ni mkazi wa wilaya ya Sikonge, ambaye anaitwa Sultan Hemed mmiliki wa mabasi ya HBS leo asubuhi majira ya saa tatu amejipiga risasi nyumbani kwake. Risasi ambayo imeingilia mdomoni na kutokea nyuma ya kichwani,“amesema Kamanda Mutafungwa. Hata hivyo, Kamanda Mutafungwa amesema kuwa jeshi la polisi...

1
929
0
Wednesday, 11 April 2018
Naibu waziri, Juliana shonza aeleza mkakati wa serikali kuinua soka la Tanzania
Local News

Serikali kupitia kwa Naibu Waziri Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Juliana Shonza imesema kuwa inatambua katika kuhakikisha michezo ikiwepo soka inaimarika nchini, imeendelea kundesha mashindano mbalimbali ya michezo mashuleni kitaifa ikiwepo umiseta na umitashunta. Waziri Shonza ameyasema hayo bungeni akiwa anajibu swali la Mbunge wa Jimbo la Singida Mjini Mussa Ramadhani Sima aliyetaka kufahamu mikakati ya Serikali juu kuinua soka la...

1
680
0
Wednesday, 11 April 2018
36 wahukumiwa kifo Misri kwa kushambulia makanisa ya Coptic
Global News

Mahakama ya kijeshi huko Misri imewahukumu watu thelathini na sita adhabu ya kifo kutokana na makosa ya mashambulizi dhidi ya makanisa ya Coptic. Watu sabini walikufa kutokana na shambulizi la bomu katika kanisa kuu la ki Coptic mjini Cairo mwishoni mwa mwaka 2016, na makanisa ya Alexandria na Tanta yaliripuliwa siku kama hiyo mwezi wa nne mwaka uliofuata. Tayari kundi la wanamgambo wa kiislamu wenye msiamamo mkali wamekiri kuhusika na mashambulizi hayo matatu. Wameendelea kukiri kuwa kazi yao kubwa ilikuwa...

Like
761
0
Wednesday, 11 April 2018
Trump aapa ”kutumia nguvu” kujibu shambulio ”la kemikali” Syria
Global News

  Rais wa Marekani Donald Trump ameahidi ” kutumia nguvu ” kujibu madai ya shambulio la kemikali nchini Syria, huku mataifa ya magharibi yakitafakari hatua watakayoichukua. “Tuna njia nyingi za kijeshi,”aliwambia waandishi wa habari. Aliongeza kuwa hatua ya kujibu shambulio hilo itaamuliwa katika kipindi cha “muda mfupi”. Bwana Trump alisema kuwa Marekani inapata ”msaada mzuri” juu ya nani aliyehusika na shambulio la Douma Jumamosi. Duru za kitabibu zinasema makumi kadhaa ya watu waliawa...

Like
371
0
Tuesday, 10 April 2018
Huyo Kamusoko Anataka Mashabiki Tu
Local News

Kiungo wa Yanga thabani kamusoko anataka nguvu ya mashabiki wa timu yao siku ya Jumamosi wakati Yanga itakapokuwa inacheza nyumbani dhidi ya Wolaitta Dicha mchezo wa mtoano kuwania nafasi ya kucheza hatua ya makundi ya kombe la shirikisho Afrika. Kamusoko amesema kipindi hiki ambacho timu ipo kwenye wakati mgumu wachezaji wanahitaji zaidi sapoti ya mashabiki kuliko kitu kingine. “Timu inapokuwa haifanyi viruri ndiyo inahitaji sapoti kubwa ya mashabiki kwa hiyo nawaomba mashabiki waje kwa wingi kuisapoti timu yao kwa sababu...

Like
711
0
Friday, 06 April 2018
Uhamiaji -Tanzania Yambana Abdul Nondo Athibitishe Uraia Wake
Local News

Mashtaka ya kujiteka nyara yanayomkabili kiongozi wa mtandao wa wanafunzi nchini Tanzania (TSNP), na mtetezi wa haki za binadamu Abdul Nondo, yanaonekana kuchukua sura mpya, baada ya maafisa wa uhamiaji kumlazimisha athibitishe ni raia wa Tanzania. Licha ya mwanafunzi huyo kutoka mkoa wa Kigoma kupata ufadhili wa masomo wa Chuo Kikuu Cha Dar es Salaam (UDSM) kutoka serikalini, anahitajika kupeleka katika idara ya uhamiaji cheti chake cha kuzaliwa, cha baba yake, mama yake, cha bibi na babu mzaa baba na...

Like
517
0
Friday, 06 April 2018
Magufuli Kuzindua Ukuta wa Machimbo ya Madini ya Tanzanite Leo
Local News

Rais John Magufuli wa Tanzania, leo anatarajiwa kuzindua ukuta wa machimbo ya madini ya Tanzanite,iliopo eneo la Mererani, kaskazini mwa nchini Tanzania Ukuta huo wenye urefu wa kilomita 24.5 na urefu wa mita tatu kwenda juu, umejengwa kufuatia agizo lililotolewa na Rais John Magufuli, kama jitihada za kudhibiti na kuzuia utoroshwaji wa madini hayo, ambayo yanapatikana nchini Tanzania pekee. Awali, Mwezi Februari, wakuu wa vyombo vya usalama, walitembelea eneo hilo, kuukagua ukuta huo uliojengwa kwa gharama za Kitanzania isiyozidi bilioni...

Like
762
0
Friday, 06 April 2018
Spika Ndugai aizungumzia hoja ya Bashe kuhusu mauaji na utekaji
Local News

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amezungumza kuhusu taarifa za Mbunge wa Nzega Mjini kwa tiketi ya CCM, Hussein Bashe aliyetangaza kuwasilisha hoja binafsi Bungeni kuhusu matukio ya kiusalama nchini. Katika mahojiano na kituo cha runinga cha Azam, Spika Ndugai amesema bado hawajapata taarifa rasmi kutoka kwa Bashe na kutoka kwa katibu wa wabunge wa CCM Bungeni kama kanuni zinavyoelekeza. “Niliona barua yake kwa Katibu wa Bunge akimtaharifu kuwa anayo nia ya kuleta hoja binafsi...

Like
508
0
Thursday, 05 April 2018
« Previous PageNext Page »